WANDISHI wa Habari wameaswa kutumia kikamilifu kalamu zao
kuandika athari za ndoa za utotoni na madhara ya ubakaji katika jamii kwa lengo la kutokomeza vitendo hivyo.
Hali hiyo inachangiwa na sehemu kubwa ya jamii kutokujali,kuwajibika
katika kutoa taarifa ya matukio hayo
ambapo kila kukicha vitendo
hushamiri ili hali viongozi wa serikali,wanasiasa na watumishi
wa mungu wanashindwa kubabanua athari na
madhara kwa walengwa kulingana na nafasi
zao.
Akifafanua hilo
Judica Losai ambaye ni msimamizi wa vipindi vya redio kutokaChama cha
Wanahabari Tanzania (Tamwa) alisema dhima ni
kuelimisha umma juu ya athari ya kufumbia macho
vitendo hivyo ambavyo
ni chachu kwa wahanga kuishi kwa kisasi,uoga,chuki dhidi ya jinsia
Fulani kulingana na tukio lilompata awali.
Wandishi wanafursa kubwa kuiboresha jamii husika endapo
itatumia kalamu kubadilisha mfumo kike unaondekeza mfumo dume ambao ni chanzo
cha ukatili wa kijinsia kwa makundi hatarishi hasa wanawake na watoto ambao
ndio wahanaga wa ndoa za utotoni na
ubakwaji.
Kwa upande wa mkufunzi wa mafunzo hayo Deo Mushi alisema
kutokana na elimu hiyo itasaidia wandishi
wa mikoa ya katavi,Rukwa na kigoma kubaini
uhalisia wa matukio katika jamii husika na namna ya kupambana
na ukatili wa ndoa za utotoni na ubakwaji ili jamii tambue athari za mila potofu
zinavyochangia vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Pia kuibua vitendo mbalimbali vya ukatili dhidi ya
wahanga wanaoathirirka na jamii inayofumbia macho matukio hayo kwa maslai
binafsi ambapo inachangia
changamoto ya kuwa na kizazi chenye kuzingatia haki na maadili
mema siku za usoni.
Aidha wametoa wito kwa vyombo vya habari wabadilike kwa
kutoa kipaumbele habari za ukatili wa kijinsia ili kuhamasisha umma wachane na mfumo wa maisha hasi kwenda chanya kwa kuzingatia mila na desturi.
Baadhi ya wafundwa wa
mafunzo hayo ya siku tatu Diana Rubanguka , Irene Temu na Peti Siyame kwa
nyakati tofauti wakili kupitia mafunzo
hayo ni mwanga wa kubaini habari zenye viashiria vya ukatili wa
kijinsia na watawajibika katika jamii
kwa kuibua na kueleimisha madhara na hatua kwa wahanga ili desturi zenye
kuboresha haki,utu wa kila mmoja ili
lengo la kuboresha mahusiano katika jamii husika.
No comments:
Post a Comment