Pages

KAPIPI TV

Monday, September 29, 2014

WAMILIKI WA DALADALA KUITUNISHIA MISULI SERIKALI KIGOMA

Na Magreth Magosso,Kigoma

Wafanyabiashara  wa mabasi ya kusafirisha abiria aina ya Hiace katika manispaa ya kigoma ujiji wilaya ya kigoma Mkoa wa Kigoma ,wapo hatarini kufutiwa leseni kutokana na  kukataa uwepo wa mfumo wa soko  huria  na kutaka kuipangia sheria serikali.

Uamuzi huo unakuja siku chache tu baada ya uongozi wa serikali ya wilaya ,kwa kushirikiana na manispaa husika kutoa onyo kwa wafanyabiashara wasiokubali kufuata sheria,kanuni na taratibu wa uwepo wa aina zingine za usafirishaji wa abiria.

Wafanyabiashara hao waliamua kufanya majarabio la mgomo  zaidi ya mara mbili baada  ya kugundua uwepo wa vibajaji na michomoko inachangia pato finyu ambapo katika ulipaji wa mapato  katika mamlaka husika hawalingani .
 
Hayo yalibainika kigoma ujiji juzi  katika taarifa ya utekelezwaji wa miradi mbalimbali ya jamii katika ziara ya kamati ya siasa ya mkoa ,iliyokuwa ikiongozwa na mwenyekiti wa ccm kigoma Dkt. Aman Kabourou  .
 
Alisema mgomo wa mara kwa mara kwa wafanyabiashara hao dhidi ya magari aina ya michomoko na Bajaji imekuwa kero isiyo na mashiko kwa wakazi na serikali husika na kuwataka waongeze ubunifu wa huduma kwa walaji.

“tume maalum  zimeundwa katika kila aina ya usafiri na idara husika ili kila mmoja akae na watu wake wajadili adha na mkakati  wa uwajibikaji na akaetengua kanuni na taratibu kukiona” alisema Maneno.
 
Kwa upande wa Mwenyekiti  ccm Dkt.Kabourou  alisema adha ya migomo ya mabasi  inadhulumu  haki za wadau wengine wa usafiri na kudumaza maendeleo ya jamii kwa kuzuia ajira binafsi kwa vijana.
 
Alisema  anaunga hoja ya kufungiwa leseni kwa wale watakaobanika ni chanzo cha kudumaza sera ya biashara ya ushindani  ambapo kwa  wakazi wa vijijini wanatumia gari za michomoko katika shughuli za biashara na kusihi wasiwe juu ya sheria.
 
Aliongeza kwa kusema wenye mabasi ya abiria waongeze wigo wa kupeleka huduma katika maeneo yaliyo pembezoni mwa kigoma ujiji na kuwataka waachane na kasumba ya kuwaweka abiria kwa  muda mrefu kituoni hali inayochangia  wakimbiwe na abiria.

 Kwa upande wa Katibu wa Itikadi na uenezi ccm Kalembe Masudi alisema changamoto ipo katika ulipaji wa kodi,sheria ya ukomo wa abiria na vituo ambapo kwa upande wa michomoko na bajaji zinapakia abiria mahali popote ilihali hiace ikifanya hivyo hulipishwa faini.
 
Ashauri kupitia kamati teule washirikiane kuondoa tofauti  na kila mmoja aridhie uwepo wa mwenzake na kutambua serikali imeridhia mfumo wa biashara  na kusihi wawe  wabunifu na kukidhi hitaji  la abiria.

MISA TAN YAADHIMISHA SIKU YA KUPATA TAARIFA KIMATAIFA

Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege (kushoto) akiwakaribisha wageni waalikwa na waandishi wa habari waliofika kweye mkutano wao uliofanyika Jana kwenye ofisi za MISA Tanzania  zilizopo jijini Dar es Salaam kulia ni  Mkurugenzi msaidi wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Andrew.
Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Jana imekutana na waandishi wa habari na wadau tofauti katika kuadhimisha Siku ya haki ya kupata taarifa kimataifa amabayo huadhimishwa kila mwaka Septemba 28.09.2014 katika ofisi zao zilizopo kinondoni Mkwajuni Jijini Dar es salaam.
 Mkurugenzi msaidi wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Andrew Marawiti (kulia) akizungumza jambo mbele ya waandishi wa habari(hawapo pichani) kwenye siku ya kimataifa ya haki za kupata taarifa zinazoadhmishwa septemba 28 kwa kila mwaka.
 Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege  (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wagene waalikwa (hawapo pichani) kwenye siku ya kimataifa ya haki za kupata taarifa zinazoadhmishwa septemba 28 kwa kila mwaka. kwenye ofisi za MISA Tanzania  zilizopo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege (kushoto) akikata utepe wakati wa uzinduzi rasmi wa chapicho la ripoti ya matumizi bora ya utoaji wa habari katika sekta za umma hapa nchini.
 Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege akiwaonesha waandishi wa habari pamoja na wageni waalikwa kitabu cha ripoti ya haki ya kupata taarifa halali katika sekta za umma.
  Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege akitangaza taasisi iliyochukua tuzo ya Kofuli la Dhahabu kwa kubana sana taarifa kwa mwaka 2014.
  Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege akionesha tuzo ya Kufuli la Dhahabu kwa kubana sana taarifa kwa mwaka 2014 iliyokwenda kwenye Idara ya Mahakama.
   Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege akitangaza taasisi iliyochukua tuzo ya Ufunguo wa Dhahabu kwa mwaka 2014 kwa kutoa taarifa bila kificho kwa mwaka 2014
 Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege (kulia) akimkabidhi tuzo ya Ufunguo wa Dhahabu Kaimu Mkurugenzi wa Shighuli za Takiwimu ofisi ya Taifa ya Takimu Bi. Aldegunda Komba(kushoto) kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya haki ya kupata taarifa jana jijini Dar es Salaam
 Kaimu Mkurugenzi wa Shighuli za Takiwimu ofisi ya Taifa ya Takimu Bi. Aldegunda Komba akionesha tuzo hiyo kwa waandishi wa habari pamoja na wageni waalikwa waliofika kwenye ofisi za Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) zilizopo eneo la Mkwajuni, Kinondoni jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Mkurugenzi wa Shighuli za Takiwimu ofisi ya Taifa ya Takimu Bi. Aldegunda Komba akizungumza na vyombo vya habari baada ya taasisi yaokutwaa tuzo ya Ufungu wa Dhahabu.
 Afisa utafiti na maelezo wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Sengiyumva Gasirigwa akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kwenye siku ya kimataifa ya haki ya kupata taarifa ambayo uadhimishwa septemba 28 kwa kila mwaka.
 Baadhi ya wageni waalikwa pamoja na waandhishi wa habari wakifuatilia shughuli zima iliyokuwa inaendelea kwenye ofisi za Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) zilizopo jijini Dar es Salaam.
Siku Ya Kimataifa Ya Haki Ya Kupata Taarifa 
TANZANIA_Most Open and Most Secret Survey(1) 

Sunday, September 28, 2014

BODABODA WATEMBELEA WAGONJWA HOSPITALINI NA KUTOA MISAADA -TABORA

Baadhi ya wanachama wa chama cha Waendesha Bodaboda mkoa wa Tabora ambao walitembelea hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete kuona wagonjwa na kufanya usafi wa mazingira ambapo tukio hilo lilikwenda sambamba na kutoa misaada kwa wagonjwa ikiwemo Sabuni,vyandarua na vinywaji kama Juisi katika Wadi ya kulaza watoto kinamama wajawazito.
Mwenyekiti wa Chama cha Waendesha Bodaboda Bw.Waziri Kipusi(mwenye shati ya draft)akikabidhi msaada wa vyandarua kwa mmoja kati ya wakunga katika Wadi ya kinamama wajawazito.
Mwenyekiti wa waendesha Bodaboda Waziri Kipusi alikabidhi vyandarua kwa kinamama waliojifungua watoto ambao hawajatimiza muda wa kuzaliwa(NJITI)
Katibu wa Waendesha Bodaboda Kassim Kiduli akikabidhi msaada wa sabuni kwa akinamama waliojifungua huku akitoa nasaha fupi zilizowafanya kinamama hawa kuangua kicheko kwa furaha.
Waziri Kipusi akimpatia juisi mmoja kati ya watoto wagonjwa

Mmoja kati ya Waendesha Bodaboda Bi.Zay Mchemba akihojiwa na waandishi wa habari wa habari namna ambavyo anashiriki katika kazi hiyo ya Bodaboda.





WIZARA YA AFYA ZANZIBAR YAPOKE MSAADA WA AMBULANCE TOKA (UNFPA).

01[2]Waziri wa Afya Rashid  Seif Suleiman akionyesha moja ya funguo za gari ya Ambulance zilizotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya watu (UNFPA), alieshikana mkono ni Mwakilishi wa Shirika hilo Dkt. Natalia Kanem.02[3]Waziri Rashid Seif  wakati akilijaribu moja ya gari hilo zilizotolewa na UNFPA katika hafla ilizofanyika  Wizara ya Afya Mnazimmoja Mjini Zanzibar.03[1]Gari  nne za  Ambulance zilizotolewa na Shirika la UNFPA zikiwa zimeegeshwa mbele ya Ofisi ya Wizara ya Afya Mnazimmoja.04[1]Waziri wa Afya Rashid Seif akizungumza na watendaji wa Wizara yake na wageni waalikwa waliohudhuria sherehe za kukabidhiwa msaada wa gari za ambulance uliotolewa na UNFPA.( Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).

Na RAMADHANI ALI /HABARI MAELEZO ZANZIBAR                      
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu (UNFPA) limekabidhi  msaada wa magari manne ya Ambulance  kwa Wizara ya Afya ya Zanzibar ambayo yatatumika katika Hospitali nne.

Mwakilishi wa UNFPA Tanzania  Dkt. Natalia Kanem alimkabidhi Waziri wa Afya Rashid Seif Suleiman magari hayo katika sherehe zilizofanyika   Wizarani Mnazimmoja.

Dkt. Natalia alitaka  magari hayo yatumike kwa uangalifu ili  kufikia malengo ya millennia  ya kupunguza idadi ya vifo vya mama wajawazito na watoto wanaozaliwa hasa katika maeneo ya vijijini.

Alisema moja ya sababu inayopelekea vifo vya mama wajawazito na watoto wachanga ni tatizo la usafiri ambalo linachangiwa na uwezo mdogo wa baadhi ya familia hasa katika maeneo ya vijijini.

Aliongeza kuwa  msaada huo ni  sehemu ya Mpango maalum wa Shirika la Umoja wa  Mataifa  ulioanza  mwaka 2011 na kumalizika Juni 2015  ambao  huenda ukaendelea hadi mwaka 2016 kusadia  masuala ya Afya na Lishe.

Amesema  mpango huo wa miaka minne  ambao unahusisha maeneo  makuu saba unaendeshwa kwa pamoja na Mashirika manne ya Umoja wa Mataifa  ambayo ni WHO, UNFPA, UNICEF na WFPA.

Mwakilishi huyo wa UNFPA amewapongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Jakaya Mrisho Kkwete na Rais wa Zanzibar Dkt Ali Muhamed Sheina kwa juhudi kubwa wanazochukua katika kuimarisha huduma za  mama wajawazito na watoto wachanga.

Aliesema UN inathamini juhudi hizo na  juhudi za kuimarisha uchumi hivyo aliahidi  kuwa wataendelea  kuunga mkono kuhakikisha mama wajawazito na watoto wanaozaliwa wanaendelea kuishi katika mazingira yaliyo  salama.

Waziri wa Afya  Rashid Seif Suleiman, alilishukuru Shirika la UNFPA kwa misaada mbali mbali inayotoa kwa Wizara hiyo  na ameahidi kuwa magari hayo yatatumika katika malengo yaliyokusudiwa.

Amekiri kuwa tatizo la usafiri kwa  mama wajawazito Zanzibar limekuwa likiwasumbua wananchi wengi na inafikia wakati akinamama hujifungua wakiwa kwenye gari  wakati wa kupelekwa Hospitali ambazo hazina stara wala hazifai kwa kazi hiyo.

Alieleza matarajio  yake kuwa tatizo hilo kwa sasa litapungua kwa kiasi kikubwa baada ya kupatiwa msaada huo ambao umekuja wakati muwafaka ambapo Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaelekeza juhudi zake kuimarisha  huduma za afya mijini na vijijini.Gari hazo za ambulance ambazo zitapelekwa katika Hospitali ya Kivunge, Mwembeladu, Mkoani na Micheweni zimegharimu shilingi milioni 245,000,000 za kitanzania.

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA AANZA ZIARA WILAYANI LUSHOTO

01Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili katika kitongoji cha Kwesimu wakati alipokitembelea kikundi cha kuhifadhi Mazingira katika eneo hilo ambapo ameshiriki kazi za mikono za kuotesha miche katika kikundi hicho, Kinana leo ameanza ziara ya kikazi wilayani Lushoto akikagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 na kuhimiza wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo, akiwa ameongoza na na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi katikati na kulia ni Mh. Henry Shekifu Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-LUSHOTO-TANGA) 
 1 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kwa vitendo katika kazi ya kuotesha miche ya miti wakati alipokitembelea na kukagua shughuli za kikundi cha kutunza Mazingira cha Kwesimu wilayani Lushoto. 3Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi akipiga gitaa huku akiimba kabla ya kunaza kwa kikao cha ndani cha halmashauri ya wilaya ya Lushoto.6Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Lushoto 9Baadhi ya wajumbe wakiwa katika mkutano huo.4Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika ujenzi wa ofisi ya CCM tawi la Jegestal mjini Lushoto. 7Baadhi ya miche ambayo imeoteshwa na kikundi cha kutunza mazingira cha Kwesimu mjini wilayani Lushoto.5Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwapungia wananchi mkono mara baada ya kuwasili katika kata ya Mlola ambapo amewahutubia wananchi. 8Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika mkutano huo. 10 11Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika mkutano huo. 12Mbunge wa jimbo la Korogwe vijijini Mh. Steven Ngonyani akiwahutubia wananchi wa Mlola wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata hiyo leo 13Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi akiwahutubia wananchi wa Mlola wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata hiyo leo 14Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo wakati akiwahutubia wananchi wa Mlola wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata hiyo leo 15Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa Mlola wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata hiyo leo 17Mkuu wa wilaya ya Lushoto Mhe. Majid Hemed Mwanga akifafanua jambo kwa wananchi mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati wa kipindi cha maswali na majibu kwa wananchi. 18Mmoja wa akina mama waliofika kwenye mkutano huo akiuliza swali kuhusu mambo ya afya.

Saturday, September 27, 2014

"WAJAWAZITO WALAZWA WAWILI,WATATU KWENYE KITANDA KIMOJA HOSPITALI YA RUFAA KITETE,HOFU YA MAGONJWA YA MLIPUKO"-TABORA

Baadhi ya akina mama wajawazito ambao wamelazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete wakisubiri kujifungua,katika kitanda kimoja chenye upana wa futi mbili na nusu wanalazimika kulala akina mama wawili hadi watatu kutokana na ufinyu wa nafasi na upungufu wa vitanda.
Kulazwa kwa kinamama hawa bado inatajwa kuwa ni hatari kiafya endapo itajitokeza mlipuko wa magonjwa.


MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA KIVUKO CHA MV TEGEMEO KUFANYA SAFARI ZA MAISOME-SENGEREMA.

1.[1]Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuzindua rsmi Kivuko cha Tegemeo tayari kuanza kufanya safari zake kati ya Kisiwa cha Maisome- Sengerema, wakati wa hafla ya uzinduzi wa kivuko hicho iliyofanyika Kijiji cha Kahunda Wilaya ya Sengerema Mkoa wa Mwanza leo, Septemba 26, 2014. Kulia kwake ni Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli na baadhi ya viongozi. Picha na OMR 2.[1]Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akibonyeza Kitufye kuashiria uzinduzi  rasmi wa Kivuko cha Tegemeo tayari kuanza kufanya safari zake kati ya Kisiwa cha Maisome- Sengerema, wakati wa hafla ya uzinduzi wa kivuko hicho iliyofanyika Kijiji cha Kahunda Wilaya ya Sengerema Mkoa wa Mwanza leo, Septemba 26, 2014. Kuhoto  kwake ni Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli na baadhi ya viongozi. Picha na OMR3.[1]
4.[1]Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala Ufundi wa Umeme-TEMESA, Eng. Mseline Magesa, wakati alipokuwa akikagua Kivuko cha Tegemeo baada ya kukizindua rasmi leo Septemba 26, 2014 kwa ajili ya kuanza kazi ya kusafirisha abiria na mizigo kati ya Kisiwa cha Maisome- Sengerema, wakati wa hafla ya uzinduzi wa kivuko hicho iliyofanyika Kijiji cha Kahunda Wilaya ya Sengerema Mkoa wa Mwanza. Picha na OMR5[2]Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na baadhi ya viongozi wakati akikagua Kivuko hicho. Picha na OMR
6.[1]Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wananchi wa Kahunda Wilaya ya Sengerema, wakati wa hafla ya uzinduzi wa kivuko hicho iliyofanyika leo, Septemba 26, 2014. Picha na OMR7[2]Picha ya pamoja