Pages

KAPIPI TV

Thursday, July 24, 2014

UZINDUZI WA MRADI WA SAEMAUL UDONG KIJIJI CHA CHEJU UNGUJA


IMG_7086Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK.ALi Mohamed Shein akipata maelezo kutoka Naibu katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na Maliasili Nd,Juma Ali Juma wakati alipotembelea kituo cha kukausha Embe Dodo katika Kijiji cha Cheju kibonde maji leo  kilichojengwa na Shirika la misaada la Koika nchini Korea kupitia    Mradi wa  SAEMAUL UDONG   .[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]
IMG_7100Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK.ALi Mohamed Shein na Balozi wa Korea Bw.IL Chung (katikati) wakiangalia embe zilizokaushwa zikiwa katika Mpango maalum wa kuhifadhiwa  wakati alipotembelea kituo cha kukausha Embe Dodo katika Kijiji cha Cheju kibonde maji leo kilichojengwa na Shirika la misaada la Koika nchini Korea kupitia Mradi wa  SAEMAUL UDONG   .[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]  
IMG_7107
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK.ALi Mohamed Shein na Balozi wa Korea Nchini Tanzania Bw.IL Chung (katikati) wakiangalia embe zilizokaushwa zikiwa katika Mpango maalum wa kuhifadhiwa  wakati alipotembelea kituo cha kukausha Embe Dodo katika Kijiji cha Cheju kibonde maji leo  kilichojengwa na Shirika la misaada la Koika nchini Korea kupitia Mradi wa SAEMAUL UDONG   .[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]  
IMG_7141 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK.ALi Mohamed Shein(katikati) na Balozi wa Korea Nchini Tanzania Bw.IL Chung wakipata maelezo kutoka Naibu katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na Maliasili Nd,Juma Ali Juma (kulia) wakati alipotembelea mitambo katika kituo cha kukausha Embe Dodo katika Kijiji cha Cheju kibonde maji leo kilichojengwa na Shirika la misaada la Koika nchini Korea kupitia  Mradi  SAEMAUL UDONG   .[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]  
IMG_7152Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK.ALi Mohamed Shein akibadilishana mawazo na  na Balozi wa Korea Nchini Tanzania Bw.IL Chung mara baada ya kutembelea  kituo cha kukausha Embe Dodo katika Kijiji cha Cheju kibonde maji leo kilichojengwa na Shirika la misaada la Koika nchini Korea kupitia  Mradi  SAEMAUL UDONG   .[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]

MBUNGE PETER MSIGWA AKABIDHI MSAADA

SAM_6953
chuo cha Kitanzani Islamic center kilichoko mjini Iringa. (Picha zote na Denis Mlowe)
SAM_6980
Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa akikabidhi msaada wa Sukari, kwa Kaimu Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Abubakari Chalamila kwa ajili ya kituo cha Kitanzani Islamic


Na Denis Mlowe,Iringa
MBUNGE wa Iringa Mjini(Chadema) Mchungaji Peter Msigwa amekikabidhi chuo cha Kitanzani Islamic Center msaada wa Sukari,Unga wa Ngano, tende na mafuta ya kupikia ikiwa ni utaratibu wake wa kila mwaka kukisaidia chuo hicho.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo jana kwa Shekhe Mkuu wa Mkoa Iringa Abubakar Chalamila, Mchungaji Msigwa alisema kuwa lengo la kugawa kipindi hiki ni kuwaunga mkono Waislamu katika mfungo wa Ramadhani na kuwakumbuka wale wote wanaoishi katika mazingira magumu.

Mchungaji Msigwa alisema ni jukumu la wadau kuweza kuwasaidia wale wote bila kujali itikadi za vyama kwa kuwa binadamu wote ni wamoja kwa sasa.

Mchungaji Msigwa alikabidhi tambi katoni zaidi ya katoni 50, katoni 40 za mafuta ya kupikia, kilo 250 za unga wa ngano na sukari kilo 750 vyote vikiwa na jumla ya thamani zaidi ya shilingi milioni 1.5.

Alisema ataendelea kutoa msaada kwa vituo vingine vya watoto yatima na wasiojiweza katika kipindi hiki cha mfungo wa Ramadhan.

Akishukuru kwa msaada huo Kwa niaba ya chuo cha Kitanzani Islamic Center chenye jumla ya wanafunzi 120 ambao wanachukua mafunzo ya dini ya kiislamu Kaimu Shekhe Mkuu wa Mkoa Iringa, Abubakar Chalamila alisema ni jambo la kujivunia kuwa na mbunge asiyechagua itikadi za dini na mbunge ni akichaguliwa anakuwa wa watu wote bila kubagua watu wake.

“Namshukuru sana Msigwa kwa kuweza kutoa msaada huu na utafikishwa kwa wale wote waliolengwa kupewa na hasa wale wasiojiweza ndio watafaidika na msaada huu wa mbunge wa iringa mjini.” Alisema |Chalamila

Chalamila aliwataka wadau wengine kuwakumbuka watu wasiojiweza na wanaoishi katika mazingira magumu mara kwa mara kwa kuwa ni thawabu kubwa kuweza kuwasaidia.

"KILA MTU ANA HAKI YA KUGOMBEA UBUNGE,KAMA ULIWAJIBIKA VIZURI KWA WANANCHI WATAKUCHAGUA TENA"-MH.MUNDE

Na Mwandishi wetu.
"Hakuna mtu mwenye haki miliki ya Ubunge,kwani hiyo ni dhamana tu tuliyopewa na wananchi,lakini kwanini ifikie hatua ya watu kuhitilafiana na kugombana pasipo sababu za msingi"hii ni kauli ya Mbunge wa vitimaalumu  mkoa wa Tabora Mheshimiwa Munde Tambwe wakati akizungumza na mtandao huu.

Wakati huu kabla  ya kuelekea kwenye mchakato wa kura za maoni  kwa Chama cha Mapinduzi kumekuwa na hali ya kupigana vikumbo kwa baadhi ya makada wa Chama hicho hatua ambayo imebadili kabisa ukurasa wa maisha ya kawaida ya kibinadamu na kujenga sura mpya ya siasa za chuki kwa mtu mmoja kumchafua mwingine au kikundi cha watu fulani kumchafua mtu mmoja jambo ambalo linadhihirisha watu wamesahau kabisa majukumu yao na kugeuza kuwa ni ajenda muhimu ya katika maisha.

Jambo hili limemsukuma Mbunge wa vitimaalum Mheshimiwa Munde Tambwe na kuona kuwa watu wanakoelekea siko ambako CCM inataka kutekeleza malengo yake katika kuwahudumia wananchi ambao kimsingi ndio wamekiweka madarakani chama hicho.

"Ninavyofikiri mimi kwa muda huu sisi kama wanaccm ni vema tushirikiane,tujenge mshikamano katika kutekeleza Ilani ya Chama chetu badala ya kukaa tunajengeana chuki zisizo na msingi,yaani huyu kamsema yule na yule kamsema huyu,hii haitusaidii kabisa itatufanya tushindwe kujibu maswali ya msingi ya wananchi watakapo tuuliza nini tumefanya tangu tuwe madarakani"alisema Mheshimiwa Munde

"Ubunge si haki miliki ya mtu,kwani yeyote anahaki ya kugombea muda ukifika lakini kwasasa tunatakiwa kuwasaidia wananchi,wewe kama umewajibika ipasavyo kwa wananchi, wenyewe watakuchagua hata kama ni vipindi vitatu,lakini kama umepewa dhamana ya kuwa mbunge halafu unashindwa kutekeleza majukumu yako huna sababu ya kugombana na watu,wananchi wenyewe wataamua na wewe utavuna ulichopanda"msisitizo wa ziada wenye lengo la kujenga.

Kwa kauli hii ni vema pia watu waliopewa dhamana au ridhaa na wananchi ya kushika wadhifa walionao wapate fursa ya kujipima,je,wanayo nafasi tena ya kujitosa wakati wa kura za maoni utakapowadia?au ndio kuanzisha chuki na vurugu kwa kila mtu mwenye uwezo wa kifedha unayemuona amevaa sare ya Chama na kutoa misaada kwa watu  unamhisi anataka kuchukua nafasi yako?

"Hakuna mtu anakatazwa kushirikiana na wengine katika kufanya kazi za chama ni vema tukafuata taratibu na kanuni za chama chetu na muda ukifika refarii atapuliza kipenga kila mmoja wetu ataona kama anauwezo wa kuomba nafasi anayoitaka kuliko kuanza kujipitisha huku na kule na kujinadi,binafsi sitofanya hivyo isipokuwa nawaombeni makada wenzangu tushirikiane kutekeleza Ilani ya chama chetu ili wenzetu wa vyama vya upinzani wakose la kuhoji"alisema Mheshimiwa Munde

"Chama cha Mapinduzi kina utaratibu mzuri sana katika kuwapata viongozi wa kada mbalimbali wakiwemo wabunge ni dhahiri kwamba mtu akifuata taratibu na kanuni za chama chetu atakuwa na haki ya kuwania nafasi anayoitaka na si kweli kwamba kutumia fedha kwa maana ya kuwahonga wapigakura inaweza ikawa sababu ya kuchaguliwa hilo si kweli"alisema huku akitahadharisha wanachama hasa makada ni vema wakashirikiana katika kutekeleza majukumu ya chama katika kutimiza ahadi zilizotolewa na viongozi wakati wa kuomba ridhaa kwa wananchi uchaguzi wa mwaka 2010.

"KWA PAMOJA TUSHIRIKIANE KUUJENGA MKOA WETU,VIONGOZI TUWASAIDIE  WATU WAONDOKANE NA UMASIKINI WA KIPATO,CCM DAIMA"      
  

MAENDELEO BANK YAANZISHA HUDUMA ZA BIMA

0D6A0674
0D6A0704
Wafanyakazi wa Maendeleo Bank na wa UAP wakiwa katika picha ya Pamoja.
maendeleo
Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Bank Ibrahim Mwangala (kulia) akipeana mkono na Nick Itunga Mkurugenzi mtendaji wa UAP Insurance Nick Itunga baada ya kuzindua huduma ya bima kupitia Maendeleo Bank
………………………………………………………………………… Maendeleo Bank imezindua huduma ya bima ikiwa ni lengo la kuwapatia wateja huduma zote muhimu ndani ya dari moja. Pia inachangia juhudi za serikali kuboresha na kufikisha elimu na huduma za bima kwa wananchi wengi ambao hawajafikiwa. Maendeleo Bank Insurance Agency imeanzishwa ili kuunga mkono mkakati wa Serikali wa huduma za kifedha jumuishi ambazo zitahamasisha wananchi wengi watumie na wafikiwe na huduma za kifedha ikiwa ni pamoja na bima.

Katika huduma za bima, Maendeleo Bank Insurance Agency imejipanga kutoa huduma zote za bima isipokuwa za maisha. Huduma zifuatazo zinapatikana Maendeleo Bank Insurance Agency: Bima za binafsi na za biashara zikiwemo bima za moto na wizi, bima za magari ya aina zote pamoja na mitambo, bima za nyumba na vitu vya majumbani, bima za wafanyakazi, bima za maofisini, bima za biashara, bima za wakandalasi, bima za vitu vinavyosafirishwa na bima za afya.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa ‘’Maendeleo Insurance Agency ‘’ Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Bank Ndugu Ibrahim Mwangalaba alisema ‘’Kwa kuungana na kampuni ya kimataifa ya Bima yaani, UAP Insurance ni faida kubwa kwa wateja wa Maendeleo Bank Insurance Agency kwani UAP Insurance inauwezo mkubwa wa kubeba bima zote zitakazopelekwa kwao na iwapo itatokea tatizo linalohitaji kugharimia madhara ya kilichowekewa bima, basi mteja wetu hatasumbuka kwani Maendeleo Bank Insurance Agency itafuatilia mambo yote kwa muda mfupi iwezekanavyo ili mteja asisumbuke.

 Mwangalaba aliongeza ‘’ Bima binafsi au za biashara ni muhimu mno katika kulinda kipato na mali za wateja wetu, uanzishwaji wa huduma za bima ni kuishi kwa vitendo katika kauli mbiu yetu ya pamoja nawe katika maendeleo, kwani tunapenda kuona maendeleo ya wateja wetu yakienda mbele si kurudi nyuma kwa matukio yanayoweza kuzuilika kwa kuwa na bima’’

SITOWACHEKEA WACHAFUZI WA MAZINGIRA - MH.MAHENGE


_DSC0298
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Mh. Dkt. Injinia Binilith Satano Mahenge akipata maelezo kutoka kwa Afisa Mazingira wa Wilaya ya Ilala bw. Abdon Mapunda (wa pili kushoto) alipotembelea bwawa la maji taka la Vingunguti jijini Dar es Salaam.
_DSC0304
Maji machafu yanayotoka katika viwanda mbalimbali vilivyopo Vingunguti jijini Dar es Salaam ambayo hutiririsha maji yake katika mto wa msimbazi, maji ambayo yanahatarisha afya ya binadamu.
_DSC0342
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Mh. Dkt. Injinia Binilith Satano Mahenge (wa katikati) akizungumza na Menejimenti ya kiwanda cha kuzalisha mafuta ya kupikia (Murza Oil Mills Limited) kilichopo vingunguti jijini Dar es Salaam, wakati wa ziara yake ya kukagua mazingira katika kiwanda hicho na kuwataka watumie mfumo sahihi wa maji taka ili kulinda mazimgira na kuepuka athari mbalimbali kwa wananchi.
_DSC0380
Meneja wa kiwanda cha Murza Oil Mills Limited Bw. Dinesh Kana (wa tatu kushoto) akitoa maelezo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Mh. Dkt. Injinia Binilith Satano Mahenge (wa nne kushoto) kuhusu mfumo wa maji taka ambao wanautumia katika kiwanda hicho.
_DSC0394
sehemu ya dampo la Pugu Kinyamwezi lilopo jijini Dar es Salaam
_DSC0398
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Mh. Dkt. Injinia Binilith Satano Mahenge akipata maelezo kutoka kwa Bw. Richard Matari ambaye ni msimamizi wa dampo la Kinyamwezi lililopo Pugu jijini Dar es Salaam, baada ya waziri kuwasili katika dampo hilo na kutaka kujua utendaji wa kazi zao katika kulinda Mazingira.
………………………………………………………………………….

Na Rashda Swedi- VPO
Viwanda vitakavyokiuka masharti na kanuni za kulinda mazingira havina budi kufungiwa mpaka vitakapofuata taratibu na  sheria za utunzaji wa Mazingira.

Hayo yamesemwa hivi karibuni jijini Dar es Salaam  na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Mzingira Mh. Dkt. Injinia Binilith Mahenge alipofanya ziara fupi ya kutembelea kiwanda cha kuzalisha mafuta  (Murza Oil Mills Limited) kilichopo Vingunguti.  

hata hivyo Mheshimiwa Mahenge alisema hayo baada ya kutoridhishwa na mfumo wa maji taka ya kiwanda hicho na kuwaambia waboreshe zaidi mfumo  wa maji taka kwa lengo la kulinda mazingira kwa sababu  wasipofanya hivyo Serikali itachukua hatua ya kukifunga  kiwanda hicho.

wakati huo huo, mwanasheria wa NEMC Bw.Manchale Heche amesema kuwa, kutokana na ziara waliyoifanya pamoja na Mh. Waziri wamegundua mengi na hawatafumbia macho suala la viwanda vinavyotumia magogo,kuni na wale wasiokuwa na mfumo mzuri wa majitaka endapo hawatafuata masharti waliyokubaliana nayo viwanda hivyo vitafungiwa.

Aidha, Waziri alitembelea pia bwawa la maji taka lililopo Vingunguti jijini Dar es Salaam na kugundua kuwa kuna uharibifu mkubwa wa Mazigira, kutokana na maji machafu yanayotoka katika viwanda mbalimbali karibu na eneo hilo kutiririsha maji yao kwenye mabwawa hayo.Kutokana na hilo amewataka  Manispaa kushirikiana na NEMC kuvijua viwanda vinavyopitisha maji machafu moja kwa moja bila kufuata utaratibu uliowekwa.

“Ni wajibu wa kila mtu kulinda mazingira na sio wajibu wa Ofisi ya makamu wa Rais tu kwani Mazingira ni yetu sote na ni muhimu kuyalinda” Mh. Mahenge alisema.Alisisitiza kuwa, huo hautakuwa mwisho wa ukaguzi wa viwanda utaratibu wa kukagua viwanda utaendelea kuangalia Mazingira rafiki kwa wananchi.

"AJIRA YA VIJANA KWA USAFIRI WA BAISKELI TABORA NI MOJA KATI YA AJIRA TULIZOZITEGEMEA"

Usafiri baiskeli mkoani Tabora wazidi kuimarisha ajira kwa vijana hatua ambayo sasa imefanya kuwepo kwa ongezeko la vijana wengi mjini kuliko ilivyokuwa hapo awali,kwa hivi sasa imeshuhudiwa baadhi ya vijana wa vijiji jirani na Tabora mjini wamekuwa wakijidamka mapema asubuhi kuja mjini kufanya kazi ya kusafirisha abiria kwa usafiri huo wa baiskeli na kujipatia fedha kwa ajili ya kujikimu kimaisha wakati huu wa majira ya kiangazi ambapo vijijini hakuna shughuli za kilimo.Hata hivyo licha ya vijana hao kupata fursa ya kujiajiri wenyewe lakini wamekuwa katika mazingira hatarishi kutokana na ukweli kwamba wengi wao hawajui sheria za usalama barabarani na hivyo kujikuta wanavunja sheria na kusababisha ajali zinazochangia vifo visivyo vya lazima au kubaki na ulemavu wa kudumu.Jambo hili linahitaji kuchukuliwa hatua ya kuwadhibiti vijana hao bila kuathiri mwenendo mzima wa ajira zao kwakuwa wengi wao kutokana na ajira hizo wanategemewa na familia zao.Ajira za vijana kwa kutumia usafiri wa baiskeli katika mtazamo wa harakaharaka ni dhahiri kwamba ni ajira tulizozitegemea kwa kile kinachoonekana katika fikra za haraka kwa vijana waliowengi ni kujipatia fedha za chapchap kupitia mpango huo usio rasmi.Aidha kwa upande mwingine ni kweli kwamba kwasasa mkoa wa Tabora hakuna viwanda au kazi nyingine zaidi ya kupata vibarua kwenye majengo ya watu binafsi ambayo malipo yake ni kati ya shilingi 3000 na 5000 kwa kutwa nzima.Ukiachilia mbali ajira kwenye makampuni ya ulinzi imekuwa na usumbufu kwa vijana kutokana na kutolipwa mishahara kwa wakati jambo ambalo linawafanya vijana wengi kuona ni bora zaidi aendeshe baiskeli kuanzia majira ya saa 12 asubuhi hadi saa tatu usiku ambapo hujipatia wastani wa kiasi cha shilingi elfu kumi.Hii inawafanya idadi kubwa vijana kuingia kwenye ajira hii bila kikwazo kwani kwa wanaoishi mjini huweza kumudu kulipa kodi ya pango ya shilingi elfu kumi kwa mwezi lakini hata kuendesha maisha yake na familia ya watu wanne yaani Mke,watoto wawili na yeye mwenyewe.Kuendesha baiskeli hakuhitaji leseni wala kikwazo chochote kinachowabana kisheria zaidi ya kujaza upepo kwenye tairi za baiskeli na kuanza kunyonga pedeli kulingana na uzito wa mteja aliobebwa kwenye usafiri huo.Ni kazi nyepesi kama waionavyo vijana wenyewe.Lakini kwa wachunguzi wa mambo wanasema kuwa hata wimbi la vibaka katika maeneo mbalimbali Tabora mjini limepungua kwa kiasi kikubwa kwakuwa kijana anayejihusisha na ajira hiyo ya usafiri wa baiskeli anapomaliza muda wake hiyo saa tatu usiku huwa amechoka sana hata hawezi kwenda kukaa  vijiweni na kujihusisha na vitendo viovu. 

Wednesday, July 23, 2014

BABAREVO AMTWANGA SHEMEJI YAKE MSIBANI-KIGOMA

MSANII  wa Muziki wa kizazi  kipya ( Bongo fleva) Clayton Revocatus (Baba Revo) anadaiwa kumshushia kichapo shemeji yake Pili Abdallah kwa madai ya kutaka shemeji mtu arudishe mali za marehemu mdogo wake Patrick Revocatus ambaye,amefariki mwishoni mwa wiki iliyopita mwaka huu.
 
Akizungumza na mwandishi wa KAPIPIJhabari.COM kigoma Ujiji juzi Pili alisema,chanzo cha kupigwa na msanii huyo ni kutokana na  msanii huyo kudai cheni aina ya silva  yenye thamani y ash.100.000 ambayo aliuziwa na mdogo na Mbunge wa Kigoma Kaskazi   Bashir  Kabwe aliyokuwa akiivaa marehemu enzi ya uhai wake.
 
“marehemu alikuwa hana mali zaidi ya sh.10,000 tu ilikuwa  katika pochi yake,ambayo nilitumia kumpeleka hospitali ya rufaa maweni,shemeji na nduguze walimtenga  marehemu wakati anaugua, haja zote anamalizia kitandani  na nilimsitiri ” alisema Pili.
 
Marehemu alivunjika mguu ambao  hakuupatia tiba kwa wakati na Julai ,18,2014 alizidiwa ,kwa kushirikiana na rafiki zake wakampeleka hospitali hiyo na usiku wa siku hiyo alifariki pasipo msanii huyo kuonyesha  hisia za huzuni  na  baada ya mazishi alimtaka shemeji yake arudishe vitu vya marehemu.
 
Mama mzazi wa mpenzi wa marehemu Janeth John  alisema  hakumuoa bali waliishi kwa kuibana yapata miezi sita sanjari na kufahamu mahusiano yao ambayo alimuonya mwanae kwa muda mrefu achane na familia hiyo.
 
Alisema ameingia gharama ya kulipa cheni hiyo ambayo binti yake anadai hakuchukua  sanjari na sh.10,000 iliyokuwa kwenye waleti ya marehemu kwa lengo la kuondoa shari na  msanii huyo.
 
Kwa upande wa msanii huyo Baba Revo alipohojiwa na gazeti hili akiri kuvurugu kwenye msiba wa nduguye na kusisitiza marehemu hakuwa na mali zaidi ya wallet na cheni ambayo shemeji mtu alipaswa awape wahusika.
 
Alisema  marehemu alitakiwa apasuliwe mguu lakini shemeji yake alimtorosha hospitalini marehemu na kudai ana haki  kuelimisha na kuadibisha  jamii husika na kuonya  wanawake waache ukatili hasa wa kunyanyasa wanaume .
 
Kamanda wa Polisi mkoani humo,Frasser Kashai alipoulizwa juu ya hilo alisema hajui na kuvilaumu baadhi ya vituo vidogo  vya Polisi vinachangia kuzorotesha baadhi ya matukio kufika kwa wakati katika vituo vikubwa na kudai kulifuatilia suala hilo .
 
Msanii huyo ni mkazi wa mtaa wa Kitabwe kata ya mwanga kusini wilaya ya kigoma mkoani hapa,ameshangaa shemeji huyo kufungulia jalada la kesi la mashambulizi kituo cha kati ambapo yeye alimfungulia kituo cha msufini wakati huohuo Kamanda Kashai anasema ni ruksa ilimradi pawe karibu na eneo analoishi mlalamikaji.

ACT YAITOLEA MACHO UKAWA - KIGOMA



Na Magreth Magosso,Kigoma

Mwenyekiti  wa  chama cha  ACT Taifa  Lucas  Limbu  aomba  umoja wa Katiba ya watanzania UKAWA wakaze buti kuishinikiza serikali ya ccm , ikubali mabadiliko ya mfumo wa serikali tatu kwa mujibu wa mapendekezo ya umma kupitia Rasimu mpya ya katiba.
 
Akitoa kauli hiyo kigoma ujiji ,Limbu alidai serikali inakaidi kupokea maboresho ya katiba ya awali ya mwaka 1977 kupitia mchakato wa maboresho ya rasimu mpya ambapo Jaji mstaafu Sinde Warioba aliikabdihi rasmi kwa wajumbe husika ili kuboresha rasimu hiyo ambayo ni mwiba kwa viongozi wachache  waliozoea  mfumo nyonyaji ambao unazalisha  mabwenyenye wanaotumika kulinda maslai ya wachache.
 
“ccm imeacha kuenzi na kutumia  falsafa ya hayati Mwalimu Nyerere sanjari na misingi ya katiba ambapo misingi ni fursa kwa kila mtanzania kunufaika na rasilimali zilizopo kwa lengo la kuondoa matabaka katika jamii ili kuepusha vurugu zinazolinyemelea taifa kwa ujumla” alibainisha Limbu
 
Alisema Ukawa wasikubali kununuliwa na chama tawala ili kudhoofisha mawazo ya wengi dhidi ya mfumo bora wa serikali ,ambao utaondoa mfumo dume  unaochangia  vyama vya upinzani kushindwa kushika hatamu ya mabadiliko kwa jamii husika.
 
Alishauri serikali itumie mfumo pendekezwa  juu ya awamu za utawala dhidi ya urais uwe wa mlinganio sawa  wa muungano kulingana na kipindi  husika ,kwa dhati ya kujenga umoja na mshikamano wa taifa,ambapo alitaka ngazi ya urais ufuatwe  yaani Bara na visiwani kwa kuzingatia usawa na haki ya utawala wa nchi.
 
Pia alisema  kitendo cha Jaji mkuu wa serikali kumtusi Mbunge wa kigoma kaskazini hakistahili kuvumiliwa na kumtaka rais  Jakaya Kikwete achukue hatua za kumwajibisha jaji huyo,ambaye ameonesha utovu wa nidhamu kwa wananchi na dunia kwa ujumla.

Naye  mwenyekiti Baraza la wazee chama hicho wa hapa Jafari Kasisiko alisema jamii ifunguke kubaini vyama sahihi vyenye lengo na nia ya kutetea maslai ya wengi na waondokane na tabia ya kukumbatia vyama vyenye kuwaangamiza pasipo wenyewe kubaini

POLISI APONGEZWA BAADA YA KUKATAA RUSHWA YA WATUMIAJI WA DAWA ZA KULEVYA-TABORA

Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Suzan Kaganda akimpongeza na kumpa zawadi ya pesa Mkaguzi wa Polisi Harun Kasubi baada ya kufanikiwa kuwakamata watu wapatao kumi na wawili waliokuwa wamejifungia ndani ya Guest house inayofahamika kwa jina la KENIOS wakiwa wanajidunga dawa za kulevya ambapo watu hao walitaka kumpa rushwa ya shilingi 90,000/=ili waachiwe huru.
Baadhi ya dawa za kulevya na vifaa vya matumizi ya dawa hizo zilizokamatwa zikiwa zinatumiwa na watu hao kumi na wawili waliokamatwa KENIOS GUEST HOUSE huko eneo la kata ya Isevya manispaa ya Tabora.
Kamanda wa Polisi ACP Suzan Kaganda ameuambia mtandao huu kuwa waliokamatwa katika operesheni ya kuwasaka watumiaji,wauzaji na wasambazaji wa dawa za kulevya mkoani Tabora ni Hamisi Athuman Mbao(39) ,Issa Abdallah(22),Ally Bakar(34),Densi Petro(34)Mrisho Shaban(22)Ramadhan Mbade(40)Haji Muki(40),Said Kasumari(24),Shaban Haruna(25)David Male(43)Ramadhan Hamis na Paschal Robert.

