Pages

KAPIPI TV

Saturday, April 12, 2014

DALADALA KIGOMA WAFANYA MGOMO

kamanda wa polisi Frasser Kashai akiwapoza madereva na konda wa vyombo vya usafiri kigomawakiwa kwenye ofisi za sumatra wasikilize maelekezo aliyopewa na mkuu wa mkoa Lt.mstaafu Issa Machibya pembeni ni Katibu tawala wa wilaya ya kigoma Joshua Elisha na aliyevaa flana nyeupe ni meneja wa sumatra picha na Magreth Magosso).
Na Magreth Magosso,Kigoma

WAKAZI wa Manispaa ya Kigoma Ujiji,wamelazimika kutembea kwa miguu kutokana na mgomo wa vyombo vya usafiri   kwa kile kinachodaiwa hawana sare mpya kwa mujibu wa Mamlaka ya usimamizi wa usafiri vyombo vya moto nchi kavu na majini (SUMATRA).
 
Hali hiyo imekuja baada ya SUMATRA kukamata zaidi ya daladala 20 ambazo zinatoa huduma kwa wakazi wa manispaa hiyo kwa dai la kutokuwa na sare husika wakati wana risiti ya sare hizo ambazo bado hawajakabidhiwa na mzabuni wa kushona sare hizo hali iliyowalazimu kugoma kutoa huduma kwa umma ili kero hiyo ifanyiwe marekebisho.
 
Kwa upande wa Naibu Katibu wa umoja wa wamiliki wa magari  kigoma (KIBOA)Hussein Kaliango alisema,mamlaka imetoa wiki mbili  kwa mwenye  daladala awe na sare hizo hali inayokwaza  mchakato huo kutokana na muda mfupi na wingi wa wateja.
 
Kwa nyakati tofauti madereva wa daladala Kalenga Kasaka na Rashid Juma walisema wanatozwa kiasi cha shilingi laki mbili na nusu endapo hauna sare hizo sanjari na kukamata gari,hata kama wakionyesha risiti ambazo tayari wamelipia sare hizo.
 
Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Kamanda  wa hapa Frasser Kashai alisema  hana mpango wa kutumia mabomu ya machozi kwa madereva na makonda ambao wapo katika mgomo huo,huku akiwataka wawakilishi watatu toka kwa walengwa waende kwa katibu tawala wa mkoa ili kuboresha mgomo huo.
 
 Meneja wa SUMATRA kigoma Adamu Mamilo alipoulizwa juu ya hilo alisema awali walikaa kikao na wadau wa vyombo vya usafiri juu ya sare mpya ziwe kamili mwanzoni mwa mwezi huu na kuingia ndani ya gari la kamanda wa polisi akidai wanaenda kwa katibu tawala kumaliza hilo.
 
Baadhi ya abiria Mawazo Mikidadi na Kamongo Sibonja walisema hali hiyo inathiri shughuri za uzalishaji mali,kutokana na wananchi kushindwa kufika maeneo yao ya kazi kwa wakati muafaka,huku wakishauri wadau wakae pamoja kumaliza adha hiyo.

No comments: