Pages

KAPIPI TV

Friday, March 21, 2014

MAUAJI YA MFANYABIASHARA MICHAEL SAMSON,POLISI TABORA YAWASHIKILIA WATU WAWILI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP SUZAN  KAGANDA akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu mauaji ya mtu mmoja ambaye alikuwa ni mfanyabiashara  wa vipuri vya pikipiki mjini Tabora marehemu Michael  Samson ambaye aliuawa usiku baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana ambapo walimpiga kwa jiwe kichwani lililosababisha kifo chake papo hapo.
Hili ndilo jiwe alilopigwa nalo Michael Samson na kupasua eneo kubwa la sehemu ya kichwa na kufariki papo hapo katika Bar ya Uhuru iliyopo mtaa wa Madrasat Kata ya Kanyenye manispaa ya Tabora,Kwa mujibu wa mashuhuda mmoja kati ya wauaji mara baada ya kuwaamuru walale chini wateja watano waliokutwa kwenye Bar hiyo alichukua jiwe lililokuwa umbali wa hatua kumi na kuja kumpiga nalo mara mbili  kichwani  kwa nguvu marehemu Michael hali iliyosababisha kupasuka vibaya kichwa....Hata hivyo Polisi hadi sasa wanawashikilia watu wawili kuhusiana na tukio hilo la kinyama.


Thursday, March 20, 2014

MASHINDANO YA REDD'S MISS TANZANIA KUZINDULIWA



Meneja wa kinywaji cha Redd's Original Victoria kimaro akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam juu ya kuzinduliwa kwa mashindano ya Redd,s Miss Tanzania 2014kulia ni   mkurugenzi wa kamÃ¥uni ya LINO International Hashi Lundenga ambao ni waandaaji wa mashindano hayo na kushoto ni  Meneja Masoko wa kinywaji cha Redd's Original Vimal Vaghmaria.

Mkurugenzi wa kampuni ya LINO International Hashi Lundenga akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam juu ya kuzinduliwa kwa mashindano ya Redd's Miss Tanzania 2014 katikakati ni meneja wa kinywaji cha Redd's Original Victoria Kimaro na mwisho ni Meneja Masoko wa kinywaji cha Redd's Original Vimal Vaghmaria.
Baadhi ya waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari waliohudhuria kwenye uzinduzi jijini Dar Es Salaam.

MAWESE KUPANDA BEI KIGOMA!!!

Na Magreth Magosso,Kigoma

Bidhaa ya Mafuta ya mawese Mkoa wa Kigoma itapanda bei,kutokana na Halmashauri ya wilaya hiyo, kukabidhiwa mradi wa  Kiwanda kidogo cha  kisasa cha uchakataji  wa mafuta hayo.

Pia kujengwa kwa kiwanda hicho ni shabaha ya  kupunguza changamoto ya uchakataji wa awali ambao ulikuwa ukitumia nguvu na muda mrefu katika uchakataji wake, sambamba na ubora usio na kiwango  cha kuteka soko la nje.

Akikabidhi mradi kwa Halmashauri,Meneja wa Mradi wa uhifadhi  Ziwa Tanganyika  Seleboni Mushi alisema bidhaa hiyo itazidishwa ubora na hivyo kuweka ushindani wa soko la nje na nchi za Bara la Asia,huku akitaka halmashauri hiyo watumie sheria,kanuni na taratibu  ili kiwanda hicho kiwe endelevu  leo na siku zijazo.

Kwa Upande wa wachakataji wa zao hilo Fatuma Hamis na Rajabu Hassan alisema kiwanda hicho ni tija kwao kutokana na ubora wa jengo na zana za kisasa ambapo itasaidia kuongeza ujazo wa lita pamoja na ufungaji wa kisasa hali itakayoongeza kipato kuanzia ngazi ya mkulima na mchuuzi wa mafuta hayo.

“hivi sasa bei ya soko la ndani tunauza dumu la lita 20 kwa sh.21,000 lakini kupitia hii itapanda zaidi ya hapa kutokana na ubora wake na kuongezeka kwa lita kutokana na kukamua makapi sahihi” alisema Hamisi

Naye Mgeni rasmi  Katibu tawala wa Mkoa Eng.John Ndunguru alisema ili kulinda mazingira maofisa kilimo wa wilaya hiyo watumie mabaki ya mawese kwenye mfumo wa mbolea ambayo italeta tija kwa wakulima wa kijiji hicho .

Mradi huo umefadhiliwa na GEF ,UNDP huku  kiasi cha milioni 247.55 kimegharimu ujenzi wa kiwanda hicho, wakilenga kupunguza changamoto ya uharibifu wa mazingira katika mfumo wa ucheketaji wa kienyeji ambao hauna tija kwa wakulima na wacheketaji wa mafuta hayo.

MILIONI 47 ZATUMIKA KUWAPA MOTISHA WALIMU KIGOMA


Na Magreth Magosso,Kigoma


Halmashauri  ya  Wialaya ya Kigoma vijijini inatarajia kutumia  zaidi ya milioni 47 kwa ajili ya motisha kwa Walimu 430 watakaokwenda kufundisha shule zilizopo mwambao wa ziwa Tanganyika  na kaskazini kwa tija ya kuboresha viwango vya ufaulu wa wanafunzi .


Hayo yalisemwa katika kikao maalum cha  wadau wa tasisi za mabenki na mifuko ya hifadhi  ya jamii lengo likiwa ni kupata maoni ili kuhakikisha changamoto ya walimu kukataa kuishi vijijini ilipungua  na kuboresha ufaulu wa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ambapo kwa miongo kadhaa imekuwa sintofahamu.


Akizungumzia hilo Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Miriam Mmbaga alisema katika maeneo ya vijijini kunachangamoto ya ukosefu wa walimu ambapo wilaya hiyo imepangiwa walimu 300 wa shule za msingi na walimu 130 shule za Sekondari tatizo hilo litapungua kwa asilimia 50.


Mmbaga alisema kuwa maeneo ya mwambao wa ziwa walimu 102 watapelekwa katika shule za msingi na walimu 37 sekondari nao watapelekwa huko ambapo waliobaki watapelekwa katika vijiji vya wilaya hiyo na kueleza kuwa licha ya kupungua kwa changamoto hiyo lakini bado kunatatizo la ukosefu wa walimu wa masomo ya mchepuo wa Sayansi.


“ Kwa ukanda wa ziwa motisha yao itakuwa godoro ,taa za sola na redio ya kuchaji ,ukanda wa kaskazini watapewa taa za solar na redio ili waweze kupata m,awasiliano na jamaa zao sanjari  na nyumba bora ya makazi “ alisema Mbaga.


Aidha aliwataka wakuu wa idara kuondoa urasimu katika maeneo yao ya kazi ili kuweka uwazi na uwajibikaji jambo litakalowafanya walimu na watumishi waliopo katika maeneo ambayo mazingira ni magumu waweze kuishi na kufanya kazi kama inavyotakiwa ikiwa ni pamoja na kuwanao karibu na kuwazungukia  mara kwa mara kujua hali halisi ya maendeleo ya ufundishaji.


 Kwa upende wa wadau walichangia kiasi cha milioni 21 ambapo kila tasisi husika itatoa milioni tatu ili kufanikisha motisha kwa walimu hao,wakati huohuo halmashauri itatoa milioni 25 ikiwemo usafiri,chakula  na malazi  kwa siku tatu ikiwa ni sehemu ya kuwafariji na kuzoea mazingira halisi ya mkoa huo.


Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Kigalya Husein  Kasala alisema changamoto kubwa inayokabili wakazi wa vijijini ni uhaba wa walimu ukilinganisha na idadi ya wanafunzi  sambamba na ukosefu wa nyumba bora za walimu hali inayochangia walimu wanaopangiwa kuishi huko kukimbia.


Alisema ili kudhibiti  hali hiyo wananchi wa kijiji chake wamejitolea nyumba bora nne kwa ajili ya walimu watakaopangiwa kufundisha huko ,wakati  vijiji vya Pamila ,Kalya na Kalema wameweka utaratibu wa kuwachangia walimu mahitaji mbalimbali ikiwemo mchele,samaki,gunia za mkaa na maharage ili wafundishe vyema.


Aidha tasisi zilizoshiriki kuchangia ni pamoja na CRDB,NMB,Benki ya Posta,Exim Bank,LAPF,NSSF,PSPF,NHIF,na kuahidi kukamilisha michango machi,25,2014,ikiwa ni sehemu ya kuboresha huduma za jamii,huku wadau wakishauri walimu kuzingatia maadili na kuipenda kazi kwa kufuata kanuni,sheria na taratibu zilizopo.

Tuesday, March 18, 2014

HOTUBA YA JAJI JOSEPH SINDE WARIOBA ALIOWASILISHA RASIMU YA PILI YA KATIBA BUNGENI LEO

MADINI YA MAGADI SODA KUIINGIZIA TANZANIA SHILINGI BILIONI 480

mmmmm_8f261.jpg
Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) Abel Ngapemba akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya habari MAELEZO. Katikati ni mkuu wa kitengo cha viwanda vya Kemikali Muhandisi Abdallah Mandwanga, na Mwisho ni ofisa Habari wa Idara mmmm3_72996.jpg
Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) Abel Ngapemba akifafanua kwa waandishi umuhimu wa mradi wa uchimbaji magadi soda katika mkutano na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya habari MAELEZO. Kushoto ni Mhandisi wa mradi Godfrey Mahundi na Kulia ni mkuu wa kitengo cha viwanda vya Kemikali Muhandisi Abdallah Mandwanga. Picha na Georgina Misama – Maelezo. 


IMEELEZWA kuwa Tanzania ni miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa magadi soda yatakayoingizia taifa Shilingi Bilioni 480 kwa mwaka. Hayo yamesemwa na Meneja Uhusiano na Mawsiliano wa Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC), Abel Ngapemba akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.

Ngapemba alisema hatua hiyo inatokana na kugunduliwa kwa kwa kiasi kikubwa cha madini hayo katika Bonde la Engaruka Wilayani Monduli mkoani Arusha. Alizitaja faida za kugundulika kwa madini ya magadi soda kuwa ni ajira zaidi ya 500 na fedha za kigeni kutokana na mauzo ya madini hayo nje ya nchi.

Alisema kuwa viwanda vinavyotegemea magadi soda kama malighafi ya uzalishaji hali itakayochochea kukua kwa sekta ya viwanda hapa nchini. Ngapemba alibainisha kuwa madini ya magadi soda yanatumika viwandani katika utengenezaji wa bidhaa kama vioo, sabuni, dawa za meno, dawa za hosipitali, uoakaji mikate, kutengeneza karatasi, nguo, na usafishaji wa maji.

Alifafanua kuwa utafiti uliofanywa na wataalamu wazalendo kuanzia mwaka 2010 hadi 2013 na ulifanyika kwa awamu tatu yakwanza ikiwa ni uchunguzi wa awali na kutafuta maeneo ya kufanyia uchorongaji ili kubaini wingi na ubora wa magadi soda. Alisema kuwa kazi iliyofanywa na kampuni ya OC, ambapo awamu iliyofuata ni kuangalia njia ya uvunaji wa magadi soda hayo iliyofanywa na JSC Service.

"Matokeo ya utafiti huo yameonyesha kuwapo kwa magadi soda kiasi cha mita za ujazo bilioni 4.7 na inakadiriwa kila mwaka wastani wa mita za ujazo milioni 1.9 zinaongezeka katika eneo hilo," alisema Ngapemba na kuongeza: Alisema kuwa NDC itahakikisha kuwa katika utekelezaji wa miradi hii mazingira hayataathiriwa na tunu za taifa zitalindwa ambapo mtazamo wa shirika hilo ni kuwapo kwa mradi wa uvunaji magadi, utalii, na ufugaji.

CHANZO:The Habari.com

MALINZI USIKUBALI TENA KULIPA MILIONI 15 UWANJA WA TAIFA, KUNJUA MAKUCHA KWA WAHARIBIFU WA VITI!!

                                   Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe, Dar es salaam
0712461967 au 0764302956

Ligi kuu soka Tanzania bara inatarajia kuendelea kesho  machi 19 mwaka huu kwa mechi kali ya vuta ni kuvute kati ya mabingwa watetezi, Young Africans dhidi ya makamu bingwa Azam fc , itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10.30 jioni.

Shirikisho la soka Tanzania kupitia kwa Afisa habari wake, Boniface Wambura Mgoyo limesema tiketi kwa ajili ya mechi hiyo zitaanza kuuzwa saa 2 asubuhi katika magari maalumu .

Vituo vilivyotajwa ni  Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Ubungo Terminal, mgahawa wa Steers uliopo Mtaa wa Samora/Ohio, OilCom Ubungo, Buguruni Shell, Dar Live- Mbagala, kituo cha daladala Mwenge na Uwanja wa Taifa.

Wambura aliongeza kuwa  baada ya saa 6 mchana mauzo yote yatahamia Uwanja wa Taifa ambapo milango kwa ajili ya mechi itakuwa wazi kuanzia saa 7.30 mchana.

 Pia afisa habari huyo alibainisha  viingilio katika mechi hiyo kuwa ni sh. 30,000 kwa VIP A, sh. 20,000 kwa VIP B na C wakati viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani kiingilio ni sh. 7,000.

Wambura alimtaja  mwamuzi Hashim Abdallah wa Dar es Salaam kuwa ndiye atakayechezesha mechi hiyo, huku  akisaidiwa na Anold Bugado (Singida), Florentina Zablon (Dodoma) na Lulu Mushi (Dar es Salaam).

Kamishna wa mechi hiyo atakuwa ni Emmanuel Kavenga kutoka Mbeya wakati mtathimini wa waamuzi ni Alfred Rwiza wa Mwanza.
016 Rais wa TFF, Jamal Emil Malinzi kesho utakubali kuingia mfukoni na kulipa milioni 15 zingine endapo uharibifu utatokea uwanja wa Taifa? 

Wakati mechi hiyo ikisubiriwa kwa hamu, kuna baadhi ya mambo yanatakiwa kuangaliwa kwa jicho la tatu.

Siku za karibuni mashabiki wa klabu za Simba na Yanga wamekuwa wakifanya vurugu ndani ya uwanja wa Taifa, huku wengine waking`oa viti kuashiria kupinga baadhi ya mambo yakiwemo maamuzzi ya waamuzi.

Mashabiki wa timu hizi kubwa wamekuwa wakikosa ustaraabu na uvumilivu pale timu zao zinaposhindwa kupata matokeo.

Pia maamuzi ya waamuzi yamekuwa chanzo cha vurugu hizi ambapo mashabiki huwa wanawalaamu marefa kuvurunda.

Kuna wakati kweli waamuzi wanakosea kwa sababu za kibinadamu,  kwani hakuna aliyeumbwa mkamilifu.

Linapokuja suala la baadhi yao kufanya maamuzi nje ya sheria 17 za soka, hapo inakuwa ngumu kutafsiri kwanini inakuwa hivyo.
yanga v al ahly 8TFF wanatakiwa kuwakumbusha waamuzi kuwa mechi ya kesho ina uzito mkubwa mno katika harakati za ubingwa wa Tanzania bara.

Yanga wanahitaji kushinda ili kupunguza pengo la pointi baina yao na vinara Azam fc.
Mpaka sasa Yanga wao nafasi ya pili kwa pointi 39 nyuma ya Azam waliopo kileleni kwa pointi 43.
Kama Azam fc atashinda kesho inawezekana ikawa mguu ndani- nje kutafuta ubingwa wake wa kwanza tangu kuingia ligi kuu msimu wa 2008/2009.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA CHINI

MWENDESHA BODABODA AMGONGA MTU NA KUMVUNJA MGUU,ATIMUA MBIO NA KUTELEKEZA PIKIPIKI

Ajali mbaya ya pikipiki ambapo mwendesha Bodaboda amemgonga mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Heri Idd mkazi wa kata ya Ng'ambo manispaa ya Tabora,  Idd aligongwa na Bodaboda hiyo wakati akiwa barabarani akiendesha usafiri wake wa baiskeli na mara baada ya kugongwa na kuvunjika mguu,Mwendesha Bodaboda ambaye hakufahamika mara moja aliamua kukimbia na kuicha pikipiki yake imezunguukwa na umati wa watu huku majeruhi akipatiwa msaada wa kupelekwa hospitali ya mkoa wa Tabora Kitete kwa ajili ya matibabu.  
Heri Idd akiwa amelazwa wadi ya majeruhi hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete.(Picha zote na Mpiga picha wetu Mrisho Juma)


MKUTANO WA MPANGO MKAKATI WA MIAKA MITANO WA KUKABILIANA NA MARADHI YASIOAMBUKIZA ZANZIBAR WAFUNGULIWA

DSC_1212
DSC_1215
Mkuu wa Kitengo cha maradhi yasio ambukiza Dk,Omar Mwalim akiwasilisha mada kuhusu Mpango mkakati wa Miaka mitano 2014 hadi 2019 juu ya kukabiliana na magonjwa yasioambukiza Zanzibar hafla iliofanyika katika Hoteli ya Zanzibar Ocean View Zanzibar.
DSC_1219
Mwakilishi kutoka Danida tawi la Zanzibar Dr.Jutta katikati akichangia mada kuhusu kukabiliana na magonjwa yasioambukiza Zanzibar hafla iliofanyika katika Hoteli ya Zanzibar Ocean View Zanzibar.
DSC_1221
Meneja wa Mradi wa Kumaliza Malaria Zanzibar Abdulla Suleiman wapili kulia akichangia mada kuhusu kukabiliana na magonjwa yasioambukiza Zanzibar hafla iliofanyika katika Hoteli ya Zanzibar Ocean View.
DSC_1238
Wasiriki wa Mkutano wa kukabiliana na magonjwa yasioambukiza Zanzibar wakijadiliana kuhusiana na maswali mbalimbali yaliojitokeza katika mkutano huo,hafla iliofanyika katika Hoteli ya Zanzibar Ocean View.
DSC_1226
Wasiriki wa Mkutano wa kukabiliana na magonjwa yasioambukiza Zanzibar wakijadiliana kuhusiana na maswali mbalimbali yaliojitokeza katika mkutano huo,hafla iliofanyika katika Hoteli ya Zanzibar Ocean View .(PICHA NA YUSSUF SIMAI-MAELEZO ZANZIBAR).

THRD YAKUTANA NA WABUNGE WA BUNGE MAALUMU LA KATIBA DODOMA

Wabunge wa Bunge Maalumu la Katiba pamoja na Sekretarieti ya Mtandao wa Watetezi wa haki za binadamu wakati wa mkutano wa utambuzi wa mtandao wa watetezi wa haki za binadamu nchini THRD uliofanyika ukumbi wa Dodoma hotel.

Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa haki za binadamu nchini Bw.Onesmo Olengulumwa akitoa ufafanuzi wa mtandao wa THRD na kuwataka wabunge wa Bunge Maalumu la Katiba kuhakikisha wanaingiza kipengele cha kuwatambua watetezi wa haki za binadamu nchini katika rasimu ya Katiba mpya ambayo inaanza kujadiliwa hivi karibuni Bungeni mjini Dodoma.
Mbunge wa Bunge Maalumu la Katiba Bw.James Mbatia akizungumza katika mkutano huo wa Wabunge wa Bunge Maalumu la Katiba na Sekretarieti ya Mtandao wa Watetezi wa haki za binadamu THRD.
Mbunge wa Bunge Maalumu la Katiba Bw. Tundu Lissu
Baadhi ya Wabunge wa Bunge Maalumu la Katiba wakisikiliza kwa makini kuhusu Mtandao wa Watetezi wa haki za binadamu namna unavyoweza kufanya kazi hapa nchini.
Mbunge wa Bunge Maalumu la Katiba Bi.Magdalena Sakaya ambaye kwa nafasi yake alipongeza kuwepo kwa mtandao wa Watetezi wa haki za binadamu nchini
Mtandao wa Watetezi wa Binadamu Wakutana na Waandishi wa habari na Wabunge wa Bunge Maalumu la Katiba Dodoma.

Sekretariati ya THRDC Jumapili ya tarehe 16 Machi ilikutana na waandishi wa habari za Bunge Maalumu la Katiba mjini Dodomakwa ajili ya semina ya uandishi wa habari za watetezi wa haki za binadamu na pia juu ya masuala kadhaa ambayo watetezi wanataka yawekwe katika katiba mpya.

Matukio yote mawili yaliyoandaliwa mjini Dodoma kati ya THRDC na waandishi na lile la wabunge na Mtandao, yote yaliratibiwa na Bw. Ali Uki ambaye ni mhadhiri wa sheria, mwandishi wa habari wa zamani.

Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Bw. Onesmo Olengurumwa alisema kwamba watetezi wa haki za binadamu wana haki ya kutambuliwa kikatiba na kulindwa. Alisema kuna umuhimu wa wanahabari kutoa taarifa nyingi za watetezi kwa umma. 

Mgeni Rasmi Bi Samia Suluhu, Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba

Aliishukuru sekretariati ya THRDC kwa mualiko huo na kusema kwamba kutambuliwa kwa watetezi wa haki za binadamu kutaisaidia serikali katika utendaji wake. Na pia akaongeza kwamba majadiliano ni njia yenye nguvu kuliko silaha yoyote.

Aliongeza kwamba watetezi wa haki za binadamu wanatambuliwa kimataifa kupitia Azimio la Umoja wa Mataifa lwa Mwaka 1998 juu ya Watetezi wa Haki za Binadamu. Na akasema kutambuliwa kwao kutaongeza ufanisi katika utawala bora kwa kushirikiana na taasisi nyingine kama vile mahakama na kwa kuheshimu mikataba mingine ya kimataifa.

Mkutano wa Mchana na Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba.

Hotuba ya Mratibu Bw. Onesmo Olengurumwa

Alisema kwamba watetezi wa haki za binadamu wanakutana na changamoto nyingi katika shughuli zao. Pia akaongeza kwamba watetezi huongozwa na miito kwa kazi hiyo na wala siyo kwa vigezo vya vyeti vya kitaaluma. Aliongeza kwamba mkutano huo ulilenga kuwafahamisha wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba juu ya shughuli za watetezi na namna ya kuyaingiza masuala yao katika katiba mpya.

Mhe. Tundu Lissu mtetezi, mwanasheria na mjumbe wa Bunge la Katiba

Aliwashukuru watetezi kwa kuandaa semina hii lakini akasema waongeze jitiahada zaidi katika mashirika yao ya haki za biandamu na hata kurekebisha lugha inayotumika katika katiba yenyewe.

Bw. James Mbatia Mbunge, Bunge Maalumu la Katiba

Alikosoa kwa kiwango kikubwa uendeshaji wa haki za baindamu nchini Tanznaia na kuadai kwamba hata sasa hali hiyo ya ukiukwaju wa hakai za biandamu inajonyesha hata katika Bunge Maalumu la Katiba lenyewe kwa viongozi kukiuka kanuni zilizotungwa na wabunge wa Baunge hilo.

Mhe. Samia Suluhu-Makamu Mwenyekiti Bunge Maalumu la Katiba

Alisema katika kipindi hiki tayari Taifa la Tanzania limepiga hatua kubwa ya haki za baindamu ikilinganishwa na hali ilivyokuwa kabla ya mwaka 1992.

Alisema kuwapo kwa mashirika ya watetezi kama vile HakiElimu, Sikika, HakiArdhi n.k. ni kiashiria tosha kwa kwamba taifa hili linaziheshimu na kuzitambua  haki za binadamu. Alisisitiza kwamba katiba mpya iwe yenye kuleta baraka kwa sababu imeundwa katika kipindi cha amani.

Prof Ibrahim Lipumba mjumbe Bunge Maalumu la Katiba

 Wakati akifunga mkutano huo alisema kwamba masuala ya haki za binadamu yasiishie mijini bali yaende hadi vijijini ambako kuna ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.

Alishauri kwamba makundi yanayotetea haki za binadamu yawe na umoja madhubuti kwa sababu Jeshi la Polisi limekuwa likiwabambikizia kesi wapinzani na watu wengine (wakiwamo watetezi) ambao kwa kulia au matendo yao huwaudhi watawala.

Sunday, March 16, 2014

ALBINO MBARONI KWA KUMCHUNA NGOZI MTOTO SEHEMU YAKE YA SIRI


DSC001791
Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Singida SACP, Geofrey Kamwela.

Na Nathaniel Limu, Singida
MKULIMA mkazi wa kijiji cha Nkalankala kata ya Mwanga,tarafa ya Nduguti wilaya ya Mkalama mkoani Singida ambaye ni mlemavu wa ngozi (albino) ,Hidaya Omari (20),anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma ya kumnyonga hadi kufa, mtoto wake wa kiume mwenye umri wa mwaka moja na nusu,na kisha kumchuna ngozi katika sehemu yake ya siri.

Mtoto aliyenyongwa na kuchunwa ngozi ya sehemu yake  ya siri na kutupwa kwenye kisima cha maji chenye kina cha mita moja,ni Richard Paulo.

Imedaiwa pia mama yake mzazi na mtuhumiwa Hidaya,Neema Paulo (35), naye anashikiliwa na polisi kwa tuhuma ya kuhusika  kumnyonga Daudi Richard na kumsababishia kifo.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Singida,SACP,Geofrey Kamwela,alisema tukio hilo la kusikitisha,limetokea machi 13 mwaka huu saa moja na nusu asubuhi huko katika kijiji cha Nkalankala wilayani Mkalama.

Alisema mtoto huyo Daudi,aliokotwa akiwa anaelea juu ya maji ya kisima chenye urefu wa mita moja.

Kamwela alisema uchunguzi wa awali wa jeshi la polisi,umebaini kuwa Daudi (marehemu) aliuawa na kuchunwa ngozi yake na kutumbukizwa katika kisima hicho.

Alisema mwili wa marehemu ulipofanyiwa uchunguzi na daktari katika eneo la tukio na kubaini kuwa kabla ya mauaji jhayo,mtoto huyo alinyongwa shingo yake.Chanzo cha mauaji hayo,inasadikiwa kuwa ni imani ya kishirikina.

Kamanda Kamwela alisema mara upelelezi utakapokamilika,watuhumiwa mtu na mama yake,watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma inayomkabili.

MISS TABORA 2012 ATEMBELEA KITUO CHA WATOTO NA KUFURAHIA SIKU YAKE YA KUZALIWA

Mrembo Sarah Paul aliposhiriki furaha yake ya siku ya kuzaliwa na watoto wa kituo cha TZ 820 FPTC NG'AMBO STUDENT CENTER - Kilichopo Tabora.
Mrembo huyo akiongea na watoto

Miss Pauline (Mshindi namba 3 wa chuo cha Utumishi wa Umma-Tabora) akiongea na watoto.
Sarah akikata keki na watoto.

Baadhi ya vitu alivyowaandalia watoto hao na kuvikabidhi kwenye shirika hilo.
Suleiman H. Halletu (Mkurugenzi wa kituo) akishukuru baada ya kupokea zawadi kutoka kwa Mrembo Sarah kwa ajili ya watoto.
Team nzima iliyomsindikiza mrembo katika hafla hiyo fupi. Kutoka kulia ni Marry, Richard, Miss Zennah (Miss Singida 2012/13), Miss Pauline, Miss Sarah (MissTabora2012), Miss Lilian (Mshindi No2 TPSC 2013), na Annah Henry (Afisa Ugani)
Sarah Paul, mshindi wa shindano la urembo la Redds Miss Tabora 2012, ambaye pia mwaka jana alishiriki katika shindano hilo hadi kufikia fainali za Miss Tanzania.
****
Leo katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa amefanikiwa kuwatembelea watoto wanakusanywa na kanisa la FPCT NG'AMBO wanaopewa msaada na Shirika la Compassion International Tanzania na kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu. Watoto hawa wanakusanywa kwa lengo la kuwatoa na kuwakomboa umaskini wa kiuchumi, kijamii, kimwili na kiroho na kuwawezesha waje wawe watu wazima wanaojua wajibu wao na kujitegemea.

Pia huwalipia ada, huwauguza na kuwapeleka hosipitali wanapoumwa, huwafundisha ujasiriamali n.k Aliyasema  Suleiman H. Halletu mkurugenzi wa kituo kinachoitwa TZ 820 FPCT NG'AMBO STUDENT CENTER na kuongeza kuwa wana watoto 254 katika kituo chao.

ACCESS BENKI YAINGIA KWA KISHINDO TABORA,HOFU YATANDA KWA MABENKI MENGINE!

Mkuu wa mkoa wa Tabora Bi.Fatma Abubakar Mwassa wakati wa ufunguzi wa tawi la benki ya Access mjini Tabora ambalo tayari limeanza kutoa huduma kwa wakazi wa Tabora hasa utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu.



Na Mwandishi wetu, Tabora


WAKAZI wa manispaa ya Tabora na halmashauri zake zote wameanza kunufaika na huduma za benki ya ACCESS yenye makao yake makuu jijini Dar es salaam baada ya kuzinduliwa kwa tawi la benki hiyo mkoani humo.


Sherehe za uzinduzi wa tawi hilo jipya zilifanyika juzi mbele ya ofisi za benki hiyo zilizoko katika jengo la NSSF mjini Tabora ambapo ziliongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Fatma Mwassa aliyeambatana na Mkuu wa wilaya ya Tabora Suleiman Kumchaya na baadhi ya wajumbe wa sekretarieti ya mkoa.


Akizungumza katika sherehe hiyo, Mwakilishi wa Mkurugenzi wa benki hiyo kutoka makao makuu jijini Dar es salaam Emanuel Evans alisema wameanzisha tawi hilo kwa lengo la kuwainua wananchi kiuchumi hususani wakulima na wajasiriamali wadogowadogo.


Alisema benki hiyo imeanza kutoa huduma zake mkoani Tabora tangu tarehe 15 Januari mwaka huu na tangu mda huo mpaka sasa wameweza kutoa mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 950 kwa wananchi zaidi ya 400 na wateja wapya zaidi ya 1,800 wamefungua akaunti.


Alisema kitendo cha wananchi kujitokeza kwa idadi kubwa namna hiyo katika kipindi kifupi cha miezi miwili tu tangu kuanza kwa huduma za benki hiyo ni jambo la kujivunia sana na benki imeahidi kuendelea kuwasaidia ili kutimiza ndoto zao kiuchumi.


‘Kuanzishwa kwa tawi la benki hii hapa Tabora ni habari njema kwa wakazi wote wa mkoa huu na mikoa ya jirani, tunaomba wananchi wote mjitokeze kwa wingi kufungua akaunti na kujipatia mikopo pasipo usumbufu wowote, kufungua akaunti ni sh 1000 tu’, alisema.


Katika taarifa yake mwakilishi huyo alisema Access ni benki iliyodhamiria kuwasaidia Watanzania wenye kipato cha chini na cha kati na pia imelenga kuwa kimbilio la wananchi wote hapa nchini kwa kuwapatia huduma bora za kibenki zitakazowainua kimaisha.


Aliongeza kuwa Access Bank Tanzania (ABT) ni benki ya kibiashara inayokua kwa haraka sana, ilianzishwa mwaka 2007 hapa Tanzania ikilenga kuwasadia wakulima na wajasiriamali wadogo na wakati ambapo mpaka sasa ina jumla ya matawi 10 katika mikoa mbalimbali na imeweza kutoa mikopo kwa zaidi ya wateja 85,000 yenye thamani ya zaidi ya sh bil.325.


Afisa huyo alimwambia Mkuu wa mkoa kuwa ABT imejiwekea utaratibu uliotofauti na taasisi nyingine hapa nchini ambapo huajiri vijana wanaomaliza vyuo na kuwapa mafunzo bila kujali uzoefu wao wa kazi lengo likiwa kuwajengea mshikamano, weredi na utamaduni wa benki.


Mpaka sasa ABT imeajiri wafanyakazi wapatao 600 tangu kuanzishwa kwake hapa nchini wakiwemo wafanyakazi zaidi ya 50 wa tawi la Tabora jambo linaloifanya benki hiyo kuwa moja kati ya benki zilizoajiri wafanyakazi wengi zaidi hapa nchini.


Akizungumzia huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo, Evans alisema ABT inatoa mikopo ya kuanzia sh.100,000 hadi sh.900,000 kulingana na uwezo wa mwombaji, mikopo ambayo hutolewa kwa masharti nafuu sana.


Huduma nyingine ni akaunti ya akiba, akaunti ya hundi, akaunti ya mda maalumu, akaunti ya malengo maalumu, akaunti ya wanafunzi, akaunti ya wafanyakazi, huduma za utumaji na uhamishaji fedha ndani na nje ya nchi kwa kutumia M-PESA, WESTERN UNION, TISS na SWIFT.