Waziri
wa Afya Rashid Seif Suleiman akionyesha moja ya funguo za gari ya
Ambulance zilizotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya watu
(UNFPA), alieshikana mkono ni Mwakilishi wa Shirika hilo Dkt. Natalia
Kanem.Waziri
Rashid Seif wakati akilijaribu moja ya gari hilo zilizotolewa na UNFPA
katika hafla ilizofanyika Wizara ya Afya Mnazimmoja Mjini Zanzibar.Gari nne za Ambulance zilizotolewa na Shirika la UNFPA zikiwa zimeegeshwa mbele ya Ofisi ya Wizara ya Afya Mnazimmoja.Waziri
wa Afya Rashid Seif akizungumza na watendaji wa Wizara yake na wageni
waalikwa waliohudhuria sherehe za kukabidhiwa msaada wa gari za
ambulance uliotolewa na UNFPA.( Picha na Makame Mshenga-Maelezo
Zanzibar).
Na RAMADHANI ALI /HABARI MAELEZO ZANZIBAR
Shirika la Umoja wa Mataifa
linaloshughulikia Idadi ya watu (UNFPA) limekabidhi msaada wa magari
manne ya Ambulance kwa Wizara ya Afya ya Zanzibar ambayo yatatumika
katika Hospitali nne.
Mwakilishi wa UNFPA Tanzania Dkt.
Natalia Kanem alimkabidhi Waziri wa Afya Rashid Seif Suleiman magari
hayo katika sherehe zilizofanyika Wizarani Mnazimmoja.
Dkt. Natalia alitaka magari hayo
yatumike kwa uangalifu ili kufikia malengo ya millennia ya kupunguza
idadi ya vifo vya mama wajawazito na watoto wanaozaliwa hasa katika
maeneo ya vijijini.
Alisema moja ya sababu
inayopelekea vifo vya mama wajawazito na watoto wachanga ni tatizo la
usafiri ambalo linachangiwa na uwezo mdogo wa baadhi ya familia hasa
katika maeneo ya vijijini.
Aliongeza kuwa msaada huo ni
sehemu ya Mpango maalum wa Shirika la Umoja wa Mataifa ulioanza mwaka
2011 na kumalizika Juni 2015 ambao huenda ukaendelea hadi mwaka 2016
kusadia masuala ya Afya na Lishe.
Amesema mpango huo wa miaka minne
ambao unahusisha maeneo makuu saba unaendeshwa kwa pamoja na
Mashirika manne ya Umoja wa Mataifa ambayo ni WHO, UNFPA, UNICEF na
WFPA.
Mwakilishi huyo wa UNFPA
amewapongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho
Kkwete na Rais wa Zanzibar Dkt Ali Muhamed Sheina kwa juhudi kubwa
wanazochukua katika kuimarisha huduma za mama wajawazito na watoto
wachanga.
Aliesema UN inathamini juhudi hizo
na juhudi za kuimarisha uchumi hivyo aliahidi kuwa wataendelea
kuunga mkono kuhakikisha mama wajawazito na watoto wanaozaliwa
wanaendelea kuishi katika mazingira yaliyo salama.
Waziri wa Afya Rashid Seif
Suleiman, alilishukuru Shirika la UNFPA kwa misaada mbali mbali inayotoa
kwa Wizara hiyo na ameahidi kuwa magari hayo yatatumika katika malengo
yaliyokusudiwa.
Amekiri kuwa tatizo la usafiri
kwa mama wajawazito Zanzibar limekuwa likiwasumbua wananchi wengi na
inafikia wakati akinamama hujifungua wakiwa kwenye gari wakati wa
kupelekwa Hospitali ambazo hazina stara wala hazifai kwa kazi hiyo.
Alieleza matarajio yake kuwa
tatizo hilo kwa sasa litapungua kwa kiasi kikubwa baada ya kupatiwa
msaada huo ambao umekuja wakati muwafaka ambapo Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar inaelekeza juhudi zake kuimarisha huduma za afya mijini na
vijijini.Gari hazo za ambulance ambazo zitapelekwa katika Hospitali ya
Kivunge, Mwembeladu, Mkoani na Micheweni zimegharimu shilingi milioni
245,000,000 za kitanzania.
No comments:
Post a Comment