Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Nachingwea Mh. Mathias Chikawe wakati alipowasili katika kijiji cha Nkotokuyana jimbo la Nachingwea katika mwendelezo wa ziara yake ya mikoa ya Lindi na Mtwara itakayomchukua siku 16 akikagua utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 inayotekelezwa na srikali kwa pamoja na wananchi huku akihimiza uhai wa Chama cha Mapinduzi katika vijiji mbalimbali , Majimbo na wilaya Katika ziara hiyo Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi. (PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-NACHINGWEA-LINDI) Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi akizungumza na Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mhe. Regina Chonjo mara baada ya msafara wa Katibu Mkuu kuwasili katika kijiji cha Mkotokuyana Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliiza Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mhe. Regina Chonjo mara baada ya kufika kwenye shamba la ufuta alilolikagua leo kijijini hapo, Kulia ni Mbunge wa jimbo la Nachingwea Mh. Mathias Chikawe na kushoto ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi Baadhi ya akina mama wanakikundi hichi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM huku wakiwa wameshika majembe yao. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kulia na Mbunge wa jimbo la Nachingwea wakikagua shamba la Mkotokuyana Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kilimo katika shamba hilo huku Mbunge wa jimbo la Nachingwea Mh. Mathias Chikawe akiwa amepanda akishuhudia kazi hiyo. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiendelea na kazi Pamoja na vumbi kubwa kutimka wakati akifanya kazi hiyo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana aliendelea na kazi. Kilimo kimepamba moto Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa ofisi ya serikali ya kijiji cha Naipanga Nachingwea. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi katika kijiji cha Naipanga Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa jiko la shule ya Sekondari Nachingwea High School. Mbunge wa jimbo la Nachingwea Mh. Mathiasa Chikawe akishiriki katika kusafisha shamba la ufuta katika kijiji cha Mkotokuyana. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kung'oa visiki katika shamba la wananchi la kijiji cha Mkotokuyana wilayani Nachingwea.
Thursday, November 20, 2014
Wednesday, November 19, 2014
MAMIA WAJITOKEZA MAZISHI YA MWENDESHA BODABODA,WALAANI VIKALI MAUAJI HAYO-TABORA
"HIVI NI NANI ANAYEFANYA MAUAJI YA BODABODA TABORA?''
"HAMU YANGU NI KUTAKA KUJUA KILICHOANDIKWA MAGAZETINI KILA SIKU"
UZUNDUZI NA UHAMASISHAJI WA MFUKO WA AFYA YA JAMII(CHF) WILAYANI kILINDI MKOANI TANGA
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya afya Mkoa wa Tanga(NHIF)Ally Mwakababu kulia akimuelezea mikakati ya mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) Mkuu wa wilaya ya Kilindi,Suleimani Liwowa kulia kwake kabla ya kufanya uzinduzi wa Uhamasishaji wa wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii wilayani humo (CHF) zoezi ambalo linaendeshwa na Meneja huyo na maafisa kutokana makao makuu na mkoani Tanga kwa muda wa siku kumi. Mkuu wa wilaya ya Kilindi,Suleimani Liwowa akizungumza na viongozi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoa wa Tanga(NHIF) na watumishi wa Halmashauri hiyo Idara ya Afya ofisini kwake kabla ya kuanza uzinduzi wa uhamasishaji wananchi kujiunga na mfuko wa Afya ya Jamii(CHF). Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kilindi,Daudi Mayeji akizungumza na viongozi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoa wa Tanga(NHIF) hawapo pichani waliomtembelea ofisini kwake kabla ya kuanza uzinduzi wa uhamasishaji wilayani humo kulia kwake ni Meneja wa Mfuko wa Bima ya Taifa Mkoa wa Tanga(NHIF) Ally Mwakababu kushoto ni Ofisa wa Mfuko huo kutoka makao makuu Isaya Shekifu. Afisa Uanachama wa Mfuko wa Bima ya Taifa Mkoa wa Tanga (NHIF) Miraji Swalehe akiwaelimisha waendesha pikipiki kwenye kijiji cha Muheza Kata ya Masagalu wilayani Kilindi juu ya umuhimu wa kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) ili kuweza kupata matibabu muda wote. Meneja wa Mfuko wa Bima ya Taifa Mkoa wa Tanga(NHIF) Ally Mwakababu akiwahimiza wananchi wa Kijiji cha Muheza Kata ya Masagalu wilayani Kilindi umuhimu wa kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) wakati wa uzinduzi wake uliofanywa na Mkuu wa wilaya ya Kilindi,Suleimani Liwowa. Mwanachama wa Mfuko wa Afya ya Jamii
(CHF) tokea ulipoanzishwa wilayani humo akimuonyesha kadi zake Meneja
wa Mfuko wa Bima ya Afya Mkoa wa Tanga(NHIF) Ally Mwakababu. Mkuu wa wilaya ya Kilindi Mkoani Tanga,Suleimani Liwowa akiwa kwenye picha ya pamoja na Meneja wa Mfuko wa Bima ya Afya Mkoa wa Tanga(NHIF)Ally Mwakababu na maafisa wengine wa mfuko huo na madereva wa pikipiki “Bodaboda”mara baada ya kuwakabidhi kadi zao za uachama wa Kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF). DC Liwowa akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Muheza Kata ya Masagalu wilayani humo wakati akiwahamasisha kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) wakati wa uzinduzi wake.
Mwisho. Afisa wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)kutoka Makao Makuu ,Isaya Shekifu akiwahamisha wananchi wa Kijiji cha Muheza Kata ya Masagalu wilayani Kilindi mkoani Tanga juu ya umuhimu wa Kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).
(CHF) tokea ulipoanzishwa wilayani humo akimuonyesha kadi zake Meneja
wa Mfuko wa Bima ya Afya Mkoa wa Tanga(NHIF) Ally Mwakababu. Mkuu wa wilaya ya Kilindi Mkoani Tanga,Suleimani Liwowa akiwa kwenye picha ya pamoja na Meneja wa Mfuko wa Bima ya Afya Mkoa wa Tanga(NHIF)Ally Mwakababu na maafisa wengine wa mfuko huo na madereva wa pikipiki “Bodaboda”mara baada ya kuwakabidhi kadi zao za uachama wa Kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF). DC Liwowa akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Muheza Kata ya Masagalu wilayani humo wakati akiwahamasisha kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) wakati wa uzinduzi wake.
Mwisho. Afisa wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)kutoka Makao Makuu ,Isaya Shekifu akiwahamisha wananchi wa Kijiji cha Muheza Kata ya Masagalu wilayani Kilindi mkoani Tanga juu ya umuhimu wa Kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).
BIASHARA YA VITENGE KIGOMA YAVURUGWA NA VITENGE FEKI ZA WACHINA KIGOMA
INADAIWA kuwa,Wachina wamechangia kufubaza Biashara ya
vitenge Mkoa wa kigoma na kupelekea kushuka kwa makusanyo ya kodi za Forodha na
hivyo Mamlaka ya Mapato Tawi la Kigoma kushindwa kufikia lengo la kukusanya kiasi cha milioni 643,300,000
kwa kipindi cha Julai-Septemba 2014.
Akifafanua hilo mbele
ya wandishi wa habari jana katika ofisi ya mamlaka hiyo Kaimu Meneja
wa tawi Patrice Mushi alisema serikali idhibiti uingizaji holela wa bidhaa kutoka nje
ya nchi ambapo, makampuni ya kichina hutumia
sera ya biashara huria hufoji bidhaa mbalimbali na hivyo kupunguza kasi ya
walaji kutumia bandari ya kigoma
kuchukua vitenge kutoka nchi za magharibi .
“wachina wameua soko la vitenge ,makusanyo halisi ya forordha ni milioni 1,062,806,736 bidhaa
hii ndio chachu ,bidhaa ya mafuta si tija kwetu haitabiriki sasa vitenge
vya wax feki za wachina wadau wanatumia bandari ya
Dar-es-salaam na wanauza hapo serikali isimamie kanuni,tratibu tunakwama
“alibainisha Mushi.
Pia alisema TRA kigoma imejiwekea mkakati wa kuimarisha
ukusanyaji wa kodi kupitia mfumo wa kisasa(EFD),vitalu(Block management system)
sanjari na kuendelea kuhamasisha wananchi wadai risiti wakati wanaponunua
bidhaa madukani,ili kuzuia ukwepaji wa kulipa kodi kwa walengwa.
Aidha alisema wafanyabiashara wenye mtaji wa kuanzia milioni
14 wanahitajika kutumia mfumo wa kisasa wa( EFD) na kuahidi kufuatilia
wasiotumia ipasavyo mashine hizo na adhabu kwa walaji wasiodai risiti za bidhaa
walizonunua kwa mujibu wa sheria ya mwaka 2000 na kuzuia bidhaa haramu kwa
walaji.
Hivyo makusanyo ya kodi kwa mwaka 2013/14 wamekusanya kodi
za forodha kiasi cha sh.bilioni 2.9
ambapo lengo ilikuwa wakusanye bilioni 3.2 sawa na 91% ya ufanisi,huku kodi za
ndani wamefanikiwa kukusanya sh.bilioni 6.2 ambapo lengo likiuwa kiasi cha
sh.7.179,400,000 sawa na 87%.
Kwa upande wauza vitenge soko la kigoma mjini na mwanga Ally
Kisala na Tatu Amani kwa nyakati tofauti wakiri hali tete katika uzaji wa vitenge
kutoka nchi ya DRC-kongo ,kutokana na bidhaa hiyo kushikwa na wachina ambao
hutumia bandari ya Dar-es-salaam kwa bei
rahisi .
Awali walikuwa wakiuza vitenge pande tatu 500 kwa mwezi
,ambapo hivi sasa wanauza pande tatu 20 kwa mwezi,hali inayowalazimu washindwe
kuagiza kwa wingi bidhaa hiyo kutoka nchini Congo ,ambapo wax kupitia kongo huuzwa sh.27,000 cha Dar-es-salaam sh.19,000.
Walisema ugumu wa maisha unachangia walaji wengi kuvamia
vitenge kutoka china ambavyo vina bei rahisi ilihali havina viwango vya ubora
na kushauri walaji wathamini ubora wa
bidhaa ili kuepukana na bidhaa rahisi ambavyo ni gharama kwa badae (uimara
mdogo).
Tuesday, November 18, 2014
IGP MANGU AONGEZA ASKARI KITETO
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,IGP
Ernest Mangu akimsikiliza Diwani wa Kata ya Matui Wilayani Kiteto
Bw.Athuman Kidawa wakati alipofanya ziara wilayani humo kufuatia kuwepo
kwa migogoro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji iliyosababisha
kutokea mapigano yaliyosababisha kutokea kwa vifo.kushoto ni Afisa
tarafa wa Matui Bw.Eliakimu Ndelekwa.(Picha na Frank Geofray-Jeshi la
Polisi)
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,IGP
Ernest Mangu akizungumza na wananchi wa Kata ya Matui Wilayani Kiteto
wakati alipofanya ziara wilayani humo kufuatia kuwepo kwa migogoro ya
ardhi baina ya wakulima na wafugaji iliyosababisha kutokea mapigano
yaliyosababisha kutokea kwa vifo. (Picha na Frank Geofray-Jeshi la
Polisi)
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,IGP
Ernest Mangu akizungumza na Mtendaji wa Kijiji cha Chekanao, Kata ya
Kiperesa , Wilayani Kiteto Bw.Omar Ndee (kulia) wakati alipofanya ziara
wilayani humo kufuatia kuwepo kwa migogoro ya ardhi baina ya wakulima na
wafugaji iliyosababisha kutokea mapigano yaliyosababisha kutokea
kwa vifo.Katikati ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Deusdedit
Nsimike pamoja na Mwenyekiti wa Kijiji hicho Bw.Japhet Chafu (Picha na
Frank Geofray-Jeshi la Polisi)
Na Frank Geofray-Jeshi la Polisi, Kiteto.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini
IGP Ernest Mangu ameahidi kuongeza idadi ya Askari katika kijiji cha
Chekanao, kata ya Kiperesa wilayani Kiteto Mkoani Manyara kufuatia
wananchi katika kijiji hicho kujitolea nyumba kwa ajili ya kuishi Askari
kwa lengo la kuimarisha usalama katika maeneo yao kufuatia kuwepo kwa
migogoro ya ardhi inayosababisha kutokea kwa mauaji.
IGP Mangu aliyasema hayo jana
wakati alipokuwa katika ziara Wilayani Kiteto ya kujionea uharibifu
uliojitokeza pamoja na kutafuta ufumbuzi wa migogoro hiyo iliyopelekea
kutokea kwa vifo vya wakulima na wafugaji hivi karibuni katika wilaya
hiyo ambapo watu kadhaa wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kutokana na
vurugu hizo.
Alisema kufuatia kuwepo kwa
umbali mrefu wa kituo cha Polisi na kijiji hicho atahakikisha askari wa
kudumu wanakuwepo ili kushirikiana na wananchi katika kuwabaini wahalifu
wanaofanya vurugu na kuendeleza migogoro hiyo ambapo wananchi nao
waliahidi kujenga kituo cha Polisi.
Kwa upande wake Mtendaji wa
Kijiji cha Chekanao Bw.Omar Ndee alisema wamekuwa wakipata shida
kutokana na umbali mrefu wa kituo cha Polisi jambo ambalo limekuwa
likifanya kuongezeka kwa vitendo vya uhalifu vinavyochangiwa na migogoro
ya ardhi katika wilaya ya Kiteto.
Naye Mwenyekiti wa Kijiji hicho
Japhet Chafu alilishukuru Jeshi la Polisi kwa kuimarisha usalama
kijijini hapo tangu kutokea kwa mauji ya wakulima na wafungaji ambapo
alibainisha kuwa bila kuwepo wao hali ingekuwa mbaya zaidi kutokana na
kutokuwepo na muafaka baina ya wakulima na wafugaji.
“IGP hawa askari wako
wasingekuwepo hapa usingekuta mtu lakini tunawashukuru sana hawa askari
kwa kuwa hivi sasa hali ya usalama imerejea na hata shambani tumeanza
kwenda” Alisema Bw.Chafu.
IGP Ernest Mangu alitumia ziara
hiyo kuzungumza na Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, kamati ya ulinzi na usalama
ya wilaya, Wakaguzi wa Tarafa pamoja na Askari Kata ili kutafuta
ufumbuzi wa migogoro hiyo na kuimarisha hali ya ulinzi na usalama.
Monday, November 17, 2014
MAJAMBAZI YA CONGO YADAIWA KUIBA INJINI ZA MABOTI NA KUMTEKA MVUVI MMOJA -KIGOMA
Na Mageth
Magosso,Kigoma
SINTOFAHAMU
ya wizi katika Ziwa Tanganyika Mkoa wa Kigoma imepelekea,leo Zaidi ya
lita 2,000 za mafuta ,injini saba za
mitumbwi zimeibwa sanjari na kutekwa kwa
mvuvi mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Bendela na majambazi wawili waliokuwa na silaha za moto.
Changamoto
kubwa inachangiwa na sekta ya uvuvi mkoani humo kutopewa kipaumbele kwa mujibu
wa vikao vya ujirani mwema baina ya nchi jirani hasa Congo DRC ambapo raia wake
hutumika kuhujumu uchumi wa wavuvi.
Sendwe
Ibrahimu ni mwenyekiti wa wavuvi Mkoa alisema Novemba 14 ,2014 saa 4.00 usiku
katika mwalo wa katonga uliopo manispaa ya kigoma ujiji na mwalo wa muyowozi
majambazi wawili wakiwa na silaha walifanikiwa kuiba injini saba,lita za mafuta
zaidi ya lita 2000 sanjari na kuteka mvuvi mmoja.
Alisema
baada ya kupewa taarifa ya tukio hilo usiku huo ndani ya dakika 15 aliwasiliana
na katibu tawala mkoa,mkuu wa idara ya majini na Novemba 15,mwaka huu majira ya saa 6.00
mchana wavuvi waliipata simu ya mkononi moja iliyosahaulika na majambazi hayo.
“tulipojaribu
kuitumia moja ya majina ya ile simu alipokea na walipohoji mahusiano na mwenye
simu alitoa lugha chafu,walielekea kusini mwa kijiji cha muyowozi askari
wangethubutu wangewakamata ,maisha ya wavuvi yapo rehani kwa sasa “ alibainisha Ibrahim.
Baadhi ya wavuvi walioibiwa mali zao ni pamoja na Hamza Juma,Ally Said,Geogre Thomas,Baruani
Mrisho,Mashaka Idd,Swabilu Mussa Bigili Sebastiani ambapo kwa nyakati tofauti wakiri kukutwa na mkasa huo huku wakibainisha kupata hasara ya vifaa mbalimbali vya uvuvi sanjari na kijana wao kutoweka anayedaiwa kuteka na wahalifu hao.
Akithibitisha
tukio hilo Kamanda wa Polisi Jafari Mohamed alisema ni kweli , kikosi cha askari kinawatafuta ziwani tangu
usiku wa 14/15 Novemba mwaka huu.
Hata hivyo baadhi ya wavuvi
wamepigwa na butwaa wakiomba serikali ingilie kati wizi wa mashine katika ziwa
hilo na kuwataka wabunge wa kigoma kaskazini na kusini wawajibike katika
hilo.
Saturday, November 15, 2014
TASWIRA YA ZIARA YA MWENYEKITI WA CHADEMA MH.FREEMAN MBOWE MIKOANI
Wananchi wa kijiji cha Igalula mkoani
Kigoma, wakimsikiliza Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), Freeman Mbowe wakati alipokuwa akiwahutubia katika mkutano wa
hadhara wa Oparesheni Delete CCM juzi.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akiwahutubia wananchi wa kijiji cha
Kazuramimba mkoani Kigoma, katika mkutano wa hadhara wa Oparesheni
Delete CCM juzi.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akisalimiana na Bi. Mariamu Ramadhani
(86), baada ya kuwasili katika kijiji cha Kapalamsenga mkoani Katavi,
ambako alihutubia mkutano wa hadhara wa Oparesheni Delete CCM juzi.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (Zanzibar), Salumu Mwalimu akiwahutubia wananchi
wa kijiji cha Kazuramimba mkoani Kigoma, katika mkutano wa hadhara wa
Oparesheni Delete CCM juzi.
Badhii ya waliokuwa viongozi wa Chama
Cha Mapinduzi (CCM) wa serikali ya kijiji cha Kapalamsenga katika jimbo
la Mpanda Vijijini, wakimkabidhi kadi za CCM Mwenyekiti wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, walipoamua kujiunga na
Chadema, baada ya mkutano wa Oparesheni Delete CCM, uliofanyika
kijijini Hapo juzi.
"MASHINDANO YA UBORA WA BANGI KUFANYIKA UHOLANZI NA MAREKANI"
Huu
si mzaha, bali ndiyo ukweli wenyewe. Mashindano hayo ya kushindanisha
ubora wabangi yanayofanyika kila mwaka yakihusisha miji kadhaa ya Ulaya
na Marekani ambapo yamejizolea umaarufu zaidi katika jiji la Amsterdam
nchini Uholanzi yatafanyika hivi karibuni.
Mashindano hayo hukutanisha wadau wanaotumia uraibu huo ambapo wanapata fursa ya kujaribu bure aina mbailmbali za Bangi zilizoletwa na wakulima wanaolima bangi kutoka pande mbalimbali za dunia na kisha kuchagua iliyo bora kuliko zote.
Labda unaweza kushangaa zaidi kwamba mashindano hayo huwa yanafadhiliwa na gazeti moja maarufu linaloitwa HIGH TIMES na mashindano hayo yamekuwa yakifanyika kwa miaka takriban 27 sasa.
Mashindano hayo ambayo yamejizolea umaarufu yanajulikana kama The Cannabis Cup na kwa jiji la Amsterdam nchini Uholanzi yatafanyika kuanzia tarehe 23 mpaka 27 Novemba 2014 na kwa nchini Marekani yatafanyika tarehe tofauti tofauti kwa kila mji na yatahusisha miji yote huku yakipambwa na matamasha ya wanamuziki maarufu watakaoalikwa kutumbuiza.
Kwa wale wakulima wa uraibu huo watakaotaka kushiriki katika mashindano hayo wanaweza kujipatia tiketi za kushiriki kupitia mtandao wa Cannabiscup.com
Kwa maelezo Zaidi mnaweza kupitia mtandao huu:
http://remainintheknow.blogspot.co.uk/2014/11/high-times-cannabis-cup.html.
Mashindano hayo hukutanisha wadau wanaotumia uraibu huo ambapo wanapata fursa ya kujaribu bure aina mbailmbali za Bangi zilizoletwa na wakulima wanaolima bangi kutoka pande mbalimbali za dunia na kisha kuchagua iliyo bora kuliko zote.
Labda unaweza kushangaa zaidi kwamba mashindano hayo huwa yanafadhiliwa na gazeti moja maarufu linaloitwa HIGH TIMES na mashindano hayo yamekuwa yakifanyika kwa miaka takriban 27 sasa.
Mashindano hayo ambayo yamejizolea umaarufu yanajulikana kama The Cannabis Cup na kwa jiji la Amsterdam nchini Uholanzi yatafanyika kuanzia tarehe 23 mpaka 27 Novemba 2014 na kwa nchini Marekani yatafanyika tarehe tofauti tofauti kwa kila mji na yatahusisha miji yote huku yakipambwa na matamasha ya wanamuziki maarufu watakaoalikwa kutumbuiza.
Kwa wale wakulima wa uraibu huo watakaotaka kushiriki katika mashindano hayo wanaweza kujipatia tiketi za kushiriki kupitia mtandao wa Cannabiscup.com
Kwa maelezo Zaidi mnaweza kupitia mtandao huu:
http://remainintheknow.blogspot.co.uk/2014/11/high-times-cannabis-cup.html.
Friday, November 14, 2014
MANISPAA YA KIGOMA UJIJI YACHUNGUZA VINARA WA KUFOJI HATI ZA ARDHI HALMASHAURI
INADAIWA kuwa,Manispaa ya Kigoma Ujiji,inanuka kwa migogoro
ya ardhi ,hali iliyopelekea ofisi ya masjala kuchomwa moto ,kwa nia ya kupoteza ushahidi wa nyaraka
kadhaa zilizopo katika ofisi hiyo,dhidi ya wateja husika.
Mbali na hilo ilielezwa kuwa kuna timu ya watumishi wanaodaiwa kufoji nyaraka
ambapo mkurugenzi husika alipewa orodha ya vinara ,hivyo aliomba muda wa
kulifanyia kazi suala zima la uchakachuaji wa faili za ardhi za wananchi .
Baadhi ya madiwani
walitaka maelezo ya kina juu ya athari zilizotokea kwenye ofisi hiyo,ingawa
tayari manispaa wameshakarabati kabla ya kutoa ufafanuzi wa hilo na hatma ya
wateja wenye madai mbalimbali ili kujua watasaidiajwe.
Akiuliza hoja hiyo katika kikao cha madiwani jana cha robo
ya fedha Julai –Septemba 2014 /15 Diwani
wa Ujiji Majengo Shaban Mkoko alisema wanashangazwa na ukimya wa idara ya ardhi,ambapo wananchi
wanahitaji kujua
athari na namna ya kudhibiti haki kwa wahanga wa nyaraka zilizoungua .
“ najua “data base” imeungua lakini `soft copy ‘zitakuwepo
,idara na mwenyekiti wa kamati ya
mipango miji semeni gharama za mali na
nyaraka zilizoteketea kwa moto na uboreshaji wa jengo mmetumia kiasi gani cha fedha ili umma ujue hatua za nidhamu kwa walengwa zimefikia wapi?
“ alihoji Mkoko.
Diwani wa kata ya Businde Makala Maulidi alisema changamoto
ya migogoro ya ardhi imekithiri kwa watuimishi wa idara husika ,kitendo ambacho
wanatoa hati feki kwa wananchi wasio na uelewa mpana wa mambo na kusisitiza
sheria ya ardhi inatumika vibaya kwa
raia wasiojua mchakato wa kumiliki ardhi kiasili hadi hati.
Akijibia hayo Mwenyekiti wa kamati ya mipango miji ,ujenzi na mazingira Adamu Musa alisema
shida ni wananchi wenyewe wanachangia kupata hati feki na manispaa itaendelea kuvunja nyumba zilizopo
nje ya mipango miji kwa mujibu wa sheria husika na kusihi hati ni chachu ya
kukopesheka na tasisi za kifedha.
Kaimu meya wa manispaa
Ruhomya Rashidi aliongeza kwa kusema kuwa,kuhusu hasara na gharama za
ujenzi wa ofisi hiyo bado zipo katika mchakato wa kisheria na kudai polisi
wanalifanyia kazi .
Akijibia hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa hapa Jafari Mohamed
alipohojiwa juu ya hilo alisema kweli mwezi mmoja ushapita ni hivi,“kiufupi
manispaa haijataka kupata taarifa za thamani ya upotevu wa mali,milango ipo
wazi kwa wateja shida wao wenyewe labda wameridhika
na uhalisia wa tukio”.
Katika kikao cha madiwani jana ilipofika kwenye taarifa ya
utumishi na utawala wandishi wa habari walitolewa nje ya ukumbi kwa madai ya kukosa
sifa za ujumbe hatimaye kikao kilihairishwa
kimya kimya
kwa
mujibu wa kablasha la mkutano husika wameazimia karani andikiwe barua
ya uzembe kazini kwa kusababisha
baadhi ya nyaraka kupotea,karani mpya wa masjara ateuliwe,vitasa vipya
viwekwe na majina manne ya watuhumiwa majina tunayo waitwe kwa ajili ya
mahojiano zaidi..
WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII AFUNGUA KONGAMANO LA NHIF NA WAANDISHI WA HABARI MJINI DODOMA
Waziri
wa Afya na Ustawi wa Jamii Mh. Dr. Seif Rashid akifungua Kongamano la
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya na wahariri pamoja na waandishi wa habari
wa vyombo mbalimbali linalofanyika kwenye hoteli ya New Dodoma mkoani
Dodoma jana, Kongamano hilo la siku mbili linaendelea leo na linajadili
mafanikio mbalimbali na changamoto zinazokabili mfuko huo katika mikoa
mbalimbali na Halmashauri ambazo unatoa huduma zake. Kongamano hilo
linamalizika leo(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DODOMA) Naibu
Katibu wa Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Dr.
Deo Mtasiwa akizungumza katika kongamano hilo wakati akimkaribisha
waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Seif Rashid ili kuzungumza na
washiriki wa kongamano hilo. Kamimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Khamis Mdee akitoa maelezo kuhusu shughuli mbalimbali kwa mwaka mzima. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa masoko na Utafiti NHIF,Raphael Mwamoto, Kaimu Mkurugenzi Tiba na Ushauri wa NHIF, Dk Mkwabi Fikirini na Mkurugenzi wa Mfuko wa Afya ya Jamii CHF Athman Rehani wakiwa katika mkutano huo. Hance John Mwankenja Afisa Mwandamizi , Matekelezo NHIF pamoja na maafisa wengine wa mfuko huo wakiwa katika kongamano hilo. Mkuu wa Wilaya ya Igunga Mh. Elibariki Kingu akitoa mada katika kongamano hilo. Mkurugenzi wa Mfuko wa Afya ya Jamii CHF Bw. Athman Rehani akitoa mada katika Kongamano hilo. Mkuu wa Wilaya ya Igunga na Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Fatma Said Ally wakiwa katika kongamano hilo. Baadhi ya wahariri na waandishi wa habari wakifuatilia mada mbalimbali katika kongamano hilo. Grace Kingalame wa TBC wa pili na wadau wengine wakiwa katika kongamano hilo. Hosea Cheyo wa TBC Mbeya kushoto na Tom Chilala wa Star TV wakifuatilia mada. Wanahabari mbalimbali wakifuatilia kongamano hilo. Baadhi ya maofisa wa NHIF wakiandika mambo muhimu katika kongamano hilo.