Thursday, July 24, 2014
Wednesday, July 23, 2014
BABAREVO AMTWANGA SHEMEJI YAKE MSIBANI-KIGOMA
MSANII wa Muziki wa kizazi kipya ( Bongo fleva) Clayton Revocatus (Baba Revo) anadaiwa
kumshushia kichapo shemeji yake Pili Abdallah kwa madai ya kutaka shemeji mtu
arudishe mali za marehemu mdogo wake Patrick Revocatus ambaye,amefariki
mwishoni mwa wiki iliyopita mwaka huu.
Akizungumza
na mwandishi wa KAPIPIJhabari.COM kigoma Ujiji juzi Pili alisema,chanzo cha kupigwa na msanii huyo
ni kutokana na msanii huyo kudai cheni
aina ya silva yenye thamani y ash.100.000
ambayo aliuziwa na mdogo na Mbunge wa Kigoma Kaskazi Bashir
Kabwe aliyokuwa akiivaa marehemu enzi ya
uhai wake.
“marehemu
alikuwa hana mali zaidi ya sh.10,000 tu ilikuwa katika pochi yake,ambayo nilitumia kumpeleka
hospitali ya rufaa maweni,shemeji na nduguze walimtenga marehemu wakati anaugua, haja zote anamalizia
kitandani na nilimsitiri ” alisema Pili.
Marehemu
alivunjika mguu ambao hakuupatia tiba kwa
wakati na Julai ,18,2014 alizidiwa ,kwa kushirikiana na rafiki zake wakampeleka
hospitali hiyo na usiku wa siku hiyo alifariki pasipo msanii huyo kuonyesha hisia za huzuni na baada ya mazishi alimtaka shemeji yake
arudishe vitu vya marehemu.
Mama mzazi
wa mpenzi wa marehemu Janeth John alisema hakumuoa bali waliishi kwa kuibana yapata
miezi sita sanjari na kufahamu mahusiano yao ambayo alimuonya mwanae kwa muda
mrefu achane na familia hiyo.
Alisema
ameingia gharama ya kulipa cheni hiyo ambayo binti yake anadai hakuchukua sanjari na sh.10,000 iliyokuwa kwenye waleti
ya marehemu kwa lengo la kuondoa shari na msanii huyo.
Kwa upande
wa msanii huyo Baba Revo alipohojiwa na gazeti hili akiri kuvurugu kwenye msiba
wa nduguye na kusisitiza marehemu hakuwa na mali zaidi ya wallet na cheni
ambayo shemeji mtu alipaswa awape wahusika.
Alisema marehemu alitakiwa apasuliwe mguu lakini
shemeji yake alimtorosha hospitalini marehemu na kudai ana haki kuelimisha na kuadibisha jamii husika na kuonya wanawake waache ukatili hasa wa kunyanyasa wanaume
.
Kamanda wa
Polisi mkoani humo,Frasser Kashai alipoulizwa juu ya hilo alisema hajui na
kuvilaumu baadhi ya vituo vidogo vya
Polisi vinachangia kuzorotesha baadhi ya matukio kufika kwa wakati katika vituo
vikubwa na kudai kulifuatilia suala hilo .
Msanii huyo
ni mkazi wa mtaa wa Kitabwe kata ya mwanga kusini wilaya ya kigoma mkoani
hapa,ameshangaa shemeji huyo kufungulia jalada la kesi la mashambulizi kituo
cha kati ambapo yeye alimfungulia kituo cha msufini wakati huohuo Kamanda
Kashai anasema ni ruksa ilimradi pawe karibu na eneo analoishi mlalamikaji.
ACT YAITOLEA MACHO UKAWA - KIGOMA
Na Magreth Magosso,Kigoma
Mwenyekiti wa chama cha
ACT Taifa Lucas Limbu
aomba umoja wa Katiba ya
watanzania UKAWA wakaze buti kuishinikiza serikali ya ccm , ikubali mabadiliko
ya mfumo wa serikali tatu kwa mujibu wa mapendekezo ya umma kupitia Rasimu mpya
ya katiba.
Akitoa kauli hiyo kigoma ujiji ,Limbu alidai serikali
inakaidi kupokea maboresho ya katiba ya awali ya mwaka 1977 kupitia mchakato wa
maboresho ya rasimu mpya ambapo Jaji mstaafu Sinde Warioba aliikabdihi rasmi
kwa wajumbe husika ili kuboresha rasimu hiyo ambayo ni mwiba kwa viongozi
wachache waliozoea mfumo nyonyaji ambao unazalisha mabwenyenye wanaotumika kulinda maslai ya
wachache.
“ccm imeacha kuenzi na kutumia falsafa ya hayati Mwalimu Nyerere sanjari na
misingi ya katiba ambapo misingi ni fursa kwa kila mtanzania kunufaika na
rasilimali zilizopo kwa lengo la kuondoa matabaka katika jamii ili kuepusha
vurugu zinazolinyemelea taifa kwa ujumla” alibainisha Limbu
Alisema Ukawa wasikubali kununuliwa na chama tawala ili
kudhoofisha mawazo ya wengi dhidi ya mfumo bora wa serikali ,ambao utaondoa
mfumo dume unaochangia vyama vya upinzani kushindwa kushika hatamu
ya mabadiliko kwa jamii husika.
Alishauri serikali itumie mfumo pendekezwa juu ya awamu za utawala dhidi ya urais uwe wa
mlinganio sawa wa muungano kulingana na
kipindi husika ,kwa dhati ya kujenga
umoja na mshikamano wa taifa,ambapo alitaka ngazi ya urais ufuatwe yaani Bara na visiwani kwa kuzingatia usawa na
haki ya utawala wa nchi.
Pia alisema kitendo
cha Jaji mkuu wa serikali kumtusi Mbunge wa kigoma kaskazini hakistahili
kuvumiliwa na kumtaka rais Jakaya
Kikwete achukue hatua za kumwajibisha jaji huyo,ambaye ameonesha utovu wa
nidhamu kwa wananchi na dunia kwa ujumla.
Naye mwenyekiti
Baraza la wazee chama hicho wa hapa Jafari Kasisiko alisema jamii ifunguke
kubaini vyama sahihi vyenye lengo na nia ya kutetea maslai ya wengi na
waondokane na tabia ya kukumbatia vyama vyenye kuwaangamiza pasipo wenyewe
kubaini
POLISI APONGEZWA BAADA YA KUKATAA RUSHWA YA WATUMIAJI WA DAWA ZA KULEVYA-TABORA
Baadhi ya dawa za kulevya na vifaa vya matumizi ya dawa hizo zilizokamatwa zikiwa zinatumiwa na watu hao kumi na wawili waliokamatwa KENIOS GUEST HOUSE huko eneo la kata ya Isevya manispaa ya Tabora. |
Kamanda Suzy amesema watu hao baada ya kukamatwa walitaka kutoa rushwa ya shilingi elfu tisini kwa kiongozi wa timu ya makachero wanaofuatilia dawa za kulevya mkoani Tabora ambaye ni mkaguzi wa Polisi Harun Kasubi ambapo alikataa na kuwafikisha kituo kikubwa cha Polisi Tabora.
TOFAUTI ZA DINI ZISIWAGAWE WATANZANIA , MWINYI.
Mkuu
wa Mkoa wa Dar es salaam, Saidi Meck Sadiki akiongea na watoto
wanaotoka katika vituo mbalimbali vya kulelea watoto yatima vya jijini
Dar es salaam , wakazi wa jiji la Dar es salaam na viongozi mbalimbali
wakati wa Futari aliyooiandaa jana usiku katika viwanja vya Karimjee.Picha na Aron Msigwa- MAELEZO.
Rais
Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi akiwasili katika viwanja vya
Karimjee kuhudhuria Futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es
salaam Saidi Meck Sadiki (wa pili kutoka kushoto) kwa watoto yatima
kutoka vituo mbalimbali vya kulelea watoto hao vya jiji la Dar es
salaam. Wengine wanaoonekana kutoka kulia ni Kamanda wa Kanda Maalum ya
Dar es salaam, Kamishna Suleiman Kova na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es
salaam Alhadi Mussa Salum.
Baadhi ya akina mama na watoto waliohudhuria Futari hiyo wakipata Chakula.
Baadhi watoto
yatima kutoka vituo mbalimbali vya kulelea watoto hao vya jiji la Dar
es salaam wakijumuika pamoja katika Futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa
wa Dar es salaam Saidi Meck Sadiki.
Rais
mstaafu wa Awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi ambaye alikuwa mgeni rasmi
wakati wa Futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam kwa
watoto yatima kutoka vituo mbalimbali vya kulelea watoto hao vya jiji la
Dar es salaam akijumuika pamoja na watoto hao na wageni mbalimbali
walioalikwa katika Futari hiyo.
Sheikh
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Alhadi Mussa Salum (wa kwanza kushoto) na
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahmani Kinana
wakijumuika katika Futari hiyo.
Rais
wa Tanzania wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi ambaye alikuwa mgeni
rasmi wakati wa Futari iliyoandaliwa na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam
akisisitiza umuhimu wa kulinda na kutunza amani iliyopo kwa kuendelea
kudumisha upendo na ukarimu ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo
yaliyomo katika vitabu vitakatifu.
Mkuu
wa mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa
Songea Dkt. Christine Ishengoma(kulia) wakiungana na viongozi wengine
kushiriki Futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam kwa
watoto yatima kutoka katika vituo mbalimbali katika viwanja vya Karimjee
jijini Dar es salaam.
Kamanda
wa Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishna Suleiman Kova (katikati)
akifafanua jambo kwa viongozi wa mkoa wa Dar es salaam Mkuu wa Mkoa wa
Dar es salaam Bw. Saidi Meck Sadiki (wa pili kutoka kulia), Mkuu wa
Wilaya ya Ilala Bw. Raymond Mushi(kulia) na Mkuu wa wilaya ya Temeke
Bi. Sophia Mjema (kushoto) wakati wa Futari iliyoandaliwa na Mkuu wa
Mkoa huo katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Na. Aron Msigwa –MAELEZO.
Dar es salaam.
Rais
mstaafu wa awamu ya pili , Ali Hassan Mwinyi ,amewataka watanzania kuwa
makini kwa kutoruhusu tofauti za dini zilizopo hapa nchini kuwa chanzo
cha mgawanyiko miongoni mwao.
Kauli
hiyo ameitoa jana usiku jijini Dar es salaam wakati wa Futari
iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Saidi Meck Sadiki kwa
watoto wanaoishi katika vituo vya kulelea watoto yatima, wananchi na
viongozi mbalimbali iliyofanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar
es salaam.
Mzee
Ali Hassan Mwinyi ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa Futari hiyo
amesema kuwa kila Mtanzania bila kujadili itikadi na dini aliyonayo ana
wajibu wa kulinda na kutunza amani iliyopo kwa kuendelea kudumisha
upendo na ukarimu kwa wenzake ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo
yaliyomo katika vitabu vitakatifu.
“Nawasihi
Watanzania wenzangu tuendelee kupendana, tuwe wamoja katika
kushirikiana, kamwe tusiruhusu wala kukubali mgawanyiko wa dini wala
itikadi zetu” Amesisitiza.
Amewashukuru
viongozi wa mkoa wa Dar es salaam wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Saidi
Meck Sadiki kwa uamuzi walioufanya wa kuandaa Futari iliyowaunganisha
watoto yatima, wananchi na viongozi mbalimbali bila kujadili itikadi na
dini zao ikiwa ni ishara ya kuonyesha upendo na ukarimu walio nao.
Kwa
upande wake Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Saidi Meck Sadiki
akizungumza wakati wa Futari hiyo aliyowaandalia wageni hao amesema kuwa
serikali ya mkoa inaendelea kutekeleza mipango mbalimbali ya
maendeleo ikiwemo ukarabati na ujenzi wa miundombinu iliyoharibiwa
vibaya wakati wa msimu wa mvua jijini Dar es salaam.
Bw.
Sadiki ameziagiza Halimashauri za Wilaya za Temeke, Ilala na Kinondoni
na Wakala wa Barabara (TANROAD) mkoa wa Dar es salaam kuhakikisha kuwa
wanarejesha hali ya kupitika kwa barabara iliyokuwepo mwanzo ili
kuwaondolea kero ya usafiri wananchi.
Amezitaka
mamlaka hizo kutumia fedha za ndani na zile zilizotolewa na Serikali
Kuu kukamilisha ukarabati wa miundombinu hiyo yakiwemo madaraja
yaliyosombwa na maji kwa muda muafaka ili kuruhusu magari kuweza kufika
katika maeneo hayo.
Katika
hatua nyingine Bw. Meck Sadiki ametoa wito kwa wakazi wa jiji la Dar es
salaam kushiriki kikamilifu katika suala la usafi na uhifadhi wa
mazingira kwa kujenga utaratibu wa kusafisha mazingira ya jiji ili
kulinda heshima ya jiji huku akisisitiza kuwa dini zote zinamtaka
mwanadamu awe mwadilifu na mwenye kuzingatia usafi.
Amezitaka
mamlaka zinazosimamia utekelezaji wa sheria za kuhifadhi mazingira
jijini Dar es salaam kufanya kazi kwa kuzingatia weledi ili kuhakikisha
maeneo yote ya jiji yanaendelea kuwa katika hali ya usafi.
Naye Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhadi Mussa Salum
akuzungumza wakati wa Futari hiyo ameeleza kuwa viongozi wa dini na
serikali kote nchini wanalo jukumu kubwa la kuwaongoza wananchi kutenda
mema na kuendelea kuvumilia.
"MWANDISHI WA HABARI WA REDIO YA MHESHIMIWA RAGE MBARONI KWA KUJIFANYA USALAMA WA TAIFA,UONGOZI WA V.O.T WAMKANA
Kitambulisho alichokuwa akikitumia Mussa kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu |
Uongozi wa Jeshi la Polisi wilaya ya Tabora ulimfikisha Mwandishi huyo mbele ya Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Suzan Kaganda |
Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Suzan Kaganda akiwaonesha waandishi wa habari kitambulisho kilichokuwa kikitumiwa na Mussa Mbeko akijifanya ni Afisa Usalama wa Taifa. |
TRA YAFUTURISHA BAADHI YA WANANCHI TABORA
Baadhi ya viongozi wa Serikali na vyama vya siasa akiwemo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake UWT mkoa wa Tabora Bi.Mwanne Mchemba walishiriki katika hafla hiyo ya Futari |
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Tabora mjini Bw.Moshi Abraham maarufu Nkokota naye alikuwa ni mmoja kati ya wageni waalikwa |
Baadhi ya walipa kodi wafanyabishara wa Tabora |
Baadhi ya watumishi wa TRA Tabora nao walishiriki hafla hiyo ya Futari |
Katibu wa ccm mkoa wa Tabora Bw.Idd Ali Ame akizungumza katika hafla hiyo ya Futari |
Mmoja kati ya viongozi wa dini ya kiislam Tabora mjini Sheikh Issa Bilali akisoma dua maalum wakati wa hafla hiyo. |
Mjumbe wa NEC Bw.John Mchele akipeana mkono na Mkurugenzi wa fedha wa TRA nchini Bw.Mshoro,pembeni ni Meya wa halmashauri ya manispaa ya Tabora Bw.Ghulam Dewij |
|
BENKI YA EXIM TANZANIA YAANDAA FUTARI KWA WATEJA WAKE WA MKOANI TANGA
Baadhi
ya wateja wa Benki ya Exim Tanzania na wafanyakazi wakifuatilia
yaliyokuwa yakizungumzwa wakati wa futari iliyoandaliwa na benki hiyo
mkoani Tanga kwa ajili ya wateja wake. Picha na mpiga picha wetu.
Meya
wa Jiji la Tanga, Mhe. Omary Uledi, ambaye pia ni mgeni rasmi (wapili
kulia) akizungumza wakati wa futari iliyoandaliwa na Benki ya Exim
Tanzania kwa wateja wake wa mkoani Tanga hivi karibuni. Wa pili kushoto
ni Meneja wa Benki ya Exim Tawi la Tanga, Deogratius Makwaia, Sheikh
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Suleiman Lighuchu (watatu kushoto)na Katibu wa
Bakwata wa Mkoa, Bw. Mohamed Riami (wa kwanza kulia). Picha na mpiga
picha wetu.
Sheikh
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Suleiman Lighuchu akizungumza wakati wa futari
iliyoandaliwa na Benki ya Exim Tanzania kwa wateja wake wa mkoani Tanga
hivi karibuni. Wa pili kushoto ni Meneja wa Benki ya Exim Tawi la Tanga,
Deogratius Makwaia, Mgeni Rasmi Meya wa Jiji la Tanga, Mhe. Omary Uledi
(Wa pili kulia)na Katibu wa Bakwata wa Mkoa, Bw. Mohamed Riami (wa
kwanza kulia). Picha na mpiga picha wetu.
Baadhi ya wateja wa Benki ya Exim
Tanzania na wafanyakazi wakichukua vyakula mbali mbali vilivyoandaliwa
malum kwa ajili ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo mkoani Tanga kwa
ajili ya wateja wake. Picha na mpiga picha wetu.
MEYA WA ILALA JERRY SILAA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA BARABARA YA UKONGA KUELEKEA MAZIZINI MPAKA MOSHI BAR
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya
Ilala Jerry Silaa Jana amefanya ziara fundi ya ukaguzi wa
ujenzi wa barabara ya ukonga Moshibar
kilometa 3 kiwango cha changalawe awamu yakwanza. Ikiwa ni
utekelezaji wa miradi ya
dharura kulingana na uharibifu wa miundo mbinuulitokea baada
ya Mvua kubwa. Mradi huo
ambao unaghalimu kiasi cha shilingi millioni 90.Pesa za
Ujenzi huohizo zinatoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilala.Pia Barabara hiyo
itawekwa Lami kwa awamu ya pili ndani ya mwaka huu kwa kilomita tatu.Picha Zote Na Dj Sek Blog
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jerry Silaa wa Kwanza kushoto akiwa na Mhandisi wa Barabara(mwenye shati Jeusi) pamoja na Diwani wa ukonga Elizabeth Mbano(katikati) na wa kwanza Kulia ni Mhandisi wa Manispaa Bwana Muhinda Kassimu wakitazama maendeleo ya ujenzi wa kipande cha barabara kutoka ukonga-mazizini mpaka moshi bar.
Mhandisi wa Manispaa Bwana Muhinda Kassimu Akielezea namna ambavyo awamu ya kwanza ya ukarabati wa barabara hiyo utakavyo kuwa kwa kiwango cha changarawe na itafuata awamu ya pili ambayo ni Lami.Diwani wa ukonga Elizabeth Mbano akiongea na vyombo vya habari kushukuru Manispaa kwa kuikumbuka barabara hiyo kwani imekuwa ikileta sana shida ya usafiri kwa wakazi wa eneo hilo hasa kipindi cha mvua.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jerry Silaa Akielezea namna Barabara hiyo itakavyotengenezwa na pia akasisitiza kwamba Pesa za Ujenzi wa Barabara Hiyo zimetoka ndani ya manispaa na si Vinginevyo.
Greda likirekebisha Barabara ya Ukonga-mazizini kulekea moshi bar
Mwonekano wa Bara barabara hiyo
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akimwelezea mkazi wa mazizini namna mradi wa barabara hiyo ulivyo.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akimuelezea kwa kumuonyesha mkazi wa mazizini gharama za mradi huo na pia pesa za mradi huo kutoka ndani ya Halmashauri na si vinginevyo.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akiwa amempa nafasi mkazi wa Mazizini kupitia majalada yenye maelezo na mikataba ya ujenzi wa barabara hiyo
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akiongea na wakazi wa mazizini waliotaka kujua mradi utachukua mda gani na utaisha lini.