Kamanda Suzy amesema watu hao baada ya kukamatwa walitaka kutoa rushwa ya shilingi elfu tisini kwa kiongozi wa timu ya makachero wanaofuatilia dawa za kulevya mkoani Tabora ambaye ni mkaguzi wa Polisi Harun Kasubi ambapo alikataa na kuwafikisha kituo kikubwa cha Polisi Tabora.

 

TOFAUTI ZA DINI ZISIWAGAWE WATANZANIA , MWINYI.

Futari - 1
Futari - 3
Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi akiwasili katika viwanja vya Karimjee kuhudhuria Futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Saidi Meck Sadiki (wa pili kutoka kushoto) kwa watoto yatima kutoka vituo mbalimbali vya kulelea watoto hao vya jiji la Dar es salaam. Wengine wanaoonekana kutoka kulia ni Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishna Suleiman Kova na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Alhadi Mussa Salum.
Futari - 7
Baadhi ya akina mama na watoto waliohudhuria Futari hiyo wakipata Chakula.
Futari -4
Baadhi  watoto yatima kutoka vituo mbalimbali vya kulelea watoto hao vya jiji la Dar es salaam wakijumuika pamoja katika Futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Saidi Meck Sadiki.
Futari -5
Rais mstaafu wa Awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa Futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam kwa watoto yatima kutoka vituo mbalimbali vya kulelea watoto hao vya jiji la Dar es salaam akijumuika pamoja  na watoto hao na wageni mbalimbali walioalikwa katika Futari hiyo.
Futari- 6
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Alhadi Mussa Salum (wa kwanza kushoto) na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahmani Kinana wakijumuika  katika Futari hiyo.
Futari -9
Futari -11
Rais wa Tanzania wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa Futari iliyoandaliwa na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam  akisisitiza umuhimu wa kulinda na kutunza amani iliyopo kwa kuendelea kudumisha upendo na ukarimu ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo yaliyomo katika vitabu vitakatifu.
Futari -12
Mkuu wa mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Songea Dkt. Christine Ishengoma(kulia) wakiungana na viongozi wengine  kushiriki  Futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam kwa watoto yatima kutoka katika vituo mbalimbali katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam.
Futari-2
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishna Suleiman Kova (katikati) akifafanua jambo kwa viongozi wa mkoa wa Dar es salaam  Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Bw. Saidi Meck Sadiki (wa pili kutoka kulia), Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bw. Raymond Mushi(kulia) na  Mkuu wa wilaya ya Temeke Bi. Sophia Mjema (kushoto) wakati wa Futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa huo katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Na. Aron Msigwa –MAELEZO.
 Dar es salaam.
 
Rais mstaafu wa awamu ya pili , Ali Hassan Mwinyi ,amewataka watanzania kuwa makini kwa kutoruhusu tofauti za dini zilizopo hapa nchini kuwa chanzo cha mgawanyiko miongoni mwao.
 
Kauli hiyo ameitoa jana usiku jijini Dar es salaam wakati wa Futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Saidi Meck Sadiki  kwa watoto wanaoishi katika vituo vya kulelea watoto yatima, wananchi na viongozi mbalimbali iliyofanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam.
 
Mzee Ali Hassan Mwinyi ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa Futari hiyo amesema kuwa kila Mtanzania bila kujadili itikadi na dini aliyonayo ana wajibu wa kulinda na kutunza amani iliyopo kwa kuendelea kudumisha upendo na ukarimu kwa wenzake ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo yaliyomo katika vitabu vitakatifu.
 
“Nawasihi Watanzania wenzangu tuendelee kupendana, tuwe wamoja katika kushirikiana, kamwe tusiruhusu wala kukubali mgawanyiko wa dini wala itikadi zetu” Amesisitiza.
 
Amewashukuru viongozi wa mkoa wa Dar es salaam wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Saidi Meck Sadiki kwa uamuzi walioufanya wa kuandaa Futari iliyowaunganisha watoto yatima, wananchi na viongozi mbalimbali  bila kujadili itikadi na dini zao ikiwa ni ishara ya kuonyesha upendo na ukarimu walio nao.
 
Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Saidi Meck Sadiki akizungumza wakati wa Futari hiyo aliyowaandalia wageni hao amesema kuwa serikali ya mkoa   inaendelea kutekeleza  mipango mbalimbali ya maendeleo ikiwemo  ukarabati  na ujenzi wa miundombinu iliyoharibiwa vibaya wakati wa msimu wa  mvua jijini Dar es salaam.
 
Bw. Sadiki ameziagiza Halimashauri za Wilaya za Temeke, Ilala na Kinondoni  na Wakala wa Barabara (TANROAD) mkoa wa Dar es salaam kuhakikisha kuwa wanarejesha hali ya kupitika kwa barabara iliyokuwepo mwanzo ili kuwaondolea kero ya usafiri wananchi.
 
Amezitaka mamlaka hizo kutumia fedha za ndani na zile zilizotolewa na Serikali Kuu kukamilisha ukarabati wa miundombinu  hiyo yakiwemo madaraja yaliyosombwa na maji kwa muda muafaka ili kuruhusu magari kuweza kufika katika maeneo hayo.
 
Katika hatua nyingine Bw. Meck Sadiki ametoa wito kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam kushiriki kikamilifu katika suala la usafi na uhifadhi wa mazingira kwa kujenga utaratibu wa kusafisha mazingira ya jiji ili kulinda heshima ya jiji huku akisisitiza kuwa dini zote zinamtaka mwanadamu awe mwadilifu na mwenye kuzingatia usafi.
 
Amezitaka mamlaka zinazosimamia utekelezaji wa sheria za kuhifadhi mazingira jijini Dar es salaam kufanya kazi kwa kuzingatia weledi ili kuhakikisha maeneo yote ya jiji yanaendelea kuwa katika hali ya usafi.
Naye Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhadi Mussa Salum akuzungumza wakati wa Futari hiyo ameeleza kuwa viongozi wa dini na serikali kote nchini wanalo jukumu kubwa la kuwaongoza wananchi kutenda mema na kuendelea kuvumilia.

"MWANDISHI WA HABARI WA REDIO YA MHESHIMIWA RAGE MBARONI KWA KUJIFANYA USALAMA WA TAIFA,UONGOZI WA V.O.T WAMKANA

Kijana mwandishi wa habari  akiwa mbaroni baada ya kukamatwa na makachero wa Jeshi la Polisi Tabora mjini akijifanya ni Afisa usalama wa Taifa,Mwandishi huyu ambaye anafahamika kwa jina la Mussa Mbeko(24)aliwahi kufanya kazi katika kituo cha Redio Voice of Tabora kinachomilikiwa na Mheshimiwa mbunge wa Jimbo la Tabora mjini Bw.Ismail Rage ambapo hata hivyo Uongozi wa VOT umesema kuwa tayari ulikwisha mfukuza kijana huyo kwa makosa mbalimbali ya Utapeli hasa kujifanya usalama wa taifa.  
Kitambulisho alichokuwa akikitumia Mussa kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu

Uongozi wa Jeshi la Polisi wilaya ya Tabora ulimfikisha  Mwandishi huyo mbele ya Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP  Suzan Kaganda
Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Suzan Kaganda akiwaonesha waandishi wa habari kitambulisho kilichokuwa kikitumiwa na Mussa Mbeko akijifanya ni Afisa Usalama wa Taifa.


TRA YAFUTURISHA BAADHI YA WANANCHI TABORA

Baadhi ya waalikwa akiwemo Meneja wa kanda wa Bima ya Afya mkoa wa Tabora Bw.Emmanuel Adina wakishiriki hafla ya Futari iliyoandaliwa na Mamlaka ya mapato Tanzania TRA katika hotel ya ORION Tabora mjini.
Baadhi ya viongozi wa Serikali na vyama vya siasa akiwemo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake UWT mkoa wa Tabora Bi.Mwanne Mchemba walishiriki katika hafla hiyo ya Futari
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Tabora mjini Bw.Moshi Abraham maarufu Nkokota naye alikuwa ni mmoja kati ya wageni waalikwa
Baadhi ya walipa kodi ambao ni wamiliki wa makampuni ya mabasi Tabora kushoto ni  Bw.Medd Nassor Hamdani,mmiliki wa mabasi ya NBS na Bw.Humud Nassor ambaye ni mmiliki wa mabasi ya SUPER SONIC nao walikuwa ni miongoni mwa wageni waalikwa 

Baadhi ya walipa kodi wafanyabishara wa Tabora
Baadhi ya watumishi wa TRA Tabora nao walishiriki hafla hiyo ya Futari
Mkurugenzi wa Fedha  wa TRA Tanzania Bw.Salehe Mshoro akizungumza katika hafla hiyo ya Futari ambapo alizungumzia mafanikio makubwa ya ukusanyaji wa kodi ya mapato nchini huku akitumia fursa hiyo kuwashukuru wafanyabishara kwa ushirikiano wanaoitapatia TRA
Katibu wa ccm mkoa wa Tabora Bw.Idd Ali Ame akizungumza katika hafla hiyo ya Futari
Mmoja kati ya viongozi wa dini ya kiislam Tabora mjini Sheikh Issa Bilali akisoma dua maalum wakati wa hafla hiyo.
Mjumbe wa NEC Bw.John Mchele akipeana mkono na Mkurugenzi wa fedha wa TRA nchini Bw.Mshoro,pembeni ni Meya wa halmashauri ya manispaa ya Tabora Bw.Ghulam Dewij