MWANAFUNZI mmoja anayesoma Darasa la saba shule ya msingi
Bukuba (14) wilaya
ya Buhigwe Mkoa wa Kigoma ahofiwa kufeli mtihani wake wa mwisho wa leo (jana)
kutokana na kitendo cha kubakwa na
kijana Amon Samweli (25) ambaye pia mkazi wa kijiji cha mwanga B wilayani humo.
Alisema saa 12 jioni siku
ya jumapili ,alimtuma mtoto huyo kwenda dukani kuchukua simu, lakini binti yake
alichelewa kurudi na aliporudi akamwambia mama yake kuhusu alichotendewa na
Amoni Samwel.
Alichanganyikiwa baada ya kupata habari hiyo kutokana na
hofu na hisia hasi kutoka kwa jamii na alipomchunguza aliona akitokwa na damu nyingi sehemu nyeti
ambazo zilitapakaa kwenye makalio ndipo akampigia simu baba yake kabla ya kwenda kwenye vyombo vya sheria.
Alitoa taarifa katika
kituo cha polisi cha wilayani hapo na kuandika mashtaka na kupewa PF3 kwa ajiri ya
kupata matibabu katika kituo cha afya cha wilayani hapo na kufanyiwa vipimo
vyote hasa ukimwi na magonjwa ya zinaa .
Wakati
huohuo Chama cha wandishi wa habari (Tamwa) waliwasihi wandishi wa
habari kanda magharibi wajikite kuibua habari zenye viashiria vya
ukatili wa kijinsia hasa ubakwaji na ndoa za utotoni.
Aliwauliza walichokuwa wanafanya, nao wakamjibu kuwa wanasoma ghafla Amoni akaanza kumpiga makofi yule mwananfunzi mwenzake
sanjari na kumfukuza eneo lile na kumshikia kisu na kumbeba juu juu na kumpelekea katika shamba la migomba
na kumtendea unyama huo.
Nae Afisa Ustawi wa Jamii wa
hapo Godfrey Kapaya alisema kuwa walifika nyumbani kwa mwanafunzi huyo
na kumfanyia vipimo vilivyothibitisha tukio hilo na alikuwa na majeraha sehemu za siri sanjari na kumpatia dawa za kupunguza
maumivu, kuzuia maambukizi ya magonjwa ya zinaa pamoja na mimba” alisema
Kapaya.
Kapaya aliongeza kuwa kwakuwa mwanafunzi alitakiwa kuingia
kwenye mtihani walimpa ushauri wa kumuondolea
hofu ili afanye mtihani akiwa katika
hari nzuri ya kimawazo.
Kamanda wa Polisi
Mkoani Kigoma, Japhari Muhamed alithibitisha tukio hilo na kuongeza kuwa
mtuhumiwa tayari yuko mahabusu na hatua za kumfikisha mahakamani zinaendelea.ingawa
awali kuna tetesi kuwa mtuhumiwa aliachiwa siku septemba ,8,2014ilihali
alitenda kosa hilo siku ya 7,septemba 2014.
No comments:
Post a Comment