Pages

KAPIPI TV

Saturday, November 15, 2014

"MASHINDANO YA UBORA WA BANGI KUFANYIKA UHOLANZI NA MAREKANI"

Huu si mzaha, bali ndiyo ukweli wenyewe. Mashindano hayo ya kushindanisha ubora wabangi yanayofanyika kila mwaka yakihusisha miji kadhaa ya Ulaya na Marekani ambapo yamejizolea umaarufu zaidi katika jiji la Amsterdam nchini Uholanzi yatafanyika hivi karibuni.

Mashindano hayo hukutanisha wadau wanaotumia uraibu huo ambapo wanapata fursa ya kujaribu bure aina mbailmbali za Bangi zilizoletwa na wakulima wanaolima bangi kutoka pande mbalimbali za dunia na kisha kuchagua iliyo bora kuliko zote.

Labda unaweza kushangaa zaidi kwamba mashindano hayo huwa yanafadhiliwa na gazeti moja maarufu linaloitwa HIGH TIMES na mashindano hayo yamekuwa yakifanyika kwa miaka takriban 27 sasa.

Mashindano hayo ambayo yamejizolea umaarufu yanajulikana kama The Cannabis Cup na kwa jiji la Amsterdam nchini Uholanzi yatafanyika kuanzia tarehe 23 mpaka 27 Novemba 2014 na kwa nchini Marekani yatafanyika tarehe tofauti tofauti kwa kila mji na yatahusisha miji yote huku yakipambwa na matamasha ya wanamuziki maarufu watakaoalikwa kutumbuiza.

Kwa wale wakulima wa uraibu huo watakaotaka kushiriki katika mashindano hayo wanaweza kujipatia tiketi za kushiriki kupitia mtandao wa Cannabiscup.com

Kwa maelezo Zaidi mnaweza kupitia mtandao huu:

http://remainintheknow.blogspot.co.uk/2014/11/high-times-cannabis-cup.html.

No comments: