Pages

KAPIPI TV

Saturday, November 22, 2014

TRA YATOA MSAADA KITUO CHA WATOTO YATIMA KIGOMA

Na Magreth Magosso,Kigoma


MAMLAKA ya mapato Tawi la kigoma (TRA) imetumia zaidi ya  sh. Milioni  1.6 kwa kutoa msaada kwa mahitaji ya wajawazito katika vituo vya afya vlivyopo Mkoani ya kigoma ili kuhamasisha jamii juu ya ulipaji kodi.


Mamlaka hiyo imetembelea vituo vya afya vya Kikunku iliyopo manispaa ya Kigoma Ujiji pamoja na Kituo Cha  kulea watoto (vichanga ) yatima  ambacho kinapatikana Halmshauri ya Wilya ya Kigoma vijijini kata ya manyovu ikiwa ni moja kati ya makundi yenye uhitaji zaidi kwaajili ya ukuaji wao.


Misaada iliyotolewa ni pamoja na  maziwa,sabuni ,sukari na mafuta ya kupaka kwa watoto huku wodi ya wajawazito wakinufaika na neti, sabuni na gloves ili kuwawezesha akina mama hawa kujifungua katika mazingira mazuri.


  Akitoa misaada hiyo, kaimu meneja wa TRA Patrice Mushi alisema hakujua kama kituo hicho kina mahitaji makubwa  zinzoendana na changamoto za  kulea watoto hao na kuhakikisha mahitaji yao yote ya muhimu yanapatikana.


“ ofisa ustawi  wilaya ya kigoma alinishauri nilete msaada ,nahisi nilicholeta hakitakidhi hitaji,watoto wana umri wa mika 0-1 wanahitaji madawa na uangalizi mzuri ,motisha kwa walezi  na hawa wenye mambukizi ya virusi vya ukimwi na huyu ana maji kichwani 


Akipokea msaada Mlezi wa kituo cha Matiazo Mary Leonard alisema changamoto iliyopo ni uhaba wa maziwa ,mafuta ya kupakaa,nepi za kisasa,madawa na usafiri na ghrama za kuwapeleka kliniki watoto walio na shida kubwa ya afya,hasa mwenye maji kichwani na wenye shida ya kutoboka kwa moyo.


“ nina miaka 19 tangu nianze kulea watoto vichanga,ambao wengi walitupwa na kufiwa na mama ,ambapo tunalea na ikifika mwaka 1 familia inawajibu wa kumchukua ,shida familia huwatelekeza hawaji kuwachukua na maofisa ustawi hutuachia jukumu la kumsomesha ,mfadhili kajitoa “ alibainisha Leonard.


Kwa upande wa mchungaji wa kanisa la Aglikana Fredy  Stephano alisema chamgamoto ya ugumu wa maisha inachangia familia kutelekeza watoto waliovuka umri wa mika miwili washindwe kuwachukua ,hasa waliofiwa na wazazi wa kike.


Naye ofisa ustawi wa jamii halmashauri ya wilaya ya kigoma  Penina Mbwete alisema awali kituo cha matyazo kilifadhiliwa na WFP kwa kushirikiana na kanisa la anglikana ,hivi sasa WFP  anafadhili wakimbizi na wanatarajia katika bajeti ya 2015/16 kituo kitawekewa bajeti ili kuendelea kutoa huduma husika.


Alisema wanawake waliowengi hivi sasa wanatupa watoto baada ya kujifungua,ambapo mwanzoni mwa mwaka huu kuna mwanamke mmoja alitundika mtoto na kondo lake juu ya mti na kuondoka ambapo wananchi wakishirikiana na ofisa ustawi walimwahisha hospitali ya rufaa na leo ana mwaka 1 na anaitwa Pamela.


Hali ya kutupa watoto vichakani inachangiwa na wanaume kuwakana wanawake wanaowapa ujauzito na wanaume wenye ndoa zaidi ya moja sanjari na michepuko ni chachu ya mimba zenye kutelekeza watoto hatimaye taifa linakabiliana na watoto waishio katika mazingira hatarishi.

No comments: