Pages

KAPIPI TV

Monday, April 7, 2014

JAPAN YATOA MSAADA WA MAGARI KWA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI.

PIX 2
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima (kulia) na Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada wakikata utepe ikiwa ishara ya makabidhiano ya magari matano yaliyotolewa na Serikali ya Japan kwa ajili ya kusaidia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini. Magari hayo yamekabidhiwa katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto Kanda ya Ilala, jijini Dar es Salaam. 
PIX 3
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima akiiwasha moja ya magari matano yaliyotolewa na Serikali ya Japan kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji. Magari hayo matano yalitolewa na Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada wakati wa tafrija fupi ya makabidhiano ya magari hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto Kanda ya Ilala, jijini Dar es Salaam. 
PIX 4
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima akitoa hotuba fupi ya kuishukuru Serikali ya Japan kwa kuisadia wizara yake kupitia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji magari matano kwa ajili ya kazi ya kuzima moto na uokoaji nchini. Kushoto ni Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada ambaye alikabidhi magari hayo kwa niaba ya Serikali yake. Kulia ni Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Kamishna Jenerali Pius Makuru Nyambacha. makabidhiano ya magari hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto Kanda ya Ilala, jijini Dar es Salaam.
PIX 5
Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Kamishna Jenerali Pius Makuru Nyambacha akitoa hotuba fupi ya kumkaribisha mgeni rasmi ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima (katikati) ili aweze kuzungumza na baadaye kukabidhiwa magari matano ya kuzima motona uokoaji. Magari hayo yametolewa na Serikali ya Japan kupitia balozi wake nchini, Masaki Okada (kushoto) katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto Kanda ya Ilala, jijini Dar es Salaam.
PIX 6
Sehemu ya magari matano yaliyokabidhiwa na Balozi wa Japan, Masaki Okada kwa niaba ya Serikali yake. Magari hayo matano yaliyotolewa kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji yalipokelewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto Kanda ya Ilala, jijini Dar es Salaam. (Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).

No comments: