Pages

KAPIPI TV

Monday, November 17, 2014

MAJAMBAZI YA CONGO YADAIWA KUIBA INJINI ZA MABOTI NA KUMTEKA MVUVI MMOJA -KIGOMA

 WAVUVI ZIWA TANGANYIKA
Na Mageth Magosso,Kigoma

SINTOFAHAMU ya wizi katika Ziwa Tanganyika Mkoa wa Kigoma imepelekea,leo  Zaidi  ya lita 2,000 za mafuta ,injini  saba za mitumbwi zimeibwa  sanjari na kutekwa kwa mvuvi mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Bendela  na majambazi  wawili waliokuwa na silaha za moto.

Changamoto kubwa inachangiwa na sekta ya uvuvi mkoani humo kutopewa kipaumbele kwa mujibu wa vikao vya ujirani mwema baina ya nchi jirani hasa Congo DRC ambapo raia wake hutumika kuhujumu uchumi wa wavuvi.

Sendwe Ibrahimu ni mwenyekiti wa wavuvi Mkoa alisema Novemba 14 ,2014 saa 4.00 usiku katika mwalo wa katonga uliopo manispaa ya kigoma ujiji na mwalo wa muyowozi majambazi wawili wakiwa na silaha walifanikiwa kuiba injini saba,lita za mafuta zaidi ya lita 2000 sanjari na kuteka mvuvi mmoja.

Alisema baada ya kupewa taarifa ya tukio hilo usiku huo ndani ya dakika 15 aliwasiliana na katibu tawala mkoa,mkuu wa idara ya majini na Novemba 15,mwaka huu majira  ya  saa 6.00 mchana wavuvi waliipata simu ya mkononi moja iliyosahaulika na majambazi hayo.

“tulipojaribu kuitumia moja ya majina ya ile simu alipokea na walipohoji mahusiano na mwenye simu alitoa lugha chafu,walielekea kusini mwa kijiji cha muyowozi askari wangethubutu wangewakamata ,maisha ya wavuvi yapo rehani kwa sasa “ alibainisha Ibrahim.

Baadhi ya wavuvi walioibiwa  mali zao ni pamoja na Hamza Juma,Ally Said,Geogre Thomas,Baruani Mrisho,Mashaka Idd,Swabilu Mussa Bigili Sebastiani  ambapo kwa nyakati tofauti wakiri kukutwa  na  mkasa  huo  huku  wakibainisha  kupata  hasara ya vifaa mbalimbali vya uvuvi sanjari na kijana wao kutoweka anayedaiwa kuteka na wahalifu  hao.

Akithibitisha  tukio  hilo Kamanda wa Polisi Jafari Mohamed  alisema ni kweli , kikosi cha askari kinawatafuta ziwani tangu usiku wa 14/15 Novemba mwaka huu.

Hata hivyo  baadhi ya wavuvi wamepigwa  na butwaa wakiomba serikali ingilie kati wizi wa mashine katika ziwa hilo na kuwataka wabunge wa kigoma kaskazini na kusini wawajibike katika hilo.

No comments: