Aden Rage ambaye ni mbunge aliyemaliza muda wake wakati akijinadi amewataka wanaCCM wampe ridhaa ya kuwania nafasi ya Ubunge kwa mara nyingine tena huku akidai kuwa yeye tayari ni mzoefu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwamba atawatumikia vyema kwa kuwaletea maendeleo,akipigia mfano wa Ujenzi wa barabara za lami,huduma za maji Tabora mjini,maboresho ya huduma za afya katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete ingawa jambo hilo wananchi waliowengi walionesha kutokubaliana nalo kwakuwa huduma za afya hospitali bado haziridhishi na waathirika wakubwa ni akinamama wajawazito ambao wanalazimika kulala wawili wawili hadi watatu katika kitanda kimoja. |
No comments:
Post a Comment