Pages

KAPIPI TV

Sunday, July 27, 2014

MBASA ALIA NA ZITTO-KIGOMA

Na Magreth Magosso,Kigoma

SAKATA la kutaka kuifuta Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwenye ulingo wa siasa Kigoma limezidi kuchukua sura mpya,ambapo imebainika kiasi cha sh.milioni 10 kutumika katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika  Octoba  2014.
 
Wakati hali ya siasa mkoani hapa kuwa tete baada ya viongozi 99 kukihujumu chama cha chadema kwa kukimarisha chama kipya cha Alliance Transparecy For Change Tanzania ,baadhi ya wanachama wa chadema wameuambia mtandao huu kuwa aliyekuwa mwenyekiti  Jaffari Kasisiko ni muuaji wa demokrasia katika chama hicho.
 
Pamoja na kujiuzulu kwa aliyekuwa mwenyekiti huyo sambamba na kutumiwa na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe kushawishi baadhi ya viongozi wakuu wa kila sekta kujiunga na chama cha  ACT.
 
Kutokana na hali hiyo chadema  imebaini Mbunge huyo katika moja ya vikao vya chama cha ACT ambacho kilifanyika katika nyumba ya aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho Kasisiko kuwa atagharamia kampeni za uchaguzi huo kwa lengo la kuweka mizizi ya chama kuanzia ngazi ya kijiji hadi mkoa.
 
Mjumbe wa Baraza la  uongozi   Chadema  kanda  ya  kati  Alphonce  Mbasa alisema wananchi  wanafahamu   mbunge huyo ni sumu katika vyama vya upinzani,kutokana na ukaidi wake ndani ya chadema sanjari na kukataa kujibu tuhuma 11 za msingi juu ya kukihujumu chama,badala yake anashawishi umma kuwa alionewa.
 
“ wazee wa kigoma baadhi  yao  wanajua kila kitu na  alionekana katika kikao hicho na kuahidi kutoa fedha hizo pamoja na kujinadi rasmi siku ya uzinduzi wa ACT  1,septemba,2014 Mwanza , wananchi wa hapa ni bendera ,baada ya miezi sita mtashuhudia siasa haina adui wala shosti” aliainisha Mbasa.
 
Alisema kwa aliyekuwa mwenyekiti chadema Jafar Kasisiko ni chachu ya kuua demokrasia ndani ya chadema kwa kuwa alihodhi nyadhifa za  ukaimu wa baraza la wazee  na mwenyekiti wa mkoa kwa miaka 20,ambapo katiba inasema kila baada ya miaka 5 kunakuwa na uchaguzi wa nafasi hiyo lakini kimkoa  hakufanya hivyo .
 
Alisema, Chadema ipo mbioni kufanya uchaguzi wa viongozi upya  katika sekta ya Bavicha,Bawacha na Bazecha kwa kuchuja makapi ya chama cha ACT kwa dhati ya kujipanga  kwenye shughuli zote za utendaji katika uchaguzi wa serikali za mitaa sambamba na wabunge 2015.
 
KAPIPIJhabari.COM imebaini  kuanzia  Julai 27 hadi 31 chadema watakuwa na mchakato wa kusimika viongozi katika idara nyeti sambamba na 2,Agosti ,2014 viongozi wa juu wa chama hicho  akiwemo Freeman Mbowe watakuwa na kibarua cha kuzuru   mikoa ya Katavi na Kigoma juu ya mustakabali wa chama kwa umma.
 
Waratibu wa ACT mkoani Kigoma  Sendwe Ibrahim na Juma Ramadhan walipohojiwa juu  ya  14, Juni, 2014 ,saa 10 alasiri  Zitto Kabwe akiwa nyumbani kwa aliyekuwa mwenyekiti wa chadema  kasisiko na wajumbe 22 wa chama cha ACT  na kutoa  ahadi hiyo akiwemo Meya wa manispaa ya kigoma ujiji  walisema si kweli na walipoulizwa ukweli hawakuwa tayari kutoa majibu sahihi.
 
Angalizo kwa  wananchi kwa ujumla wasome alama za nyakati kwa kujitambua, kutafakari  jambo kwa umakini ili kufanya maamuzi bora bila kushinikizwa kabla ya  kujiunga na chama husika,wahenga walinena miluzi mingi humpoteza mbwa.

No comments: