Pages

KAPIPI TV

Wednesday, December 24, 2014

UEFA GOO NIGHT CLUB IMEKAMILIKA TAYARI KWA KUTOA BURUDANI LEO KATIKA MKESHA WA KRISMAS

1qKiwanja kipya cha maraha Uefa Goo Night Club kiko tayari kuzinduliwa leo katika mkesha wa sikukuu ya Krismas jijini Dar es salaam Kiwanja hiki ni cha Kisasa sana kama utakavyoona taswira zake zikionyesha maeneo mbalimbali ndani ya klabu hiyo ambayo iko maeneo ya Ukonga Mombasa Barabara ya kuelekea Moshi Baa Karibu na njia panda ya Mahita mita 200 kutoka barabara kuu iendayo Pugu, siku ya katika siku ya mkesha wa Krismas burudani kibao zimeandaliwa na kiwanja hicho kikamilika kila kitu ili kuwapa burudani wateja wake ikiwa ni pamoja na Ligi mbalimbali za ulaya, muziki wa kisasa kama vile Bongofleva, Zuku, Bolingo na miziki mingine mingi ambapo pia vyakula mbalimbali vitapatikana. 2qHii ndiyo mandari yake kwa ndani 3q 5q 6q 7q 8qInjinia wa sauti akiweka sawa mambo yake 9qKaunta ikiwa imesheheni vinywaji mbalimbali tayari kwa kutoa huduma kwa wateja, 10qKaunta ya chini nayo ikiwa imesheheni vinywaji.

ALEX MSAMA AMWAGA ZAWADI ZA KRISMAS KWA VITUO VYA WATOTO YATIMA JIJINI DAR ES SALAAM

1Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akikabidhi vyakula mbalimbali kwa Bi. Honorata wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Honorata kilichopo Temeke jijini Dar es salaam leo wakati alipokabidhi msaada wa vyakula kwa vituo mbalimbali vya jijini Dar es salaam ikiwa ni zawadi yake ya sikukuu ya Krismas kwa vituo hivyo, Bw. Alex Msama amesema pia katika Tamasha la Pasaka litakalofanyika kesho wakati wa sikukuu ya Krismas mkoani Mbeya, kiasi cha fedha zitakazopatikana zitakwenda kulipia ada za watoto yatima katika vituo mbalimbali vitakavyofikiwa na msaada huo, Ameongeza kwamba msaada huo wa vyakula una thamani ya shilingi milioni Nne na Nusu.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM) 2Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akikabidhi vyakula mbalimbali kwa Bi. Halima Mpeta wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Mwandaliwa kilichopo Mbweni jijini Dar es salaam. 3Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akikabidhi vyakula mbalimbali kwa Bw. Rashid Mpinda katibu wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Maunga Centre cha Kinondoni. 4Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akigwa vyakula mbalimbali baada ya kukabidhi kwa vituo vya kulelea watoto yatima jijini Dar es salaam. 5 7Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akifafanua jambo kwa wanahabari mara baada ya kukabidhi msaada wa vyakula kwa vituo vya kulelea watoto yatima jijini Dar es salaam.

UNIC YAELIMISHA SIKU YA CHOO KWA VIJANA WALIO NJE YA SHULE

Siku ya choo duniani ambayo huadhimishwa tarehe 19 Novemba. UNIC waliadhimisha siku hii kwa kuwakutanisha vijana walioko nje ya shule tarehe 23 Desemba 2014 kwa lengo la kuwaelimisha na kuwahamasisha utumiaji wa vyoo ili na wao waweze kuelimisha jamii zinazowazunguka juu ya umuhimu wa kuwa na vyoo.
Tukio hili liliwakutanisha vijana toka vikundi 5: Azimio Youth Group, Makangarawe Youth Development Fund, Mashine Ya Maji Youth Development Centre,Temneke Youth Development Foundation na Tanzania Youth Development Society. Yafuatayo ni baadhi ya matukio katika picha.
TOILET DAY 2014 3 blog 1
Vijana wakiwa katika makundi kujadili na kuweka mikakati watakavyosaidia jamii kuhusu utumiaji wa vyoo na usafi wa mazingira.
TOILOET DAY 2014 4 blog 1
Afisa Habari wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Usia Nkhoma-Ledama akitoa mada kuhusu siku ya Choo duniani pamoja na umuhimu wa utumiaji vyoo, na kampeni maalumu ya uhamasishaji wa kuwa na vyoo.
TOILET DAY 2014 8 blog 2
TOILET DAY 2014 14 blog 2
Mwenyekiti wa Mtandao wa Asasi za Vijana Temeke (Temeke Youth Development Network -TEYODEN), Ismail Mnikite akitambulisha vijana waliohudhuria kutoka makundi mbalimbali.
TOILET DAY 2014 13 blog 2
Baada ya majadiliano, vijana wakiwasilisha maazimio na mikakati waliyoyakusudia kufanya ndani ya vikundi vyao katika jamii zinazowaunguka.
TOILET DAY 2014 25 blog 2
TOILET DAY 2014 19 blog 1

CHANGAMOTO YA UCHAFUZI WA MAZINGIRA-MWANZA

Na Kibada Kibada -Mwanza
MWALO.
 Wafanyabiashara ya samaki na bidhaa nyingine za maliasili katika soko la samaki la Mwalo Halmashauri ya Manispaa ya Ilemeala  Jijini Mwanza wako hatarini kupatwa  na Magonjwa ya mlipuko hasa wakati huku mvua zinazoendelea kunyesha kutokana na changamoto ya uchafuzi wa mazingira uliopo katika soko hilo.
 
Mbali  ya uchafuzi huo pia zipo changamoto nyingine za uhaba  wa vitendea kazi na miundo mbinu mibovu ya kutolea maji kwenye meza za kupokelea samaki pamoja na mrundikano wa taka ngumu na taka nyepesi katika maeneo mbalimbali ya   Soko hilo la Mwalo wa Samaki.
 
Upungufu wa  vitendea kazi kwa wafanyakazi wanashughulikia usafi katika soko hilo hasa samaki ambapo wafanyakazi wanaparua samaki bila kuwa kinga yeyote kwenye mikono yao na wala mabuti ya kuvaa wakati wakiwa kazini hali inayowafanya wafanye kazi katika mazingira magumu.
 
 Changamoto hizo zimebainika  hivi karibuni  pale Madiwani wa Halmashauri ya Mpanda Mkoani Katavi walipofanya ziara ya mafunzo katika Mwalo huo wa samaki kwa lengo la kujifunza namna ya uendeshaji wa Mwalo.
 
Ziara hiyo iliwatembeza maeneo mbalimbali ya soko na kupata ufafanuzi wa kina namna ya uendeshaji wa Mwalo kutoka kwa Viongozi wa Soko hilo,Halmashauri na kutembezwa maeneo mbalimbali hadi  kufika katika maeneo  ya kupokelea na samaki na kujionea jinsi hali ya usafi wa soko ulivyo ambapo walikutana na changamoto hiyo ya  uchafuzi wa mazingira kama uwepo wa taka ngumu na nyepesi.
 
 Soko hilo la Mwaloni  hali  ya usafi  hairidhishi kutokana  na kurudikana kwa taka ngumu, taka nyepesi na miundo mbinu duni ya vitendea kazi kwa watenda kazi wanaoshughulika na shughuli za kila siku katika soko hilo ambalo limesheheni kila aina ya bidhaa hasa mazao ya majini kama samaki pamoja na mazao mengine ya kilimo kama matunda na mbogamboga.
 
Akizungumza na Madiwani waliotoka Halmashauri ya Mpanda kwenda kujifunza masuala ya mwalo Jijini Mwanza Afisa Uvuvi wa Halmashauri ya Manispa ya Ilemela Fabiani Maha ameleza kuwa ipo changamoto kubwa ya uzalishaji wa taka ngumu katika soko hilo kama inavyoonekana  ingawa zinashughulikiwa kadiri inavyowezekana ingawa bado miundo mbinu bado ni changamoto.
 
Mbali ya changamoto ya miundo mbinu pia ameleza kuwa ameeleza kuwa soko linapokea na kuuza biashara za maliasili,kilimo na kuchukua takwimu za uvuvi ,pia kutoa vibali vya uvui na ubora wa mazao ya uvuvi na ushuru wake.  
 
Awali Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza Mhandisi  Lukaza Justini  alieleza kuwa ziwa ni uchumi na maisha na soko hilo lilijengwa mwaka 2006 kwa gharama ya shilingi bilioni sita na shirika la misaada la kijapani JAICA.
 
Mhandisi Lukaza akaeleza kuwa soko linalohudumia wakazi wa Mwanza, Mikoa ya jirani na wale wa ndani na nje ya  nchi ambazo ni Kenya, Uganda,Kongo DRC,Rwanda na Burundi pamoja na Sudani Kusini kwa sasa dagaa wa mwanza na samaki wameonekana kupata soko katika nchi za Asia.

SKYLIGHT BAND YATOA RATIBA YAKE YA WIKI TUKIANZA NA MKESHA WA X-MASS USIKU WA LEO NDANI YA ESCAPE ONE

10675565_408778115946839_5013196848087740184_n
24.12.14 Mkesha wa XMASS tutakua ESCAPE1, show itaanzaa saa mbili usiku, kiingilio buku 7000/= tu: tukutane ESCAPE1 tuikaribishe XMASS
Vile vile tunapenda kutoa taarifa na kuwaomba radhi wadau wetu kutokana na safari yetu ya kanda ya ziwa XMASS hii, show zetu za ijumaa tarehe 26.12.14 thai village na jumapili 28.12.14 ESCAPE1 hazitofanyika.
Ila tukutane tena kwenye mkesha wa mwaka mpya 31.12.14 ndani ya ESCAPE1. .. Burudika na bendi yako katika msimu huu wa siku kuu...Skylight Band...just follow the light ♫
 

OLOLOSOKWAN WAJIWEKA TAYARI KUTIMIZA NDOTO YA KIJIJI CHA DIJITALI

DSC_0010
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues aliposimama kwenye Kijiji cha Ngeresero kwa ajili ya kuwaungisha wanawake wa kimasai wanaofanya biashara ya kuuza bidhaa mbalimbali za shanga kwa watalii wanaosimama kwenye kijiji hicho kwa ajili ya kupata mahitaji mbalimbali, wakati akielekea kijiji cha Ololosokwan kilichopo wilayani Ngorongoro mkoani Arusha kukagua miradi mbalimbali inayofadhiliwa na shirika lake la UNESCO.

Na Mwandishi wetu, Arusha
NDOTO ya kuwa na kijiji cha dijitali nchini Tanzania itaanza kutimia Januari mwakani wakati vifaa vinavyotakiwa kukamilisha mradi huo vitakapowasili kutoka kampuni ya Samsung Electronics.

Kwa mujibu wa watekelezaji wa mradi huo mkubwa unaotarajiwa kutumia dola za Marekani milioni 1, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) vifaa hivyo vinatarajiwa kuingia Bandari ya Dar es Salaam Januari tano mwakani.

Mkataba wa kuanzishwa kwa kijiji cha dijitali eneo la Ololosokwan tarafa ya Loliondo wilayani Ngorongoro ulitiwa saini kati ya Unesco na Samsung electronics Novemba 6 mwaka huu.

Akizungumza na halmashauri ya kijiji cha Ololosokwan , Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la UNESCO Tanzania, Zulmira Rodrigues amewataka wanakijiji kujiandaa kwa mabadiliko makubwa ya kijiji chao kinapoingia katika dunia ya dijitali.
DSC_0007
Alisema mambo ambayo wanastahili kuyaweka sawa ili kufanikisha ndoto zao kuhakikisha eneo ambalo mitambo na miundombinu ya mradi ipo ni lazima lisajiliwe kisheria ili kusiwepo na tatizo katika siku za usoni.

Aidha kutokana na ukubwa wa mashine zinazohusika, hasa makontena ni vyema wanakijiji wakaangalia maeneo korofi katika barabara za kuelekea huko na kuzirekebisha, ili magari hayo makubwa yenye vifaa yapite kwa usalama.

Alisema mradi huo wa miaka mitatu unatarajia kuwawezesha wananchi wa eneo hilo kuwa na ujasirimali, matumizi ya teknolojia ya kisasa katika mawasiliano na utafutaji wa masoko, elimu na afya.

Kwa mujibu wa Bi. Rodrigues kijiji hicho pia kitakuwa na shule iliyoungwa na mtandao wa kompyuta duniani (intaneti), kliniki ya kisasa, tiba kwa kutumia teknolojia ya kompyuta na jenereta kubwa linalotumia nishati ya jua.
DSC_0019
Bw. Abdulaziz Ali wa kitengo cha Transportation and Logistic kutoka UNESCO akitafsiri bei za bidhaa hizo za kimasai kwa wakimama hao wanaofanya biashara za urembo wa shanga kwa watalii na wazawa wanaopita katika kituo kijiji hicho ambapo wengine wao husimama kupata huduma ya chakula na vinywaji.

Aidha kuwapo na mtandao wa kompyuta kutawezesha UNESCO kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kuanzisha mtaala utakaowawezesha vijana wa kimasai ambao ni wafugaji kupata elimu wanayoihitaji.

Mwakilishi huyo wa UNESCO amesema kwamba amefurahishwa na namna watu walivyoitikia mradi huo ambao umelenga kubadili maisha ya wafugaji hao kwa kuwawezesha pia kuitumia vilivyo sekta ya utalii.

“Kupitia mradi huu wananchi wanaweza kujifunza kusoma, kupata maarifa na katika harakati hizo kujua lugha ya kiingereza ili kuwasaidia kuwa na mawasiliano na watalii na watu wengine”, alisema Rodrigues.
DSC_0038
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akiwasili kwenye kata ya Ololosokwan kijiji cha Ololosokwan na kupokelewa na diwani wa kata hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Irkiramat Foundation (RAMAT) Bw. Yannick Ndoinyo.

Alisema ni nia ya Unesco kuhakikisha kwamba inasaidia kufuta ujinga miongoni mwa wafugaji hao bila kuathiri utamaduni wao wanapoingia katika maisha ya kisasa.

Kijiji cha digitali cha Ololosokwan kitakuwa cha nne barani Afrika na yapo makubaliano ya msingi kwamba kijiji kingine kitajengwa Zanzibar mwakani.
DSC_0039
Diwani wa kata ya Ololosokwan, Bw. Yannick Ndoinyo akiongozana na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues aliyefika kijijini hapo kukagua miradi mbalimbali inayofadhiliwa na shirika la UNESCO pamoja na kukagua eneo maalum lililotengwa kwa ajili ya kijiji cha digitali cha Samsung.
DSC_0048
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akisalimiana na baadhi ya kinamama wa mradi wa utalii unaofadhiliwa na shirika la UNESCO kata ya Ololosokwan kijiji cha Ololosokwan wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
DSC_0063
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akizungumza na wakina mama wa kimasai waliojumuika na waume zao mara baada ya kuwasili kijijini hapo ambapo aliwaasa kushiriki elimu ya afya ya uzazi wa mpango ili waweze kuzaa watoto wachache watakaoweza kuwahudumia na aliwaahidi kuwaanzisha program ya kusoma na kuandika kwa ajili ya kuboresha mawasiliano yao na watalii wanaotembelea kijiji chao na kununua biashara zao.
DSC_0111
Pichani juu na chini ni Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akiwaonyesha jambo wakina mama wa kimasai jinsi gani teknolojia inayvowaleta watu kwa ukaribu zaidi kupitia "Tablet" ambapo katika kijiji hicho cha digitali cha Samsung wakazi wa eneo hilo watakua wakipewa mafunzo kutumia kifaa hicho cha "Tablet".
DSC_0129
DSC_0192
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akifafanua jambo nje ya maktaba inayofadhiliwa na UNESCO na kuwanufaisha wanafunzi wa shule ya sekondari Ololosokwani na vijana wa kata hiyo kupanua uelewa zaidi kwa kusoma vitabu mbalimbali wakati akikagua miradi mbalimbali inayofadhiliwa na shirika lake. Kushoto ni Diwani wa kata hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Irkiramat Foundation (RAMAT) Bw. Yannick Ndoinyo.
DSC_0356
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akiwa kwenye mazungumzo na viongozi wa juu wa halmashauri ya kijiji wakati wa ziara yake kijijini hapo mwishoni mwa wiki iliyopita.
DSC_0422
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues katika picha ya pamoja na uongozi wa halmashauri ya kijiji cha Ololosokwan mara baada ya mazungumzo.
DSC_0427
Bi. Zulmira Rodrigues katika picha ya pamoja na baadhi ya wanakijiji wa kijiji cha Ololosokwan kata ya Ololosokwan wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
DSC_0432
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues katika picha ya pamoja na wakina mama wa kimasai wa kata ya Ololosokwan kijiji cha Ololosokwani wilayani Ngorongoro mkoani Arusha mara baada ya kikao na halmashauri ya kijiji hicho.
DSC_0440
Bi. Zulmira Rodrigues akiagana na baadhi ya wakinamama wa kimasai mara baada ya kikao cha halmashauri ya kijiji hicho.
DSC_0228
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues (kulia) akifafanua jambo wakati wa kukagua eneo ambalo mitambo na miundombinu ya mradi itawekwa kwenye sehemu iliyotengwa na halmashauri ya kijiji kwa ajili ya kijiji cha dijitali cha Samsung. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa bodi ya RAMAT, Pokare Koitumet, Diwani wa kata hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Irkiramat Foundation (RAMAT) Bw. Yannick Ndoinyo pamoja na Chifu wa kijiji cha Ololosokwan kata ya Ololosokwan wilayani Ngorongoro mkoa wa Arusha.
DSC_0204
Muonekano wa eneo hilo huku Bi. Zulmira Rodrigues akiendelea kulikagua.

Tuesday, December 23, 2014

TTCL YAANZISHA HUDUMA YA AFYA MTANDAO,YATOA MSAADA WA VYAKULA KWA TAASISI YA KANSA YA OCEAN ROAD


1qLaibu Leonard Meneja Huduma wa kampuni ya simu ya TTCL akikabidhi vyakula mbalimbali kwa Mary Haule Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Ocean Road ya jijini Dar es salaam ambavyo vimetolewa na kampuni hiyo kwa waginjwa wa hospitali hiyo, kulia ni Devotha Kovaga Afisa habari wa hospitali ya Ocean Road. 2qBenjamin Bizele mmoja wa maofisa kutoka kampuni  ya simu ya TTCL akishusha vyakula hivyo huku muugumzi mkuu wa hospitali hiyo Mary Haule akivipokea. 3qMuuguzi Mkuu wa hospitali ya Ocean Road Mary Haule akitoa shukurani zake kwa kampuni ya simu ya TTCL kwa msaada ilioutoa kwa wagonjwa wa hospitali hiyo.
………………………………………………………………………………………………..
 
Na Mwandishi wetu
Dar es Salaam. Wagonjwa wa saratani wa mikoani sasa watapata matibabu ya ugonjwa huo kwa njia ya mtandao baada ya kampuni ya simu Tanzania (TTCL kuzindua huduma  ijulikanayo kwa jina la Afya Mtandao ambayo itamwezesha mgonjwa kupata huduma akiwa katika moja ya hospitali ya rufaa.
 
Akizungumza wakati wa kukabidhi misaada ya vyakula kwa Taasisi ya Kansa ya Ocean Road jana, Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa wateja cha TTCL, Laibu Leonard alisema kuwa kupitia kwa Afya-Mtandao ambayo inatumia mkongo wa taifa wa mawasiliano, madaktari wa Taasisi ya Ocean Road wataweza kuendesha huduma mbalimbali za matibabu pamoja na upasuaji huku wakiwa katika chumba maalum ambacho kitawawezesha kuona na kutoa mtazamo wa wa zoezi la upasuaji linaloendelea mikoani.
 
Laibu alisema kuwa hata huduma ya mionzi itafanyika kwa kushirikisha madaktari bingwa waliounganishwa na huduma hiyo ambayo ni ya kisasa zaidi. Alifafanua kuwa mbali ya mikoani, tiba hiyo inaweza kufanywa hata kwa kushirikisha hospitali kubwa za nchi mbalimbali na hivyo kupunguza gharama kubwa za matibabu.
 
“Hakuna haja ya kwenda India, Uingereza, Ujerumani na nchi nyingine kwa ajili ya upasuaji au huduma nyingine za tiba, unaweza kufanyiwa upasuaji Bugando, madaktari wa Ocean Road, KCMC, Tumbi, Temeke, Mwanyamala na nchi ya Tanzania wataona na kushiriki ipasavyo katika tiba hiyo, hii inatokana na kuunganishwa kwa mtandao ambao utaonyesha picha za video, za kawaida na huduma ya sauti,” alisema Leonard.
 
Alisema kuwa lengo la TTCL ni kuunganisha hospitali zote za rufaa nchini ifikapo mwezi Machi mwakani ili kuraisisha huduma hiyo. Kuhusiana na msaada wa vyakula wenye thamani ya Sh Milioni 3, Leonard alisema kuwa wameamua kutoa msaada huo ili kupunguza gharama za vyakula kwa wagonjwa ambao wamelazwa katika taasisi hiyo.

WANACHAMA WA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA WILAYANI URAMBO WAFURAHIA HUDUMA BORA ZA MATIBABU

Baadhi ya wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya wilayani Urambo wameelezea upatikanaji wa huduma bora za matibabu pindi wanapougua na kufika hospitali ya wilaya ya Urambo mahali ambapo wamepangiwa dirisha lao maalumu kwa ajili ya kusikilizwa na kupatiwa huduma hizo pasipo usumbufu.....Mmoja kati ya wanachama wa Mfuko huo wa NHIF Bi.Mariam Shaban alizungumza na mtandao huu(KAPIPIJhabari.COM) ambapo alibainisha kuwa huduma zinazotolewa kwa wanachama wa mfuko huo zimekuwa ni za kuridhisha na kwamba hakuna mtu anayepanga foleni wakati wa kuonana na Daktari na hata kupatiwa matibabu.

