Pages

KAPIPI TV

Thursday, April 23, 2015

MMOJA AFARIKI DUNIA KWA KUGONGWA NA GARI-KIGOMA

Na MagrethMagosso, Kigoma.

MKAZI mmoja amekufa papo hapo na mweingine kujeruhiwa mara baada ya kugongwa na gari aina ya Toyota  maarufu kwa jina la Mchomoko lililokuwa likitokea Manyovu kuelekea Mjini katika barabara ya Kigoma- Kasulu eneo la Sido lililopo Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma.

Akitoa taarifa ya tukio hilo Kamanda wa polisi Mkoa wa Kigoma SACP Fredinandi Mtui alisema tukio hilo lilitokea majira ya saa tatu usiku katika eneo Mlole - Sido  ambapo gari aina ya Toyota lenye namba za usajiri T616 DXR lililokuwa likiendesha na Pitolus Silasi (33), lilisababisha ajali hiyo.

Kamanda alimtaja marehemu kuwa ni Pantoleo Philipo (30) ambaye alikufa popa hapo haku abiria aliyekuwa amembeba katika pikipiki yake akiwa amejeruhiwa vibaya maeneo ya kichwani na kuvunjika mkono na mguu.

Alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa gari ambapo mara baada ya ajali dereva wa gari alitokomea kusiko julikana na kwamba jitihadi za kumsaka zilifanyika na kumkamata ambapo atafikishwa mahakamani mara baada ya kukamilika kwa upelelezi.

Akithibitisha kupokea maiti na majeruhi katika Hospitali ya rufaa Maweni mganga mfawidhi wa hospitali Fadhili Kibaya amesema majira ya usiku alipokea mwili wa marehemu pamoja na majeruhi mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Michael Madyane ambaye amelazwa katika hospitali ya Rufaa maweni kwa matibabu.

Kibaya alisema hali ya majeruhi ni mbaya na kwamba anatakiwa kufanyiwa upasuaji wa mifupa na hivyo kulazimika kumpatia rufaa katika hospitali ya Bugando ambapo kuna  madaktari bingwa wa upasuaji huo.

Alisema licha ya hospitali hiyo kuwa ya rufaa lakini bado inakabiliwa na changamoto ya madaktari bingwa wa magonjwa mbalimbali pamoja na vifaa tiba ambapo jitihada za maksudi zinaendelea ili kukabiliana na changamoto hiyo.

No comments: