Pages

KAPIPI TV

Monday, July 28, 2014

BOMU LA KUTUNGUA NDEGE LAOKOTWA KIGOMA

Na Magreth Magosso,Kigoma

IMEFAHAMIKA kuwa,Mabomu yenye uwezo wa kulipua Ndege za kivita angani yaliyotupwa ziwa Tangayika Mkoa wa Kigoma,yanaendelea kuibukia ufukwe wa bandari kongwe ya forodhani  iliyopo manispaa ya kigoma ujiji.
 
Akifafanua hilo Kamanda wa Polisi mkoani hapa Frasser Kashai alisema Julai,27,mchana walipata taarifa uwepo wa bomu kubwa linalotumika kutungua ndege angani maeneo hayo ambapo watoto walikuwa wakicheza nalo.
 
Alielezea kwamba,mabomu hayo yalitupwa katika ziwa hilo kwa miaka kadhaa ambapo  kutokana na mabadiliko ya tabia nchi ,ziwa linatema mabomu hayo hali  inayohatarisha usalama wa wananchi walio wengi hawajui bomu  hatimaye watoto huyatumia kama mpira.
 
“wenzetu wa JWTZ kikosi 24 wamelichukua na kwenda kulifanyia kazi,wananchi watoe taarifa mapema pindi waonapo bomu lolote katika fukwe ya forodhani ambayo ni sugu kwa kutema zana hizo kwa usalama wa jamii “ alibainisha  Kashai.
 
 Mkazi wa kigoma Ujiji  Hussein Kaliango alipohojiwa ni kweli awali bandari ya forodhani  ilitema bomu la aina hiyo,alisema ni kweli matukio ya bomu hujitokeza ambapo mika mitatu iliyopita mwananchi mmoja alikufa kwa bomu la aina hiyo.
 
Alisema baada ya kuliokota akalitumia kama figa la jikoni ,mwisho wa siku moshi mkubwa ulikuwa ukifuka sana yeye alijua ni kuni inatoa moshi ndipo alipoingia ndani  ili  akapulize  ndipo  umauti ukamkuta .

No comments: