Pages

KAPIPI TV

Friday, November 14, 2014

MANISPAA YA KIGOMA UJIJI YACHUNGUZA VINARA WA KUFOJI HATI ZA ARDHI HALMASHAURI

Na Magreth Magosso,Kigoma


INADAIWA kuwa,Manispaa ya Kigoma Ujiji,inanuka kwa migogoro ya ardhi ,hali iliyopelekea ofisi ya masjala kuchomwa  moto ,kwa nia ya kupoteza ushahidi wa nyaraka kadhaa zilizopo katika ofisi hiyo,dhidi ya wateja husika.


Mbali na hilo ilielezwa kuwa kuna timu ya watumishi wanaodaiwa  kufoji nyaraka ambapo mkurugenzi husika alipewa orodha ya vinara ,hivyo aliomba muda wa kulifanyia kazi suala zima la uchakachuaji wa faili za ardhi za wananchi .


 Baadhi ya madiwani walitaka maelezo ya kina juu ya athari zilizotokea kwenye ofisi hiyo,ingawa tayari manispaa wameshakarabati kabla ya kutoa ufafanuzi wa hilo na hatma ya wateja wenye madai mbalimbali ili kujua watasaidiajwe.


Akiuliza hoja hiyo katika kikao cha madiwani jana cha robo ya fedha Julai –Septemba 2014 /15  Diwani wa Ujiji Majengo  Shaban  Mkoko alisema wanashangazwa na ukimya wa  idara ya ardhi,ambapo  wananchi   wanahitaji  kujua  athari na namna ya kudhibiti haki kwa wahanga wa nyaraka zilizoungua .


“ najua “data base” imeungua lakini `soft copy ‘zitakuwepo ,idara na mwenyekiti wa kamati ya  mipango miji  semeni gharama za  mali  na nyaraka zilizoteketea kwa moto na uboreshaji wa jengo mmetumia kiasi  gani cha fedha ili umma ujue  hatua za nidhamu kwa walengwa zimefikia wapi? “ alihoji Mkoko.


Diwani wa kata ya Businde Makala Maulidi alisema changamoto ya migogoro ya ardhi imekithiri kwa watuimishi wa idara husika ,kitendo ambacho wanatoa hati feki kwa wananchi wasio na uelewa mpana wa mambo na kusisitiza sheria ya ardhi inatumika vibaya  kwa raia wasiojua mchakato wa kumiliki ardhi kiasili hadi hati.


Akijibia hayo Mwenyekiti wa kamati ya  mipango miji ,ujenzi na mazingira Adamu Musa alisema shida ni wananchi wenyewe wanachangia kupata hati feki na  manispaa itaendelea kuvunja nyumba zilizopo nje ya mipango miji kwa mujibu wa sheria husika na kusihi hati ni chachu ya kukopesheka na tasisi za kifedha.


Kaimu meya wa manispaa  Ruhomya Rashidi aliongeza kwa kusema kuwa,kuhusu hasara na gharama za ujenzi wa ofisi hiyo bado zipo katika mchakato wa kisheria na kudai polisi wanalifanyia kazi .


Akijibia hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa hapa Jafari Mohamed alipohojiwa juu ya hilo alisema kweli mwezi mmoja ushapita ni hivi,“kiufupi manispaa haijataka kupata taarifa za thamani ya upotevu wa mali,milango ipo wazi kwa wateja  shida wao wenyewe labda wameridhika na uhalisia wa tukio”.


Katika kikao cha madiwani jana  ilipofika kwenye taarifa ya utumishi na utawala wandishi wa habari walitolewa nje ya ukumbi kwa madai ya kukosa sifa za ujumbe hatimaye  kikao kilihairishwa kimya kimya

kwa mujibu wa kablasha la mkutano husika wameazimia karani andikiwe barua ya uzembe kazini kwa kusababisha baadhi ya nyaraka kupotea,karani mpya wa masjara ateuliwe,vitasa vipya viwekwe na majina manne  ya watuhumiwa majina tunayo waitwe kwa ajili ya mahojiano zaidi..

No comments: