TANGAZA BIASHARA YAKO NA KAPIPIJhabari.COM KWA BEI NAFUU: 0767456259| 0784-456259| Email: jumakapipi@yahoo.com

Pages

Tuesday, May 21, 2013

WANANCHI TABORA WAMUUNGA MKONO ZITTO,AWAUMBUA WABUNGE,WANANCHI WASEMA SASA BASI....!!!

Naibu Katibu mkuu bara  wa  Chadema na mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini akihutubia umati mkubwa wa wananchi katika viwanja vya Stand ya zamani manispaa ya Tabora.


Na Hastin Liumba,Tabora
KITENDO cha naibu katibu mkuu bara wa chama cha demokrasia na maendeleo, (CHADEMA),Zitto Kabwe kutamka hadharani kwenye mkutano wa hadhara kuwa wabunge wa CCM mkoani Tabora ni wasaliti,wanafiki na watoro kwenye majimbo yao, kimepokelewa kwa hisia tofauti na wapiga kura wakiunga mkono kauli hiyo.
Kabwe alitoa kauli hiyo juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika stendi ya mabasi zamani, ikiwa ni sehemu ya ziara yake kuimarisha CHADEMA kanda ya magaharibi yenye mikoa ya Tabora,Katavi na Kigoma.
Aidha mbunge huyo alisema wabunge hao wamekuwa wakiwasaliti wapiga kura hasa kwenye miradi ya maendeleo kwani hivi karibuni walijpanga kukwamisha bajeti ya wizara ya ujenzi inayoongozwa na Dk. John Magufuli,lakini waliitwa na waziri mkuu Mizengo Pinda na kukalipiwa kutofanya hivyo.
Wabunge wa majimbo ya mkoa wa Tabora,ni Ismail Rage (Tabora mjini),Shaffin Sumar (Tabora Kaskazini), Samweli Sitta (Urambo),Profesa Juma Kapuya (Kaliua),Dk Athuman Mfutakamba (Igalula),Suleiman Zedi (Bukene),Dk Hamis Kigwangalah (Nzega),Said Nkumba (Sikonge),na Dk Dalali Kafumu (Igunga), ambaye amerejeshewa ubunge wake na mahakama kuu kanda ya Tabora.
Aidha wabunge wa viti maalumu CCM Tabora kwa tiketi ya CCM ni Munde Tambwe na Magreth Sitta.
Alisema alifikia mahali akawa anawashangaa wabunge hao wa CCM kila aliyesimama aliunga mkono hoja kwa asilimia 100.
Kutokana na kauli ya Zitto kudai ni wasaliti na watoro majimboni mwao hata wale wa viti maalumu,baadhi ya wananchi baada ya mkutano huo wa hadhara walionekana kwenye vikundi sehemu mbalimbali ikiwemo sehemu za starehe kama baa,vijiweni  wakijadili na kukubaliana na kauli ya Zitto.
“Jamani kauli ya Zitto ni ya kweli hebu angalieni wabunge karibu wote utawaona wanakuja mara chache sana majimboni na wanaweza kuja na wasifanye mikutano yoyote na wananchi.”alisema kijana mmoja ambaye anayefahamika kwa jina  la  Haruna.
Walisema wanaungana na kauli hiyo ya utoro kwani hata kwenye vikao vya DCC na RCC ni nadra sana wabunge hao kuhudhuria mara kadhaa ukisoma kwenye muhtasari utaona labda ni mbunge mmoja tu alikuwepo wengine wote ni udhuru kwa kwenda mbele.
Kiongozi mmoja wa chama siasa cha NRA Nkumila, alisema yeye vikao vya kamati za ushauri za wilaya na mkoa yaani DCC na RCC mjumbe halali lakini wabunge wengi hawahudhurii kabisa sasa mkoa utapataje maendeleo ikiwa yale yanayojadiliwa hawayasikii ili wakasaidie kwenye kikao kama cha bunge.
Aidha wakazi hao walionekana kukunwa na kauli ya Zitto wakisema alichosema kina ukweli na kwamba baadhi ya miradi ikikamilika kwa  haraka itakuwa nguvu ya CHADEMA kwani wabunge wa CCM wanazibwa midomo wasipige kelele kwa kigezo wa kuibomoa serikali yao.
Hali hiyo waliendelea kujadiliana hata katika maeneo  kadhaa mjini hapa wakidai wamechoshwa na wabunge wa kuja hata wale waliojifanya wamezaliwa Tabora siku hizi wamehamia jijini Dar-es-Slaam kwenye shughuli zao binafsi.
Walisema wanatafakari kwa umakini mkubwa maneno ya Zitto kuwa Tabora CCM imepafanya ni sehemu ya kuchota kura na kamwe wataendelea kubaki kama walivyo kwenye kisiwa na hawajui lini wataokolewa labda pale watakapofanya maamuzi magumu ya kuitosa CCM 2015.
Wakati wananchi wakijadiliana hayo na wengine kuongea na waandishi wa habari tayari mwenyekiti wa CCM taifa,Dk Jakaya Mrisho kikwete kwenye kikao cha wabunge wa CCM amekemea tabia ya wabunge watoro wasiotembelea majimbo yao.
Katika kikao hicho kilichofanyika mjini Dodoma, rais alisema kuwa baadhi ya wabunge wameyatelekeza kwa kutorudi kusikiliza kero za wananchi na kutimiza ahadi zao.
Aliwaonya kuwa kwa tabia hiyo wala wasije kuwaonea donge wale wanachama wengine watakaochaguliwa kuwa wabunge badala yao.

Monday, May 20, 2013

ZITTO KABWE-"MAGUFULI TUMECHOKA NA MAMBO YA TAKWIMU TUNAHITAJI BARABARA TABORA"

Naibu katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema  Bw.Zitto Kabwe akizungumza na umati mkubwa wa baadhi ya wakazi wa Tabora mjini katika mkutano wa hadhara.
Baadhi ya wakazi wa Tabora mjini ambao ni wakereketwa wa Chadema wakifurahia hotuba ya Bw.Zitto Kabwe,ambapo wananchi hao walionesha kuvutiwa sana na hotuba ya Zitto ambayo walidai ilijawa na wimbi la ukweli mtupu na kugusa maisha yao ya kila siku.
Wananchi baada ya kuguswa sana na hotuba ya Zitto Kabwe wengine walilazimika kujaribu kutumia Simu zao za mkononi kujiwekea kumbukumbu ya hotuba hiyo kwa kurekodi angalau sauti na Picha.
Mmoja kati ya Maafisa wa Chadema akimwandikia kadi mama mmoja ambaye alihitaji kujiunga na Chadema baada ya hotuba ya Bw.Zitto Kabwe
Umati wa watu Tabora mjini katika viwanja vya Stand ya Zamani






Saturday, May 18, 2013

TAMASHA LA MTEMI MILAMBO TABORA

Tamasha la Mtemi Milambo lililofanyika Tabora mjini,Huyu ni mmoja kati ya wasanii waliokuwa kivutio kikubwa katika Tamasha hilo ambalo hufanyika kila mwaka likiwa na lengo la kuenzi tamaduni na mila za mkoa wa Tabora kwa kupitia kumbukumbu mbalimbali zikiwemo za Mtemi Milambo ambaye alikuwa ni kiongozi wa kabila ya Wanyamwezi,msanii huyu mwenye kipaji cha kuchezea Nyoka hapa alikuwa akimeza kichwa cha Nyoka mwenye urefu kwa mita 3.


Sunday, May 12, 2013

WAANDISHI WA HABARI WAPO HATARINI - TUNDU LISSU


lisu1 fda6e
Mh Tundulisu akitoa Vyeti kwa wana chaso katika Haflahio,

WAANDISHI wa habari wapo katika hatari kubwa ya kutoweka nchini kutokana na kuandika maovu yanayofanywa na viongozi wa serikali.
Haya yamezungumzwa na Mbunge wa Singida Mashariki na mnadhimu Mkuu wa kambi ya upinzani Tundu Lissu katika mahafali ya shirikisho la wanafunzi wa vyuo vikuu Mkoa wa Iringa (CHASO) katika ukumbi wa Chuo Kikuu Huria kilichopo katika Manispaa ya Iringa.
Lissu alisema waandishi wa habari wapo katika hatari ya kutoweka hasa kwa kuuawa kutokana na ukweli wao wanaouandika hasa kuyaweka madudu ya baadhi ya viongozi wa serikali.
Alisema hasa katika ripoti ya uchunguzi ya mauaji ya mwandishi wa habari Daudi Mwangosi ya tume iliyoundwa na vilabu vya waandishi wa habari Tanzania (UTPC) inaonesha wazi juu ya hatari walionayo waandishi wa habari.

Alitaja chanzo cha kuwamaliza waandishi hao kuwa ni polisi wanaotumiwa na viongozi hao kama njia ya kuzuia kuendelea kuandika madudu yao.
Hata hivyo alisema waajiri wa waandishi ni chanzo moja wapo cha kinachochangia waandishi kuwa katika hatari hiyo kwa kuwatengenezea mazingira mabovu ya utendaji wao hasa wawapo kazini.
Lissu alisema waandishi wa habari ambao wapo katika hatari kubwa ni wa Iringa ambao tayari wapo katika listi ya kupotezwa kwa namna yoyote kwa kile kilichoelezwa kuwa hawaandiki habari zao kwa unafiki.
"Tuwalinde sana waandishi wa habari kwa kweli wapo katika hatali kubwa sana. Kila mmoja awe mlinzi wa waandishi hawa na ifike mahali tukasema hatutaki Mwangosi mwingine. Hasa waandishi hawa wa Iringa wapo katika wakati mgumu sana" alisema.
Pia aliwaasa wanafunzi waliomaliza kwenda kuungana na wananchi kuendeleza harakati za Mageuzi kuanzia katika Mashina,kata, na Majimbo ili kufanikisha mpango wa kuelekea ikulu vinginevyo ni ndoto hapondipo utatokea ukombozi wa Waalimu, Madaktari, na Wanasheria
Wasio na kazi kwasababu ya Mipango mibovu ya utawala uliopo kupata furusa ya kuitumikia nchihii kukiandaliwa mipango mizuri ya ajira,
Historia inaonyesha hakuna Mzee aliefanikisha mapinduzi ya kisiasa katika nchiyake kama hakuanza wakati akiwa kijana na kuelekea katika Mafanikio ndipo uzee unamkuta akiwemo ndani ya Harakati,

WAFANYAKAZI WA MRADI WA MILENIA MBOLA WAFANYA SHEREHE

 Kiongozi wa mradi wa vijiji vya Milenia Mbola Dr.Gerson Nyadzi akizungumza katika hafla fupi ya jioni ya wafanyakazi wa Mbola Mvp ilyofanyika katika ukumbi wa Polisi mjini Tabora.
 Hapa ni wakati ulipowadia kwa wafanyakazi hao kulisakata Rumba kwa kila mmoja kwa Staili yake na akionesha ufundi juu ya hilo.
 Ilikuwa vigumu kuvumilia kwa Kiongozi wa Mradi Dr.Gerson Nyadzi kuwaachia Staff peke yao kunyoosha viungo vyao akaamua kuwasindikiza kwa kucheza Kiduku kama inavyoonekana hapa ambapo ukumbi ukachangamka.
 Ikafikia hatua hata ya viatu kuwa vizito na uchangamfu ukakolea bila kujali muda wa kukamilisha hafla hiyo ya jioni.
 Wakati wa maakuli ulipewa kipaumbele cha kwanza kabla ya mambo mengine ili kusawazisha mambo.



Thursday, May 9, 2013

"DR.KAFUMU NI MBUNGE HALALI WA JIMBO LA IGUNGA"-MAHAKAMA YA RUFAA

Dr.Dalali Peter Kafumu mbunge halali wa jimbo la Igunga - Mahakama ya Rufaa kanda ya Tabora.
Aliyekuwa mgombea wa nafasi ya Ubunge kwa tiketi ya Chadema  Mwalimu Joseph Kashindye mstari wa pili kutoka kulia ni mtu wa pili aliyevaa sare ya Chadema akizungumza jambo na mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Tabora muda mfupi kabla ya kutolewa kwa maamuzi ya Mahakama ya Rufaa dhidi ya kesi ya kutenguliwa Ubunge Dr.Dalali Kafumu.
Baadhi ya viongozi wa Chadema na CCM ngazi za wilaya wakiwa mahakamani kushuhudia kesi ya rufaa ya kutenguliwa kwa matokeo ya Ubunge wa Jimbo la Igunga Dr.Kafumu

Viongozi wa Chadema wakitoka nje ya mahakama  baada ya Dr.Kafumu kurejeshewa Ubunge wa Jimbo la Igunga.





Tuesday, May 7, 2013

MUUJIZA TENA NYUMBANI KWA SHEIKH SHARIFF - DAR-ES-SALAAM

Kipande cha nyama ya ng'ombe iliyoandikwa kwa lugha ya kiarabu ikimaanisha jina la Mwenyezi Mungu ''ALLAH''..ni tukio ambalo limejirudia tena kwa Sheikh Shariff Mikidadi ambapo kwa mara ya kwanza tukio kama hilo la kuwepo kwa nyama ya aina hiyo lilitokea nyumbani kwao Sheikh Shariff huko mkoani Tabora katika kata ya Kiloleni na hivi sasa tena limejitokeza nyumbani kwake Sheikh Shariff huko Magomeni jijini Dar-es-Salaam
Sheikh Sharifff Mikidadi akiwa ameshika nyama hiyo akimuonesha mwandishi wetu huko nyumbani kwake Magomeni jijini Dar-es-Salaam.


 Na  Mwandishi wetu maalum.

Siku chache baada ya  tukio la kugundulika kwa nyama ya ng'ombe iliyoandikwa kwa  maandishi  ya lugha ya kiarabu  jina  la  Mwenyezimungu  yaani  ALLAH  huko nyumbani kwao Sheikh Shariff Mikidadi eneo la kata  ya  Kiloleni Tabora  mjini, tukio la aina hiyo limejitokeza tena huko nyumbani kwake eneo la Magomeni jijini Dar-es-Salaam na kusababisha mshangao mkubwa kwa watu walioshuhudia.

Kutokea kwa kipande hicho  cha nyama ambacho kilitokana na nyama  ambayo ilikwenda kununuliwa  kwenye moja ya  maduka ya nyama  eneo  la  Magomeni  kwa  ajili  ya  kitoweo nyumbani  kwa  Sheikh  Shariff,,maswali  mengi yameendelea  kujitokeza na  kukosa  majibu  hata  kufikia  hatua  kwa  wengine  kumwachia  Mungu.

Maelezo  ya awali  yaliyotolewa  na mmoja  wa  kaka  wa  Sheikh Shariff  anayefahamika  kwa jina  la  Abdillah  Mikidadi  alithibitisha   kuwa  mara  baada  ya  nyama  hiyo  kufikishwa  nyumbani  kwa  Sheikh Shariff  taratibu  za  mapishi  ziliendelea  na  baada  ya  kuiva  kipande kimoja  kilionekana  kikiwa  kimeandikwa  maandishi  hayo  ya  kiarabu  kwa  maana  ya  ALLAH.

Alisema  watu  mbalimbali  wakiwemo  baadhi  ya  viongozi  wa  dini  ya  kiislamu  wamefika  nyumbani  kwa  Sheikh Shariff kushuhudia  kipande  cha  nyama  hiyo  na  huku  wengine  wakizidi  kukumbwa  na  mshangao.

MAELEZO  YA  SHEIKH  SHARIFF MWENYEWE.
Alipohojiwa  kuhusu  kuwepo  kwa  tukio  hilo  ambalo pia  limejitokeza  katika  familia yake  tena  kwa  mara  ya  pili  mfululizo,Sheikh Shariff  Mikidadi  ambaye  pia  ni  kijana  mwenye historia  kubwa  kutokana  na  kuzaliwa  kwake  katika  mazingira  ya  miujiza,alisema  kuwepo  kwa  nyama  hiyo  ni  tukio linalodhihirisha  uwepo  wa  Mwenyezimungu  na  kwamba  hakuna  haja  ya  kuleta  fikra  potofu  juu  ya  hilo.

Sheikh Shariff  aliendelea  kusema  kuwa  jambo la  msingi    kwa  waumini  wa  dini  ya  kiislamu ni  kuimarisha  imani  zao  kwa  kufanya  ibada  ipasavyo  na  kumtukuza  Mola  wao  na si  vinginevyo.

''Mimi binafsi  katika  hili  naamini  kuwa  ALLAH anadhihirisha  uwepo  wake  kwetu  sisi  na  kwamba kuna  haja  kwa  waislamu  kushikamana  katika  dini  yao na  kwamwe  tusifarikiane na  kusababisha  madhara  kwetu  sisi  kama  waislamu  pia  hata  na  kwa wenzetu  wa  dini  nyingine  na  hata  wale  wasiokuwa  na  dini''alisema  Sheikh Shariff

Aidha  katika  siku  za  hivi  karibuni  tukio  la kugundulika  kwa  nyama  ya  aina  hiyo  lilijitokeza  nyumbani  kwao  Sheikh  Shariff  huko  kata  ya  Kiloleni  Tabora  mjini  ambapo  tukio  hilo  liliripotiwa  katika  vyombo  mbalimbali  vya  habari na kushangaza  idadi kubwa  ya  watu. 

LHRC YATOA MAFUNZO KWA WAANDISHI WA HABARI WA MIKOANI KUHUSU HAKI ZA BINADAMU KWA UFADHILI WA EU -DAR ES SALAAM


Balozi wa nchi za Ulaya(EU)nchini Tanzania Filberto Sebregond(kulia )akizungumza kwenye ufunguzi wa semina ya waandishi wa habari kutoka mikoa mbalimbali nchi inayohusu masuala ya haki za binadamu,Kwenye ukumbi wa  Wanyama Hotesl Jijini Dar Es Salaam.

Picha ya pamoja Kati ya Balozi wa nchi za Ulaya(EU)nchini Tanzania Filberto Sebregond na washiriki na waandaji wa wa mafunzo ya haki za binadamu

Rose Mwalongo ambaye ni afisa habari wa kituo cha sheria na haki za binadamu(LHRC)akisalimiana na Balozi wa nchi za Ulaya(EU)nchini Tanzania Filberto Sebregond


waandishi wakimfanyia mahojiano Balozi wa nchi za Ulaya(EU)nchini Tanzania Filberto Sebregond

KISIMA CHAENDELEA KUUA WATU,WANANCHI WAKUMBWA NA HOFU KUBWA KILOLENI-TABORA MJINI

Askari wa kikosi cha zimamoto mjini Tabora wakiutoa mwili wa mwanamke ambaye amekutwa amekufa katika kisima cha maji maarufu Bombamzinga kilichopo kata ya Kiloleni Tabora mjini,Mwanamke huyo ametambulika kwa jina la Hawa Ramadhani Mzee ambaye alikuwa na umri wa miaka 42 ambaye pia inasemekana alikuwa na matatizo ya akili.
Diwani wa kata ya Kiloleni Bw.Juma Matalu (katikati)akishuhudia tukio la kifo cha mwanamke huyo katika kisima ambacho kimekuwa kikihusishwa na matukio ya mauaji ya watu kadhaa kwasasa hali inayotishia amani kwa wakazi wa kata ya Kiloleni.
Baadhi ya Askari wa Jwtz,Polisi na wa kikosi cha zimamoto Tabora mjini waliposhirikiana kuutoa mwili wa mwanamke huyo.












Saturday, May 4, 2013

"SUALA LA KUTOA SIRI ZA SERIKALI LIMENIKERA SANA" - WAZIRI KOMBANI

Waziri Cerina Kombani awataka wahitimu wa Chuo cha utumishi wa Umma nchini kutotoa siri za Serikali kwani kufanya hivyo ni utovu wa nidhani kazini.

MAHAFALI YA CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA TPSC YANAFANYIKA TABORA HIVI SASA.

 Mahafali ya 14 ya chuo cha utumishi wa umma TPSC yanafanyika hivi sasa mkoani Tabora.

Wednesday, May 1, 2013

RAIS DKT. JAKAYA KIKWETE AONGOZA SHEREHE ZA MEI MOSI MBEYA

8E9U2311Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akishirikiana na viongozi wengine kuimba wimbo wa Solidarity Forever wakati wa maadhimisho ya Sikuukuu ya Wafanyakazi duniani iliyofanyika kitaifa mkoani Mbeya.Wengine katika picha kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa TUCTA Nicolaus Mgaya, Mke wa Rais Mama Salma Kikwete,Waziri wa Kazi na ajira Mhe.Gaudensia Kabaka, Kaimu Rais wa TUCTA Bibi Nortubunga Maskini, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro na kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Mh.Abdulrahman Kinana.
8E9U2015Baadhi ya wafanyakazi wakishiriki katika maandamano  yaliyofanyika wakati wa maadhimisho ya Mei Mosi  katika Uwanja wa michezo  wa Sokoine mjini Mbeya(picha na Freddy Maro)

Tuesday, April 30, 2013

ETI HUYU MTOTO ANAWEZA KUWA NI WA MKOA GANI NA KABILA LIPI?

Jamaa wanauliza...."Eti huyu mtoto anaweza kuwa ni wa kutoka mkoa gani jamani na ni kabila gani?"

AJALI KAZINI ?