Pages

KAPIPI TV

Tuesday, July 28, 2015

LOWASSA AKABIDHIWA RASMI KADI YA CHADEMA


MMGL0885
Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema,Freeman Mbowe akimkabidhi kadi ya uanachama wa chama hicho, Mh.Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa leo katika hoteli ya Bahari Beach jijini Dar es Salaam.
MMGL0688
 Waziri Mkuu Mstaafu,Edward Lowassa akizungumza na mamia wakati wa kutangaza adhima yake ya kujiunga na Chadema katika Hoteli ya Bahari Beach jijini Dar es Salaam.
MMGL0816
 Waziri Mkuu Mstaafu,Edward Lowassa akijibu maswali ya waandishi wa habari juu ya kujunga kwake katika Hoteli ya Bahari Beach leo jijini Dar es Salaam.
Picha zaidi ingia Michuziblog

WAGOMBEA UBUNGE NDANI YA CCM WAENDELEA KUJINADI KWENYE KATA,WANANCHI WACHAMBUA MBIVU NA MBICHI

Emmanuel Mwakasaka akijinadi mbele ya wakazi wa kata ya Kiloleni ambapo aliwataka wamchague ili aweze kushirikiana nao katika kuleta maendeleo,katika mazungumzo yake wakati wa kujinadi aliepuka ahadi za uongo katika kutekeleza majukumu yake ya Ubunge endapo atapata ridhaa ya kuwa Mbunge wa Jimbo la Tabora mjini.Amesema kutokana na kutambua vema matatizo yanayowakabili wakazi wa Jimbo la Tabora mjini atahakikisha anayaunganisha makundi ya Wanawake,Vijana na Wazee na kutumia fursa zilizopo katika mfuko wa Jimbo kuwainua kiuchumi pamoja na kuwatafutia fursa nyinginezo zitakazokuwa chachu ya maendeleo kwa kushirikiana nao.Amesema atakuwa Mbunge wa kuwatumikia wananchi na kamwe hatowakimbia kama wanavyofanya Wabunge wengine ambao wanakabiliwa na Uchoyo wa kupindukia.  
Mkangala akijinadi kwa baadhi ya wakazi wa kata ya Kiloleni ambapo alihimiza umuhimu wa kuchagua viongozi wenye nia ya kuwatumikia wananchi huku akieleza kuguswa kwake na namna ambavyo viongozi waliopita walivyoshindwa kuleta maendeleo katika jimbo la Tabora mjini na hata kusababisha huduma za kijamii zikiwemo za Afya na nyinginezo kuwa kero kubwa kwa wananchi hususani akinamama wajawazito wanapokwenda kujifungua hospitali ya mkoa wa Tabora Kitete ambapo hukosa huduma zinazostahili kwa wakati muafaka.

Kamaliza Kayaga mgombea aliyejinadi kwa kuwataka wanaCCM  wamchague ili aweze kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Tabora mjini ambalo wananchi wake wamekuwa na migogoro ya ardhi isiyokwisha kwakuwa yeye kitaaluma ni Mwanasheria hivyo amesema atatumia uwezo wake na elimu aliyonayo kusaidia kuondosha adha hiyo ambayo ni kero kubwa kwa wananchi,atafanya hivyo endapo atachaguliwa kuwa Mbunge na kuahidi kuwa akiwa Bungeni  atatetea baadhi ya Sheria kandamizi ziondolewe ili kumpa fursa wananchi kuishi katika mazingira yenye kuzingatia haki na usawa.  
William Masubi akijinadi mbele ya wananchi wa kata ya Kiloleni ambapo alizungumzia suala la elimu bora kwa wanafunzi pamoja na changamoto nyingine zinazokwamisha maendeleo ya Jimbo la Tabora mjini,aliahidi kuwa karibu na wananchi na kusikiliza kero zao kwakuwa yeye ni mkazi wa Tabora na hata kama endapo atachaguliwa kuwa Mbunge kamwe hatokuwa kama walivyo wabunge waliotangulia ambao baada ya kuchaguliwa wanakimbilia kuishi jijini Dar-es-salaam huku wananchi wakiendelea kukosa mtu wa kupokea na kufanyia kazi changamoto zinazowakabili.


Aden Rage ambaye ni mbunge aliyemaliza muda wake wakati akijinadi amewataka wanaCCM wampe ridhaa ya kuwania nafasi ya Ubunge kwa mara nyingine tena huku akidai kuwa yeye tayari ni mzoefu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  na kwamba  atawatumikia vyema kwa kuwaletea maendeleo,akipigia mfano wa Ujenzi wa barabara za lami,huduma za maji Tabora mjini,maboresho ya huduma za afya katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete ingawa jambo hilo wananchi waliowengi walionesha kutokubaliana nalo kwakuwa huduma za afya hospitali bado haziridhishi na waathirika wakubwa ni akinamama wajawazito ambao wanalazimika kulala wawili wawili hadi watatu katika kitanda kimoja.

Bandora Mirambo amesema endapo atapata ridhaa ya wanaCCM na kufanikiwa kushinda katika uchaguzi mkuu atashirikiana na wananchi katika masuala mbalimbali ya maendeleo kwakuwa ofisi yake kama mbunge itafungua milango ya dawati la kusikiliza kero za wananchi huku akiwaasa kuwapima wagombea wote kwakumuangalia ambaye ana hofu ya MwenyeziMungu kwani ndiye atakuwa mgombea bora atakayewatumikia wananchi.Amesema tatizo la linalokwamisha maendeleo ya Jimbo la Tabora mjini ni kukosa Mbunge anayeyatambua matatizo yanayowakabili wananchi kwani kila anayechaguliwa kushika nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Tabora mjini anasahau na kutowajali waliomuweka madarakani.



Amon Mkoga amejinadi kwa kuwataka wananchi wamchague kwani yeye ndiye mtu sahihi anayefaa kuwatumikia kwakuwa amekuwa akifanya mambo mengi ya Maendeleo hususani ya elimu kwa kuyahamasisha baadhi ya makampuni na mashirika kusaidia Shule za msingi na Sekondari,amesema endapo atapata ridhaa ya kuwania Ubunge na kufanikiwa atasaidia vikundi mbalimbali vya wajasiliamali kwa kuwapa elimu itakayowawezesha kuondokana na umasikini.

Monday, July 27, 2015

BASI LAGONGA TRENI YA MIZIGO NA KUUA WANNE - TABORA MJINI



Askari Polisi wakifanya ukaguzi kwa maiti zilizokutwa eneo la ajali hiyo

Kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Juma Bwire akizungumza na waandishi wa habari katika eneo la tukio la ajali mbaya iliyotokea eneo la kata ya Malolo manispaa ya Tabora ambapo watu wanne walikuwa wamepanda basi hilo la kampuni ya Dont Worry ambapo lilisababisha ajali hiyo baada ya kugonga treni ya mizigo,watu kadhaa wamejeruhiwa vibaya na kulazwa hospitali ya mkoa wa Tabora Kitete.
Eneo la chini la basi hilo la kampuni ya Dont Worry ambalo lilisababisha ajali hiyo ambapo mbali na uzembe wa dereva lakini basi hilo lililokuwa likifanya safari zake kutoka Tabora mjini kwenda Ufuluma wilaya ya Uyui limeonekana sehemu hiyo ya chini imefungwa kamba za mipira kuzuia vyuma vinavyunganishwa na usukani visichomoke kitu ambacho ni hatari kwa usalama wa maisha ya wasafiri.





"NITALETA MABADILIKO MAKUBWA YA MAENDELEO KATA YA CHEYO"-YUSUPH KITUMBO

Mkurugenzi wa Kitumbo Security Guard Bw.Yusuph Kitumbo akisalimiana na baadhi ya akina mama wa Kata ya Cheyo wakati wa mkutano wa kujinadi kwa wajumbe wa halmashauri ya Kata wa Chama cha Mapinduzi ikiwa ni hatua ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa kupata nafasi ya kuwa mgombea nafasi ya Udiwani kupitia CCM kata ya Cheyo manispaa ya Tabora......''Endapo nitapata ridhaa yenu na kushinda kwenye uchaguzi mkuu,nitahakikisha ninashirikiana na ninyi wananchi wenzangu kuleta heshima ya kata yetu ya Cheyo kwa kushughulikia kero mbalimbali zinazokwamisha maendeleo katani kwetu"alisema Kitumbo ambaye amekuwa akishiriki kikamilifu shughuli mbalimbali za kijamii na kusaidia vikundi vya akina mama,Waathirika wanaoishi na virusi vya Ukimwi ikiwa ni pamoja na kuwachimbia visima virefu.
Wagombea wa nafasi ya Udiwani wakiwa katika mkutano wa wajumbe kuomba ridhaa ya Chama ili wachaguliwe kuwania nafasi hiyo wakati wa Uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Yusuph Kitumbo akiteta jambo  muhimu   na Diwani wa kata ya Cheyo aliyemaliza muda wake.
Baadhi ya akinamama wakiwa na shauku kubwa ya kuzungumza na mgombea udiwani kata ya Cheyo
"Wewe kama kijana wetu Kuna mambo muhimu ambayo utalazimika kuyashugulikia endapo utafanikiwa kupata nafasi hiyo ya udiwani na ninapenda kukuasa usitutupe kabisa sisi Wazee wako ambao kero zetu kubwa ni huduma za matibabu bure,wastaafu tumetelekezwa kabisa na Serikali,tunaomba pia tupatiwe mikopo  yenye masharti nafuu ili tufanye hata biashara ndogo ndogo"-Ndivyo mmoja kati ya Wazee wa kata ya Cheyo alisikika akimnong'oneza jambo hilo Bw.Kitumbo. 





MAHOJIANO NA CHARLES MAGALI NDANI YA WASHINGTON DMV

Charles Magali akiwa ndani ya Kilimanjaro Studio zinazomilikiwa na Vijimambo Radio, Kwanza Production na NesiWangu Media
Ijumaa ya Julai 24, 2015, mwigizaji na mwimbaji wa muziki nchini Tanzania Charles Magali alipata fursa ya kutembelea studio zetu zilizopo Beltsville Maryland. Hapo akazungumza nasi kwa ufupi
Karibu umsikilize akihojiwa na Mbunifu na Mtayarishaji wa kipindi hiki Dj Luke Joe na Mubelwa Bandio

MBUNGE CHIKU ABWAO WA CHADEMA AMFUATA ZITTO KABWE ACT-WAZALENDO


 Katibu wa Mipango na Mikakati wa Chama cha ACT-Wazalendo, Habibu Mchange (kushoto), akimkabidhi kadi ya chama hicho, aliyekuwa mbunge wa Viti maalumu kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Iringa mjini, Chiku Abwao baada ya kuhamia rasmi ACT-Wazalendo Dar es Salaam leo mchana.
 Mbunge Chiku Abwao (kulia), akionesha kadi ya chama cha ACT-Wazalendo baada ya kukabidhiwa.
  Mbunge Chiku Abwao (kulia), akizungumza na wanahabari baada ya kukabidhiwa kadi ya chama cha ACT-Wazalendo.

Friday, July 24, 2015

UZINDUZI WA KAMPENI YA WAZAZI NIPENDENI AWAMU YA PILI WAFANYIKA VIWANJA VYA MWEMBE YANGA TEMEKE JIJINI DAR ES SALAAM LEO

 Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dk.Neema Rusibamayila kwa niaba ya Waziri wa wizara hiyo Dk. Seif Rashid  (wa pili kushoto), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa  kampeni ya Wazazi Nipendeni awamu ya pili  katika viwanja vya Mwembe Yanga Temeke Dar es Salaam leo mchana. Wa kwanza kushoto ni Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID), Anna Bodipo Memba na wa pili kulia ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Grace Magema. 
 Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID), Anna Bodipo Memba (kulia), akitoa hutuba yake kwenye uzinduzi huo.
 Mshauri wa masuala ya Afya ya Jamii kutoka Taasisi ya HBC, Mdadike Thabit (kulia), akimuelekeza jambo mgeni rasmi katika uzinduzi huo Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dk.Neema Rusibamayila wakati alipokuwa akitembelea mabanda ya watoa huduma kabla ya kufanyika uzinduzi huo.
 Wananchi wakiwa wamejipanga foleni kwa ajili ya kupata huduma za afya ya jamii kwenye uzinduzi huo.
 Wanamuzi wa bendi ya muziki wa dansi ya FM Academia 
wakitoa burudani.
 Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Grace Magema akizungumzia mikakati ya Afya ya Jamii katika mkoa huo.



 Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dk.Neema Rusibamayila, akitoa hutuba yake ya uzinduzi.
 Watoto nao walikuwepo kwenye uzinduzi huo.
 Mwanamuziki Juma Nature akitoa burudani kwenye uzinduzi huo.
 Wananchi walioshiriki uzinduzi huo.
Kiongozi wa kundi la muziki la Wanaume Family, Chege (kulia), akishambulia jukwaa katika uzinduzi huo.
Msanii wa kundi la utamaduni la HD Entertainment la Mbezi Beach, Michael Kamugisha, akiwa ameruka juu wakati wa kundi hilo lilipokuewa likitoa burudani katika uzinduzi huo.


Na Dotto Mwaibale

TANZANIA imeweza kufikia lengo la milenia namba 4 la kupunguza vifo vya watoto kwa theluthi mbili kutoka vifo 152 hadi 54 kwa kila watoto 1,000 wanaozaliwa hai.

Hayo yalibainishwa na Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dk.Neema Rusibamayila kwa niaba ya Waziri wa wizara hiyo Dk. Seif Rashid wakati akizindua kampeni ya awamu ya pili ya Wazazi Nipendeni katika viwanja vya Mwembe Yanga Temeke Dar es Salaam leo mchana.

Alisema pamoja na kutofikia lengo la melenia namba 5 la kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kwa robo tatu kufikia vifo 193 kwa kila vizazi hai laki moja, taarifa za umoja wa mataifa za mwaka 2014 zinaonyesha kuwa Tanzania imeweza kupunguza vifo hivyo toka 770 kwa kila vizazi hai 100,000 mwaka 1990 hadi kufikia 410 kwa kila vizazi hai 100,000 mwaka 2014.

"Sababu zinazosababisha watoto waliochini ya miaka mitano kupoteza maisha ni kuharisha, nimonia na malaria na kuwa zinachangia takribani asilimia 50 ya vifo vya watoto hao waliochini ya miaka mitano" alisema Dk.Rusibamayila.

Alisema utapiamlo nao ni tatizo linalochangia vifo vya watoto hao kwani takwimu za mwaka 2010 zinaonyesha kuwa kiwango cha udumavu ni asilimia 42 kwa watoto waliochini ya umri wa miaka mitano.


Dk.Rusibamayila aliongeza kuwa vifo vya watoto wachanga havijapungua kwa kasi inayoridhisha na vinachangiwa na wale watoto wanaozaliwa njiti, kushindwa kupumua vizuri mara baada ya kuzaliwa na maambukizi ya bakteria. 

RAIS KIKWETE AIFARIJI FAMILIA YA MAREHEMU JOHN EDWARD MCHECHU.

1
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa(NHC) Bw. Nehemia Mchechu. Rais Kikwete alikwenda nyumbani kwa Mkurugenzi huyo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam julai 23, 2015 kumpa pole kufuatia kifo cha Baba yake aliyekuwa anaugua ugonjwa wa kiharusi.
Marehemu atasafirishwa kuelekea Muheza, Tanga kwa ajili ya Mazishi. Mazishi yatafanyika Kijiji cha Enzi, Muheza – Tanga siku ya Jumamosi tarehe 25/07/2015.
PICHA ZOTE NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM
2
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Marehemu John Edward Mchechu ambaye ni baba wa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa(NHC) Bw. Nehemia Mchechu. Rais Kikwete alikwenda nyumbani kwa Mkurugenzi huyo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam julai 23, 2015 kumpa pole kufuatia kifo cha Baba yake aliyekuwa anaugua ugonjwa wa kiharusi.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho kikwete akiifariji familia ya marehemu John Edward Mchechu Mbezi beach jijini Dar es Salaam julai 23, 2015. (wapili kushoto) mtoto wa Marehemu ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bwana Nehemia Mchechu.
4
Familia ya marehemu John Edward Mchechu.
5 6
Rais Dkt.Jakaya Mrisho kikwete akiondoka mara baada ya kuifariji familia ya marehemu John Edward Mchechu (katika) mtoto wa Marehemu ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bwana Nehemia Mchechu.
7
Rais Dkt.Jakaya Mrisho kikwete akiagana viongozi mara baada ya kuifariji familia ya marehemu John Edward Mchechu (katika) mtoto wa Marehemu ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bwana Nehemia Mchech.
8
Waombolezaji.
9
????????????????????????????????????

"NITASHUGHULIKIA IPASAVYO KERO NA MATATIZO YA WANANCHI WA JIMBO LA TABORA MJINI"-BANDORA MIRAMBO

NA LUCAS RAPHAEL,TABORA

Kazi ya uwakilishi wa wananchi kwenye vyombo vya maamuzi sio kukaa ofisini na kutembelea  gari lenye  kiyoyozi bali ni kuyajua  matatizo na changamoto zinazowakabili na kisha kuzipatia ufumbuzi.


Imekuwa mazoea mara baada ya uchaguzi wabunge na madiwani wa vyama vyote kusahau  wajibu wao kwa wananchi jambo linalowafanya kuhaha unapokaribia wakati wa uchaguzi.



Hebu jaribu kukumbuka nyakati za mwisho wa Bunge hili lililopita la mwisho lililokuwa na bajeti,lilikuwa halina wawakilishi wa kutosha  kwa kuwa wengi wao walijaribu kujirudisha majimboni kwao ili kuanza kujenga upya  imani ya wananchi kuelekea uchaguzi mkuu baada ya kushindwa kufanya hivyo kwa miaka minne na nusu.



Tabia ya kutowajali wananchi imegharimu kwa kiasi kikubwa kasi ya maendeleo kuwa ndogo, Miradi kutokukamilika kwa wakati, Miradi kutekelezwa kwa viwango duni na matumizi mabaya ya fedha za umma na madaraka.



Mmoja kati ya vijana mahili anayeteka kuwani nafasi ya ubunge jimbo la Tabora mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi, Bandora Salum Mirambo (40) ambaye ni mkurungezi wa kampuni ya Salu Security Services Ltd ya Tabora imemkera sana hali hiyo na hata kufikia hatua ya kutoa kauli hiyo.



Anasema wabunge wengi kwa makusudi wamekuwa hawawatumikii wananchi waliowachagua ipasavyo jambo ambalo limekuwa likirudisha nyuma maendeleo ya maeneo husika.



Anasema, “Mimi  nikipewa ridhaa ya kuwa mbunge wa jimbo la Tabora mjini nitahakikisha navitumia vizuri vyombo vya maamuzi kwa maana ya baraza la madiwani na bunge la Jamhuri ya Muungano kutatua matatizo na kero mbalimbali  za wananchi.”



Anasema vyombo hivyo vya maamuzi vikitumiwa vizuri vinaweza kuleta matokeo chanya na kuharakisha maendeleo ya wananchi kwa kuwa ndipo maamuzi ya kibajeti ufanyika.



Anasema wabunge wengi wanaomaliza muda wao wameshindwa kuwatetea wananchi wao bungeni na wala hawakuonekana kwenye vikao vya mabaraza ya madiwani na hivyo kushindwa kujua kinachoendelea kwenye ngazi ya halmashauri.





Anasema ubunge au udiwani unahitaji kiongozi ambaye ni mbunifu, mwenye maono na dira ya kuwavusha watu wake kutoka kwenye umasikini kwa kuzibadili changamoto kuwa fursa.





