Pages

KAPIPI TV

Thursday, July 24, 2014

"AJIRA YA VIJANA KWA USAFIRI WA BAISKELI TABORA NI MOJA KATI YA AJIRA TULIZOZITEGEMEA"

Usafiri baiskeli mkoani Tabora wazidi kuimarisha ajira kwa vijana hatua ambayo sasa imefanya kuwepo kwa ongezeko la vijana wengi mjini kuliko ilivyokuwa hapo awali,kwa hivi sasa imeshuhudiwa baadhi ya vijana wa vijiji jirani na Tabora mjini wamekuwa wakijidamka mapema asubuhi kuja mjini kufanya kazi ya kusafirisha abiria kwa usafiri huo wa baiskeli na kujipatia fedha kwa ajili ya kujikimu kimaisha wakati huu wa majira ya kiangazi ambapo vijijini hakuna shughuli za kilimo.Hata hivyo licha ya vijana hao kupata fursa ya kujiajiri wenyewe lakini wamekuwa katika mazingira hatarishi kutokana na ukweli kwamba wengi wao hawajui sheria za usalama barabarani na hivyo kujikuta wanavunja sheria na kusababisha ajali zinazochangia vifo visivyo vya lazima au kubaki na ulemavu wa kudumu.Jambo hili linahitaji kuchukuliwa hatua ya kuwadhibiti vijana hao bila kuathiri mwenendo mzima wa ajira zao kwakuwa wengi wao kutokana na ajira hizo wanategemewa na familia zao.Ajira za vijana kwa kutumia usafiri wa baiskeli katika mtazamo wa harakaharaka ni dhahiri kwamba ni ajira tulizozitegemea kwa kile kinachoonekana katika fikra za haraka kwa vijana waliowengi ni kujipatia fedha za chapchap kupitia mpango huo usio rasmi.Aidha kwa upande mwingine ni kweli kwamba kwasasa mkoa wa Tabora hakuna viwanda au kazi nyingine zaidi ya kupata vibarua kwenye majengo ya watu binafsi ambayo malipo yake ni kati ya shilingi 3000 na 5000 kwa kutwa nzima.Ukiachilia mbali ajira kwenye makampuni ya ulinzi imekuwa na usumbufu kwa vijana kutokana na kutolipwa mishahara kwa wakati jambo ambalo linawafanya vijana wengi kuona ni bora zaidi aendeshe baiskeli kuanzia majira ya saa 12 asubuhi hadi saa tatu usiku ambapo hujipatia wastani wa kiasi cha shilingi elfu kumi.Hii inawafanya idadi kubwa vijana kuingia kwenye ajira hii bila kikwazo kwani kwa wanaoishi mjini huweza kumudu kulipa kodi ya pango ya shilingi elfu kumi kwa mwezi lakini hata kuendesha maisha yake na familia ya watu wanne yaani Mke,watoto wawili na yeye mwenyewe.Kuendesha baiskeli hakuhitaji leseni wala kikwazo chochote kinachowabana kisheria zaidi ya kujaza upepo kwenye tairi za baiskeli na kuanza kunyonga pedeli kulingana na uzito wa mteja aliobebwa kwenye usafiri huo.Ni kazi nyepesi kama waionavyo vijana wenyewe.Lakini kwa wachunguzi wa mambo wanasema kuwa hata wimbi la vibaka katika maeneo mbalimbali Tabora mjini limepungua kwa kiasi kikubwa kwakuwa kijana anayejihusisha na ajira hiyo ya usafiri wa baiskeli anapomaliza muda wake hiyo saa tatu usiku huwa amechoka sana hata hawezi kwenda kukaa  vijiweni na kujihusisha na vitendo viovu. 

No comments: