Pages

KAPIPI TV

Tuesday, January 27, 2015

MWANAMKE ALIVYOUWA WATOTO WAKE WAWILI NA KUWACHIMBIA SHIMO NDANI YA NYUMBA YAKE

Mwili wa mtoto Mwamvua Mrisho(6)aliyeuawa kwa kunyongwa na mama yake mzazi Zuhura Sudi ambaye aliuwa watoto wake wawili na kuwachimbia mashimo na baadaye kuwafukia chumbani na Sebuleni
Askari Polisi wa Kituo kikubwa cha Polisi Tabora akiweka ulinzi mkali kwa Zuhura Sudi baada ya kuwauwa watoto wake wawili kwa kuwanyonga huko katika mtaa wa Utusi(Bakari)kata ya Chemchem manispaa ya Tabora.
Zuhura Sudi mara baada ya kuwanyonga watoto wake
Mwili wa mtoto Sudi(miezi saba)baada ya kufukuliwa ndani ya shimbo alilofukiwa na mama yake mzazi baada ya kuuawa kwa  kunyongwa,Sudi na Mwamvua walinyongwa na kuwekwa kwenye mifuko ya Sandarusi na kufukiwa kwenye mashimo yaliyochimbwa na mama yao mzazi Zuhura Sudi.
Mwili wa Mwamvua baada ya kufukuliwa na Askari Polisi
Miili ya watoto wote wawili baada ya kufukuliwa.

 Na Mwandishi wetu.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida mwanamke mmoja mkazi wa mtaa wa Utusi kata ya Chemchem Manispaa ya Tabora Zuhura Sudi(26) anadaiwa kuwaua watoto wake wawili kwa kuwakaba  shingoni  na baadae kuwachimbia  mashimo  mawili  na kuwafukia.


Tukio hilo ambalo lilihuzunisha baadhi ya watu waliofurika nyumbani kwa mwanamke huyo mtaa wa Utusi(Bakari)   imedaiwa kuwa alilifanya wakati akiwa amebaki nyumbani hapo alipokuwa akiishi yeye na babu yake ukiachilia mbali watoto hao wawili ambao ni marehemu  wakifahamika kwa majina ya  Mwamvua  Mrisho(6) na Sudi mwenye umri wa miezi saba.


Taarifa iliyotolewa  kwa vyombo vya habari na kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora  ACP Juma Bwire imeeleza  kuwa Zuhura akiwa nyumbani kwake na watoto hao wawili aliwakaba shingo hadi kufa,kisha kuwafunga kwenye mifuko ya sandarusi  na kuwafukia katika mashimo mawili aliyoyachimba sebuleni na chumbani.


Taarifa hiyo kutoka Jeshi la Polisi imebainisha kuwa mtuhumiwa Zuhura atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika huku ikilaani vikali tukio hilo la kinyama lililofanywa na mwanamke huyo.


Kwa mujibu wa maelezo ya Mwenyekiti wa mtaa wa Utusi, Bibi Aziza  Mwenya,ushirikiano mkubwa  baina  ya  wananchi  wa mtaa  huo  ndio uliofanikisha  kugundulika  kwa tukio  hilo  la  kinyama  lililopoteza  maisha  ya  watoto  hao  wasiokuwa  na  hatia.


Bibi  Aziza  alisema  baada  ya  kupokea taarifa  kutoka  kwa   Babu  wa  mwanamke  huyo  Zuhura  anayefahamika kwa jina la Shabani Ramadhani  kuhusu  kutoweka  kwa watoto  hao wawili katika  mazingira  ya kutatanisha,walilazimika  kufika  nyumbani  hapo  na kuanza  kumhoji  Zuhura  ambaye alikuwa akizuia watu  kuingia ndani kutokana na tukio hilo la kinyama alilolifanya.


Hata hivyo majirani kwa kushirikiana na Mwenyekiti wao wa mtaa na baba wa mmoja wa watoto hao waliouawa  Bw.Mrisho Abdallah  ambae alikuwa mume wa Zuhura walimvamia na kumshika kwa nguvu  Mwanamke huyo  ili waingie ndani na kubaini kuwa kulikuwa na mashimo mawili aliyokuwa amewafukia watoto hao ambao baadae walikuja kufukuliwa kwa msaada wa Jeshi la Polisi.


Katika mahojiano ya awali yaliyofanywa na mwandishi wetu na muuaji huyo wakati akiwa chumbani mara baada ya kubainika kwa tukio hilo,Zuhura alionekana kutokuwa na wasiwasi  wowote hatua ambayo baadhi ya watu walidai kuwa mwanamke huyo ana lengo la kupoteza ushahidi  kwa kuonesha ametokwa na akili timamu.


Hata hivyo kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa majirani zake wa karibu,mwaka 2013 Zuhura anadaiwa kumsababishia kifo mtoto wake mchanga  wa kiume baada ya kumzidishia dozi ya malaria wakati alipokuwa akiumwa.






No comments: