Saturday, April 12, 2014
DALADALA KIGOMA WAFANYA MGOMO
Na Magreth Magosso,Kigoma
WAKAZI wa Manispaa ya Kigoma Ujiji,wamelazimika kutembea kwa
miguu kutokana na mgomo wa vyombo vya usafiri kwa kile kinachodaiwa hawana sare mpya kwa
mujibu wa Mamlaka ya usimamizi wa usafiri vyombo vya moto nchi kavu na majini (SUMATRA).
Hali hiyo imekuja baada ya SUMATRA kukamata zaidi ya daladala
20 ambazo zinatoa huduma kwa wakazi wa manispaa hiyo kwa dai la kutokuwa na
sare husika wakati wana risiti ya sare hizo ambazo bado hawajakabidhiwa na
mzabuni wa kushona sare hizo hali iliyowalazimu kugoma kutoa huduma kwa umma
ili kero hiyo ifanyiwe marekebisho.
Kwa upande wa Naibu Katibu wa umoja wa wamiliki wa magari kigoma (KIBOA)Hussein Kaliango alisema,mamlaka
imetoa wiki mbili kwa mwenye daladala awe na sare hizo hali inayokwaza mchakato huo kutokana na muda mfupi na wingi
wa wateja.
Kwa nyakati tofauti madereva wa daladala Kalenga Kasaka na Rashid
Juma walisema wanatozwa kiasi cha shilingi laki mbili na nusu endapo hauna sare
hizo sanjari na kukamata gari,hata kama wakionyesha risiti ambazo tayari
wamelipia sare hizo.
Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Kamanda wa hapa Frasser Kashai alisema hana mpango wa kutumia mabomu ya machozi kwa
madereva na makonda ambao wapo katika mgomo huo,huku akiwataka wawakilishi
watatu toka kwa walengwa waende kwa katibu tawala wa mkoa ili kuboresha mgomo
huo.
Meneja wa SUMATRA
kigoma Adamu Mamilo alipoulizwa juu ya hilo alisema awali walikaa kikao na
wadau wa vyombo vya usafiri juu ya sare mpya ziwe kamili mwanzoni mwa mwezi huu
na kuingia ndani ya gari la kamanda wa polisi akidai wanaenda kwa katibu tawala
kumaliza hilo.
Baadhi ya abiria Mawazo Mikidadi na Kamongo Sibonja walisema
hali hiyo inathiri shughuri za uzalishaji mali,kutokana na wananchi kushindwa
kufika maeneo yao ya kazi kwa wakati muafaka,huku wakishauri wadau wakae pamoja
kumaliza adha hiyo.
WANAFUNZI WA SAUTI WANACHAMA WA CHADEMA TABORA WALALAMIKIA UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA
Thursday, April 10, 2014
KLINIKI YA SOKA YA MAN U KUFANYIKA JIJINI DAR
Mkurugenzi
wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano akiongea na waandishi
wa Habari wakati wa kutangaza Kliniki ya Kimataifa ya mpira wa soka ya
Manchester United ambayo itafanyika Jijini Dar es Salaam April 23-27
chini ya wakufunzi kutoka Klabu ya Manchester United. Kushoto ni
Mkurugenzi wa Mashindano ya Vijana Ayoub Nyenzi.
-Kuendeshwa na wakufunzi wa Man U
-Kushirikisha nchi 12
-Tanzania kuwakilishwa na wachezaji 19
Kampuni
ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania leo imetangaza kufanyika kwa
kliniki ya soka ya Kimataifa ya Manchester United hapa Dar es Salaam
kuanzania 23 -27 Aprili mwaka huu.
Kliniki
hiyo ambayo itafanyika kwenye uwanja wa Azama FC (Chamazi Complex
Stadium), ina nia ya kuwaendeleza vijana waliofanya vizuri kwenye
michuano ya mwaka jana ya kimataifa ambayo ilifanyika Lagos, Nigeria na
kushirikisha nchi 12 ambapo timu ya Tanzania ya wasichana iliibuka
mabingwa.
