Pages

KAPIPI TV

Wednesday, November 19, 2014

BIASHARA YA VITENGE KIGOMA YAVURUGWA NA VITENGE FEKI ZA WACHINA KIGOMA

Na Magreth Magosso,Kigoma

INADAIWA kuwa,Wachina wamechangia kufubaza Biashara ya vitenge Mkoa wa kigoma na kupelekea kushuka kwa makusanyo ya kodi za Forodha na hivyo Mamlaka ya Mapato Tawi la Kigoma kushindwa kufikia lengo  la kukusanya kiasi cha milioni 643,300,000 kwa kipindi cha Julai-Septemba 2014.

Akifafanua hilo  mbele ya  wandishi wa habari  jana katika ofisi ya mamlaka hiyo Kaimu Meneja wa tawi  Patrice Mushi  alisema serikali  idhibiti uingizaji holela wa bidhaa kutoka nje ya nchi  ambapo, makampuni ya kichina hutumia sera ya biashara huria hufoji bidhaa mbalimbali na hivyo kupunguza kasi ya walaji kutumia bandari ya  kigoma kuchukua vitenge kutoka nchi za magharibi .

“wachina wameua soko la vitenge ,makusanyo halisi  ya forordha ni milioni 1,062,806,736 bidhaa hii ndio chachu ,bidhaa ya mafuta si tija kwetu haitabiriki sasa vitenge vya  wax   feki za wachina wadau wanatumia bandari ya Dar-es-salaam  na wanauza  hapo serikali isimamie kanuni,tratibu tunakwama “alibainisha Mushi.

Pia alisema TRA kigoma imejiwekea mkakati wa kuimarisha ukusanyaji wa kodi kupitia mfumo wa kisasa(EFD),vitalu(Block management system) sanjari na kuendelea kuhamasisha wananchi wadai risiti wakati wanaponunua bidhaa madukani,ili kuzuia ukwepaji wa kulipa kodi kwa walengwa.

Aidha alisema wafanyabiashara wenye mtaji wa kuanzia milioni 14 wanahitajika kutumia mfumo wa kisasa wa( EFD) na kuahidi kufuatilia wasiotumia ipasavyo mashine hizo na adhabu kwa walaji wasiodai risiti za bidhaa walizonunua kwa mujibu wa sheria ya mwaka 2000 na kuzuia bidhaa haramu kwa walaji.

Hivyo makusanyo ya kodi kwa mwaka 2013/14 wamekusanya kodi za forodha kiasi cha  sh.bilioni 2.9 ambapo lengo ilikuwa wakusanye bilioni 3.2 sawa na 91% ya ufanisi,huku kodi za ndani wamefanikiwa kukusanya sh.bilioni 6.2 ambapo lengo likiuwa kiasi cha sh.7.179,400,000 sawa na 87%.

Kwa upande  wauza  vitenge soko la kigoma mjini na mwanga Ally Kisala na Tatu Amani kwa nyakati tofauti wakiri hali tete katika uzaji wa vitenge kutoka nchi ya DRC-kongo ,kutokana na bidhaa hiyo kushikwa na wachina ambao hutumia bandari ya  Dar-es-salaam kwa bei rahisi .

Awali walikuwa wakiuza vitenge pande tatu 500 kwa mwezi ,ambapo hivi sasa wanauza  pande tatu  20 kwa mwezi,hali inayowalazimu washindwe kuagiza kwa wingi bidhaa hiyo kutoka nchini Congo ,ambapo wax  kupitia kongo  huuzwa sh.27,000  cha Dar-es-salaam  sh.19,000.

Walisema ugumu wa maisha unachangia walaji wengi kuvamia vitenge kutoka  china ambavyo  vina bei rahisi ilihali havina viwango vya ubora  na kushauri walaji wathamini ubora wa bidhaa ili kuepukana na bidhaa rahisi ambavyo ni gharama kwa badae (uimara mdogo).

No comments: