Pages

KAPIPI TV

Tuesday, May 7, 2013

MUUJIZA TENA NYUMBANI KWA SHEIKH SHARIFF - DAR-ES-SALAAM

Kipande cha nyama ya ng'ombe iliyoandikwa kwa lugha ya kiarabu ikimaanisha jina la Mwenyezi Mungu ''ALLAH''..ni tukio ambalo limejirudia tena kwa Sheikh Shariff Mikidadi ambapo kwa mara ya kwanza tukio kama hilo la kuwepo kwa nyama ya aina hiyo lilitokea nyumbani kwao Sheikh Shariff huko mkoani Tabora katika kata ya Kiloleni na hivi sasa tena limejitokeza nyumbani kwake Sheikh Shariff huko Magomeni jijini Dar-es-Salaam
Sheikh Sharifff Mikidadi akiwa ameshika nyama hiyo akimuonesha mwandishi wetu huko nyumbani kwake Magomeni jijini Dar-es-Salaam.


 Na  Mwandishi wetu maalum.

Siku chache baada ya  tukio la kugundulika kwa nyama ya ng'ombe iliyoandikwa kwa  maandishi  ya lugha ya kiarabu  jina  la  Mwenyezimungu  yaani  ALLAH  huko nyumbani kwao Sheikh Shariff Mikidadi eneo la kata  ya  Kiloleni Tabora  mjini, tukio la aina hiyo limejitokeza tena huko nyumbani kwake eneo la Magomeni jijini Dar-es-Salaam na kusababisha mshangao mkubwa kwa watu walioshuhudia.

Kutokea kwa kipande hicho  cha nyama ambacho kilitokana na nyama  ambayo ilikwenda kununuliwa  kwenye moja ya  maduka ya nyama  eneo  la  Magomeni  kwa  ajili  ya  kitoweo nyumbani  kwa  Sheikh  Shariff,,maswali  mengi yameendelea  kujitokeza na  kukosa  majibu  hata  kufikia  hatua  kwa  wengine  kumwachia  Mungu.

Maelezo  ya awali  yaliyotolewa  na mmoja  wa  kaka  wa  Sheikh Shariff  anayefahamika  kwa jina  la  Abdillah  Mikidadi  alithibitisha   kuwa  mara  baada  ya  nyama  hiyo  kufikishwa  nyumbani  kwa  Sheikh Shariff  taratibu  za  mapishi  ziliendelea  na  baada  ya  kuiva  kipande kimoja  kilionekana  kikiwa  kimeandikwa  maandishi  hayo  ya  kiarabu  kwa  maana  ya  ALLAH.

Alisema  watu  mbalimbali  wakiwemo  baadhi  ya  viongozi  wa  dini  ya  kiislamu  wamefika  nyumbani  kwa  Sheikh Shariff kushuhudia  kipande  cha  nyama  hiyo  na  huku  wengine  wakizidi  kukumbwa  na  mshangao.

MAELEZO  YA  SHEIKH  SHARIFF MWENYEWE.
Alipohojiwa  kuhusu  kuwepo  kwa  tukio  hilo  ambalo pia  limejitokeza  katika  familia yake  tena  kwa  mara  ya  pili  mfululizo,Sheikh Shariff  Mikidadi  ambaye  pia  ni  kijana  mwenye historia  kubwa  kutokana  na  kuzaliwa  kwake  katika  mazingira  ya  miujiza,alisema  kuwepo  kwa  nyama  hiyo  ni  tukio linalodhihirisha  uwepo  wa  Mwenyezimungu  na  kwamba  hakuna  haja  ya  kuleta  fikra  potofu  juu  ya  hilo.

Sheikh Shariff  aliendelea  kusema  kuwa  jambo la  msingi    kwa  waumini  wa  dini  ya  kiislamu ni  kuimarisha  imani  zao  kwa  kufanya  ibada  ipasavyo  na  kumtukuza  Mola  wao  na si  vinginevyo.

''Mimi binafsi  katika  hili  naamini  kuwa  ALLAH anadhihirisha  uwepo  wake  kwetu  sisi  na  kwamba kuna  haja  kwa  waislamu  kushikamana  katika  dini  yao na  kwamwe  tusifarikiane na  kusababisha  madhara  kwetu  sisi  kama  waislamu  pia  hata  na  kwa wenzetu  wa  dini  nyingine  na  hata  wale  wasiokuwa  na  dini''alisema  Sheikh Shariff

Aidha  katika  siku  za  hivi  karibuni  tukio  la kugundulika  kwa  nyama  ya  aina  hiyo  lilijitokeza  nyumbani  kwao  Sheikh  Shariff  huko  kata  ya  Kiloleni  Tabora  mjini  ambapo  tukio  hilo  liliripotiwa  katika  vyombo  mbalimbali  vya  habari na kushangaza  idadi kubwa  ya  watu. 

No comments: