Pages

KAPIPI TV

Saturday, August 30, 2014

"ACHENI KULA NYAMA ZA PORINI,WANYAMA WA PORINI WENGINE WANAVIMELEA VYA EBOLA"-MACHIBYA


Na Magreth Magosso,Kigoma
 
MKUU wa Mkoa wa kigoma Kanali mstaafu Issa Machibya ,awaasa  wananchi wache kula nyama za mwituni, kwa lengo la kudhibiti ugonjwa wa Ebola mkoani hapa.
 
Akizungumzia hilo jana kwenye uzinduzi wa mkakati wa kutokomeza vifo kwa watoto wenye virusi vya ukimwi ,ikiwa na dhima ya kuhamasisha jamii ibadilike na vitendo vya unyanyapaa kwa waathirika  hasa wajawazito sanjari na matumizi sahihi  ya dawa aina ya ARVs .

Machibya alisema kigoma ipo hatarini kuwa na wagonjwa wa Ebola kutokana na na mwingiliano wa karibu kwa wakazi wa DRC-Congo ambao wanahistoria ya maradhi hayo ambapo kwa sasa wanakabiliwa na janga hilo.
 
“najua kuna watu wanauza nyama za pori huko mitaani,lakini kwa sasa acheni kula nyama hovyohovyo,sokwe ,nyani,ngedele,popo hawa wanaasili ya vimelea vya ugonjwa huo,kule congo ni kawaida hata jamii ya swala  pori msile tutalipuka” alibainisha Machibya.
 
Pia amewapa wananchi jukumu la kuweka ulinzi kwa watu wenye ulemavu wa ngozi huku akidai  wasiige tabia hasi za mauwaji hao yanayofanywa na mikoa ya simiyu,shinyanga na tabora .
 
Alisema changamoto ya umaskini inachangiwa na jamii husika ,kushindwa kutumia elimu ya uraia na sayansi ili kutambua fursa zilizopo hapa na nje ili  kuongeza kipato cha kila mtu na taifa kwa ujumla.
 
Kwa upande wa Meneja wa ICAP Itrosi Sanga na Mganga Mkuu  Leonard Subi wa hapa kwa nyakati  tofauti walisema  sekta ya afya inakabiliwa na uhaba wa vifaa vya DBS ambavyo hubainisha  mtoto aliyezaliwa na mama mwenye virusi vya ukimwi kama ameambukizwa.
 
Walisema kwa mkoa wa kigoma wanapeleka sampo ya damu ya mtoto husika katika hospitali ya Bugando kupata majibu ya mtoto ,hali inayochangia ucheleweshaji wa majibu kwa mlengwa.
 
Baadhi ya wahanga Dafroza Bernad,Gati Matiku na Shida Seleman walipongeza asasi ya Icap kwa kuwawezesha katika maisha yao na kuongeza kuwa,shida ipo upande wa serikali hasa wahudumu wa afya kutowapa haki sahihi za mahitaji ya afya zao.
 
Akijibia hilo Mratibu wa Afya ya Uzazi  na mtoto Martha Ndalituke alisema lengo ni kutokomeza mabukizi  ya vvu kwa mama kwenda kwa mtoto kutoka 15% hadi 5%  na wahudumu wakikiuka madili ,wahanga wapeleka adha kwake ili walengwa wawajibishwe .

No comments: