Pages

KAPIPI TV

Thursday, September 11, 2014

TAMWA YAWAFUNDA WANDISHI WA HABARI KATAVI,RUKWA NA KIGOMA KUHUSU UKATILI WA KIJINSIA

HABARINa Magreth Magosso,Kigoma

WANDISHI wa Habari wameaswa kutumia kikamilifu kalamu zao kuandika athari za ndoa za utotoni na madhara ya ubakaji katika jamii  kwa lengo la  kutokomeza vitendo hivyo.

Hali hiyo inachangiwa na sehemu kubwa ya jamii kutokujali,kuwajibika katika kutoa taarifa ya matukio hayo  ambapo kila kukicha vitendo  hushamiri  ili hali  viongozi wa serikali,wanasiasa na watumishi wa mungu  wanashindwa kubabanua athari na madhara kwa  walengwa kulingana na nafasi zao.

Akifafanua hilo   Judica Losai ambaye ni msimamizi wa vipindi vya redio kutokaChama cha Wanahabari Tanzania (Tamwa) alisema dhima   ni kuelimisha umma juu ya athari ya kufumbia macho  vitendo  hivyo  ambavyo  ni chachu kwa wahanga kuishi kwa kisasi,uoga,chuki dhidi ya jinsia Fulani kulingana na tukio lilompata awali.

Wandishi wanafursa kubwa kuiboresha jamii husika endapo itatumia kalamu kubadilisha mfumo kike unaondekeza mfumo dume ambao ni chanzo cha ukatili wa kijinsia kwa makundi hatarishi hasa wanawake na watoto ambao ndio wahanaga wa ndoa za utotoni  na ubakwaji.
 
Kwa upande wa mkufunzi wa mafunzo hayo Deo Mushi  alisema  kutokana na elimu hiyo itasaidia  wandishi wa mikoa ya katavi,Rukwa na kigoma  kubaini uhalisia wa matukio katika jamii husika na namna ya  kupambana  na ukatili wa ndoa za utotoni na ubakwaji  ili jamii tambue athari za mila potofu zinavyochangia vitendo vya ukatili wa kijinsia.
 
Pia kuibua vitendo mbalimbali vya ukatili dhidi ya wahanga  wanaoathirirka na jamii  inayofumbia macho matukio hayo kwa maslai binafsi ambapo inachangia  changamoto  ya kuwa na  kizazi chenye kuzingatia haki na maadili mema  siku za usoni.

Aidha wametoa wito kwa vyombo vya habari wabadilike kwa kutoa kipaumbele habari za ukatili wa kijinsia ili kuhamasisha umma wachane na  mfumo wa maisha hasi kwenda chanya  kwa kuzingatia mila na desturi.

 Baadhi ya wafundwa wa mafunzo hayo ya siku tatu Diana Rubanguka , Irene Temu na Peti Siyame kwa nyakati tofauti wakili  kupitia mafunzo hayo  ni mwanga wa kubaini  habari zenye viashiria vya ukatili wa kijinsia na watawajibika katika jamii  kwa kuibua na kueleimisha madhara na hatua kwa wahanga ili desturi zenye kuboresha haki,utu wa kila mmoja  ili lengo la kuboresha mahusiano katika jamii husika.

No comments: