Pages

KAPIPI TV

Saturday, September 13, 2014

KITUMBO ASHANGAZWA NA VIPAJI VYA SOKA KWA VIJANA VIJIJINI - TABORA

Mwenyekiti  wa Chama cha Soka mkoani Tabora  Yusuph Kitumbo akitoa zawadi ya kombe kwa mshindi wa kwanza katika mashindano ya kuibua vipaji vya Soka kwa vijana  katika kata ya Ikomwa ambapo Kitumbo mbali na kuwa mgeni rasmi katika mashindano hayo alielezea kuridhishwa kwake na vipaji vya vijana waliopo vijijini katika mchezo huo wa Soka.
Zawadi ya mpira kwa mshindi wa pili

KINANA AHUTUBIA MAMIA YA WANANCHI KIMANZICHANA

Kinana akihutubia Kimanzichana wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani leo (Picha Bashir Nkoromo)

ANUWAR KASHAGA AZIDI KUIBOMOA CHADEMA IGUNGA!!!

Aliyekuwa mjumbe wa Baraza la Vijana wa Chadema ngazi ya taifa Bw.Anuwar Kashaga akichana kadi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema katika mkutano wa hadhara wilayani Igunga baada ya kujiunga na Chama cha Mapinduzi hivi karibuni,Katika mkutano huo wa hadhara ambao mgeni rasmi alikuwa ni Naibu Katibu mkuu wa CCM Bw.Mwigulu Mchemba,...Kashaga licha ya kuzungumza maovu mengi yanayotendeka ndani ya Chadema alichana hadharani kadi aliyokuwa akiitumia wakati bado mwanachama wa Chadema hatua ambayo ilikuwa gumzo kwa wakazi wa Igunga ambao waliokuwa wakimfahamu Kashaga ambaye alikuwa kada mahili wa Chadema. 

KUANGALIA SOKA VIJIJINI KUNA RAHA ZAKE!!

Baadhi ya wakazi wa vijijini  Manispaa ya Tabora wakionesha mwamko wa kupenda mpira wa soka.

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AWASILI TANGA KWA ZIARA YA SIKU MOJA YA KIKAZI.

PG4A5383 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akisalimiana na wasanii wa kikundi cha wanawake wa cha Tanga  cha Msanja baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Tanga kwa ziara ya siku moja ya kikazi Kulia ni Mkuu wa Mkoa huo Chiku Gwao.PG4A5378Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akisalimiana na wasanii wa kikundi cha wanawake wa cha Tanga  cha Msanja baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Tanga kwa ziara ya siku moja ya kikazi.

NHIF YATETA NA WACHEZAJI, WATENDAJI KLABU YA YANGA

7Katibu Mkuu wa Yanga Bw. Beno Njovu akizindua semina ya Mfuko wa Bima ya Afya na Watendaji na wachezaji wa Klabu ya Yanga  iliyofanyika jana makao makuu ya klabu hiyo mtaa Jangwani katikati ni Mkurugenzi wa Uendeshaji (NHIF),Eugen Mikongoti na kushoto ni Christopher Mapunda Meneja wa NHIF Wilaya ya Ilala klabu ya Yanga imekuwa ya kwanza kuanza utaratibu wa kuijunga na mfuko wa Bima ya afya. 8Mkurugenzi wa Uendeshaji (NHIF),Eugen Mikongoti akizu.ngumza na watendaji wa Yanga na wachezaji wakati wa semina hiyo jana 9Mkurugenzi wa Uendeshaji (NHIF),Eugen Mikongoti akizu.ngumza na watendaji wa Yanga na wachezaji wakati wa semina hiyo jana 10Mmoja wa maofisa wa Mfuko wa Bima ya Afya akiwaonyesha makocha wa Yanga baadhi ya picha alizpoiga  nao Kulia ni kocha wa yanga Marcio Maximo. 11Christopher Mapunda Meneja wa NHIF Wilaya ya Ilala akitoa mada wakati wa semina na wachezaji wa timu ya Yanga jana. 12Baadhi ya wachezaji na maofisa pamoja na wanachama wa Yanga wakiwa katika semina hiyo. 13Baadhi ya wanachama wa Yanga wakiwa katika semina hiyo kushoto ni mwanachama wa Yanga Bw Said Hassan Kipara 14Katibu Mkuu wa Yanga Bw. Beno Njovu akizungumza katikasemina hiyo kulia niHance John Mwankenja Afisa Matekelezo wa NHIF  15Mmoja wa maofisa akigawa majarida yanayoelezea faida za Mfuko wa Bima ya Afya ya jamii katika semina hiyo  17Ofisa   Mawasiliano mwandamizi  NHIF  Bw. Luhende Andrew Singu akizungumza na wachezaji hao jana wakati wa semina hiyo

Friday, September 12, 2014

MBOWE ACHACHAMAA!!


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, ameonya kuwa iwapo kiongozi yeyote wa chama hicho ataruhusu mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa ngazi yoyote ya uongozi katika uchaguzi, kupita bila kupingwa katika eneo lake, atawajibika.

Alitoa onyo hilo alipokuwa akifungua Mkutano Mkuu wa Bavicha, jijini Dar es Salaam jana.
“Misiruhusu uongozi, kuanzia serikali ya mtaa kupita bila kupingwa. Ikitokea hivyo, na wewe kiongozi (wa Chadema) jiandae kuwajibika,” alisema Mbowe.

Aliutaka uongozi mpya wa Bavicha utakaochaguliwa kuendeleza kazi nzuri iliyoachwa na uongozi wa baraza hilo uliopita.

Kazi hizo ni pamoja na namna ya kuwaandaa vijana, wazee na wanawake, kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapigakura na kushiriki chaguzi zote, kuanzia ule wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji, udiwani, ubunge na urais mwakani.

Mbowe, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) alisema muda mwafaka ukifika, watakutana na viongozi wenzake wa vyama vinavyounda umoja huo vya CUF na NCCR-Mageuzi kuangalia namna watakavyofanya kazi pamoja katika chaguzi zijazo.

Alisema kifungu cha 6 (3) na (4) cha katiba ya Chadema kinaelezea ukomo wa uongozi, hivyo akasema wana kazi kubwa ya kupanua wigo wa chama.
 
Kwa kuzingatia hilo, alisema watakuwa na kazi ya kutathmini utendaji wa kila kiongozi katika chama kila baada ya miezi sita kuona namna alivyochangia kukuza na kukiimarisha chama.

“Kiongozi atakayeruhusu katika eneo lake chama kisikue, atawajibika kabla ya miaka mitano,” alisema Mbowe.

Alisema Chadema siyo ya fujo, bali ni chama chenye dhamira ya kweli, hivyo akaonya kuwa iwapo mwanachama wake yeyote anayegombea uongozi kwa kutumia mbinu chafu, ikiwamo rushwa, atang’olewa hata kama atakuwa amekwishakupitishwa katika uchaguzi.

Awali, akimkaribisha Mbowe kufungua mkutano huo, Mwenyekiti wa Bavicha anayemaliza muda wake, John Heche, alisema Chadema imekua na kwamba, kigezo cha hilo ni namna ilivyofanikiwa kufanya kwa mara ya kwanza uchaguzi, kuanzia ngazi za msingi.

Aliushukuru uongozi wa Chadema kwa kuwashughulikia wasaliti ndani ya chama na kusema kamwe vijana hawatavumilia kuona mtu yeyote anakivuruga chama hicho.

Mapema, Katibu Mkuu wa Bavicha anayemaliza muda wake, Deogratius Munishi, alisema wajumbe waliotakiwa kuhudhuria ni 336 na kwamba, hadi kufikia saa 5.40 asubuhi, waliosajiliwa walikuwa 301 sawa na asilimia 89 ya akidi ya wajumbe wote wa mkutano huo.

SEKTA ZA MADINI ,UMEME NA KILIMO ZAKUZA PATO LA TAIFA.

NBS -PATO 1Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Bw. Morrice Oyuke (katikati) akizungumza  na waandishi wa habari kuhusu ukuaji wa Pato la Taifa kwa bei ya Soko leo jijini Dar es salaam. Wengine ni Bw. Oswald Ruboha (kulia) Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Sera na Mipango, Wizara ya Kilimo na Dkt. Stephen Kirama (kushoto), Mhadhiri wa Uchumi, Chuo Kikuu cha Dar es salaam.
 
Na. Aron Msigwa – MAELEZO, Dar es salaam.
Sekta ya Kilimo,Uvuvi,  Viwanda , Nishati na Madini zimeelezwa kuwa miongoni mwa sekta muhimu zinazoongoza zaidi katika kuchangia kukua kwa pato la Taifa hadi asilimia 7.4 katika robo ya kwanza ya mwaka 2014.
 
Kwa mujibu wa taarifa zilizokusanywa kutoka katika vyanzo mbalimbali vya uzalishaji nchini na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kutumia kanuni za kimataifa kukokotoa pato la Taifa zinaonyesha kuwa sekta hizo zimetoa mchango mkubwa wa kukua kwa pato la Taifa  kwa asilimia 7.4 kuanzia mwezi Januari hadi  Machi, 2014 ikilinganishwa na asilimia 7.1 za mwaka 2013.
 
Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Bw. Morrice Oyuke akizungumzia ukuaji wa Pato la Taifa kwa bei ya Soko leo jijini Dar es salaam amesema kuwa Pato la Taifa katika robo ya mwaka 2014 kuanzia Januari hadi Machi limekua kwa asilimia 7.4 kutokana na kukua kwa sekta za Kilimo, Uvuvi, Viwanda, Ujenzi, Umeme na  utoaji wa huduma.
 
Amesema sekta zilizofanya vizuri katika ukuaji huo ni pamoja na sekta ya uchimbaji wa Madini, mawe na kokoto ambayo imekua kwa asilimia 8.7 ikilinganishwa na asilimia 1.7 za mwaka uliopita kutokana na kukua kwa masoko ya uuzaji ya nje ya nchi. 
 
Ameongeza kuwa sekta uzalishaji wa bidhaa za viwandani imekua kwa asilimia 8.5 kutoka 8.3 huku shughuli za utoaji wa huduma na uchumi zikiwemo za ukarabati wa magari, pikipiki na vifaa vingine vya majumbani zikikua kwa asilimia 8.0 kwa robo ya mwaka 2014.
 
Bw. Oyuke ameeleza kuwa shughuli za uchukuzi na mawasiliano zimefikia kasi ya ukuaji wa asilimia 16.5 katika kipindi hicho na kuongeza kuwa huduma za hoteli na migahawa zimefikia kasi ya ukuaji wa asilimia 3.0, huku shughuli za uendeshaji wa Serikali zikifikia asilimia 5.1, Elimu asilimia 5.2, huduma za Sfya na  shughuli nyingine zikikua kwa asilimia 4.5.
 
Aidha, amefafanua kuwa sekta ya umeme katika robo ya mwaka 2014 imekua kwa asilimia 12.6 ikilinganishwa na asilimia 6 ya mwaka uliopita kutokana na kupatikana kwa vyanzo mbadala vya kuzalisha umeme hususan ugunduzi wa gesi nchini ambao umeondoa tatizo la utegemezi wa umeme wa maji katika kuzalisha umeme.
 
“Kwa kipindi kirefu sekta ya umeme imekuwa na mawimbi kwa kiasi kikubwa , umeme wetu umekuwa wa kutegemea maji ya mvua, baada ya juhudi za Serikali na kugundulika kwa nishati ya Gesi nchini na kupatikana chanzo mbadala cha nishati tatizo hili limeshghulikiwa sasa sekta hii imeimarika” Amesisitiza.
 
Amesema Tanzania sasa inafanya vizuri kiuchumi katika nchi za Afrika ya Mashariki kwa kuwa ya pili ikifuatiwa na Uganda, Rwanda na Burundi na kuongeza kuwa hali ya amani na utulivu iliyopo nchini inaiweka Tanzania katika nafasi nzuri ya kukua zaidi kiuchumi.
 
Kwa upande wake mtaalam wa wa Uchumi kutoka Benki Kuu ya Taifa (BOT) Bw. Davidi Kwimbere akifafanua kuhusu hali iliyopo ya ukuaji wa uchumi amesema kuwa imechangiwa na kuongezeka kwa shughuli za uzalishaji .
 
Amesema sekta ya Kilimo na uzalishaji wa mazao imekua kutokana na matumizi ya mbolea, zana bora za kilimo, mbegu bora, madawa na kufafanua kuwa endapo juhudi zaidi zitaendelea kufanywa na wananchi kwa kuingia katika shughuli mbalimbali za uzalishaji uchumi utaendendelea kuonekana kwa mtu mmoja mmoja.
 
Amefafanua kuwa maendeleo katika nchi yoyote  yanachukua muda na kutoa wito kwa nchi za Afrika kuendelea kujifunza  na kufafanua kuwa nchi zote zilizopiga hatua kimaendeleo mpaka kufikia asilimia 15 ikiwemo China iliwachukua miaka 20 kuondoa umasikini.
 
Amesema Tanzania inayo nafasi nzuri kukua kiuchumi kutokana na kuendelea kuimarika kwa miundombinu  na ukuaji wa sekta za ujenzi, Nishati, madini, Viwanda, umeme , kilimo na uvuvi hali inayochangia kuongezeka kwa uwekezaji.

WANANCHI WA KATA ZA NYANGAMARA, NANGARU HALMASHAURI YA LINDI VIJIJINI WAPIMWA AFYA ,ZAIDI YA 170 WAJIUNGA PAPO KWA PAPO NA CHF.

093 - Copy MENEJA WA NHIF MKOA WA LINDI FORTUNATA RAYMOND  MWENYE MIWANI KULIA ,AKIENDELEA KUTOA UFAFANUZI KWA WANANCHI KUHUSU FAIDA ZA KUCHANGIA HUDUMA ZA MATIBABU KABLA CHINI YA MFUKO WA AFYA YA JAMII,KUSHOTO NI SALUM KAZIKAZI  MWANANCHI WA KATA YA NYANGAMARA LINDI VIJIJINI. 098MZEE ALLI G. CHIKOLO AKIPATA HUDUMA YA UPIMAJI WA KIWANGO CHA SUKARI (RBG) KUTOKA KWA MTAALAMU WA MAABARA DKT S.MWAMPALE,AMBAPO UPIMAJI WA AFYA KWA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA  ULIKUWA UKITOLEWA BURE  NA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA SANJARI NA ELIMU YA KUJIUNGA NA MFUKO WA AFYA WA JAMII,KATIKA KATA YA NYANGAMARA HALMASHAURI YA LINDI VIJIJINI.
110WANANCHI WA KATA YA NYANGAMARA WAKIWA KWENYE FOLENI WAKIELEKEA KUPATA HUDUMA YA UPIMAJI WA AFYA BAADA YA KUPEWA ELIMU YA KUJIUNGA NA CHF.NHIF OFISI YA MKOA WA LINDI UNATEKELEZA MPANGO WA ELIMU KWA UMMA KWA KUYAFIKIA MAKUNDI MBALIMBALI YA WANANCHI ILI KUHAKIKISHA AZMA  YA KUWAFIKIA WANANCHI WOTE WANACHANGIA MATIBABU KWA ASILIMIA 30% IFIKAPO JUNI 2015 INAFIKWA. 548AFISA UANACHAMA WA WA NHIF MARGRETH  JACKA AKIWAPA ELIMU YA MFUKO WA AFYA YA JAMII SAMBAMBA NA NHIF KWA WANANCHI NA WANACHAMA WALIOJITOKEZA KUPIMA AFYA NA ELIMU. 615KUSHOTO MWANANCHI WA KATA YA NANGARU ASHA MTIMBWELE AKIJIUNGA NA CHF PAPO KWA PAPO BAADA YA KUHAMASIKA NA KUAMUA KUUZA KUKU KWA SHS 10,000.ILI APATE HUDUMA KWA MWAKA BAADA YA KUGUNDULIKA KUWA SHINIKIZO LA DAMU  ( BP) NA KISUKARIKULIA MRATIBU WA CHF WILAYA YA LINDI VIJIJINI GOODLUCK KHATIBU AKIMFANYIA USAJILI  NA  KUPATIWA VITAMBULISHO.

WAHANGA WA MAFURIKO WAPO HATARINI .....KIGOMA

 
Na Magreth Magosso,Kigoma
 
IMEFAHAMIKA kuwa, Uongozi wa Mkoa wa Kigoma umeshindwa kuwapatia eneo la makazi ya kuishi zaidi ya wahanga 100 waliokutwa na mafuriko mwaka jana,  katika Manispaa ya kigoma Ujiji eneo la Katosho Kata ya Kibirizi wilayani hapa kutokana na ukata wa mfuko wa Maafa huku baadhi ya familia zikiwa  hatarini kwa ubakwaji .
 
Pia  manispaa, ilitoa mabati chakavu 70, ili wapewe  wananchi wenye maisha duni , lakini kutokana na ukubwa wa familia hizo wameamua kuyafungia katika ofisi ya serikali ya mtaa wa kahabwa katosho wakisubiri mchakato wa kufidiwa kwa wahanga hao ambao eneo lao limeteuliwa kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa Bandari kavu.
 
Akifafanua hilo Mjane mmoja Bahati Luseba alisema kaya yake ni miongoni mwa wahanga hao ambao wanaoishi kwa kutangatanga kutafuta mahali pa kuishi hali inayowalazimu  watoto wake  watano wakiwemo  wawili wa kike walale katika nyumba isiyosalama huku akisubiri fedha za fidia ili ajue pa kujenga makazi maalum.
 
“ awali mganga wa zahanati ya jibulenu alinipa chumba kwa muda katika zahanati yake ,  hili tuta ndio eneo la  kibanda changu sina msaada ,pakwenda sina  watoto wanazulula hovyo mtaani shule wanasuasua nabeba maboksi ya dagaa ziwani ndo napata kahela ka kula na watoto ” alisema mjane huyo.
 
Alisema aliishi hapo zaidi ya miaka 40 ndipo Desemaba ,2013 walipokutwa na mafuriko ,ambayo  yalibomoa nyumba yake na kumlazimu alale nje  zaidi ya miezi kumi akisubiri hatma ya malipo ya fidia kutoka serikalini ili aondokane na adha ya kutangatanga .
 
Jamboleo lilimtafuta Dkt.Jibulenu ili athibitishe ikiwa alimuhifadhi mjane huyo katika zahanati yake Dkt.Abuurashid Jibulenu akiri kufanya hivyo kutokana na mvua kubwa iliyobomoa kaya kadhaa za umma na kudai mjane huyo ni kuli wa kubeba mizigo mwalo wa kibirizi hivyo hali duni ya maisha inachangia  watoto wake kuzulula hovyo mitaani.

Alisema zahanati ipo karibu na ilipokuwa nyumba ya mjane  huyo mwenye watoto mapacha wawili  wa kike wenye umri(4)baada ya diwani kudai hana eneo la kumuhifadhi ndipo  alimpatia chumba kimoja kwa muda  alale na watoto kwa lengo la kuwaepusha na baridi na magonjwa hasa kichomi .
 
Alishindwa kuendelea kumhuhifadhi kutokana na sheria,kanuni na taratibu za kikazi kuwa ,zahanati  si makazi rasmi kwa asiye mgonjwa .Naye mtendaji wa mtaa wa husika Musa Kiumbe alisema wahanga wa mafuriko wapo mashakani hadi leo na kudai wanasubiri mthamini mkuu aweke saini ili  wafidiwe na wajue cha kufanya.
 
Akijibia hilo Diwani wa kata husika Rashid Yunus ambaye pia ni Kaimu meya wa manispaa ya kigoma ujiji alisema changamoto ya kushindwa kuwasaidia wahanga wa mafuriko inatokana na idadai kubwa ya walengwa  na  walitoa tulubai 52 kwa kaya 9 sambamba na kuyafungia mabati ili kuepusha lawama kwa umma kutokana na hali duni za wahanga hao.
 
Aliongea na mkuu wa wilaya husika Ramadhan Maneno ambaye alidai mfuko wa maafa hauna fedha za kuondoa adha za wahanga hao Jamboleo lilimuhoji Maneno juu ya wahanga na hatma ya kusaidiwa alisema hivi`mafuriko yalitokea mwaka jana ni sababu ipi inayowakera ‘alidai kiongozi huyo.
 
Maneno alisema waliokubwa na adha ya mafuriko waende katika manispaa hiyo ili waboreshewe changamoto zao na si kumpa mzigo wa kuwajibika kwa raia husika.Aidha uchunguzi mdogo umebaini kuwa mbali ya uongozi wa mkoa kushindwa kuwajibika kwa walengwa.
 
Pia wanategea fidia zitakazotolewa na mradi  wa bandari kavu  ziwasaidie kupata makazi mapya wakati ilihali  mthamini wa manispaa akiwa jijini Dare salaam akisubiri saini ya mtathimini mkuu wa serikali ili wahanga wa katosho walipwe na mradi uanze.

Huku chama cha wandishi wa habari wanawake(Tamwa) kinadai maendeleo na GBV yanamahusiano katika ustawi wa jamii,changamoto za umma zishughulikiwe ili amani na utulivu udumu.

Thursday, September 11, 2014

MWANAMKE AOKOTWA IGUNGA AKIWA TAABANI,NGUO ZALOWA DAMU!!

Mwanamke mmoja ambaye amefahamika kwa jina la Sarah  ameokotwa  na askari Polisi huko wilayani Igunga maeneo ya Masanga akiwa na michubuko mikononi na miguuni huku nguo zake zikiwa zimelowa kwa damu.Taarifa zilizotolewa na Afisa Maendeleo ya Jamii Bi.Mwashamba Kapipi zimethibitisha kuwa mwanamke huyo ambaye amelazwa katika hospitali ya wilaya ya Igunga hajatambulika na hawezi kuelezea kwa kirefu kwa mkasa uliompata.Mwashamba ametoa wito kwa jamii yeyote atakaye mtambua mwanamke huyo awasiliane nae kwa simu no. 0714 335929 au 0754 976520 au 0784 761776. 

DR.KEBWE AZINDUA RASMI MFUMO WA UBORESHAJI WA UPATIKANAJI WA DAWA NA VIFAA TIBA KUPITIA MZABUNI MMOJA MKOA WA DODOMA


Na Benedict Liwenga, Maelezo-Dodoma.
 
Serikali imezindua rasmi Mfumo wa uboreshaji  na kusaidia  upatikanaji wa Dawa na Vifaa Tiba kupitia Mzabuni mmoja Mkoa wa Dodoma.
 
Uzinduzi huo umefanywa na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Steven Kebwe  katika sherehe zilizofanyika leo mjini Dodoma na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo wawakilishi kutoka Wilaya saba za Mkoa wa Dodoma.
 
Mhe. Dkt. Kebwe amesema kuwa mfumo huo ni mzuri na utakuwa shirikishi kwani utahakikisha kuwa jamii inapata mahitaji sahihi ya dawa na pia wanafanya wa sekta wanafanyakazi kwa bidii  kwa lengo la kupambana na upungufu wa dawa unaoweza kujitokeza nchini. 
Amesema kuwa moja ya vitu vikubwa wanavyovifanya sasa ni kutekeleza sera ya Matokeo Makubwa Sasa katika sekta ya afya kwani Barani Africa, Tanzania na Afrika ya Kusini zimekuwa nchi zinazojitahidi kufuata mifumo mizuri ya dawa kutokana na taarifa ya shirika la Afya Ulimwenguni (WHO).
 
“Mifumo hii itatusaidia na kuboresha mahitaji ya dawa katika vituo vya afya, na hivyo kupunguza vifo  mbalimbali  vinavyotokana na wananchi kutumia dawa na tiba ambazo sio sahihi kwa sababu ya kukosa dawa katika vituo vya afya”, alisema Mhe. Kebwe.
 
Hivyo Mhe. Dkt. Kebwe ameziagiza Wilaya zote za Mkoa wa Dodoma kuhakikisha zinatekeleza mfumo kwa ufanisi ili mikoa mingine ije kujifunza kutoka kwao kwa ajili ya kusaidia kupunguza upungufu wa dawa na vifaa vya tiba hapa nchini.
 
Amesema kuwa wananchi wanakwenda katika vituo vya afya wanapenda wakute huduma nzuri na za kuridhisha huku wakipata dawa na huduma nyingine za upimaji kwa gharama nafuu.
Aidha, Mhe. Dkt. Kebwe amefafnua kuwa, sasahivi wameamua kuja na mfumo huo kwa kuwa utasaidia sana kuboresha afya za wananchi na kutekeleza malengo ya Minelia.
 
Ameongeza kuwa Serikali itaendelea kujipanga zaidi katika kufundisha na kuelekeza watumishi na  kutengeneza mifumo mipya ambapo kwa ajili ya  kusogeza huduma karibu na wananchi kulingana na bajeti.
 
Nae Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Rehema Nchimbi ameishukuru Serikali ya Uswisi kwa msaada mkubwa  kwa Tanzania hasa mkoani Dodoma katika Wilaya husika kwani utasaidia kuboresha afya za wakazi wa Dodoma.
 
Dkt. Nchimbi ameongeza kuwa anaamini kuwa mfumo huo utasimamia na kutekelezwa kama ilivyopangwa ili mikoa mingine ipate kuja kujifunza kupitia mkoa wa Dodoma.
 
“Naomba Mhe. Mgeni rasmi wakati tunasherehekea Uzinduzi huu, tuombe tupate mwongozo kwa udhibiti wa dawa zinazosambaa kwa kasi kupitia vyombo vya habari”, alisema Mhe. Nchimbi.
 
Mfumo huo utatoa fursa kwa Duka la Dawa la Bahari Limited kuzindua mfumo wa usambazaji wa dawa na vifaa tiba katika vituo vya afya na Hospitali katika Wilaya zote saba za mkoa wa Dodoma.
 
Duka hilo limepewa jukumu hilo baada ya kushinda zabuni na hivyo linatarajiwa kupata fedha zake kupitia Mfuko wa Afya ya Jamii, Mfuko wa Bima ya Afya na vyanzo mingine vya Halmashauri za Wilaya zote.
 
Mfumo huo ni wa kwanza kuanza kutekelezwa hapa nchini na kwa majaribio umeanzia mkoani Dodoma chini ya mradi tuimarishe Afya.

WAGONJWA WA SARATANI WAIOMBA SERIKALI IWEZE KUTOA HUDUMA YA MATIBABU KATIKA HOSPITALI NYINGI ZAIDI

Anna Nkinda – Maelezo
11/9/2014 Serikali imeombwa kuangalia uwezekano wa kutoa huduma ya matibabu ya ugonjwa wa saratani za wanawake  kwenye Hospitali zingine nchini kwani hivi sasa huduma hiyo inatolewa katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road pekee.

Ombi hilo limetolewa leo na wanawake wanaokabiliwa  na tatizo la ugonjwa wa saratani ya mlango wa  kizazi na matiti wakati wakiongea na  waandishi wa habari waliohudhuria mkutano wa siku tatu wa saratani za wanawake unaofanyika katika Hoteli ya Court Yard jijini Dar es Salaam.

Wanawake hao walisema inachukua muda mrefu pale ambapo utagundulika una ugonjwa wa saratani hadi kupata matibabu lakini kama huduma hiyo itatolewa katika Hospitali zingine itarahisisha kwa mgonjwa kupata matibabu kwa wakati.

Mmoja wa wanawake  anasumbuliwa na saratani ya titi alisema wanawake wengi wanafikiria ukiugua saratani unakwenda kufa jambo ambalo siyo kweli kwani yeye ameishi na ugonjwa huo kwa muda wa miaka 16 sasa.

“Nawashauri wanawake wenzangu waende kufanya vipimo vya mara kwa mara kwani kuna vipimo ambavyo ukipima utajua kama unatatizo  au la na kama utakutwa  na ugonjwa  utapata dawa mapema”, alisema mgonjwa huyo.

Naye mmoja wa wanawake  anayeumwa ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi alisema dalili ya kwanza aliyoiona ni kutokwa na damu ukeni akaamua kwenda  kufanya vipimo na baada ya kukutwa na tatizo akapata matibabu katika Taasisi ya Saratani ya  Ocean Road.

“Nawashauri wanawake wenzangu wakiona dalili za ugonjwa huu wasikae kimya na kujidanganya kwa kutumia dawa za miti shamba bali wawahi Hospitali mapema ambako watapata matibabu na kupona. Mimi nilipata tatizo la ugonjwa huo mwaka 2011 nilitibiwa na kupona”, alisema.

Kwa upande wake Dkt. Sara Maongezi ambaye ni Mkurugenzi wa uboreshaji Afya kutoka Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) alisema Saratani ya mlango wa kizazi ni moja ya saratani inayoongoza kwa kuua wanawake wengi nchini.

Alisema  mkutano huo ambao umehudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka  nchi za Kenya, Uganda, Malawi, Zambia, Madagasca, Rwanda na Burundi unalengo la kuwafanya wanawake waweze kuufahamu ugonjwa huo ili waweze kujikinga kwa wale ambao hawajapata na kwa walioupata waweze kuwahi mapema Hospitali kwa ajili ya kupata huduma za matibabu.  

“Baada ya Mkutano huu tutatoka na maazimio ambayo tutayafanyia kazi na kuona jinsi gani tunaweza kuboresha utendaji wetu  wa kazi za kuielimisha jamii kuhusu ugonjwa huu”, alisema Dkt. Maongezi.

Dkt. Maongezi alisema, katika nchi za Afrika ya Mashariki takwimu zinaonyesha Tanzania inaongoza kuwa na wagonjwa wengi wa saratani za wanawake lakini bado hakuna ukusanyaji sahihi wa takwimu kwani wagonjwa wengi wanafia majumbani na wanaofika Hospitali kupata matibabu ni wachache.

Walengwa wa mkutano huo ni wanawake wanaoishi na saratani pamoja na Asasi zinazofanya kazi za saratani lengo lake ni kwa wadau hao kuweza kuilemisha jamii  ili iweze kuchukua hatua dhidi ya ugonjwa huo.

Mkutano huo umeandaliwa na Women’s Empowerment Cancers Advocacy Network, (WE CAN) kwa kushirikiana na Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii pamoja na wadau wengine wa Saratani .

WATANZANIA WAASWA KUTUNZA VIPATO VYAO WAWE NA MAISHA BORA


01Mwezeshaji wa Taasisi ya MAYEPS Tanzania Lucas Marco (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) hivi karibuni jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa kitabu kiitwacho “NITUNZE NIKUTUNZE FAINALI UZEENI”, chenye maudhui ya kuwasaidia watu wanaofanyakazi ya kujiajiri au kuajiriwa kufanya maamuzi yaliyosahihi ili waweze kuishi maisha bora wakati wakiwa kwenye ajira na baada ya kustaafu. Katikati ni Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Rose Mang’enya na kushoto ni Meneja wa Taasisi hiyo John Masumba 02Mwezeshaji wa Taasisi ya MAYEPS Tanzania Lucas Marco (wa pili kulia) akimpongeza Mwenyekiti wa Taasisi ya MAYEPS Tanzania Rose Mang’enya wakati wa uzinduzi wa kitabu kiitwacho “NITUNZE NIKUTUNZE FAINALI UZEENI” hivi karibuni jijini Dar es salaam. Wa kwanza kushoto ni Meneja wa Taasisi hiyo John Masumba na Afisa Habari Idara ya Habari MAELEZO Eleuteri mangi (kulia).
(Picha na MAELEZO)
……………………………………………………
BeatriceLyimo- MAELEZO
Taasisi isiyo ya kiserikali ya MAYEPS Tanzania imezindua kitabu kiitwacho “NITUNZE NIKUTUNZE FAINALI UZEENI”, chenye maudhui ya kuwasaidia watu wanaofanyakazi ya kujiajiri au kuajiriwa kufanya maamuzi yaliyosahihi ili waweze kuishi maisha bora wakati wakiwa kwenye ajira na baada ya kustaafu.

Akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni jijini Dar es salaam, Meneja wa Taasisi hiyo John Masumba amesema kuwa uzoefu unaonesha kuwa wafanyakazi katika jamii ya Kitanzania hawaweki akiba kwa ajili ya kuwekeza kwa madhumuni ya kujenga uchumi.

Meneja Masumba amesisitiza kuwa MAYEPS imetambua kwamba ikiandaa warsha moja kwa mwezi juu wafanyakazi kufanya maamuzi yaliyo sahihi, itawafikia watu 600 kwa mwaka.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Rose Mang’enya aliwapitisha waandishi wa habari juu ya yaliyomo kwenye kitabu hicho kwa kuendesha warsha fupi iliyowafungua macho waandishi hao kuhusu namna ya kutunza fedha kuandaa maisha ya baadaye.

Akinukuu kauli ya mtaalamu wa uongozi John Maxwell Mwenyekiti huyo alisema kuwa “Watu wanaofanikiwa na wasiofanikiwa hawatofautiani sana kiuwezo bali wanatofautiana katika dhamira ya kufika kilele au upeo wa uwezo wao”.

Mang’enya aliongeza kuwa jukumu la kujenga maisha binafsi   lipo kwa muhusika binafsi, hivyo, watumishi wawe na msimamo sahihi utakaowawezesha kuwa na maisha bora.
Aidha, MAYEPS hutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa Umama na binafsi namna ya kupanga matumizi.

Pia hutoa mafunzo ambayo yatawezesha wafanyakazi kutambua kuwa fedha za mafao au pensheni hupungua thamani mwaka hadi mwaka hivyo uwekezaji wa fedha hizo ni muhimu ufanywe kwa uangalifu.

TAMWA YAWAFUNDA WANDISHI WA HABARI KATAVI,RUKWA NA KIGOMA KUHUSU UKATILI WA KIJINSIA

HABARINa Magreth Magosso,Kigoma

WANDISHI wa Habari wameaswa kutumia kikamilifu kalamu zao kuandika athari za ndoa za utotoni na madhara ya ubakaji katika jamii  kwa lengo la  kutokomeza vitendo hivyo.

Hali hiyo inachangiwa na sehemu kubwa ya jamii kutokujali,kuwajibika katika kutoa taarifa ya matukio hayo  ambapo kila kukicha vitendo  hushamiri  ili hali  viongozi wa serikali,wanasiasa na watumishi wa mungu  wanashindwa kubabanua athari na madhara kwa  walengwa kulingana na nafasi zao.

Akifafanua hilo   Judica Losai ambaye ni msimamizi wa vipindi vya redio kutokaChama cha Wanahabari Tanzania (Tamwa) alisema dhima   ni kuelimisha umma juu ya athari ya kufumbia macho  vitendo  hivyo  ambavyo  ni chachu kwa wahanga kuishi kwa kisasi,uoga,chuki dhidi ya jinsia Fulani kulingana na tukio lilompata awali.

Wandishi wanafursa kubwa kuiboresha jamii husika endapo itatumia kalamu kubadilisha mfumo kike unaondekeza mfumo dume ambao ni chanzo cha ukatili wa kijinsia kwa makundi hatarishi hasa wanawake na watoto ambao ndio wahanaga wa ndoa za utotoni  na ubakwaji.
 
Kwa upande wa mkufunzi wa mafunzo hayo Deo Mushi  alisema  kutokana na elimu hiyo itasaidia  wandishi wa mikoa ya katavi,Rukwa na kigoma  kubaini uhalisia wa matukio katika jamii husika na namna ya  kupambana  na ukatili wa ndoa za utotoni na ubakwaji  ili jamii tambue athari za mila potofu zinavyochangia vitendo vya ukatili wa kijinsia.
 
Pia kuibua vitendo mbalimbali vya ukatili dhidi ya wahanga  wanaoathirirka na jamii  inayofumbia macho matukio hayo kwa maslai binafsi ambapo inachangia  changamoto  ya kuwa na  kizazi chenye kuzingatia haki na maadili mema  siku za usoni.

Aidha wametoa wito kwa vyombo vya habari wabadilike kwa kutoa kipaumbele habari za ukatili wa kijinsia ili kuhamasisha umma wachane na  mfumo wa maisha hasi kwenda chanya  kwa kuzingatia mila na desturi.

 Baadhi ya wafundwa wa mafunzo hayo ya siku tatu Diana Rubanguka , Irene Temu na Peti Siyame kwa nyakati tofauti wakili  kupitia mafunzo hayo  ni mwanga wa kubaini  habari zenye viashiria vya ukatili wa kijinsia na watawajibika katika jamii  kwa kuibua na kueleimisha madhara na hatua kwa wahanga ili desturi zenye kuboresha haki,utu wa kila mmoja  ili lengo la kuboresha mahusiano katika jamii husika.

MWANAFUNZI WA DARASA LA SABA ABAKWA AINGIA CHUMBA CHA MTIHANI AKIWA HOI ...KIGOMA

Na Magreth Magosso, Kigoma.
 
MWANAFUNZI mmoja anayesoma Darasa la saba shule ya msingi Bukuba  (14)   wilaya ya Buhigwe Mkoa wa Kigoma ahofiwa kufeli mtihani wake wa mwisho wa leo (jana) kutokana na kitendo cha kubakwa  na kijana Amon Samweli (25) ambaye pia mkazi wa kijiji cha mwanga B wilayani humo.
 
 
Alisema  saa 12 jioni siku ya jumapili ,alimtuma mtoto huyo kwenda dukani kuchukua simu, lakini binti yake alichelewa kurudi na aliporudi akamwambia mama yake kuhusu alichotendewa na Amoni Samwel.
 
Alichanganyikiwa baada ya kupata habari hiyo kutokana na hofu na hisia hasi kutoka kwa jamii na alipomchunguza  aliona akitokwa na damu nyingi sehemu nyeti ambazo zilitapakaa kwenye makalio ndipo akampigia simu baba yake  kabla ya kwenda kwenye vyombo vya sheria.
 
Alitoa  taarifa katika kituo cha polisi  cha wilayani hapo na  kuandika mashtaka na kupewa PF3 kwa ajiri ya kupata matibabu  katika  kituo cha afya  cha wilayani hapo na kufanyiwa vipimo vyote  hasa ukimwi na magonjwa ya zinaa .
 
Wakati huohuo Chama cha wandishi wa habari (Tamwa) waliwasihi wandishi wa habari kanda magharibi wajikite kuibua habari zenye viashiria vya ukatili wa kijinsia hasa ubakwaji na ndoa za utotoni.


Kwa upande wa mwanafunzi husika (linahifadhiwa,)  alisema kuwa baada ya kutumwa na mama yake alikutana na mwanafunzi mwenzake wa kiume na kumuomba amuelekeze walichofundishwa darasani na ndipo Amoni Samweli alipowakuta.
 
Aliwauliza walichokuwa wanafanya, nao  wakamjibu kuwa wanasoma ghafla Amoni  akaanza kumpiga makofi yule mwananfunzi mwenzake sanjari na kumfukuza eneo lile na kumshikia kisu na kumbeba  juu juu na kumpelekea katika shamba la migomba na kumtendea unyama huo.
 
 
Nae Afisa Ustawi wa Jamii wa  hapo Godfrey Kapaya alisema kuwa walifika nyumbani kwa mwanafunzi huyo na kumfanyia vipimo vilivyothibitisha tukio hilo na alikuwa na majeraha sehemu  za siri sanjari na kumpatia dawa za kupunguza maumivu, kuzuia maambukizi ya magonjwa ya zinaa pamoja na mimba” alisema Kapaya.
 
Kapaya aliongeza kuwa kwakuwa mwanafunzi alitakiwa kuingia kwenye mtihani walimpa  ushauri wa kumuondolea hofu  ili afanye mtihani akiwa katika hari nzuri ya kimawazo.
 
 
 Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma, Japhari Muhamed alithibitisha tukio hilo na kuongeza kuwa mtuhumiwa tayari yuko mahabusu na hatua za kumfikisha mahakamani zinaendelea.ingawa awali kuna tetesi kuwa mtuhumiwa aliachiwa siku septemba ,8,2014ilihali alitenda kosa hilo siku ya 7,septemba 2014.

MSHINDI WA TANZANIA MOVIE TALENTS (TMT) 2014, MWANAAFA MWINZAGO APOKELEWA KWA SHANGWE NA NDELEMO MKOANI KWAO MTWARA

Mara baada ya kutua katika Uwanja wa Ndege wa Mtwara, Mshindi wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 Mwanaafa Mwinzago akitoa Maneno ya Shukrani kwa Wakazi wa Mtwara waliojitokeza kuja Kumpokea uwanja wa Ndege wa Mtwara mapema Leo. Vilevile alitoa Shukrani zake zote kwa Watanzania Wote kwa Kuweza umpigia Kura na Kumfanya aibuke mshindi wa Milioni 50 za Tanzania katika fainali ya Shindano la  Kusaka vipaji vya Kuigiza lijulikanalo Kama Tanzania Movie Talents (TMT).
Wapenzi, Mashabiki na wana Mtwara wakiwa Nje ya Uwanja wa Ndege wa Mtwara wakisubiri Kumpokea Mshindi wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 Mwanaafa Mwinzago kwaajili ya Kumpongeza kwa Kuibuka MShindi wa SHilingi Milioni 50 za Kitanzania katika Fainali ya Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT)lililofanyika Mwisho wa Mwezi wa nane katika Ukumbi wa Mlimani City, Jijini Dar Es Salaam.
Wakazi wa Mkoa wa Mtwara wakimpongeza Mshindi wa TMT 2014 Mwanaafa Mwinzago ambaye amewasili Mkoani Mtwara ambapo ndio Nyumbani Kwao akitokea Dar Es Salaam mara baada ya Kuibuka Mshindi na Kujinyakulia Kitita Cha Shilingi Milioni 50 za Kitanzania.
Ndugu, Jamaa na Marafiki wa Mshindi wa TMT 2014 Mwanaafa Mwinzago wakipiga picha ya Pamoja mara baada ya Kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Mtwara akitokea Dar Es Salaam.
Shangwe na Ndelemo zilitawala katika Viunga Vya Uwanja wa Ndege wa Mtwara kabla na Baada ya Mshindi wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) 2014, Mwanaafa Mwinzago kutua katika Uwanja wa Ndege wa Mtwara akitokea Dar Es Salaam ambapo fainali ya Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) lilifanyika katika Ukumbi wa Mlimani City.
Msafara wa Kuelekea Nyumbani Kwa MShindi wa TMT 2014 , Mwanaafa Mwinzago Ukitoka katika Uwanja wa Ndege wa Mtwara.
Msafara Ukielekea Nyumbani kwa Mshindi wa TMT 2014 Mwanaafa Mwinzago,
 Wazee kwa Vijana wakimpongeza Mwanaafa Mwinzago wakati alipokuwa akipelekwa Nyumbani Kwao kwa Msafara wakati akitokea Uwanja wa Ndege
 Vijana nao wakimpongeza Mshindi wa TMT 2014 Mwanaafa Mwinzago BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI»