Na Magreth Magosso,Kigoma
IMEFAHAMIKA kuwa, Uongozi wa Mkoa wa Kigoma umeshindwa
kuwapatia eneo la makazi ya kuishi zaidi ya wahanga 100 waliokutwa na mafuriko mwaka jana, katika Manispaa ya kigoma Ujiji eneo la
Katosho Kata ya Kibirizi wilayani hapa kutokana na ukata wa mfuko wa Maafa huku
baadhi ya familia zikiwa hatarini kwa ubakwaji .
Pia manispaa, ilitoa mabati
chakavu 70, ili wapewe wananchi wenye
maisha duni , lakini kutokana na ukubwa wa familia hizo wameamua kuyafungia
katika ofisi ya serikali ya mtaa wa kahabwa katosho wakisubiri mchakato wa
kufidiwa kwa wahanga hao ambao eneo lao limeteuliwa kwa ajili ya mradi wa
ujenzi wa Bandari kavu.
Akifafanua hilo Mjane mmoja Bahati Luseba alisema kaya yake
ni miongoni mwa wahanga hao ambao wanaoishi kwa kutangatanga kutafuta mahali pa
kuishi hali inayowalazimu watoto wake watano wakiwemo wawili wa kike walale katika nyumba isiyosalama
huku akisubiri fedha za fidia ili ajue pa kujenga makazi maalum.
“ awali mganga wa zahanati ya jibulenu alinipa chumba kwa
muda katika zahanati yake , hili tuta ndio
eneo la kibanda changu sina msaada ,pakwenda
sina watoto wanazulula hovyo mtaani
shule wanasuasua nabeba maboksi ya dagaa ziwani ndo napata kahela ka kula na
watoto ” alisema mjane huyo.
Alisema aliishi hapo zaidi ya miaka 40 ndipo Desemaba ,2013
walipokutwa na mafuriko ,ambayo yalibomoa
nyumba yake na kumlazimu alale nje zaidi
ya miezi kumi akisubiri hatma ya malipo ya fidia kutoka serikalini ili
aondokane na adha ya kutangatanga .
Jamboleo lilimtafuta Dkt.Jibulenu ili athibitishe ikiwa alimuhifadhi
mjane huyo katika zahanati yake Dkt.Abuurashid Jibulenu akiri kufanya hivyo
kutokana na mvua kubwa iliyobomoa kaya kadhaa za umma na kudai mjane huyo ni
kuli wa kubeba mizigo mwalo wa kibirizi hivyo hali duni ya maisha inachangia watoto wake kuzulula hovyo mitaani.
Alisema zahanati ipo karibu na ilipokuwa nyumba ya mjane huyo mwenye watoto mapacha wawili wa kike wenye umri(4)baada ya diwani kudai
hana eneo la kumuhifadhi ndipo alimpatia
chumba kimoja kwa muda alale na watoto
kwa lengo la kuwaepusha na baridi na magonjwa hasa kichomi .
Alishindwa kuendelea kumhuhifadhi kutokana na sheria,kanuni
na taratibu za kikazi kuwa ,zahanati si
makazi rasmi kwa asiye mgonjwa .Naye mtendaji wa mtaa wa husika Musa Kiumbe
alisema wahanga wa mafuriko wapo mashakani hadi leo na kudai wanasubiri mthamini
mkuu aweke saini ili wafidiwe na wajue
cha kufanya.
Akijibia hilo Diwani wa kata husika Rashid Yunus ambaye pia
ni Kaimu meya wa manispaa ya kigoma ujiji alisema changamoto ya kushindwa
kuwasaidia wahanga wa mafuriko inatokana na idadai kubwa ya walengwa na
walitoa tulubai 52 kwa kaya 9 sambamba na kuyafungia mabati ili kuepusha
lawama kwa umma kutokana na hali duni za wahanga hao.
Aliongea na mkuu wa wilaya husika Ramadhan Maneno ambaye
alidai mfuko wa maafa hauna fedha za kuondoa adha za wahanga hao Jamboleo
lilimuhoji Maneno juu ya wahanga na hatma ya kusaidiwa alisema hivi`mafuriko
yalitokea mwaka jana ni sababu ipi inayowakera ‘alidai kiongozi huyo.
Maneno alisema waliokubwa na adha ya mafuriko waende katika
manispaa hiyo ili waboreshewe changamoto zao na si kumpa mzigo wa kuwajibika
kwa raia husika.Aidha uchunguzi mdogo umebaini kuwa mbali ya uongozi wa mkoa kushindwa
kuwajibika kwa walengwa.
Pia wanategea fidia zitakazotolewa na mradi wa bandari kavu ziwasaidie kupata makazi mapya wakati ilihali mthamini wa manispaa akiwa jijini Dare salaam
akisubiri saini ya mtathimini mkuu wa serikali ili wahanga wa katosho walipwe
na mradi uanze.
Huku
chama cha wandishi wa habari wanawake(Tamwa) kinadai maendeleo na GBV
yanamahusiano katika ustawi wa jamii,changamoto za umma zishughulikiwe
ili amani na utulivu udumu.
No comments:
Post a Comment