Pages

KAPIPI TV

Sunday, August 31, 2014

CHAMA CHA MPIRA WA MIGUU KIGOMA CHAWATEGA WANASIASA

WITO umetolewa kwa wanasiasa,watumie fursa walizonazo katika jamii ili kuendeleza tasnia ya michezo Nchini.

Akielezea hilo jana Kigoma Ujiji Katibu wa Chama cha Mpira Kigoma (KRF) Issa  Bukuku alisema  wanasiasa wananafasi kubwa ya kuleta maendeleo katika jamii  kutokanan na kuwa na makundi ya watu wenye uwezo wa aina mbalimbali ambapo wakitumiwa vyema ni tija kwa raia husika.
 
Ofisi za serikali ya mkoa wa hapa na halmashauri  zinadai idara husika  hazina bajeti ya kuendesha michezo ili hali serikali kuu inadhihirisha  kuwa  kuna fungu la  fedha zinatengwa katika wizara husika za utamaduni na michezo zipo katika halmashauri na manispaa lakini uhalisia wa mambo ni utata.
 
Hali hiyo imefika KRF ya hapa kufunga ofisi zake zaidi ya miezi mitatu kufuatia hali ngumu ya uchumi kwa watendaji hatimaye ofisi kufungwa kwa masaa yote na kufunguliwa pale inapotokea kuna ajenda ya mchakato wa mashindano ya ligi daraja la kwanza ya Vodacom ama Kopa cokacola .
 
 “unashangaa kuona  KRF ya kigoma kubip nyakati za kipute ,mikoa yote utata itafanya kazi kwa wakati maalum si tija ya kujiwekeza ili ziwe na uwezo wa kujiendesha kwa  leo na kesho  tunatafuta mkate wa kila siku , katiba ya vyama vya mpira haina taratibu za kutoa fedha kwa watendaji tumeshindwa kuajiri  mhudumu wa kuwepo katika ofisi ” alibainisha Bukuku.
 
Alisema  mwaka 2010 waliomba watengewe eneo kwa ajili ya shule maalum ya Vipaji  lakini  hadi leo hakuna  majibu kutoka kwa viongozi wa mkoa na kusisitiza soka la hapa ni la msimu si ajira yenye kuwekeza na kuajiri kutokana na  mfumo  mbovu uliopo na kuomba wanasiasa wawajibike katika hili ili wakidhi hitaji la wapiga kura.

Pamoja na kufanya harambee 2010  kupata fedha za kuendesha ofisi ili kusaidia kambi ya vijana katika moja ya mashindano makubwa ya Vodacom  mwitikio kutoka kwa wadau katika hilo walifika  watano tu,hali iliyowavunja nguvu na moyo kwa viongozi  na vijana husika  na kusihin wanasiasa waingilie kati kuokoa jahazi husika.

Kwa upande wa Katibu Mkoa Chama cha Chadema mkoani hapa Shaban Madede alipohojiwa na gazeti hili juu ya kuhamasisha wadau wawekeze katika michezo akiri kupitia mikutano ya hadhara ya chama hicho atalisemea hilo na kuwasihi viongozi wasifunge ofisi bali  waweke utaratibu wa ratiba itakayobainisha siku za uwajibikaji wao.

Huku katibu  mwenezi wa Chama cha ACT   wilayani hapa Anzuruni Kibera adai viongozi wa KRF  wanajingiza kwenye vyama vya siasa hali inayochangia ugumu wa vyama kuwekeza nguvu,akili na mali kwa walengwa na kushauri ikiwa wanahitaji hilo wakubali mawazo ya wanasiasa .

Mwandishi wetu alimtafuta Meya wa manispaa ya Ujiji kwa njia ya simu ya mkononi  Bakari Beji  kupata ufafanuzi juu ya bajeti ya fedha  kwa idara husika,alidai lipo na alipoulizwa  mchanganuo wa utendaji kazi wa fedha hizo hakuwa tayari kujibu.

CHUO CHA MAFUNZO YA NYUKI TABORA KUPANDISHWA HADHI

Waziri wa maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu katika picha ya pamoja na Wahitimu wa mahafali ya tatu Chuo cha Nyuki Tabora

Na Allan Ntana, Tabora

SERIKALI imeahidi kupandisha hadhi ya Chuo cha Mafunzo ya Nyuki kilichoko mkoani Tabora ili kuwavutia wanafunzi wengi zaidi kutoka ndani na nje ya nchi kujiunga na chuo hicho.

Hayo yalibainishwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Razaro Nyarandu aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 3 ya Chuo hicho yaliyofanyika juzi chuoni hapo.

Alisema kutokana na umuhimu wa Chuo hicho atahakikisha kinaboreshwa zaidi ili kiwe kitovu cha ubora katika taaluma ya sayansi ya misitu na nyuki na hifadhi zake na kwa kuanzia ameahidi kuwasiliana na wataalamu wa wizara hiyo ili wahuishe mitaala yake ili kukiongezea hadhi.

‘Tunataka chuo hiki kiwe kimbilio la wanafunzi kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini na hata nje ya nchi, tutakiboresha zaidi ili kiwe kitovu cha ubora katika sayansi ya misitu na nyuki’, alisema Waziri Nyarandu.

Aliongeza kuwa Wizara yake itajitahidi kuzishughulikia changamoto zote zinazokikabili ikiwemo suala la upungufu wa watumishi ili kuhakikisha chuo hicho na sekta zingine zilizoko ndani ya Wizara hiyo zinakuwa na watumishi wa kutosha sambamba na kutoa fursa za ajira kwa askari wa wanyama pori na wataalamu wengineo.

Lengo ni kuhakikisha ulinzi wa kutosha unakuwepo katika maeneo yote ya hifadhi za misitu sambamba na kuwezesha shughuli zingine zote ziendelee vizuri katika maeneo hayo ikiwemo ufugaji nyuki.

Awali akisoma risala ya Chuo mbele ya Waziri, Mkuu wa Chuo hicho Semu L. Daud alisema tangu Mafunzo ya Chuo hicho yarudishwe rasmi mkoani Tabora chuo hicho kimeanza kupata mafanikio makubwa ikiwemo kuongeza udahili wa wanafunzi  kutoka 34 kwa mwaka 2010/2011 hadi 115 kwa mwaka 2014/15, huku akibainisha kuwa wanafunzi 58 wa kike na kiume kwa mwaka 2013/14 wamehitimu mafunzo hayo katika ngazi ya Astashahada na Stashahada ya Ufugaji Nyuki .

Alitaja mafanikio mengine kuwa ni pamoja na Chuo kupata utambulisho maalumu toka Baraza la Elimu ya Ufundi (NACTE) wa Ithibati ya muda (Partial Accreditation), ili kuthibitisha umuhimu wa taaluma inayofundishwa na Chuo hicho wamepewa fursa ya kushiriki katika Maonyesho ya Biashara na Kilimo (Sabasaba na NaneNane) kuanzia mwaka 2009 mpaka sasa ili kuelimisha wananchi.

Aidha Mkuu wa Chuo alitaja changamoto mbalimbali zinazokikabili chuo hicho kuwa  pamoja na upungufu wa watumishi wasio wakufunzi hususani Afisa Utumishi, Wakutubi, Wapishi, Madereva, Afisa Ugavi, walinzi na mwangalizi wa masijala.

Changamoto nyingine ni tatizo la uhaba wa vifaa vya kisasa vya kufundishia ikiwemo vitabu na chombo cha usafiri hasa kwa shughuli za utawala na shughuli za mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi.

Aidha alibainisha kuwa hadhi ya Chuo hicho itaongezeka pale tu mikakati yote ya kukipanua na kukiboresha itakapotekelezwa ipasavyo hivyo akaiomba serikali kupitia Waziri mwenye dhamana kuangalia uwezekano wa kuongeza fungu la bajeti ya Chuo hicho ili jitihada za kuboresha miundombinu hiyo zianze mra moja.


MWANAAFA MWINZAGO AIBUKA KINARA WA SHINDANO LA TANZANIA MOVIE TALENTS(TMT)2014 NA KUONDOKA NA KITITA CHA SHILINGI MILIONI 50 ZA KITANZANIA

Mwenyekiti wa Makampuni ya Proin, Bw Johnson Lukaza akitoa neno kwa wadau waliojitokeza kushuhudia fainali ya Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) lililokuwa pia likirushwa live kupitia Kituo Cha Runinga cha ITV
Mwanaafa Mwinzago (katikati) akishangilia Mara baada ya kutangazwa Mshindi wa Kitita Cha Milioni 50 za Kitanzania katika Fainali ya Kumsaka Mshindi wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 lililofanyika usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa Mlimani City na Kuhudhuriwa na Mamia ya Watanzania.
Mwanaafa Mwinzago (katikati) akiwa katika picha ya Pamoja na wazazi wake na timu ya wafanyakazi wa TMT na washiriki wenzie mara baada ya kukabidhiwa mfano wa Hundi ya Shilingi Milioni 50 za Kitanzania Mara baada ya Kuwabwaga Washiriki wenzie tisa na Kuibuka Mshindi wa Kitita Cha Milioni 50 za Kitanzania katika Fainali ya Kusaka Vipaji Vya Kuigiza Nchini lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents (TMT) ambalo limefikia Ukingoni Jana Katika Ukumbi wa Mlimani City.
Washiriki wa Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 waliofanikiwa kuingia Kumi Bora wakiwa wanasubiri mshindi atangazwe 
Host Wa TMT 2014 Joti akimpongeza Baba wa Mwanaafa Mwizago kwa Mwanae kuibuka Mshindi wa Fainali ya Tanzania Movie Talents (TMT) na kuibuka na kitita cha Shilingi Milioni 50 za Kitanzania
Mwanaafa Akiwa amembeba Mdogo wake mara baada ya kutangazwa Mshindi wa Fainali ya Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 na kuibuka na kitita cha Shilingi milioni 50.
Lulu akionyesha Bahasha iliyokuwa na JIna la Mshindi wa Tanzania Movie Talents (TMT) ambae ni Mwanaafa Mwinzago na Kumfanya kujishindia Shilingi Milioni 50 za Kitanzania
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar waliojitokeza kushuhudia fainali ya TMT ambayo ilikua ikirushwa live kupitia ITV.

MTEMVU: CCM ITAUPUKUTISHA UPINZANI TEMEKE UCHAGUZI WA MITAA, SIYO KWA NGUVU ILA KWA MATUNDA YA UTEKELEZAJI ILANI


Mbunge wa Temeke, Abbas  Mtemvu akihutubia mkutano wa hadhara uliofabyika kwenye Uwanja wa shule ya Sokoine, Temeke jijini Dar es Salaam, jana, Agosti 30, 2014.
Mtemvu akishangiliwa wakati akihutubia mkutano huo wa hadhara
Mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu akimpa kadi ya Uanachama wa UWT Maridha Rajabu wakati wa mkutano huo, wanachama wapya 45 wa jumuia hiyo walipewa kadi
Mbunge wa temeke,  Mtemvu akimtuza msanii Omari Tego baada ya kukunwa na msanii huo kwa kuimba wimbo maalum wa CCM wakati wa mkutano huo
Mbunge wa temeke,  Mtemvu akimpongeza baada ya kumtuza msanii Omari Tego baada ya kukunwa na msanii huo kwa kuimba wimbo maalum wa CCM wakati wa mkutano huo
Umati wa wananchi ukiwa umefurika wakati wa mkutano huo
Mwenyekiti wa UWT Kata ya Azimio, Tatu Hassan akifungua mkutano huo, kwenye Uwanja wa Sokoine Temeke kabla ya kuhutubiwa na Mtemvu
Diwani wa Kata ya Azimio, Hamisi Mzuzuri akieleza utekelezaji wa ilani ya CCM katika kata hiyo wakati wa mkutano huo
Ofisa Kutoka Makao Makuu ya CCM, Idara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Gifti Isaya akipata picha kupitia simu yake kwenye mkutano huo
Waalikwa wakiwa kwenye mkutano huo. Wapili walioketi kulia ni Ofisa katika Idara ya Mambo ya Nje Makao Makuu ya CCM,  Gift Isaya akifuatilia kwa makini pamoja na wenzake
Msanii Yusuf Peter wa Kikundi cha hamasa Temeke, akionyesha vimbwanga vyake mbele ya mke wa Mbunge wa Temeke  Mama Mtemvu (kulia)
Msanii Ahmadi Juma wa kikundi cha hamasa Temeke, akionyesha uhodari wa 'kula' moto wakati kikundi hicho kikitoa burudani wakati wa mkutano huo
Mtemvu akiwatuza wasanii waliotia fora uwanjani wakati wa mkutano huo. Picha zote na Bashir Nkoromo wa CCM Blog

Na Bashir Nkoromo

Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu ametamba kuwa, CCM itapukutisha kwa kishindo upinzani wote katika jimbo hilo kwa kushinda mitaa yote katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.

"Wala hatutatumia nguvu bali tutaichukua mitaa yote hata hiyo michache iliyopo sasa chini ya upinzani, kwa kutumia mtaji wa mafanikio makubwa tuliyoonyesha katika utekelezaji wa ilani ya CCM katika kipindi hiki", alisema Mtemvu.

Mtemvu alitoa tambo hizo wakati akihutubia mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Jumuia ya Wanawake Tanzania, Kata ya Azimio, kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi Sokoine, katika Kata hiyo, Temeke jijini Dar es Salaam.

Alisema, CCM inao uhakika wa kutwaa viti vyote hadi kurejesha vichache vilivyopo sasa chini ya upinzani kwa kuwa mengi ambayo CCM iliahidi kupitia yeye wakati akiomba kuwa mbunge wa jimbo hilo katika uchaguzi mkuu uliopita yamefanyika.

Mtemvu alitaja baadhi ya yaliyotekelezwa kuwa ni pamoja na ujenzi wa barabara katika maeneo mbalimbali ambazo karibu zote zimeboreshwa kwa kujengwa kwa kiwngo cha lami tofauti na awali ambapo ilikuwa kero kubwa kwa kuwa zilikuwa hazipitiki kutokana na ubovu tena za vumbi.

"Zamani nilikuwa kila nikisimama jukwaani mnaniolea matatizo na kero lukuki hasa kuhusu hizi barabara, sasa leo hatuzungumzii matatizo ya barabara, tunazungumzia tu sasa kuboresha taa kwenye mitaa na barabara hizi", alisema Mtemvu.

Alisema, kuanzia mwezi huu Septemba, taa zote katika barabara na mitaa kwenye jimbo hilo zitawaka ambapo sasa zinafanyiwa maboresho ili zitumie nishati ya jua (solar) ili kupunguza changamoto ya gharama za malipo ya umeme wa taa hizo.

Mtemvu alisema, kukamilika kwa taa hizo itakuwa janga kwa vibaka ambao wamekuwa wakitumia fursa ya giza kujificha wakati wakivizia kuiba kwenye nyumba za watu na pia kukwapua wapitanjia nyakati za usiku.

Alisema mbali na kuboresha barabara CCM pia kupitia uongozi wake imeweza kuboresha hali za wananchi hasa kina mama na vijana kwa kuviwezesha vikundi vyao vya ujasiriamali kwa kuwakopesha fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali ambapo sasa zaidi ya vikundi 100 vimenufaika.

Mtemvu aliahidi kuendelea kushirikiana na wabunge wengine wa Temeke na mkoa wa Dar es Salaam kwa jumla kuhakikisha watendaji wabovu serikalini wanakabwa koo ili wawajibike ipasavyo kutumikia wananchi.

Pia aliahidi kuhakikisha anaedelea kupigania kupatikana kwa mazingira bora ya kufanya kazi zao mamalishe na bodaboda kwa kuwa wana mchango mkubwa katika maendeleao ya jamii.

"Najua haiwezekani bodaboda zote zikaingia mjini, lakini tunachofanya ni kupigania kuhakikisha unakuwepo utaratibu mzuri utakaowezesha baadhi kufika mjini bila kuharibu taratibu na sheria zilizopo. Pia Mamalishe kwa kuwa lazima waendelee na shughuli zao tunawatafutia utaratibu bora kufanya shughuli zao kwa amani badala ya kukimzwa kimbizwa na mgambo kila mara", alisema Mtemvu.

Katika mkutano huo, uliosheheni burudani mbalimbali ikiwemo msanii Omari Tego kuimba wimbo maalum wa CCM ambao ulikonga nyoyo za waliohudhuria, Mtemvu aligawa kadi kwa wanachama wapya 45 wa UWT.

Saturday, August 30, 2014

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. JANETH MBENE ATEMBELEA BANDA LA NSSF MAONYESHO YA WAJASIRIAMALI KANDA YA KATI

Meneja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa
Kigoma, Josephat Komba akimuelezea Mgeni Rasmi, Naibu Waziri wa Viwanda na
Biashara, Janeth Mbene huduma mbalimbali zitolewazo na NSSF kwenye banda lao
wakati wa maonesho ya wajasiriamali Kanda ya Kati.
 Banda la NSSF linavyooneka kwenye maonesho ya Wajasiriamali
wa Kanda ya Kati yanayofanyika 
 Maofisa wa NSSF walioshiriki Kwenye Maonesho ya
wajasiriamali kanda ya Kati wakiwa na Meneja wa Mkoa wa Kigoma, Josephat Komba
wakimsubiri Mgeni Rasmi kuja kutembelea banda la NSSF.
Daktari wa NSSF akimpima Shinikizo la Damu Afisa Uhusiano
Mwandamizi wa NSSF ,Theopista Muheta wakati wa maonesho ya wajasiriamali anda
ya kati.
Mmoja ya Washiriki wa Maonesho ya Wajasiliamali Kanda ya kati akipima uzito tayari kupewa Ushauri juu ya uwiano wa uzito wake na urefu (BMI) na Daktari wa NSSF.
 Wakazi wa Mkoa wa Kigoma wakipata maelekezo ya Mafao
yatolewayo na NSSF kwa wanachama wa Hiari na wasio wa Hiari.
 
 
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) limeshiriki
kwenye maonesho ya wajasiriamali Kanda ya Kati yanayofanyika Mkoani Kigoma
kwenye viwanja vya Community Centre kuanzia Tarehe 27/08/2014 mpaka tarehe
02/09/2014.
 
Katika Maonesho hayo NSSF imekuwa ikitoa Elimu ya Uanachama
wa HIARI kwa Wajasiriamali wanaoshiriki kwenye maonesho hayo na kuandikisha
wanachama kwa HIARI. Pia NSSF inatoa Elimu kwa wajasiliamali jinsi ya kukopa
NSSF kupitia SACCOS.
 
Mgeni Rasmi, Naibu waziri wa Viwanda na Biashara, Janeth
Mbene aliwapongeza NSSF kwa kushiriki kwenye maonesho hayo na pia kwa juhudi
zao za kutoa elimu kwenye maonesho mengi .
Mgeni Rasmi aliusifia mpango wa Wakulima Scheme kwa kuweza
kuwafikiria wakulima na kuwapa mafao ya hifadhi ya jamii.

"ACHENI KULA NYAMA ZA PORINI,WANYAMA WA PORINI WENGINE WANAVIMELEA VYA EBOLA"-MACHIBYA


Na Magreth Magosso,Kigoma
 
MKUU wa Mkoa wa kigoma Kanali mstaafu Issa Machibya ,awaasa  wananchi wache kula nyama za mwituni, kwa lengo la kudhibiti ugonjwa wa Ebola mkoani hapa.
 
Akizungumzia hilo jana kwenye uzinduzi wa mkakati wa kutokomeza vifo kwa watoto wenye virusi vya ukimwi ,ikiwa na dhima ya kuhamasisha jamii ibadilike na vitendo vya unyanyapaa kwa waathirika  hasa wajawazito sanjari na matumizi sahihi  ya dawa aina ya ARVs .

Machibya alisema kigoma ipo hatarini kuwa na wagonjwa wa Ebola kutokana na na mwingiliano wa karibu kwa wakazi wa DRC-Congo ambao wanahistoria ya maradhi hayo ambapo kwa sasa wanakabiliwa na janga hilo.
 
“najua kuna watu wanauza nyama za pori huko mitaani,lakini kwa sasa acheni kula nyama hovyohovyo,sokwe ,nyani,ngedele,popo hawa wanaasili ya vimelea vya ugonjwa huo,kule congo ni kawaida hata jamii ya swala  pori msile tutalipuka” alibainisha Machibya.
 
Pia amewapa wananchi jukumu la kuweka ulinzi kwa watu wenye ulemavu wa ngozi huku akidai  wasiige tabia hasi za mauwaji hao yanayofanywa na mikoa ya simiyu,shinyanga na tabora .
 
Alisema changamoto ya umaskini inachangiwa na jamii husika ,kushindwa kutumia elimu ya uraia na sayansi ili kutambua fursa zilizopo hapa na nje ili  kuongeza kipato cha kila mtu na taifa kwa ujumla.
 
Kwa upande wa Meneja wa ICAP Itrosi Sanga na Mganga Mkuu  Leonard Subi wa hapa kwa nyakati  tofauti walisema  sekta ya afya inakabiliwa na uhaba wa vifaa vya DBS ambavyo hubainisha  mtoto aliyezaliwa na mama mwenye virusi vya ukimwi kama ameambukizwa.
 
Walisema kwa mkoa wa kigoma wanapeleka sampo ya damu ya mtoto husika katika hospitali ya Bugando kupata majibu ya mtoto ,hali inayochangia ucheleweshaji wa majibu kwa mlengwa.
 
Baadhi ya wahanga Dafroza Bernad,Gati Matiku na Shida Seleman walipongeza asasi ya Icap kwa kuwawezesha katika maisha yao na kuongeza kuwa,shida ipo upande wa serikali hasa wahudumu wa afya kutowapa haki sahihi za mahitaji ya afya zao.
 
Akijibia hilo Mratibu wa Afya ya Uzazi  na mtoto Martha Ndalituke alisema lengo ni kutokomeza mabukizi  ya vvu kwa mama kwenda kwa mtoto kutoka 15% hadi 5%  na wahudumu wakikiuka madili ,wahanga wapeleka adha kwake ili walengwa wawajibishwe .

WABUNGE WA BUNGE LA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI WATEMBELEA BANDARI YA DAR-ES-SALAAM


02Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) Dkt. Magret Zziwa (wa pili kulia) akipewa maelezo na Mtendaji Mkuu wa kampuni ya TICS Paul Wallace namna kampuni yake inavyofanyakazi ya kupakua na kupakia mizigo katika bandari ya Dar es salaam wakati wa ziara ya Wabunge wa bunge hilo walipotembelea ofisi za Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) jana jijini Dar es salaam.
Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO)
…………………………………………………
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
29/08/2014
Jumuiya ya Afrika Mashariki iko makini katika kutekeleza majukumu yake na iko karibu na watu wake kwa kuwahudumia kupitia nchi washirika.

Kauli hiyo imetolewa na Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) Dkt. Magret Zziwa wakati wa ziara yake alipotembelea ofisi za Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) pamoja na wabunge wa bunge hilo jana jijini Dar es salaam.

Spika Dkt. Zziwa alibainisha kuwa lengo la ziara ya wabunge hao ni kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na TPA na Bandari ya Dar es salaam kwa ujumla katika kuhudumia nchi washirka kiuchumi na kujiamii.

“Ni muhimu kuifanya Jumuiya kuwa imara zaidi kiuchumi na kijamii ili kuwahudumia watu wetu kwa umahiri na umakini mkubwa katika mahitaji yao” alisema Spika Dkt. Zziwa.

Wabunge hao walitembelea maeneo mbalimbali bandarini hapo na kujionea shughuli zinazofanywa ikiwa ni pamoja na kupakia na kupakua mizigo inapoingia au kutoka ili kusafirishwa kwenda nchi husika.

Spika Dkt. Zziwa alisisitiza kuwa wananchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wanahitaji kuona jumuiya yao inavyowajali na kuwahudumia wanapotekeleza majukumu yao ikizingatiwa kuwa kwa sasa hakutakuwa na urasimu wa kusafirisha mizigo kutoka nchi moja kenda nyingine kwa kukaguliwa mara mbili ambapo kwa sasa utaratibu wa Himaya Moja ya Forodha umeanza kutekelezwa kwa mafanikio makubwa.

Akionesha umuhimu wa uchukuzi na usafirishaji wa mizigo kati ya nchi washirika, Naibu Waziri wa Wizara ya Ushirikiano ya Afrika Mashariki, Dkt. Abdala Juma Abdulla Saadalla amefananisha bandari, reli na barabara katika nchi kuwa ni sawa na “moyo na mishipa ya damu” ambapo amebainisha kuwa Serikali ya Tanzania inaendelea kuboresha reli zilizopo ili ziweze kutoa huduma kwa wakati.

“Tayari Serikali kupitia wataalamu wake wa ndani imeboresha vichwa vya treni nane hadi sasa ambapo vinatarajiwa kuanza kutumika Januari mwakani pamoja na makasha” alisema Naibu Waziri Saadalla.

Kwa upange wake Meneja wa Bandari ya Da es salaam Awadh Massawe alipokuwa akiwaeleza Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki namna TPA inavyofanya kazi, amesema kuwa kwa mwaka 2013/2014 mizigo inayosafirishwa kutoka bandarini hapo imeongezeka kutoka tani milioni 4.05 mwaka 2012/13 hadi tani milioni 4.45 mwaka 2013/2014 ambayo ni sawa na asilimia 9.8.

Massawe amesema kuwa mizigo hiyo ilisafirishwa kutoka bandari ya Dar es salaam kwenda nchi za Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo, Burundi, Rwanda, Malawi and Uganda kwa kutumia mifumo ya barabara na reli.

DAKTARI BINGWA WA MAGONJWA YA SARATANI YA MATITI KUTOKA INDIA ATOA SEMINA YA UGONJWA HUO KWA MADAKTARI WA TANZANIA

Daktari bingwa wa ugonjwa wa saratani ya matiti kutoka nchini India, Profesa Anthony Pais, akitoa mafunzo kuhusu ugonjwa huo kwa madaktari wa kitanzania na wadau mbaliombakli wa sekta ya afya. Semina hiyo ilifanyika Dar es Salaam jana, Hoteli ya Protea Courtyard Seaview.
Profesa Anthony Pais, akiwa na madaktari wa kitanzania. Kutoka kushoto ni Executive Chairman Tanzania Creative Industries Network (TACIN), Anic Kashasha na Dk.Paul Mareale.
Profesa Anthony Pais (kushoto), akielezea jambo kuhusu ugonjwa huo.
Mkurugenzi Mtendaji  wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) ,
Dk.Malina  Njelekela(kulia), akizungumza na wadau mbalimbali katika semina hiyo.

Mshauri wa Kimataifa wa Kujitegemea, James Rugemalira akizungumza na waandishi wa habari. Kulia ni mke wake ambaye ni  Mkurugenzi wa Kampuni ya Mabibo Beer wines and Spirits Limited, Benedicta Rugemalira na Profesa Anthony Pais.
Profesa Pais (katikati), akiwa na wenyeji wake. Kutoka kulia ni Dk.Paul Mareale, James Rugemalira, Dk.Malina Njelekela na Benedicta Rugemalira.
Profesa Pais akizungumza na waandishi wa habari.
Mshauri wa Kimataifa wa Kujitegemea, James Rugemalira (kushoto), akipeana mkono na daktari bingwa wa ugonjwa wa saratani ya matiti kutoka India, Profesa Anthony Pais (kulia), baada ya kutoa mafunzo kwa madaktari wa Tanzania na wadau wa sekta ya afya kuhusu ugonjwa huo, Dar es Salaam jana. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd, Benedicta Rugemalira, waliodhamini mafunzo hayo ya siku moja.
Profesa Pais (mwenye suti katikati), akiwa katika picha ya pamoja na wenyeji wake.
Profesa Pais (mwenye suti katikati), akiwa katika picha ya pamoja na wenyeji wake.
Mkurugenzi Mtendaji  wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) ,
Dk.Malina  Njelekela(kulia), akiteta jambo na viongozi wengine kwenye semina hiyo.
Profesa Pais akifurahia jambo na Executive Chairman Tanzania Creative Industries Network (TACIN), Anic Kashasha.
Wadau wakiwa kwenye semina hiyo. Kulia ni Mmoja wa Wakurugenzi wa Kampuni iliyokuwa ikifua umeme ya VIP, Joe Mgaya.
Wanahabari wakiwa kwenye semina hiyo.
Continue reading →