Mkurugenzi wa Kitumbo Security Guard Bw.Yusuph Kitumbo akisalimiana na baadhi ya akina mama wa Kata ya Cheyo wakati wa mkutano wa kujinadi kwa wajumbe wa halmashauri ya Kata wa Chama cha Mapinduzi ikiwa ni hatua ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa kupata nafasi ya kuwa mgombea nafasi ya Udiwani kupitia CCM kata ya Cheyo manispaa ya Tabora......''Endapo nitapata ridhaa yenu na kushinda kwenye uchaguzi mkuu,nitahakikisha ninashirikiana na ninyi wananchi wenzangu kuleta heshima ya kata yetu ya Cheyo kwa kushughulikia kero mbalimbali zinazokwamisha maendeleo katani kwetu"alisema Kitumbo ambaye amekuwa akishiriki kikamilifu shughuli mbalimbali za kijamii na kusaidia vikundi vya akina mama,Waathirika wanaoishi na virusi vya Ukimwi ikiwa ni pamoja na kuwachimbia visima virefu. |
No comments:
Post a Comment