Tuesday, January 27, 2015
LOCAL EU STATEMENT ON CLOSURE OF A NEWSPAPER IN TANZANIA
MWANAMKE ALIVYOUWA WATOTO WAKE WAWILI NA KUWACHIMBIA SHIMO NDANI YA NYUMBA YAKE
Mwili wa mtoto Mwamvua Mrisho(6)aliyeuawa kwa kunyongwa na mama yake mzazi Zuhura Sudi ambaye aliuwa watoto wake wawili na kuwachimbia mashimo na baadaye kuwafukia chumbani na Sebuleni |
Zuhura Sudi mara baada ya kuwanyonga watoto wake |
Mwili wa Mwamvua baada ya kufukuliwa na Askari Polisi |
Miili ya watoto wote wawili baada ya kufukuliwa. |
Katika hali isiyokuwa ya kawaida mwanamke mmoja mkazi wa
mtaa wa Utusi kata ya Chemchem Manispaa ya Tabora Zuhura Sudi(26) anadaiwa
kuwaua watoto wake wawili kwa kuwakaba
shingoni na baadae
kuwachimbia mashimo mawili
na kuwafukia.
Tukio hilo ambalo lilihuzunisha baadhi ya watu waliofurika
nyumbani kwa mwanamke huyo mtaa wa Utusi(Bakari) imedaiwa kuwa alilifanya wakati akiwa amebaki
nyumbani hapo alipokuwa akiishi yeye na babu yake ukiachilia mbali watoto hao
wawili ambao ni marehemu wakifahamika
kwa majina ya Mwamvua Mrisho(6) na Sudi mwenye umri wa miezi saba.
Taarifa iliyotolewa
kwa vyombo vya habari na kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Juma Bwire imeeleza kuwa Zuhura akiwa nyumbani kwake na watoto
hao wawili aliwakaba shingo hadi kufa,kisha kuwafunga kwenye mifuko ya
sandarusi na kuwafukia katika mashimo
mawili aliyoyachimba sebuleni na chumbani.
Taarifa hiyo kutoka Jeshi la Polisi imebainisha kuwa
mtuhumiwa Zuhura atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika huku
ikilaani vikali tukio hilo la kinyama lililofanywa na mwanamke huyo.
Kwa mujibu wa maelezo ya Mwenyekiti wa mtaa wa Utusi, Bibi
Aziza Mwenya,ushirikiano mkubwa baina
ya wananchi wa mtaa
huo ndio uliofanikisha kugundulika
kwa tukio hilo la
kinyama lililopoteza maisha
ya watoto hao
wasiokuwa na hatia.
Bibi Aziza alisema
baada ya kupokea taarifa kutoka
kwa Babu
wa mwanamke huyo
Zuhura anayefahamika kwa jina la
Shabani Ramadhani kuhusu kutoweka
kwa watoto hao wawili katika mazingira
ya kutatanisha,walilazimika
kufika nyumbani hapo
na kuanza kumhoji Zuhura
ambaye alikuwa akizuia watu
kuingia ndani kutokana na tukio hilo la kinyama alilolifanya.
Hata hivyo majirani kwa kushirikiana na Mwenyekiti wao wa
mtaa na baba wa mmoja wa watoto hao waliouawa
Bw.Mrisho Abdallah ambae alikuwa
mume wa Zuhura walimvamia na kumshika kwa nguvu
Mwanamke huyo ili waingie ndani
na kubaini kuwa kulikuwa na mashimo mawili aliyokuwa amewafukia watoto hao
ambao baadae walikuja kufukuliwa kwa msaada wa Jeshi la Polisi.
Katika mahojiano ya awali yaliyofanywa na mwandishi wetu na
muuaji huyo wakati akiwa chumbani mara baada ya kubainika kwa tukio hilo,Zuhura
alionekana kutokuwa na wasiwasi wowote
hatua ambayo baadhi ya watu walidai kuwa mwanamke huyo ana lengo la kupoteza
ushahidi kwa kuonesha ametokwa na akili
timamu.
Hata hivyo kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa majirani zake wa
karibu,mwaka 2013 Zuhura anadaiwa kumsababishia kifo mtoto wake mchanga wa kiume baada ya kumzidishia dozi ya malaria
wakati alipokuwa akiumwa.
Sunday, January 25, 2015
KAYMU TURNS TWO WITH A PROMISE OF EXPANSION TO FURTHER SHORES
Kaymu Tanzania Country Manager, Erfaan Mojgani says “The significant growth of Kaymu over the past two years has been great motivation for us especially with our launch in Tanzania. The consumer demand for e-commerce has pushed Kaymu to grow and as 2015 goes on, we are looking to grow even further than we already have”
Friday, January 23, 2015
PATA FILAMU YA FOOLISH AGE KUPITIA MTANDAO
Katika maisha binadamu ana nyakati tatu, Wakati uliopita, wakati uliopo na wakati ujao. Wakati uliopita na ujao hana mamlaka nao bali wakati uliopo ndio hazina yake ya kujenga mustakabali wake ila kikwazo kikuu ni umri wake. Kuna umri anahitaji matunzo na ulinzi unaitwa utoto na kuna umri anahitaji heshima na matunzo unaitwa uzee halafu kuna umri unaitwa mtu kamili ila kabla yake upo umri matata unaitwa FOOLISH AGE . Fuatilia hii kupitia mtandao .......
Kwa Kuangalia Filamu hii ya Kitanzania iitwayo Foolish Age au Knunua na iwe yako kupitia mtandao.
Ili kuweza kuangalia au kununua kupitia Mtandao unachotakiwa kufanya ni kutembelea tovuti hii
WANACHAMA WA FIBUCA TAWI LA ATTT WALALAMIKIA VITISHO TOKA KWA MWAJIRI WAO
CHAMA cha wafanyakazi wa asasi za fedha,viwanda,Benki,Uzalishaji wa nishati,Biashara na Kilimo FIBUCA tawi la Tabora kimelalamikia hatua za vitisho wanavyopatiwa wanachama wa chama hicho tawi la kampuni ya tumbaku ya ATTT kutoka kwa mwajiri wao na kusababisha baadhi ya wanachama kutaka kujitoa kwa kuhofia kupoteza ajira zao.
Akisoma taarifa fupi mbele ya kaimu mkuu wa mkoa wa Tabora Suleiman Kumchaya wakati wa semina ya viongozi wa tawi la chama hicho katika kampuni ya ATTT,Katibu wa FIBUCA mkoani hapa Ramadhani Wakulichombe alisema moja kati ya changamoto kubwa inayowakabili ni pamoja na vitisho dhidi ya wanachama na viongozi wa tawi hilo.
Wakulichombe amebainisha kuwa licha ya FIBUCA kuendelea kujitangaza sehemu mbalimbali za waajiri na kufanikiwa kuingiza wanachama wengi ikiwemo wafanyakazi wa kampuni ya Association of Tanzania Tobacco Traders ATTT,lakini jambo la kushangaza ni kuona uongozi wa kampuni ya ATTT ikihoji kwanini wafanyakazi hao wamejiunga na chama hicho jambo ambalo limekuwa likiwatishia na hata kufikia hatua ya kuanza kujitoa wakihofia kupoteza ajira.
Alisema hatua ya kampuni ya uongozi wa kampuni ya ATTT kutishia wanachama ni kinyume na sheria ya ajira na mahusiano kazini sehemu ndogo 'd' inayozungumzia uhuru wa kujumuika(Employees right to freedom of association)kifungu namba tisa(9) kwamba kila mwajiriwa anayo haki na kujiunga na chama cha wafanyakazi anachokiona kinamfaa.
Hata hivyo Katibu huyo wa FIBUCA ameiomba Serikali ya mkoa wa Tabora kuingilia kati na kulifanyia kazi suala hilo ambalo linawafanya wafanyakazi au wanachama wa chama hicho tawi la ATTT kutokuwa na uhuru wa kisheria katika maeneo yao ya kazi.
Akifungua semina hiyo kaimu mkuu wa mkoa wa Tabora Suleiman Kumchaya aliwataka vingozi wa FIBUCA kusimama imara wakati wanapotetea haki za wanachama wao pasipo kuvunja sheria.
Kumchaya alisema vitisho imekuwa ni jambo ambalo linalotumiwa sana na baadhi ya waajiri ikiwa ni moja ya hatua ya kuwanyonya wafanyakazi mahala pa kazi ili wao waweze kunufaika zaidi.
Aidha katika hatua nyingine baadhi ya wafanyakazi wa ATTT ambao hawakutaka kutaja majina yao wameeleza kuwa mwajiri wao amekuwa akilazimisha wafanyakazi wake wajiunge na chama cha Wafanyakazi wa Mashambani na Kilimo TPAWU ambacho wamedai kuwa kimekuwa kikilinda zaidi maslahi ya mwajiri kuliko mfanyakazi.
Walisema TPAWU ni chama ambacho kilikuwepo tangu awali kabla ya FIBUCA na hivyo wamedai kuwa kimeshindwa kutetea maslahi ya wafanyakazi ndio maana wakaamua kujiunga na FIBUCA ambacho mwajiri hakubaliani nacho na ndio sababu ya kuwepo kwa vitisho kwakuwa chama hicho kimekuwa kikiweka wazi na kutoa elimu ya haki za wafanyakazi na namna ya kuzidai.
Chama cha wafanyakazi FIBUCA ni chama huru kilichoanzishwa kwa mujibu wa sheria ya ajira na mahusiano kazini namba sita(6)ya mwaka 2004 na kupata usajiri wa kudumu mnamo tarehe 24 Julai 2009 kwa kupewa cheti namba 24 ambapo kilianzishwa na wafanyakazi wapatao 20 kutoka Benki ya NMB,NBC,NSSF na DAWASCO.
UZINDUZI WA UPANDAJI MITI KIMKOA ULIOFANYIKA KIJIJI CHA NKINTO WILAYA YA MKALAMA -SINGIDA
Mkuu wa wilaya ya Mkalama mkoa wa Singida,Edward Ole Lenga,akipanda mti katika uzinduzi wa upandaji miti kimkoa uliofanyika katika kijiji cha Nkinto wilayani Mkalama |
Na Nathaniel Limu-Mkalama.
MKOA wa Singida umefanikiwa kupanda miti ya aina mbalimbali ipatayo 10,347, 870 sawa na asilimia 37 ya lengo la mkoa kupanda miti 27,500,000 kati ya mwaka 2010 na mwaka jana.
Hata
hivyo kwa mujibu wa wataalamu, asilimia 50 ya miti hiyo imekufa
kutokanana uhaba wa mvua, kuliwa na mchwa, uharibifu wa binadamu na
mifugo.
Hayo
yamesemwa juzi na mkuu wa mkoa wa Singida, Dr. Parseko Kone, wakati
akizungumza kwenye siku ya upandaji miti kimkoa ilifanyika katika kijiji
cha Nkito halmashauri ya wilaya ya Mkalama.
Alisema kutokana na mkoa kukabiliwa na tatizo la mvua haba, jitihada za kupanda miti huwa hazifikii malengo yanayokusudiwa.
“Hata
hivyo hilo halitukatishi tamaa. Napenda kutoa wito kwamba tupande miti
inayovumilia ukame, kutumia njia mbalimbali kwa vile pingili (cuttings)
za mininga mikuyu na jamii zingine zote zinazokubali hali ya hewa ya
mkoa wetu.
Aidha,mkuu
huyo wa mkao alitaja baadhi ya hatua mbalimbali zinazochukuliwa na
mkoa katika kupambana na hali ya kuenea kwa jangwa, ambazo ni kuanzisha
kampeni mbalimbali za upandaji miti ikiwemo kampeni ya msitu ni mali na
msitu ni mazingira.
“Pia
kampeni ya uhamasishaji wa kila kaya kupanda miti isiyopungua 10 na
taasisi zenye matumizi maalumu ya miti, tunaziagiza kuanzisha mashamba
yao ya miti,ili ziweze kujitosheleza kwa nishati hiyo”,alisema.
Katika
hatua nyingine Dr. Kone ametoa wito juu ya umuhimu wa wananchi
kuhakikisha wanahifadhi uoto wa asili uliopo kwa faida ya kizazi cha
sasa na kile kijacho.
“Kwa
kuwa miti mingi tunayopanda inakufa ni vyema watu binafsi na vijiji
watenge maeneo ya hifadhi za misitu ya uoto wa asili kwani hutoa kwa
haraka”,alisema.
Kwa
mujibu wa Dr. Kone, hadi sasa kuna vijiji 230 mkoa wa Singida vyenye
misitu ya asili ya ukubwa wa hekta zipatazo 520, 325.48.
Amesema misitu hiyo ya asili itumike kwa shughuli za ufugaji nyuki kibiashara, ili kumkomboa mwananchi kiuchumi.
SKYLIGHT BAND YAIBUA KIFAA KIPYA MITHILI YA KASUKU SI MWINGINE NI ASHURA KITENGE,NJOO LEO UMSHUHUDIE LIVE THAI VILLAGE
Mratibu wa Skylight Band, Lubea akimkaribisha mdau wa bendi hiyo Miryam Kamaliza shot ya Tequila wakati wa show iliyobamba wakazi wa Dar Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki.
Mratibu wa Skylight Band, Lubea akimimina kinywaji cha Tequila kwa Meneja wa Skylight Band, Aneth Kushaba AK47 Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha Thai Village.
Meneja wa Skylight Band, Aneth Kushaba AK47 akipiga kilaji cha Tequila kupasha mwili joto kabla ya kupanda jukwaani, kinywaji hicho ni maalum kwa mashabiki wa bendi hiyo pindi wanapoingia kwenye kizingiti cha ukumbi huo wa Thai Village, Masaki jijini Dar.
Msanii wa Skylight Band Joniko Music (katikati), akifungua dimba la burudani kwa mashabiki wa bendi hiyo huku akipewa sapoti na Aneth Kushaba AK 47 pamoja na Sam Mapenzi (kulia) wakati show zao za kila Ijumaa ndani ukumbi wa Thai Village Masaki, jijini Dar.
Aaaah Komando Kipensi weeeeeee... si mwingine ni Le Manager her self Aneth Kushaba AK 47 mutoto ya Kisukuma akifanya yake jukwaani Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar......Tukutane baadae pale kati....Full MAU-KODAK kuwa huru kuomba picha na washikaji zako mdau wetu.
Murembo mupya binti mwenye sauti ya kumtoa Nyoka pangoni, Ashura Kitenge akitoa burudani kwa mashabiki wa Skylight Band (hawapo pichani) ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar es Salaam Ijumaa iliyopita huku akipewa sapoti na Rapa mkongwe Joniko Flower pamoja na Aneth Kushaba AK47.
Mashabiki wa Skylight Band wakijimwaga kwa raha zao.
Meneja wa Skylight Band, Aneth Kushaba AK47 a.k.a #KomandoKipensi akiwa kwenye hisia kali wakati akitoa burudani kwa mashabiki wa bendi hiyo (hawapo pichani) Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar.
Sam Mapenzi akiwapa raha mashabiki wa Skylight Band (hawapo pichani) huku akipewa sapoti ya back vocal na Rapa Joniko Flower pamoja na Sony Masamba.
Daudi Tumba akifanya yake jukwaani kuhakikisha mashabiki wa Skylight Band wanapata ladha nzuri ya muziki wa Live ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar Ijumaa iliyopita.
Majembe ya Skylight Band yakijimwaga na sebene jukwaani kwenye show za bendi hiyo zinazofanyika kila Ijumaa ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar.
Mashabiki wa Skylight Band wakijiachia kwa raha zao ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar.
Vijana wa Skylight Band wakitimua vumbi jukwaani wakiongozwa na Sony Masamba.
Twende kazi.... Sony Masamba akilisongesha na vijana wenzake.
Rapa mkongwe kwenye muziki wa Live Joniko Flower (kushoto) akichana mistari huku wenzake wakitimua vumbi jukwaani.
Sam Mapenzi asali ya warembo akiwa kenye hisia kali alipokuwa akiwapa haki yao mashabiki wa Skylight Band na nyimbo za kisasa zikiwemo Naija Flava, Reggae na zingine kibao....jamaa ni mkali asiyekubali ni mchawi...!
Mashabiki wa Skylight Band wakijinafasi kwa raha zao.
Rais wa #Wanamanyoya Sultan Gijegije (kulia) akipata ukodak na wanamanyoya Joshua Ndege (katikati) pamoja na mdau.
Sura mpya ndani ya Skylight Band yenye sauti mithili ya ndege Kasuka si mwingine ni Ashura Kitenge akishow love na Joshua Ngoje back stage.
Kisura mwingine wa Skylight Band anayefamika kwa jina la Baby (kulia) akipata ukodak na shosti yake back stage.
Wadau nambari One wa Skylight Band wakishow love na Ukodak.
Wanafahamika kwa jina moja #Wadananda a.k.a CUSTOMER CARE nao walipata Ukodak.
#TeamWadananda wakishow love na mdau.
Rapa wa Skylight Band Sony Masamba akishow love na wadau wa bendi hiyo baada ya kuhitimisha show ya Ijumaa iliyobamba ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar. Tukutane baadae.
Thursday, January 22, 2015
FILAMU YA MDUNDIKO SASA YAPATIKANA KUPITIA MTANDAO
Katika maisha tunayoishi duniani sio vizuri kufanyiana mabaya, Kwani hujui kesho itakuaje. Malipo ni hapahapa Duniani . Fuatilia hii kupitia mtandao .......
Kwa Kuangalia Filamu hii ya Kitanzania iitwayo Fedheha au Knunua na iwe yako kupitia mtandao.
Ili kuweza kuangalia au kununua kupitia Mtandao unachotakiwa kufanya ni kutembelea tovuti hii
GOFU LA KIONGOZI WA WAJERUMANI LA MWAKA 1905
Mti aina ya mbuyu uliopo kwenye yaliyokuwa makazi ya Wajerumani mwanzoni mwa miaka ya 1900 ambao ulitumika kunyongea watuhumiwa waliokuwa wakitiwa hatiani.Picha zote na Nathaniel Limu. |
Jengo
lililotumiwa na Wajerumani kama mapokezi kuanzia mwaka 1905 huko
katika kijiji cha Mkalama wilaya ya Mkalama.Jengo hilo baadae Waingereza
waligeuza matumizi na kuwa posta.
|
HALMASHAURI ya
wilaya
ya Mkalama Mkoa wa Singida, imeshauriwa kuzingatia uwezekano wa
kulikarabati na kulilinda jengo lililojengwa na Wajerumani mwaka 1905
lililopo
katika kijiji cha Mkalama, ili liwe makumbusho kwa kizazi cha sasa na
kile kijacho pia liwe kivutio kwa watalii wa ndani na nje ya
nchi.
Alisema aina ya ujenzi uliotumika kujenga jengo la makazi kiongozi
wa Wajerumani hao, likiwa pamoja na jengo ya mapokezi, mahakama
chumba cha kuhifadhia (mahabusu) wafungwa na lile la utawala, ni wa kipekee,
tofauti kabisa na ujenzi unaofanyika
hivi sasa.
Kidimanda alisema katika makazi hayo, pia upo mti aina ya mbuyu,
uliokuwa ukitumika kunyongea watuhumiwa wa makosa mbalimbali waliokuwa wanapewa adhabu ya kunyongwa hadi
kufa.
“Makazi haya ya Wajerumani ambayo baadaye walinyang’anywa na Waingereza,
yamejengwa juu ya mlima uliopo kwenye kijiji chetu. Kwa ujumla yanavutia mno. Kama
yatakarabatiwa na kulindwa, kwa vyo vyote yatakuwa chanzo kikubwa sana cha
mapato ya halmashauri yetu”,alisema Kidimanda.
Aidha,aliweza kutoa ushauri mwingine kwa kushauri kuwa halmashauri
inaweza kutafuta mwekezaji akajenga hoteli yenye ubora kwenye yaliyokuwa
makazi ya Wajerumani,itavutia watalii wa ndani kufika mahali hapo ili kuona majengo yaliyojengwa miaka 110
iliyopita.
Kwa mujibu wa Kidimanda , Wajerumani hao walikuwa
wanajishughulisha zaidi na kilimo na ilikuwa ni kosa kubwa kwa mtu ye yote
kwenda kinyume na matakwa yao.
Anasema baada ya kunyonga hadi kufa watu wengi kwenye mbuyu uliopo
kwenye makazi yao, na kubaini kuwa bado baadhi ya watu waliendelea na tabia ya
kutokutii maelekezo yao bila kuogopa adhabu hiyo, walianza kunyonga watu kwenye
mbuyu uliopo kwenye uwazi kijijini hapo, ili kila mtu aweze kushuhudia kwa
lengo la kuwaogofya.