BENKI YA POSTA YAENDESHA SEMINA KWA WAJASILIAMALI MKOANI MBEYA


Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mjini, Profesa Norman Sigallah (aliyesimama) akizungumza akifungua semina kwa ajasiriamali iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mtenda Sunset mjini Mbeya.
Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mjini, Profesa Norman Sigallah (aliyesimama) akizungumza akifungua semina kwa ajasiriamali iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mtenda Sunset mjini Mbeya.
Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mjini, Profesa Norman Sigallah akizungumza akifungua semina kwa ajasiriamali iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mtenda Sunset mjini Mbeya.
Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mjini, Profesa Norman Sigallah akizungumza akifungua semina kwa ajasiriamali iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mtenda Sunset mjini Mbeya.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta, Sabasaba Moshingi akizungumza katika semina kwa ajasiriamali iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mtenda Sunset mjini Mbeya.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta, Sabasaba Moshingi akizungumza katika semina kwa ajasiriamali iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mtenda Sunset mjini Mbeya.
Baadhi ya wajasiriamali wakiwa katika semina hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mtenda Sunset mjini Mbeya.
Baadhi ya wajasiriamali wakiwa katika semina hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mtenda Sunset mjini Mbeya.
Baadhi ya wajasiriamali wakiwa katika semina hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mtenda Sunset mjini Mbeya.
Baadhi ya wajasiriamali wakiwa katika semina hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mtenda Sunset mjini Mbeya.
Baadhi ya wajasiriamali wakiwa katika semina hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mtenda Sunset mjini Mbeya.
Baadhi ya wajasiriamali wakiwa katika semina hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mtenda Sunset mjini Mbeya.
Baadhi ya Maofisa kutoka Benki ya Posta Tanzania (TPB) wakifuatilia mkutano huo.
Baadhi ya Maofisa kutoka Benki ya Posta Tanzania (TPB) wakifuatilia mkutano huo.
Baadhi ya wajasiriamali wakiwa katika semina hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mtenda Sunset mjini Mbeya.
Baadhi ya wajasiriamali wakiwa katika semina hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mtenda Sunset mjini Mbeya.

BENKI ya Posta Tanzania (TPB) Tawi la Mbeya, imetoa semina kwa Wajasiriamali wa mkoa ikiwa na lengo la kuwaongezea ujuzi kwenye biashara zao. Semina hiyo ya siku moja imefanyika kwenye ukumbi wa Mtenda Sunset mjini Mbeya na kufunguliwa na Mkuu wa Wilaya, Profesa Norman Sigallah.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa semina hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta, Sabasaba Moshingi, Mkuu wa Wilaya alitoa wito kwa wajisiriamali kutoogopa kukopa kwenye mabenki ili kukuza mitaji yao na hatimae biashara zao.

Prof. Sigallah alitoa changamoto kwa wajasiriamali kuhakikisha biashara zao zinaubora unaotakiwa ili kuweza kujenga imani na ushindani kwenye soko. Mkuu huyo wa Wilaya alitoa changamoto kwa benki ya Posta kuweka dawati maalum la wataalam watakaotoa ushauri kwa wajasiriamali pindi wanapokuja kuomba mikopo. Aliwashauri wajasiriamali kujiepusha na makundi yenye muelekeo wa kuleta vurugu na kuvunja amani, kwani ili kukua biashara yoyote inahitaji amani na utulivi.

Kwa upande wake, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta, Sabasaba Moshingi, akijibu maswali mbalimbali yaliyoulizwa na wajasiriamali hao zaidi ya 150 waliohudhuria semina hiyo, alisema benki yake itaendelea kuboresha huduma zake hasa upande wa mikopo, na pia kuangalia suala la riba zinazotozwa kwa aina tofauti ya biashara.

“Benki yangu itaendelea kuangalia ni namna gani tunaweza kuweka wataalam watakaotoa ushauri mzuri kwa wajasiriamali ili kupunguza mlolongo mrefu wa nenda rudi kwa mkopaji. Hii ni katika jitihada za kuhakikisha kuwa mkopaji anapata mkopo kwa wakati ili kuwahi fursa iliyojitokeza,”.

Akiongea kwa niaba ya wajasiriamali hao, Bi. Joyce Mkongo, aliishukuru sana benki ya Posta kwa kutoa mafunzo hayo kwao,ambayo yamewafungua macho na kuwaondolewa woga wa kutumia huduma za kibenki. Alisema wajasiriamali wengi wanasita kuchukua mikopo kwa hofu kuwa mali zao zitataifishwa pindi watakaposhindwa kulipa mkopo.