Bandora anasema suala hilo limekuwa gumu kwa wabunge wengi ambao wamekuwa wakisubiri fedha za kibajeti au za mfuko wa jimbo ambazo zinaukomo na hivyo kushindwa kutatua matatizo na changamoto zinazowakabili wananchi.



Kazi ya uwakilishi inahitaji mtu mwenye upeo wa kupambanua na kuchambua mambo mbalimbali kuanzia ngazi ya kitongoji hadi ngazi ya vikao vya kamati za maendeleo za mitaa, vijiji na kata.



Aidha anasema mtu huyo anapaswa kuutumia upeo wake kuchambua mambo kwenye vikao vya ushauri vya wilaya DCC na mkoa RCC ili kushawishi mwelekeo wa kuzipatia ufumbuzi kero za wananchi wa jimbo lake.



Vikao hivyo muhimu vimekuwa vikipuuzwa na wabunge wengi na hata wanapohudhuria wamekuwa hawatoi mchango chanya au kutoongea kabisa.



Anabainisha kuwa kwa muda mrefu wabunge wengi wameshindwa kuonekana majimboni sio kwa sababu ya vikao vya bunge au vya kamati za kudumu za bunge bali wanaogopa kuombwa misaada na wapiga kura wao.



Jambo hili la kihekima linapaswa kutatuliwa na mbunge kwa kuwaonesha wapiga kura wake fursa zinazowazunguka ili waanzishe shughuli za uzalishaji mali badala ya kuwakimbia kwa hofu ya kuombwa.



Anasema, “Nikifanyikiwa kuwa mbunge nitasimamia upatikanaji wa mikopo ya fedha ,zana za kazi pamoja na maarifa ambayo yatawafanya wananchi kuziona fursa za uzalishaji mali na kuzitumia.”





Anasema kwa kuwashirikisha wananchi wa kada zote tutaimarisha shughuli za VICOBA uanzishwaji wa SACCOS zenye nguvu ambazo zitapambana na masharti ya dhamana yanayotolewa na taasisi za kifedha.



Bandora anasema jambo lingine atakalo lifanya ni kuibana halmashauri ya Manispaa ya Tabora kutenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vijana na wanawake.



Anasema endapo halmashauri hiyo ingekuwa ikitenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa mujibu wa sheria ingesaidia kubadili maisha ya wananchi wake kwa kiwango kikubwa.



Anabainisha jambo lingine atakalolipa kipaumbele ni uwazi katika kutekeleza majukumu yake ya kibunge kwa maana ya wapiga kura kujua utaratibu na ratiba ya mikutano ya kibunge, na vikao vya kamati za bunge ili kuondoa visingizio vya kutowajibika kwao.



Jambo lingine atafanya mikutano ya hadhara na wananchi na makundi mbalimbali ya kisekta ili kujua matatizo na changamoto zinazowakabili kabla ya kwenda bungeni tofauti na ilivyosasa ambapo mbunge anakwenda Bungeni kuwasilisha mambo anayoyawaza kutoka kichwani kwake.



Anasema wananchi wa Manispaa ya Tabora wamekabiliwa na migogoro ya ardhi kwa muda mrefu ambayo imedhoofisha shughuli zao za uzalishaji mali na uwekezaji wa makazi na mambo mengine.



Anasema, “Jambo hili nitalisimamia kwa kuwakosoa na kuwakemea waziwazi watu wanaotumia madaraka yao ya utumishi wa umma au ya kisiasa kutengeneza migogoro ya ardhi kwa manufaa yao.”



Kwa kuwa njia nyingine bora ya kukabiliana na vitendo vya dhuluma kwenye ardhi ni kuwawezesha wananchi kuzijua sheria za ardhi za mwaka 1999 na sheria ya mipango miji ya mwaka 2007.



”nitahakikisha wakazi wa mji wa Tabora wanarasimisha shughuli zao pamoja na makazi kwa kupata hati zitakazowawezesha kupata mikopo kwenye taasisi za fedha.”



Anabainisha kuwa atahakikisha vyombo vya kisheria vinavyoshughulikia migogoro ya ardhi vinawezeshwa kwa kupatiwa wataalamu,vitendea kazi na kutekeleza majukumu yake kwa uwazi na haki.



Anavitaja vyombo hivyo  kwa mujibu wa sheria kuwa ni mabaraza ya Ardhi ya kijiji, kata, mabaraza ya Ardhi na nyumba ya wilaya , mahakama kuu kitengo cha Ardhi na mahakama ya Rufaa.



Bandora anaweka wazi kuwa akiwa mbunge ataweka daraja la wazi kati yake na asasi za kiraia, makundi maalumu ya watu wenye ulemavu ambayo yamesahauliwa na wabunge na madiwani.



Aidha anaeleza kuwa ataimarisha misingi ya utawala bora kwa kujenga ofisi za wenyeviti wa mitaa kila kata kwa lengo la kuimarisha uwajibikaji kwa wananchi.



 Anasema kwa kufanya hivyo kutapunguza malalamiko ya rushwa na kwamba atawawezesha kupata posho na vitendea kazi kila mwezi.



Anasema atasimamia kikamilifu sekta za maji, elimu na afya ambazo zinagusa na kuchochea ustawi wa sekta nyingine.

Bandora anasema atahakikisha zahanati zinakuwa na watumishi wa afya, dawa, vifaa tiba ili kupunguza msongamano kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete.


Aidha atahakikisha mpango wa ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Tabora unaanza mara moja kwa fedha kutengwa na pia kutafuta misaada kwa wadau wa sekta ya afya.


Mkakati huo anasema ni wa makusudi utasaidia kupunguza vifo vya watoto wenye umri chini ya miaka mitano na akinamama wajawazito.


Atahimiza uimarishwaji wa mpango wa damu salama ambao umepuuzwa na wabunge na madiwani wengi huku wahitaji wakubwa ni watoto na akinamama wajawazito.



Bandora anasema kama wanawake ni jeshi kubwa linalotumika kwenye uchaguzi kwanini limekuwa likisahaulika mara baada ya uchaguzi kwa kuruhusu vifo vyao wakiwa wajawazito?.



Anasema atasimamia mipango ya uboreshaji wa huduma ya maji kutoka mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira TUWASA pamoja na kuhimiza serikali kulipa madeni ya taasisi zake ambayo ni zaidi ya shilingi bilioni moja.

Atahimiza pia utekelezaji wa mradi wa maji ya ziwa Victoria kutokea kijiji cha Solwa Shinyanga kupitia Nzega kuja Tabora na wilaya nyingine za mkoa wa Tabora.


Aidha kwenye elimu atahakikisha hakuna mtoto anayekaa chini katika shule za msingi za manispaa ya Tabora ambako kuna miti ya mbao na mbao za kutosha.



Akizungumzia michezo anasema kwamba atashirikiana na vyama vyote vya michezo kuinua michezo kuanzia ngazi za mitaa, vijiji na kata tofauti na ilivyosasa nguvu  zisizo na utaratibu zimewekwa kwenye soka la wanaume pekee.



Anasema ameamua kufanya hivyo ili kurudisha hadhi ya michezo ya mkoa wa Tabora iliyokuwepo miaka ya nyuma.



“Kukosekana kwa mikakati madhubuti katika michezo kumefanya vipaji vingi vya vijana wa Tabora  kupotea  jambo ambalo limesababisha kupoteza ajira kupitia michezo.”anasema Bandora.



Anasisitiza kukitumikia Chama Cha Mapinduzi na kukifanya kuwakomboa wananchi na wanachama wake kwa kuwaletea maendeleo halisi.

LISTEN TO ERICA LULAKWA’S BRAND NEW SONG “DUNDIKA”

maxresdefault
Debut Album "Piga Moyo Konde" is out! On Itunes http://itunes.apple.com/album/id10046...
Dundika is the 2nd Song released from this Album. Listen free on Spotify and Tidal. If you like the music, I would truly appreciate your support in writing a review or sharing links to iTunes or Google Play on social media.
Listen to her music on you tube below here.