Pages

KAPIPI TV

Wednesday, July 23, 2014

"MWANDISHI WA HABARI WA REDIO YA MHESHIMIWA RAGE MBARONI KWA KUJIFANYA USALAMA WA TAIFA,UONGOZI WA V.O.T WAMKANA

Kijana mwandishi wa habari  akiwa mbaroni baada ya kukamatwa na makachero wa Jeshi la Polisi Tabora mjini akijifanya ni Afisa usalama wa Taifa,Mwandishi huyu ambaye anafahamika kwa jina la Mussa Mbeko(24)aliwahi kufanya kazi katika kituo cha Redio Voice of Tabora kinachomilikiwa na Mheshimiwa mbunge wa Jimbo la Tabora mjini Bw.Ismail Rage ambapo hata hivyo Uongozi wa VOT umesema kuwa tayari ulikwisha mfukuza kijana huyo kwa makosa mbalimbali ya Utapeli hasa kujifanya usalama wa taifa.  
Kitambulisho alichokuwa akikitumia Mussa kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu

Uongozi wa Jeshi la Polisi wilaya ya Tabora ulimfikisha  Mwandishi huyo mbele ya Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP  Suzan Kaganda
Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Suzan Kaganda akiwaonesha waandishi wa habari kitambulisho kilichokuwa kikitumiwa na Mussa Mbeko akijifanya ni Afisa Usalama wa Taifa.


No comments: