Pages

KAPIPI TV

Wednesday, July 23, 2014

POLISI APONGEZWA BAADA YA KUKATAA RUSHWA YA WATUMIAJI WA DAWA ZA KULEVYA-TABORA

Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Suzan Kaganda akimpongeza na kumpa zawadi ya pesa Mkaguzi wa Polisi Harun Kasubi baada ya kufanikiwa kuwakamata watu wapatao kumi na wawili waliokuwa wamejifungia ndani ya Guest house inayofahamika kwa jina la KENIOS wakiwa wanajidunga dawa za kulevya ambapo watu hao walitaka kumpa rushwa ya shilingi 90,000/=ili waachiwe huru.
Baadhi ya dawa za kulevya na vifaa vya matumizi ya dawa hizo zilizokamatwa zikiwa zinatumiwa na watu hao kumi na wawili waliokamatwa KENIOS GUEST HOUSE huko eneo la kata ya Isevya manispaa ya Tabora.
Kamanda wa Polisi ACP Suzan Kaganda ameuambia mtandao huu kuwa waliokamatwa katika operesheni ya kuwasaka watumiaji,wauzaji na wasambazaji wa dawa za kulevya mkoani Tabora ni Hamisi Athuman Mbao(39) ,Issa Abdallah(22),Ally Bakar(34),Densi Petro(34)Mrisho Shaban(22)Ramadhan Mbade(40)Haji Muki(40),Said Kasumari(24),Shaban Haruna(25)David Male(43)Ramadhan Hamis na Paschal Robert.

Kamanda Suzy amesema watu hao baada ya kukamatwa walitaka kutoa rushwa ya shilingi elfu tisini kwa kiongozi wa timu ya makachero wanaofuatilia dawa za kulevya mkoani Tabora ambaye ni mkaguzi wa Polisi Harun Kasubi ambapo alikataa na kuwafikisha kituo kikubwa cha Polisi Tabora.

 

No comments: