Pages

KAPIPI TV

Thursday, April 23, 2015

UVCCM WILAYA YA KIGOMA MJINI WAFANYA ZIARA NA KUBAINI CHANGAMOTO ZA HUDUMA ZA AFYA

Na Magreth  Magosso, Kigoma.

KAMATI  ya utekelezaji ya baraza kuu la umoja wa vijana UVCCM wilaya,  mkoani Kigoma imefanya ziara katika vijiji vya mwambao wa ziwa Tanganyika na kubaini changamoto mbalimbali zinazo wakabili wananchi wa maeneo hayo.

Katibu wa vijana wilaya Pantaleon Rumanyika akizungumza na wandishi wa habari mkoa wa Kigoma alisema  baada ya ziara na  kubaini changamoto kadhaa ikiwemo ya ukosefu wa mganga pamoja na nesi katika zahanati ya Kijiji cha Kagunga.

Amesema zahanati hiyo ina mtumishi mmoja ambaye analalamikiwa na wananchi kutokuwa na vigezo vya kitaalamu sanjari na akinamama wajawazito kutokubali kujifungulia katika zahanati hiyo kwa kuhofia aibu.
 
Rumanyika alisema mtumishi aliyepo ni mwanaume na hivyo kuwa ngumu kwa akinamama wajawazito kufika katika zahanati hiyo na kulazimika kwenda katika vituo vingine na wengina kujifungulia majumbani.

Alisema sambamba na hilo wakazi hao waliiomba serikali iweze kuwatatulia tatizo la ukosefu wa miundombinu ya barabara ya Chankere, Mwamgongo hadi Kagunga ambayo imekuwa ni kero ya muda mrefu licha ya diwani wa kata hiyo Kassimu Nyamkunga kupiga kelele ujenzi wa barabara hiyo katita vijao vya baraza la madiwani.

Alisema kukamilika kwa barabara hiyo itasaidia kuponguza ajali na vifo vinavyojitokeza kwa wasafiri pamoja na akinamama wajawazito ambapo kwa usafiri wa boti hutumia masaa kumi na moja kufika Kigoma mjini kufuata huduma ya kujifungua.

Rumanyika alisema lengo hasa la ziara hiyo katika vijiji vya Kagongo, Mwamgongo, Kagunga, Mahembe pamoja Nyarubanda  ni kuwaandaa vijana kuwa tayari kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura, kusoma vizuri  rasimu ya katiba mpya pamoja na kuwahamasisha kujiunga katika vikundi vya ujasiliamali.

Mganga mkuu wa wilaya Dkt. Jems Jumanne alikiri kuwepo kwa tatizo hilo na kueleza kuwa taratibu za kuagiza mtumishi katika Zahanati zinaendelea na kwamba taratibu za kupata nesi  kwa lengo la kuwahudumia wajawazito zitafanyika.

Alisema tatizo kubwa ni upungufu wa watumishi katika wilaya hiyo ambapo ina jumla ya watumishi 130 na hivyo kuwa na upungufu wa watumishi 294 ambapo kila kijiji kina Zahanati katika wilaya hiyo.

No comments: