Pages

KAPIPI TV

Monday, July 28, 2014

MTEMVU ATOA MKONO WA IDD WA VYOMBO NA SH. 10,000 KWA VIONGOZI 912 WA MATAWI YA CCM TEMEKE

Mtemvu akimkabidhi Mwenyekiti wa UWT CCM tawi la Mji Mpya Kata ya Buza, Temeke.
Baadhi ya viongozi wakiondoka na vyombo vyao huku wakiwa na sh. 10,000 kibindoni.
Shehena ya vyombo vilivyokuwa vinagawiwa
Sehemu ya umati wa viongozi wa CCM wa matawi waliofika kupata zawadi hizo. Wengi walimpongeza Mtemvu kwa moyo wake wa kujitolea.
Ni furaha tele kwa mama huyo
                          Mary wa Yombo Kilakala akifurahia zawadi yake na kitita cha sh. 10,000
Mwenyekiti wa CCM Tawi la Mlimani, Kata ya Kilakala, Temeke, Dar es Salaam, Omar Kichapwi huyoooo na vyombo vyake . ndani ya vyombo hivyo kuna vikombe, birika vijiko na chupa ya chai
Mke wa Mbunge wa Jimbo la Temeke, Mariam Mtemvu akimkabidhi zawadi ya vyombo na sh. 10,000 mmoja wa viongozi wa CCM wa Jimbo hilo.
Naibu Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke,  akimkabidhi vyombo na sh. sh. 10,000 mmoja wa viongozi wa matawi wa CCM wa Jimbo hilo. Zawadi hizo zilitolewa na Mbunge wa Jimbo hilo, Abbas Mtemvu (kulia).
Wakifurahia kupata zawadi hizo

MZEE WA UPAKO AFUTURU KWA WAZIRI MKUU

PG4A6659

BOMU LA KUTUNGUA NDEGE LAOKOTWA KIGOMA

Na Magreth Magosso,Kigoma

IMEFAHAMIKA kuwa,Mabomu yenye uwezo wa kulipua Ndege za kivita angani yaliyotupwa ziwa Tangayika Mkoa wa Kigoma,yanaendelea kuibukia ufukwe wa bandari kongwe ya forodhani  iliyopo manispaa ya kigoma ujiji.
 
Akifafanua hilo Kamanda wa Polisi mkoani hapa Frasser Kashai alisema Julai,27,mchana walipata taarifa uwepo wa bomu kubwa linalotumika kutungua ndege angani maeneo hayo ambapo watoto walikuwa wakicheza nalo.
 
Alielezea kwamba,mabomu hayo yalitupwa katika ziwa hilo kwa miaka kadhaa ambapo  kutokana na mabadiliko ya tabia nchi ,ziwa linatema mabomu hayo hali  inayohatarisha usalama wa wananchi walio wengi hawajui bomu  hatimaye watoto huyatumia kama mpira.
 
“wenzetu wa JWTZ kikosi 24 wamelichukua na kwenda kulifanyia kazi,wananchi watoe taarifa mapema pindi waonapo bomu lolote katika fukwe ya forodhani ambayo ni sugu kwa kutema zana hizo kwa usalama wa jamii “ alibainisha  Kashai.
 
 Mkazi wa kigoma Ujiji  Hussein Kaliango alipohojiwa ni kweli awali bandari ya forodhani  ilitema bomu la aina hiyo,alisema ni kweli matukio ya bomu hujitokeza ambapo mika mitatu iliyopita mwananchi mmoja alikufa kwa bomu la aina hiyo.
 
Alisema baada ya kuliokota akalitumia kama figa la jikoni ,mwisho wa siku moshi mkubwa ulikuwa ukifuka sana yeye alijua ni kuni inatoa moshi ndipo alipoingia ndani  ili  akapulize  ndipo  umauti ukamkuta .

MUME ADAIWA KUMUUA MKEWE - TABORA

Mwanamke aliyejeruhiwa baada ya kupigwa na mumewe.
Na  Mwandishi wetu maalumu.
Mwanamke mmoja mkazi wa Kijiji cha Ntarikwa manispaa ya Tabora aliyefahamika kwa jina la Rehema Hassan(28) anadaiwa kuuawa kwa kupigwa na mumewe baada ya ugomvi uliotokana na wivu wa kimapenzi majira usiku wakiwa nyumbani kwao.

Tukio hilo la kusikitisha limetokea  mwishoni mwa wiki  majira ya saa saba usiku wakati wanandoa hao walipokuwa wameingia ndani kwa lengo la kutaka kulala.

Akizungumzia tukio hilo Mwenyekiti wa Kijiji cha Ntarikwa Bw. Ali  Hamisi Mdaki amemtaja mwanaume aliyemuua  mkewe ni Hamad Mohammed Kasanzu(25)ambaye alidai alifanya mauaji hayo baada ya kumkuta na barua iliyokuwa ikihisiwa ya mahusiano ya kimapenzi na mwanaume mwingine.

Mdaki alisema ugomvi huo wa wivu wa kimapenzi kati ya Hamad na mkewe ambaye kwasasa ni marehemu ulisababisha mwanaume huyo kumpiga na kumjeruhi vibaya mkewe na baada ya kutekeleza unyama huo alikimbia kusikojulikana na kumuacha mkewe chumbani akiwa amepoteza maisha huku chumba cha pili mke mwingine ambaye ni bimkubwa akimuonya kutoeleza ukweli wa tukio hilo la kinyama.

Aidha alipoulizwa kuhusu tukio hilo kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora kamishna msaidizi Suzan Kaganda alithibitisha kuwepo kwa mauaji hayo huku akieleza Jeshi la Polisi bado linamsaka mtuhumiwa wa mauaji hayo ya kikatili.

Hata hivyo duru kutoka maeneo ya Ntarikwa zinaeleza kuwa mwaume huyo ambaye ni dereva wa Bodaboda Hamad Kasanzu amefichwa na ndugu zake wa karibu akijaribu kukwepa mkono wa sheria kuhusiana na tukio la kinyama alilolitenda.

Aidha kwa upande mwingine inakadiriwa kuwa wastani wa asilimia 65 ya wanawake walio ndani ya ndoa na nje ya ndoa wamekuwa wakifanyiwa ukatili wa kijinsia na wanaume na hivyo mbali ya kusababisha vifo visivyo na hatia lakini wanawake wamekuwa na unyonge wa kupindukia. 

Sunday, July 27, 2014

MWENGE WA UHURU WAWASILI MKOA WA DAR ES SALAAM

IMG_5919
Kikundi cha vijana toka Halmashauri ya Manispaa ya Temeke wakisherehesha wakati wa kuwasili kwa mwenge wa Uhuru uliokabidhiwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik kutoka kwa mkuu wa Mkoa wa Pwani Bi. Mwantumu Mahiza Leo Jijini Dar es Salaam IMG_5923
Kikundi cha vijana toka Halmashauri ya Manispaa ya Ilala wakisherehesha wakati wa kuwasili kwa mwenge wa Uhuru uliokabidhiwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik kutoka kwa mkuu wa Mkoa wa Pwani Bi. Mwantumu Mahiza Leo Jijini Dar es Salaam
IMG_5940
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Slaa(mwenye miwani) akishiriki kucheza pamoja na Kikundi cha vijana toka Manispaa hiyo wakati wa kuwasili kwa mwenge wa Uhuru leo Jijini Dar es Salaam. IMG_5966
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana James Kajugusi(katikati) akiwaeleza jambo Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga(Kulia) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara Hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel wakati wa kuwasili kwa mwenge wa Uhuru leo Jijini Dar es Salaam.
IMG_5968
Mkuu wa Wilaya ya Mafia Sauda Salum Mtondoo akisalimiana na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara Hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana James Kajugusi alipowasili wakati wa kuukabidhi mwenye wa uhuru kutoka wilaya yake.
IMG_5976
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akisalimiana na Vijana wakimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa walipowasili kutoka Wilaya ya Mafia IMG_5994
Mkuu wa Wilaya ya Mafia Sauda Salum Mtondoo akikimbiza Mwenge wa Uhuru kwa ajili ya kuukabidhi tayari kuanza ziara yake Mkoani Dar es Salaam.

IMG_6017
Mkuu wa Wilaya ya Mafia Sauda Salum Mtondoo (Mwenye T-shirt nyeupe) akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Pwani Bi. Mwantumu Mahiza Leo Jijini Dar es Salaam
IMG_6032
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Bi. Mwantumu Mahiza akikimbiza mwenge wa Uhuru Tayari kwa kuukabidhi kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Said Meck Sadiki.
IMG_6040
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akisalimiana na Kiongozi wa mbio za Mwenge Taifa, Rachel Kasanda wakati wa kuwasili kwa mwenge wa uhuru leo Jijini Dar es Salaam IMG_6043
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Bi. Mwantumu Mahiza akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki leo Jijini Dar es Salaam. IMG_6058Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akitoa neno la shukrani kwa Mkuu wa Pwani Bi. Mwantumu Mahiza kwa Kuukabidhi mwenge wa Uhuru Salama Mkoani Dar es Salaam. IMG_6064
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akishika mwenge wa Uhuru ulipowasili mkoani Dar es Salaam.
IMG_6065
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akishika mwenge wa Uhuru ulipowasili mkoani Dar es Salaam.

RAIS KIKWETE ATUNUKU WAHITIMU WA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI KATIKA MAHAFALI YA KOZI YA PILI

1
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Kanali James Ruzibiza Stashahada ya Usalama na Stratejia (Diploma in Security and Strategic Studies) katika mahafali ya Kozi ya Pili ya Chuo Cha Taifa cha Ulinzi (NDC) chuoni hapo Kunduchi jijini Dar es salaam leo Julai 26, 2014. Kanali Ruzibiza, ambaye anatokea Rwanda, ni mmoja wa washiriki tisa wa kozi waliotoka nchi za nje. Washiriki wengine kutoka nje y nchi walitoka Kenya, Malawi, Namibia, Nigeria, Uganda, zambia na Zimbabwe. Jumla ya wahitimu 30, wakiwemo maafisa wandamizi katika utumishi wa umma, ambapo 11 wametoka JWTZ na 10 kutoka vyombo vingine vya usalama na idara mbalimbali. 
2
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku Luteni Jenerali C.L. Makakala Shahada ya Uzamili ya Falsafa ya Usalama na Stratejia katika mahafali ya Kozi ya Pili ya Chuo Cha Taifa cha Ulinzi (NDC) chuoni hapo Kunduchi jijini Dar es salaam leo Julai 26, 2014. Luteni jenerali Makakala, ambaye ni Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi wa kwanza, amekuwa mtunukiwa wa kwanza wa Shahada hiyo hapo chuoni.
  4
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia baada ya kutunuku shahada katika  mahafali ya Kozi ya Pili ya Chuo Cha Taifa cha Ulinzi (NDC) chuoni hapo Kunduchi jijini Dar es salaam leo Julai 26, 2014.Jumla ya wahitimu 30 wamehudhuria kozi hiyo wakiwemo maafisa wandamizi katika utumishi wa umma, ambapo 11 wametoka JWTZ na 10 kutoka vyombo vingine vya usalama na idara mbalimbali. Washiriki wengine tisa wametoka  nchi za nje ambazo ni Kenya, Malawi, Namibia, Nigeria, Rwanda Uganda, Zambia na Zimbabwe.
5
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwaambia kuwa sasa ni zamu yao kupiga picha ya kumbukumbu bila yeye wahitimu wa Kozi ya Pili ya Chuo Cha Taifa cha Ulinzi (NDC) chuoni hapo Kunduchi jijini Dar es salaam leo Julai 26, 2014   8
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika  picha ya kumbukumbu na wahitimu wa Kozi ya Pili ya Chuo Cha Taifa cha Ulinzi (NDC) chuoni hapo Kunduchi jijini Dar es salaam leo Julai 26, 2014

TAMKO LA JUKWAA KUHUSU BUNGE MAALUM LA KATIBA LINALOANZA DODOMA AGOSTI 5, 2014

Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), Deus Kibamba (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, wakati akitoa tamko kuhusu Bunge la Katiba litakaloanza Agosti 5, 2014 ambapo walishauri Bunge hilo likae wiki mbili badala ya miezi miwili kama ilivyopangwa ili kupunguza matumizi makubwa ya fedha za Umma. Kutoka kushoto ni Mjumbe wa Kamati na Uongozi Jukata Omar Ali Omar,  Meneja Habari na Mawasiliano wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Kenny Ngomuo, Makamu Mwenyekiti wa Jukata, Hebron Mwakagenda na  Mratibu wa Jukata, Diana Kidara.
Makamu Mwenyekiti wa Jukata, Hebron Mwakagenda, akisoma tamko hilo.
 Waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini.




MAMA SALMA KIKWETE AHIMIZA WANAFUNZI WA KIKE WA VYUO VYA UALIMU KUVAA MAVAZI YA HESHIMA

IMG_0086
Na Anna Nkinda – Maelezo, Nachingwea
Wanafunzi wa kike wa vyuo vya ualimu nchini wametakiwa kuvaa mavazi nadhifu yanayoendana na maadili ya kazi yao ili wanafunzi na jamii inayowazunguka ijifunze kutoka kwao kwani wao ni kioo cha jamii.

Mwito huo umetolewa hivi karibuni na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati akiongea na baadhi ya wanafunzi wa kike wa chuo cha Ualimu Nachingwea mara baada ya kumalizika kwa futari aliyoiandaa kwa ajili ya viongozi wa wilaya iliyofanyika chuoni hapo.

Mama Kikwete ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa kupitia wilaya ya Lindi mjini alisema siyo jambo jema kwa mwalimu kuvaa mavazi yanayoonyesha sehemu za miili yao ikiwemo kata mikono, nguo zinazobana na sketi fupi kwa kufanya hivyo ni kwenda kinyume na haiba ya ualimu.

Alisema, “Sikuhizi kuna baadhi ya watu wanavaa mavazi yasiyoendana na utamaduni wa mtanzania, nyinyi kama walimu ambao ni kioo cha jamii na mnawafundisha wanafunzi madarasani msifanye hivyo kwa kufanya hivyo watoto wataiga na kufikiria kuwa kuvaa mavazi hayo ni sawa”.

Mama Kikwete pia aliwataka wanafunzi hao kutokuchagua maeneo ya kwenda kufanya kazi pindi wamalizapo masomo yao na kupangiwa vituo vipya vya kazi kwani kazi ya ualimu ni wito na kama mtu hakuipenda kazi hiyo basi angechagua fani nyingine za kusoma.

“Baadhi ya walimu wamekuwa wakikataa kwenda kufanya kazi katika maeneo ya vijijini, na wengine wakipangiwa vituo vya mbali na mjini wanaogopa na kudiriki hata kuacha kazi, kama ni hivyo kwa nini ulipoteza fedha na muda wako kusomea ualimu?” , aliuliza Mama Kikwete.

MNEC huyo alimalizia kwa kuwataka wanafunzi hao kusoma kwa bidii na kujiepusha na mahusiano ya kimapenzi wawapo masomoni kitendo ambacho kitawasaidia kumaliza masomo yao salama na kurudi nyumbani bila ya kufukuzwa chuo kwa ajili ya kupata ujauzito.

Mama Kikwete ambaye kitaaluma ni mwalimu miaka ya nyuma alisoma chuo cha ualimu Nachingwea na juzi akiwa chuoni hapo alitembelea Bweni la wasichana la Kawawa ambalo ndilo alilokuwa analala wakati akiwa mwanafunzi wa chuo hicho.

MBASA ALIA NA ZITTO-KIGOMA

Na Magreth Magosso,Kigoma

SAKATA la kutaka kuifuta Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwenye ulingo wa siasa Kigoma limezidi kuchukua sura mpya,ambapo imebainika kiasi cha sh.milioni 10 kutumika katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika  Octoba  2014.
 
Wakati hali ya siasa mkoani hapa kuwa tete baada ya viongozi 99 kukihujumu chama cha chadema kwa kukimarisha chama kipya cha Alliance Transparecy For Change Tanzania ,baadhi ya wanachama wa chadema wameuambia mtandao huu kuwa aliyekuwa mwenyekiti  Jaffari Kasisiko ni muuaji wa demokrasia katika chama hicho.
 
Pamoja na kujiuzulu kwa aliyekuwa mwenyekiti huyo sambamba na kutumiwa na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe kushawishi baadhi ya viongozi wakuu wa kila sekta kujiunga na chama cha  ACT.
 
Kutokana na hali hiyo chadema  imebaini Mbunge huyo katika moja ya vikao vya chama cha ACT ambacho kilifanyika katika nyumba ya aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho Kasisiko kuwa atagharamia kampeni za uchaguzi huo kwa lengo la kuweka mizizi ya chama kuanzia ngazi ya kijiji hadi mkoa.
 
Mjumbe wa Baraza la  uongozi   Chadema  kanda  ya  kati  Alphonce  Mbasa alisema wananchi  wanafahamu   mbunge huyo ni sumu katika vyama vya upinzani,kutokana na ukaidi wake ndani ya chadema sanjari na kukataa kujibu tuhuma 11 za msingi juu ya kukihujumu chama,badala yake anashawishi umma kuwa alionewa.
 
“ wazee wa kigoma baadhi  yao  wanajua kila kitu na  alionekana katika kikao hicho na kuahidi kutoa fedha hizo pamoja na kujinadi rasmi siku ya uzinduzi wa ACT  1,septemba,2014 Mwanza , wananchi wa hapa ni bendera ,baada ya miezi sita mtashuhudia siasa haina adui wala shosti” aliainisha Mbasa.
 
Alisema kwa aliyekuwa mwenyekiti chadema Jafar Kasisiko ni chachu ya kuua demokrasia ndani ya chadema kwa kuwa alihodhi nyadhifa za  ukaimu wa baraza la wazee  na mwenyekiti wa mkoa kwa miaka 20,ambapo katiba inasema kila baada ya miaka 5 kunakuwa na uchaguzi wa nafasi hiyo lakini kimkoa  hakufanya hivyo .
 
Alisema, Chadema ipo mbioni kufanya uchaguzi wa viongozi upya  katika sekta ya Bavicha,Bawacha na Bazecha kwa kuchuja makapi ya chama cha ACT kwa dhati ya kujipanga  kwenye shughuli zote za utendaji katika uchaguzi wa serikali za mitaa sambamba na wabunge 2015.
 
KAPIPIJhabari.COM imebaini  kuanzia  Julai 27 hadi 31 chadema watakuwa na mchakato wa kusimika viongozi katika idara nyeti sambamba na 2,Agosti ,2014 viongozi wa juu wa chama hicho  akiwemo Freeman Mbowe watakuwa na kibarua cha kuzuru   mikoa ya Katavi na Kigoma juu ya mustakabali wa chama kwa umma.
 
Waratibu wa ACT mkoani Kigoma  Sendwe Ibrahim na Juma Ramadhan walipohojiwa juu  ya  14, Juni, 2014 ,saa 10 alasiri  Zitto Kabwe akiwa nyumbani kwa aliyekuwa mwenyekiti wa chadema  kasisiko na wajumbe 22 wa chama cha ACT  na kutoa  ahadi hiyo akiwemo Meya wa manispaa ya kigoma ujiji  walisema si kweli na walipoulizwa ukweli hawakuwa tayari kutoa majibu sahihi.
 
Angalizo kwa  wananchi kwa ujumla wasome alama za nyakati kwa kujitambua, kutafakari  jambo kwa umakini ili kufanya maamuzi bora bila kushinikizwa kabla ya  kujiunga na chama husika,wahenga walinena miluzi mingi humpoteza mbwa.

TANZANIA YAPOKEA TUZO YA USAFIRI WA ANGA DUNIANI

20140704_114713
Tanzania imekuwa moja ya nchi nne Afrika iliyotunukiwa tuzo ya kimataifa ya usafiri wa anga duniani na Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga duniani (ICAO) kutokana na mchango wake mkubwa katika ukuaji na usalama wa anga katika bara la Afrika.
Tuzo hiyo ilitolewa hivi karibuni mjini Dakar, Senegal na Rais wa ICAO, Dk. Bernard Aliu katika kikao cha 24 cha Kamisheni ya usafiri wa anga afrika.
Pichani Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania, John Chacha akipokea tuzo hiyo kutoka kwa Rais wa ICAO, Dk. Aliu

WANANCHI WA UKANDA WA ZIWA TANGANYIKA WALIA NA JK

 
Na Magreth Magosso,Kigoma

WANANCHI wa vijiji vya ukanda wa Ziwa Tanganyika mkoa wa Kigoma,wataka ahadi ya ujenzi wa Barabara ya Chankele,Mwamgongo na  Kagunga iliyotolewa na Rais  Jakaya Kikwete itimizwe, ili waondokane  na  adha ya kutozwa  kodi  wa bidhaa  za  madukani kila watumiapo  usafiri wa maboti .
 
Kutokana na dhati na juhudi za rais huyo  kutaka kufufua na kuboresha miundombinu  ya vyombo vya usafiri katika mikoa iliyopo pembezoni mwa nchi,ambayo  zaidi ya miaka 50 ya uhuru hazina huduma bora za barabara,nishati na mitandao ya maji safi .
 
Changamoto hizo ni pamoja na mkoa wa kigoma hasa vijiji vya ukanda wa ziwa hilo,ambapo wakazi wake ni wahanga wa  kukosa usafiri wa maboti  yenye kukidhi viwango  bora vya usafiri huo, kutokana na kutopatiwa tiketi ,laifu jaketi  kwa tija ya  kufidiwa  pale janga  linapotokea  ziwani .
 
Wakizungumzia hilo katika kikao cha madiwani juzi kigoma ujiji, Baadhi ya madiwani Mathias Bwami na Habibu Hebeye walisema adha hiyo inachangiwa na halmashauri husika kushindwa kuwajibika katika maeneo lengwa ya kutoza ushuru hatimaye kutoza wananchi hao wasio na hatia .
 
Diwani wa Kata ya Mwamgongo Kassim Nyamkunga  na Hamis Betese  kata ya Mkigo walisema  Waziri Mizengo Pinda aliahidi kutoa milioni 300 katika mradi huo huku Katibu wa wizara ya Tamisemi akiwatupia lawama wataalamu wa halmashauri husika kwa kushindwa kuingiza katika  mchakato wa Bajeti za kitaifa.
 
Akichangia hilo kwa niaba ya Mkuu wa wilaya Ramadhan Maneno Katibu tawala wa wilaya hiyo Elisha Joshua alisikitishwa na kitendo cha wananchi kutozwa kodi kwa bidhaa za madukani kisa kutumia usafiri wa boti ili hali wanajua tayari kodi walishalipia katika maduka husika.
 
Agiza   katika kikao cha kamati husika wahakikishe adha hiyo iwe moja ya ajenda Huku mwenyekiti wa halmashauri hiyo Betese akidai  wanakijiji  wa ziwani wanaishi katika maeneo hatarishi kiusafiri na kusisitiza mradi wa barabara hiyo itaondoa urasimu kwa watumishi wa idara husika kwa kutoza kodi marambili .
 
Aidha kero hiyo ni ya muda mrefu,ambapo baraza la madiwani walipeka katika kikao cha Rcc Mkoa ili kulipatia ufumbuzi lakini wananchi bado watozwa hadi leo,baadhi ya madiwani wa vijiji husika akiwemo Kassim Nyakunga anayetaka ahadi ya rais na waziri mkuu itimie kuondoa adha hiyo.

SIMANZI ZAENDELEA KUTAWALA NDANI YA NYUMBA YA TANZANIA MOVIE TALENTS (TMT) MARA BAADA YA MSHIRIKI MWINGINE KUAGA SHINDANO

Majaji wa shindano la TMT wakimsikiliza kwa makini Mshiriki wa TMT, Mwanaafa Mwinzago (anayeonekana kwenye runinga mbele) wakati akijielezea kabla ya filamu fupi aliyoshiriki kuonyeshwa ili majaji waweze kutoa hukumu kwa washiriki wa kundi hilo
 Majaji wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) katikati wakiwasikiliza washiriki wa kundi la kwanza wanavyojielezea kabla ya filamu fupi waliyochezwa kuonyeshwa katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa wiki iliyopita
 Majaji wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) wakiangalia filamu fupi iliyochezwa na washiriki wa shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) katika ukumbi wa makumbusho kabla ya kuanza kutoa hukumu kwa washiriki ni nani anatoka na nani anabaki.
Jaji Vyonne Cherry au Monalisa akitoa maoni kwa washiriki waliokuwa wameshiriki kwenye filamu fupi iliyochezwa na washiriki wa TMT
  Kundi la Kwanza la Washiriki wa TMT waliocheza filamu fupi iitwayo LUGHA GONGANA wakiwa mbele ya meza ya Pilato katika ukumbi wa makumbusho ya Taifa mwanzoni mwa wiki.
 Mshiriki wa TMT, Mwanaafa Mwinzago akifunika uso wake kwa kutoamini kuwa ameponea kwenye tundu la sindano kutokana na kuondolewa katika maumivu ya Jua la Utosi na kuendelea na mashindano hayo
 Mshiriki Wa TMT, Moses Obunde (Mwenye Suti) akimpongeza Mshiriki Mwenzie Mzee Kapalata Mtawa kwa kuweza kuondolewa Kwenye Jua la Utosi na Kupelekwa Kivulini katika Shindano la TMT linaloendelea.
 Washiriki walioingia kwenye Jua la Utosi wakiwa mbele ya Meza ya Pilato huku mshiriki mmoja kutoka kwa washiriki hao aliyaaga mashindano ya TMT.
 Simanzi Zikianzia hapo sasa mara baada ya Washiriki kupunguzwa ili apatikane mmoja wa kuondoka
 Wakabaki wawili na hatimaye mmoja kati ya hao aliweza kuondolewa katika mashindano hayo
 Hatimaye Mshiriki Isalito Isaya Akaweza kurudi ndani ya Mjengo wa TMT kutokana na Kura zake kumzidi Mshiriki mwenzie Pendo ambaye aliweza kuaga mashindano hayo kutokana na kura kuwa chache
Baadhi ya Washiriki wa TMT wakimuaga Mshiriki mwenzao Pendo Edward (Katikati) ambaye aliweza kutolewa kwenye mashindano kutokana na kura kuwa chache.Picha Zote na Josephat Lukaza
Na Josephat Lukaza - Proin Promotions Limited - Dar Es Salaam.
Hatua ya mchujo katika Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) limeingia wiki ya tatu ya mchujo sasa mara baada ya mshiriki mmoja kuaga shindano hilo wiki hii. Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) limekuwa shindano bora ambalo kadri siku zinavyozidi kwenda linazidi kuteka nyoyo za watanzania wengi waliopo ndani na nje ya Nchi kutokana na utofauti wake na uzuri wake pia.
Mshiriki mmoja ambaye ni Pendo Edward aliweza  kuchomwa na jua la utosi lililompelekea kutoka kwenye shindano hilo kubwa la Tanzania Movie Talents (TMT) ambapo mpaka sasa washiriki kumi na tano (15) ndio wamebaki katika nyumba ya TMT na hali ya simanzi bado inaendelea katika nyumba ya TMT kwa wiki hii ambapo mshiriki mwingine atatakiwa kutoka.
Shindao la TMT limekuwa likivuta hisia za watanzania wengi waliopo ndani na Nje ya Tanzania kutokana na Utofauti wake na ubora wake na kupelekea watanzania wengi sana kufuatilia shindano hilo kwa ukaribu na umakini zaidi.
Hatimaye wiki hii Tanzania Movie Talents iliamua kuzindua Zoezi la kuwapigia kura washiriki wake kupitia ukurasa wetu wa facebook ambapo sasa watanzania na wapenzi wa TMT ambao wanauwezo wa kupata na kutumia internet sasa wanaweza kuwapigia kura washiriki waliowavutia kupitia ukurasa wetu wa facebook na vilevile kuendelea kuwapigia kura washiriki kwa kutumia simu zao za mkononi.
Jinsi ya Kumpigia kura Mshiriki umpendae kwa Kutumia Simu ya Mkononi Andika Neno "TMT" ikifuatiwa na namba ya ushiriki halafu tuma kwenda 15678. Mfano TMT 00 tuma kwenda 15678
Na Jinsi ya Kumpigia kura mshiriki kupitia ukurasa wetu wa facebook BOFYA HAPA  kwa kupata maelezo.