Hii
ni mara ya pili kwa kliniki kama hiyo kufanyika hapa nchini kufuatia
kliniki kama hii liyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa 2011. Kliniki
nyingine ilifanyika Nairobi 2012 na Tanzania iliwakilishwa na wavulana
watatu na wasichana watatu.
Kama
ilivyokuwa kwenye kliniki zilizopita, kliniki ya mwaka huu itaendeshwa
na makocha kutoka shule za soka za Klabu ya Manchester United na
wanatarajiwa kutoa mafunzo ya awali ya mpira wa miguu kama vile kupiga
pasi, kukimbia na mpira, kupiga mashoot, nidhamu na nyingine nyingi.
Akiongea
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi wa
Mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano alisema kliniki hiyo ni
sehemu ya mpango kapambe wa Airtel kusaka na kuendeleza vipaji vya soka
hapa Tanzania na Barani Afrika kwa ujumla.
Mkurugenzi
wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano akiongea na waandishi
wa Habari wakati wa kutangaza Kliniki ya Kimataifa ya mpira wa soka ya
Manchester United ambayo itafanyika Jijini Dar es Salaam April 23-27
chini ya wakufunzi kutoka Klabu ya Manchester United. Kulia ni Afisa
Uhusiano Airtel Tanzania Tanzania Public Relations Officer Jane Matinde.
‘Airtel
inajivunia kuwekeza kwenye soka ambayo ina uwezo wa kuileta jamii
pamoja kupitia hamasa ya mashabiki na yenye uwezo wa kuwafanya wachezaji
kupata elimu pamoja na ajira’, anasema Singano.
Aliongeza
kuwa Airtel inajivunia programu ya Airtel Rising Stars kwa kuleta
furaha na hamasa kubwa miongoni mwa vijana wa Tanzania na pande nyingine
za Bara la Afrika hivyo kuifanya kampuni ya Airtel kuhamasika kuendelea
kuwekeza kwenye soka.
Kwa
upande wake, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Celestine
Mwesigwa ameishukuru kampuni ya Airtel kwa mpango huu makini wenye nia
ya kutafuta na kuendeleza vipaji chipukizi vya soka Tanzania.
‘Ninaamini
ya kwamba Tanzania imebarikiwa kuwa na vipaji vingi vya soka.
Tunachohitaji ni uwezo wa kifungi na raslimali za kutuwezesha kusonga
mbele na ndio maana tunawashukuru Airtel kwa kujitokeza kutuunga mkono
kupitia programu hii ya vijana’, Anasema katibu wa TFF.
Washiriki
wa kliniki hii watatoka nchi za Kenya, Uganda, Malawi, Chad, Burkina
Fasso, Sierra Leon, Sheli sheli, Congo Brazzaville, Nigeria, Zambia na
wenyeji Tanzania ambao watawakilishwa na wachezaji 19.
Airtel
Rising Stars ni programu inayojumuisha Africa nzima ili kutoa nafasi
kwa wanasoka chipukizi chini ya umri wa miaka 17 kuonyesha uwezo wao
mbele ya mawakala wa soka, makocha na kupata fursa ya kujiendeleza
zaidi. Mpango huu unawalenga wavulana na wasichana Barani Afrika.
MARUFUKU BODA BODA NA BAJAJI ZA ABIRIA KUVUKA MWENGE KWENDA POSTA
Oparesheni Kamata Bodaboda na Bajaji ikiwa inaendelea upande wa Mwenge mataa ambapo Bajaji nyingi zimekamatwa.
Askari wa Usalama wa
Barabarani akiwa anawaandikisha Baadhi ya Bodaboda na Bajaji wenye
makosa mbalimbali ili waweze kulipia tozo pamoja na kupelekwa kituo cha
Polisi.
Baadhi ya Bodaboda na Bajaji wakiwa wanangojea Hatma yao baada ya kukamatwa.
Baadhi ya Bodaboda zikiwa zimekamatwa.
Madereva wa Boda Boda na Bajaji wakipata maelezo ya kina ya kwanini wamezuiliwa kwenda Posta wakitokea Mwenge.
Mmoja wa Madereva wa Bodaboda akiwa amekaa kwa mawazo asijue anafanya nini Baada ya Bodaboda yake kukamatwa na Kupelekwa Polisi.(Picha na Dar es salaam yetu).
Kwa mujibu wa Msemaji na Muongozaji wa Oparesheni hiyo ambaye hakutaka kutajwa jina lake alisema kwamba wameamua kufanya hivyo ili kuzuia Msongamano wa Magari pamoja na bodaboda pia Bajaji kuelekea Mjini Posta, Aliongeza kuwa kumekuwa na uhalifu sana wa Silaha unaotumiwa na bodaboda hasa maeneo ya mjini hivyo ndio maana wameamua kuzuia.
“Tumefanya hivi ili kuepusha msongamano kuelekea Posta, lakini pia kumekuwa na uhalifu sana unaotumiwa kwa njia ya Bodaboda hivyo tunafanya oparesheni hii ili kupunguza tatizo hili.
Tulicho kifanya tumewaruhusu kufanya safari pembezoni mwa mji tuu hivyo Eneo la Mwenge kwa sasa Limeingia katika zone ya eneo la Mjini,Kama tuliweza kuzuia Daladala ndogo”Hiace” pia na hawa watakuja kuelewa ingawa ni zoezi gumu na linalo hitaji elimu ya ziada ambayo tumesha anza kuwapa na tunaendelea kuwapa” alimalizia kwa kusema “Pia hii ni Oparesheni ya kawaida tuu ya kukamata wale ambao hawana Leseni za kuendesha vyombo hivi pamoja na makosa mbalimbali” alisema Polisi huyo.
Kwa mujibu wa madereva wa Bodaboda na Bajaji wamesema kwamba huo ni uonevu kuwakataza wao wasiweze kwenda Mjini kwani na wao wanatafuta ridhiki yao na wameomba Serikali iwasaidie wapatiwe njia mbadala ya wao kwenda maeneo hayo.
Wanao ruhusiwa kwenda Posta na Bajaji au Bodaboda ni wale ambao ni wamiliki binafsi na wanatakiwa wapite njia hizo wakiwa Bila abiria yoyote.
Baadhi ya Bodaboda na Bajaji wakiwa wanangojea Hatma yao baada ya kukamatwa.
Baadhi ya Bodaboda zikiwa zimekamatwa.
Madereva wa Boda Boda na Bajaji wakipata maelezo ya kina ya kwanini wamezuiliwa kwenda Posta wakitokea Mwenge.
Mmoja wa Madereva wa Bodaboda akiwa amekaa kwa mawazo asijue anafanya nini Baada ya Bodaboda yake kukamatwa na Kupelekwa Polisi.(Picha na Dar es salaam yetu).
Oparesheni Nzito ya kuzuia
Bodaboda na Bajaji zisifanye safari zake kutoka Mwenge na maeneo
mengine kuelekea mjini Posta imechukua sura mpya leo baada ya Askari wa
Usalama wa Barabarani kuanza kukamata Bodaboda na Bajaji zote zinazovuka
Mwenge kuelekea Posta, Zoezi hilo ambalo limefanyika Mwenge Mataa
Jijini Dar limeendelea kufanyika na kufamikiwa kuwanasa wengi.
Kwa mujibu wa Msemaji na Muongozaji wa Oparesheni hiyo ambaye hakutaka kutajwa jina lake alisema kwamba wameamua kufanya hivyo ili kuzuia Msongamano wa Magari pamoja na bodaboda pia Bajaji kuelekea Mjini Posta, Aliongeza kuwa kumekuwa na uhalifu sana wa Silaha unaotumiwa na bodaboda hasa maeneo ya mjini hivyo ndio maana wameamua kuzuia.
“Tumefanya hivi ili kuepusha msongamano kuelekea Posta, lakini pia kumekuwa na uhalifu sana unaotumiwa kwa njia ya Bodaboda hivyo tunafanya oparesheni hii ili kupunguza tatizo hili.
Tulicho kifanya tumewaruhusu kufanya safari pembezoni mwa mji tuu hivyo Eneo la Mwenge kwa sasa Limeingia katika zone ya eneo la Mjini,Kama tuliweza kuzuia Daladala ndogo”Hiace” pia na hawa watakuja kuelewa ingawa ni zoezi gumu na linalo hitaji elimu ya ziada ambayo tumesha anza kuwapa na tunaendelea kuwapa” alimalizia kwa kusema “Pia hii ni Oparesheni ya kawaida tuu ya kukamata wale ambao hawana Leseni za kuendesha vyombo hivi pamoja na makosa mbalimbali” alisema Polisi huyo.
Kwa mujibu wa madereva wa Bodaboda na Bajaji wamesema kwamba huo ni uonevu kuwakataza wao wasiweze kwenda Mjini kwani na wao wanatafuta ridhiki yao na wameomba Serikali iwasaidie wapatiwe njia mbadala ya wao kwenda maeneo hayo.
Wanao ruhusiwa kwenda Posta na Bajaji au Bodaboda ni wale ambao ni wamiliki binafsi na wanatakiwa wapite njia hizo wakiwa Bila abiria yoyote.
NHIF YAKUTANA NA WAKUU WA SHULE ZA SEKONDARI MIKOA YA SHINYANGA,SIMIYU NA TABORA.
CHAMA CHA AMCOS NGURUKA KUFANYIWA UPYA UKAGUZI WA HESABU
Na Magreth Magosso,Kigoma
CHAMA cha wakulima wa zao la tumbaku cha Hongera Amcos Kata ya Nguruka wilayani Uvinza Mkoa wa Kigoma, kimetakiwa kifanyiwe upya ukaguzi wa mahesabu,kutokana na sintofahamu ya mwenendo wa viongozi wake kutokuzingatia misingi ya utawala bora,hali inayowakwaza wananchama wa chama hicho.
Kauli hiyo imekuja baada ya Naibu Waziri wa kilimo na chakula Godfrey Zambi kubainika kuwa kuna baadhi ya viongozi wanakitumia chama hicho kwa maslai yao binafsi badala ya kuwakwamua wahusika ili waondokane na umaskini katika familia zao na jamii husika.
Aidha,Waziri huyo aliitaka Ofisi ya Mlajisi Mkuu wa mjini Dododoma,asikilize kero za wananchama wa chama hicho wakiwemo wanachama tisa ambao wamefukuzwa bila kanuni,taratibu na sheria kwa misingi ya kujenga utawala bora ili kujenga usawa na haki kwa kila mwanachama.
CHAMA cha wakulima wa zao la tumbaku cha Hongera Amcos Kata ya Nguruka wilayani Uvinza Mkoa wa Kigoma, kimetakiwa kifanyiwe upya ukaguzi wa mahesabu,kutokana na sintofahamu ya mwenendo wa viongozi wake kutokuzingatia misingi ya utawala bora,hali inayowakwaza wananchama wa chama hicho.
Kauli hiyo imekuja baada ya Naibu Waziri wa kilimo na chakula Godfrey Zambi kubainika kuwa kuna baadhi ya viongozi wanakitumia chama hicho kwa maslai yao binafsi badala ya kuwakwamua wahusika ili waondokane na umaskini katika familia zao na jamii husika.
Aidha,Waziri huyo aliitaka Ofisi ya Mlajisi Mkuu wa mjini Dododoma,asikilize kero za wananchama wa chama hicho wakiwemo wanachama tisa ambao wamefukuzwa bila kanuni,taratibu na sheria kwa misingi ya kujenga utawala bora ili kujenga usawa na haki kwa kila mwanachama.
Kwa nyakati tofauti baadhi ya wanachama wa chama hicho Godfrey
Muhoza na Rose Rutaba walisema viongozi wao wanatumia vibaya nyadhifa
zao kwa wanachama wake,ambapo wakibaini mwanachama anayefuatilia nyendo
na mwenendo wa mapato na matumizi ya chama anaonekana ni muhasi na hivyo
humtoa kwenye chama.
Pia walidai hali ya viongozi kutokujali utawala bora ni chachu ya wakulima wa zao hilo kuwa na maisha duni ili hali wachache wanaishi maisha bora kwa migongo ya wakulima ambao wao wanakuwa daraja la mafanikio ya wakubwa katika vyama vya ushirika,hali inayowakwaza baadhi ya wakulima wasijiunge na vyama hivyo baada ya kuona hujuma ndani yake.
Pia walidai hali ya viongozi kutokujali utawala bora ni chachu ya wakulima wa zao hilo kuwa na maisha duni ili hali wachache wanaishi maisha bora kwa migongo ya wakulima ambao wao wanakuwa daraja la mafanikio ya wakubwa katika vyama vya ushirika,hali inayowakwaza baadhi ya wakulima wasijiunge na vyama hivyo baada ya kuona hujuma ndani yake.
Chama
hicho ni miongoni mwa vyama vyenye utata wa kumaliza changamoto ya
utawala bora na matumizi mazuri ya fedha na hiyo itakuwa
ni tume ya pili kukagua chama hicho baada ya ile ya mkoa wa
kigoma,ilishindwa
kutatua hilo, na kwa mujibu wa Naibu waziri maafisa ushirika wa wilaya
na mkoa
hawatakuwa sehemu ya tume hiyo kwa lengo la kutenda haki kwa lengwa.
Tuesday, April 8, 2014
BENKI YA NBC YAZINDUA HUDUMA YA BIMA YA BURE YA MKOPO JIJINI DAR
Mkuu
wa Idara ya Bima wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Bi. Kemibaro
Omuteku (wa tatu kushoto) akiwa na baadhi ya maofisa wa benki hiyo
wakionyesha vipeperushi ikiwa ni ishara ya kuzindua huduma ya Bima ya
Bure ya Mkopo jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni; Mkuu wa
Idara ya Mikopo, Andrew Lyimo, Meneja Bima ya Maisha, William Mapela na
Mkuu wa Idara ya Mauzo, Mongateko Makongoro.
Mkuu
wa Idara ya Mikopo wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Andrew Lyimo,
(kulia) akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa huduma ya Bima ya Bure
ya Mkopo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Bima wa
NBC, Bi. Kemibaro Omuteku.
MWENYEKITI WA BUNGE MAALUM LA KATIBA SAMWEL SITTA AKUTANA NA VIONGOZI WA DINI
Mhe.
Mufti Sheikh Issa Shaaban Simba akimkaribisha Mwenyekiti wa Bunge
Maalum la Katiba Mhe. Samuel Sitta leo jijini Dar es Salaam wakati
alipomtembelea kumuelezea maendeleo ya vikao vya Bunge linaloendelea
mjini Dodoma.
Mwenyekiti
wa Bunge Maalum la Katiba Mhe. Samuel Sitta (kulia) akiongea na
waandishi wa habari mara baada ya ziara yake katika Ofisi za Bakwata
kuelezea maendeleo ya cikao vya Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma.
Kushoto ni Katibu Mkuu wa Bakwata Suleiman Lolila.(PICHA ZOTE NA BUNGE
MAALUM LA KATIBA).
Na. Benedict Liwenga-Maelezo
MWENYEKITI
wa Bunge maalum la Katiba Samweli Sitta amesema katiba mpya ni kwa
manufaa ya wanachi wote kwa ajili ya kuwaletea maendeleo katika nyanja
mbalimbali.
Hayo
yamesemwa leo jijini Dar es salaam alipokutana na Mhe. Mufti Sheikh
Issa Shaaban Simba katika Ofisi za Bakwata zilizoko Kinondoni jijini
Dar es Salaam ikiwa ni utaratibu aliojiwekea kwa ajili ya kuwashirikisha
Viongozi wa madhehebu na dini ili nao wapate taarifa ya maendeleo ya
bunge la katiba.
Mhe.
Sita amesema kuwa Viongozi wa dini ni watu muhimu sana kwakuwa wanabeba
wafuasi wengi katika jamii na kuwepo kwao kunasaidia katika maendeleo
ya nchi hususani kujenge Amani ya nchi yetu na kuwahamasisha wananchi
kuwa wavumilivu,watulivu,waelewa na wenye kupenda Amani.
Namuomba
Mhe. Mufti pamoja viongozi wengine wa dini waizidi kutuombea ili tuweze
kufikia muafaka katika kupata katiba mpya na bora yenye kuleta
mabadiliko katika nch yetu” Alisema Mhe. Sitta.
Mhe.
Sita Ameongeza kuwa Watanzania wanataka katiba itakayoijenga Taasisi
imara zitakazoweza kusimamia mambo muhimu na kuweza kuondokana na
uhalifu ikiwemo janga la madawa ya kulevya ambalo limekuwa likiisumbua
sana nchii kwa msaada wa sheria mpya janga hili linawezekana
kudhibitiwa.
Pia
amewaomba wajumbe wa kamati kumi na mbili za bunge la katiba,wasome kwa
makiini ibala ya sura ya 1 na ya 6 ambazo ni muhimu sana katika
kuijenga nchi, ili waweze kutoka na mawazo mazuri na yakinifu kwa
manufaa ya nchi na watu wake na kuweza kukuza uchumi na kuleta
maendeleo.
“Katiba
itunge sheria ambazo ni imara zenye kufuata kanuni na taratibu dhabiti
ili kuleta mabadiliko katika kuiongoza nchi na kuweza kuwasaidia
wananchi wake” Alisema Mhe. Sitta.
Aidha,
ameongeza kuwa Bunge hilo maalum linatarajia kuhailishwa mwezi wa nne
tarehe 28 kwa ajili ya kupisha bunge la Bajeti,na kwa kuwa siku 70
hazitoshi kumaliza bunge hilo amemuomba Mheshimiwa Rais Kuwaongezea muda
hivyo wanatarajia kurudi tena mwezi wa nane kuweza kuendelea na
mijadala ya katiba mpya.
Monday, April 7, 2014
WAZIRI NYALANDU AZINDUA MAJENGO YA CHUO CHA MUSOMA UTALII TABORA
Waziri wa Maliasili na Utalii Bw.Lazaro Nyalandu akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa Majengo ya Chuo cha Musoma Utalii Tabora wakati wa mahafali ya kumi ya Chuo hicho. |
Waziri Nyalandu akiweka jiwe la msingi katika Chuo cha Musoma Utalii mkoani Tabora,Kulia ni Mkurugenzi wa Chuo hicho Bw.Shabani Mrutu. |
Waziri Nyalandu akipatiwa maelezo ya malengo ya uanzishwaji wa Chuo cha Musoma Utalii Tabora kutoka kwa Mkurugenzi wa Chuo hicho Bw.Shabani Mrutu ofisi kwake. |
Waziri wa maliasili na Utalii Bw.Lazaro Nyalandu akiwasalimia baadhi ya wahitimu wa kozi mbalimbali wakati wa mahafali ya kumi ya chuo cha Musoma Utalii Tabora. |
Mkurugenzi wa Chuo cha Musoma Utalii Bw.Shaban Mrutu akisoma taarifa fupi ya Chuo kwa mgeni rasmi wakati wa mahafali ya kumi ya chuo hicho. |
Mmoja wa wahitimu wa Chuo cha Musoma Utalii akimpa mkono mgeni rasmi Waziri Nyalandu wakati wa mahafali hayo ya kumi. |
Waziri wa maliasili ya Utalii Bw.Lazaro Nyalandu akiwa na mwenyeji wake Mkurugenzi wa Chuo cha Musoma Utalii Tabora Bw.Shaban Mrutu. |
Jengo la Utawala Chuo cha Musoma Utalii Tabora ambalo ni miongoni mwa majengo yaliyozinduliwa na Waziri wa maliasili na Utalii Bw.Lazaro Nyalandu wakati wa mahafali ya kumi ya chuo hicho. |
JAPAN YATOA MSAADA WA MAGARI KWA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima (kulia) na Balozi
wa Japan nchini, Masaki Okada wakikata utepe ikiwa ishara ya
makabidhiano ya magari matano yaliyotolewa na Serikali ya Japan kwa
ajili ya kusaidia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini. Magari hayo
yamekabidhiwa katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto Kanda ya Ilala,
jijini Dar es Salaam.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima akiiwasha moja ya
magari matano yaliyotolewa na Serikali ya Japan kwa Jeshi la Zimamoto na
Uokoaji. Magari hayo matano yalitolewa na Balozi wa Japan nchini,
Masaki Okada wakati wa tafrija fupi ya makabidhiano ya magari hayo
yaliyofanyika katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto Kanda ya Ilala,
jijini Dar es Salaam.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima akitoa hotuba fupi
ya kuishukuru Serikali ya Japan kwa kuisadia wizara yake kupitia Jeshi
la Zimamoto na Uokoaji magari matano kwa ajili ya kazi ya kuzima moto na
uokoaji nchini. Kushoto ni Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada ambaye
alikabidhi magari hayo kwa niaba ya Serikali yake. Kulia ni Mkuu wa
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Kamishna Jenerali Pius Makuru Nyambacha.
makabidhiano ya magari hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Kituo cha
Zimamoto Kanda ya Ilala, jijini Dar es Salaam.
Mkuu
wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Kamishna Jenerali Pius Makuru
Nyambacha akitoa hotuba fupi ya kumkaribisha mgeni rasmi ambaye ni Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima (katikati) ili
aweze kuzungumza na baadaye kukabidhiwa magari matano ya kuzima motona
uokoaji. Magari hayo yametolewa na Serikali ya Japan kupitia balozi wake
nchini, Masaki Okada (kushoto) katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto
Kanda ya Ilala, jijini Dar es Salaam.
Sehemu
ya magari matano yaliyokabidhiwa na Balozi wa Japan, Masaki Okada kwa
niaba ya Serikali yake. Magari hayo matano yaliyotolewa kwa Jeshi la
Zimamoto na Uokoaji yalipokelewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya
Nchi, Pereira Ame Silima katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto Kanda ya
Ilala, jijini Dar es Salaam. (Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi).
KANISA LA T.A.G TABORA WASHEHEREKEA MIAKA 75
Maandamano ya maadhimisho ya miaka 75 ya Kanisa la TAG nchini ambayo yamefanyika mjini Tabora kuanzia uwanja wa Ally Hassan Mwinyi hadi kanisa la TAG jirani na hospitali ya mkoa wa Tabora Kitete. |
Baadhi ya waumini walioshiriki maandamano hayo ya amani wakisheherekea maadhimisho hayo mjini Tabora. |
Maandamano ya maadhimisho ya miaka 75 yalipewa ulinzi wa kutosha na Jeshi la Polisi ambapo usalama ulikuwa wa kuridhisha. |
Friday, April 4, 2014
KANISA KATOLIKI JIMBO KUU TABORA LADAIWA KUTAKA KULIPULIWA!!!
Thursday, April 3, 2014
WAVUVI KUVAMIA BUNGE LA RASIMU YA KATIBA-KIGOMA
Na Magreth Magosso,Kigoma
CHAMA Cha Wavuvi Mwalo wa Kibirizi Manispaa ya Kigoma Ujiji,watishia kwenda
mkoani Dodoma kwenye Bunge Maalumu la
Mchakato wa rasimu ya pili ya Katiba,kwa kile wanachodai kutaka kujua
sintofahamu ya wizi wa mashine za mitumbwi sanjari na kutekwa kwa wavuvi katika
Ziwa Tanganyika.
Akifafanua hilo Salum Shaban Kiongozi wa Wavuvi pia Miongoni
mwa tume maalum iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa Lt. Issa Machibya hivi karibuni iliyokwenda
DRC-Congo kwa lengo la kurudi na mashine
18 zilizoibwa eneo la mwalo wa
katonga na kibirizi Machi,3,2014,kugonga mwamba, ndio chachu ya kufika bungeni ili kupeleka kilio chao.
Hali hiyo ya sintofahamu ya kuvamiwa kwa wavuvi na mali zao inatokana na serikali ya
DRC-Congo kukaidi Mkataba wa Ujirani
mwema waliowekeana mwaka jana kuwa ,`mali ya wizi dhidi ya kigoma naWilaya ya
kaleme zirudishwe bila masharti magumu endapo mali zitathibitika zimetoka kati
ya wilaya hizo’.
Shabani alisema, mkataba
huo una maslai ya kulinda ujirani mwema sambamba na kuweka mkakati wa kubaini
majambazi yanayozidi kuwateka wavuvi toka wilaya ya kigoma ambapo wengi
wanaotuhumiwa na vitendo hivyo ni raia wa DRC-congo baada ya kubaini mashine
zao zipo mikononi mwa serikali hiyo sanjari na kuwatia nguvuni wahalifu husika.
“Tumegundua wenzetu hawako vyema na mfumo wa sheria zaidi ya
kutumia ubabe haiwezekani anawatarifu zana zipo lakini tulipofika anabadilika
hali iliyotufanya tukae kule zaidi ya siku tano cha kushangaza hili suala hata
WaziriMkuu anajua akadai muhusika wa wizara hayupo nchini”
“kumbuka wilaya ya kigoma na Uvinza mapato yao makubwa ni
masoko ya samaki ambayo yote ukanda wa ziwa Tanganyika,ulinzi duni ziwani ,sheria haing`ati ,ajira zinapungua kwa
vijana,hatari 2020 soko za samaki kutoweka” alibainisha Shabani.
Kwa upande wa Mwenyekiti wa wavuvi Ramadha Kanyongo na Kaimu
wake Sendwe Ibrahim alisema zao la samaki ni uchumi wa kigoma mjini na uvinza
ambapo kwa mwalo wa kibirizi halmashauri
ya kigoma ujiji inakusanya milioni11,kwa mwezi,katonga M. 8 ambapo kwa wilaya ya kigoma vijijini soko la
muyobozi m.5 na kagongo M.2, wilaya ya
Uvinza soko la samaki Buhingu million 6.
Aliongeza kwa kusema serikali ikishindwa kudhibniti 2020
uchumi wa halmashauri hizo zipo mashakani kutokana na wadu wa uvuvi kushindwa
kusonga mbele kwenye kazi hiyo kutokana na gharama kubwa ya mashine ya boti
ambapo mashine moja si chini ya milioni 5 mpya ,iliyotumika milioni 3.5.
Akijibu hoja ya raia wa DRC-congo kujikita na wizi wa
mashine kwa wavuvi wa kigoma,Balozi ndogo ya nchi hiyo Ricky Molema akiri Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Lt.Machibya anahaja ya
kusaidia wananchi wake sanjari na wavuvi kushuka kiuchumi na kupotea kwa ajira
ya vijana.
Molema alibainisha kuwa,viongozi wa juu wa Nchi
husika,wanawajibu wa kuwa na moyo wa dhati kuondoa changamoto ya wavuvi na mali
zao ziwe salama, ili jamii husika zisibadili mwelekeo wa kuishi kwa leo na siku
za usoni na kushauri kuwepo na doria ya pamoja ziwani ili kuthibiti uhalifu.
Hivyo kutokana na madhira hayo wanajipanga kwenda Bungeni
ili wakaonane na waziri mwenye dhamana na Uvuvi na Mifugo sanjari na Wabunge wa
Mkoa wa Kigoma ili wajue hatma ya hilo.
Aidha mtandao huu mebaini kuwa mwaka 2003 mwalo wa
kibirizi ulikuwa na mitumbwi yenye mashine 160 ambapo kwa sasa imebaki mitumbwi
45,katonga walikuwa na vipe 200 na sasa 168 ,Mtandao huu naamini dhati ya
viongozi itathubutu kuongeza ulinzi katika Ziwa Tanganyika kwa kuboresha
uhitaji wake.
Tuesday, April 1, 2014
TABORA HALI SI SHWARI,MAJAMBAZI HUVAMIA KWA BUNDUKI KILA SIKU USIKU.
MAHAFALI YA 18 CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA TABORA NA SINGIDA
Mgeni Rasmi akikabidhi zawadi mbalimbali kwa wahitimu waliofanya vizuri katika vitengo vyao.
Maandamano kuelekea ukumbini yakiongozwa na mgeni rasmi Mh. Celina Kombani aliyevaa Joho jekundu.
Viongozi ngazi za juu Chuo cha Utumishi wa Umma nchini
Mtendaji mkuu Chuo cha Utumishi wa Umma TPSC nchini Bw.Said Nassor akizungumza mikakati endelevu ya Chuo hicho wakati wa mahafali hayo.