Pages

KAPIPI TV

Thursday, April 23, 2015

CCM YAONYA UVUVI HARAMU ZIWA TANGANYIKA

Na Mwajabu Kigaza, Kigoma.

WAVUVI katika ziwa Tanganyika mkoa wa Kigoma  wametakiwa kuacha tabia ya kufanya uvuvi haramu unaosababisha uharibifu wa mazalia ya samaki yaliyopo katika ziwa hilo na kusababisha samaki kutoweka siku za badae.

Kauli hiyo imetolewa na katibu wa umoja wa Vijana UVCCM wilaya Pantaleon Rumanyika wakati wa ziara ya kamati ya utekelezaji  baraza kuu la umoja wa vijana wilaya iliyofanywa katika vijiji mbalimbali vilivyopo mwambao wa ziwa Tanganyika Mkoa wa Kigoma.

Alisema tabia ya uvuvi haramu kwa kutumia nyavu zisizo kubalika kisheria zinaadhiri uharibifu wa mazingira katika ziwa hilo kwa kuuwa mazalia na kusababisha siku za usoni kutoweka kwa samaki katika ziwa Tanganyika.

“Samaki hao wanapo vuliwa huwa wanaoza kwa muda mfupi kutokana na nyavu zinazotumika kusababisha majeraha kwa samaki na hivyo wadudu kushambulia na kuleta madhara kwa binadamu”alisema Rumanyika.

Rumanyika alisema lengo hasa la ziara hiyo katika vijiji vya Kagongo, Mwamgongo, Kagunga, Mahembe pamoja Nyarubanda  ni kuwaandaa vijana kuwa tayari kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura, kusoma vizuri  rasimu ya katiba mpya pamoja na kuwahamasisha kujiunga katika vikundi vya ujasiliamali.

Akizungumzia hilo  ofisa uvuvi wilaya Josephat Gowele alisema tatizo la uvuvi haramu ni changamoto hasa ipo katika maeneo ya Kaskazini ambapo  chanzo kikubwa cha uvuvi haramu ni wavuvi wanaotoka nchi jirani ya Burundi.
Amesema licha ya kuharibu mazalia ya samaki wakati wa uvuvi lakini pia nyavu hizo huwa haziozi mara baada zinapotupwa ziwani na hivyo kusababisha kila samaki anayepita karibu na nyavu hizo kunaswa.

 Amesema uvuvi wa aina hiyo unatoka nchi jirani ya Burundi wakishirikiana na wenyeji wa maeneo hayo hivyo inakuwa vigumu kutokomeza uvuvi huo ambapo watu saba kutoka Burundi walifikishwa mahakamani mara baada ya kufanya doria.

Gowele amesema ili kutokomeza tabia hiyo hakuna budi kufanya doria za mara kwa mara, ulinzi shirikishi baina ya maafisa uvuvi na jamii ambapo vikundi vya BMU  vimeanzishwa katika maeneo yote ya uvuvi lengo likiwa ni kulinda rasilimali zilizopo ziwani.

No comments: