Pages

KAPIPI TV

Monday, July 27, 2015

"NITALETA MABADILIKO MAKUBWA YA MAENDELEO KATA YA CHEYO"-YUSUPH KITUMBO

Mkurugenzi wa Kitumbo Security Guard Bw.Yusuph Kitumbo akisalimiana na baadhi ya akina mama wa Kata ya Cheyo wakati wa mkutano wa kujinadi kwa wajumbe wa halmashauri ya Kata wa Chama cha Mapinduzi ikiwa ni hatua ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa kupata nafasi ya kuwa mgombea nafasi ya Udiwani kupitia CCM kata ya Cheyo manispaa ya Tabora......''Endapo nitapata ridhaa yenu na kushinda kwenye uchaguzi mkuu,nitahakikisha ninashirikiana na ninyi wananchi wenzangu kuleta heshima ya kata yetu ya Cheyo kwa kushughulikia kero mbalimbali zinazokwamisha maendeleo katani kwetu"alisema Kitumbo ambaye amekuwa akishiriki kikamilifu shughuli mbalimbali za kijamii na kusaidia vikundi vya akina mama,Waathirika wanaoishi na virusi vya Ukimwi ikiwa ni pamoja na kuwachimbia visima virefu.
Wagombea wa nafasi ya Udiwani wakiwa katika mkutano wa wajumbe kuomba ridhaa ya Chama ili wachaguliwe kuwania nafasi hiyo wakati wa Uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Yusuph Kitumbo akiteta jambo  muhimu   na Diwani wa kata ya Cheyo aliyemaliza muda wake.
Baadhi ya akinamama wakiwa na shauku kubwa ya kuzungumza na mgombea udiwani kata ya Cheyo
"Wewe kama kijana wetu Kuna mambo muhimu ambayo utalazimika kuyashugulikia endapo utafanikiwa kupata nafasi hiyo ya udiwani na ninapenda kukuasa usitutupe kabisa sisi Wazee wako ambao kero zetu kubwa ni huduma za matibabu bure,wastaafu tumetelekezwa kabisa na Serikali,tunaomba pia tupatiwe mikopo  yenye masharti nafuu ili tufanye hata biashara ndogo ndogo"-Ndivyo mmoja kati ya Wazee wa kata ya Cheyo alisikika akimnong'oneza jambo hilo Bw.Kitumbo. 





No comments: