Pages

KAPIPI TV

Thursday, November 20, 2014

"ILI KUONDOKANA NA HALI HII SULUHISHO NI KUJIUNGA NA MFUKO WA BIMA YA AFYA"

"Ni vema kwa kila Mtanzania bila kujali rangi,dini,kabila au itikadi za kisiasa akawa na mtazamo wa kujali afya yake na familia kwa ujumla.....Kuna kila sababu ya kutambua kuwa msingi mkuu wa maisha ya binadamu ni kutambua umuhimu wa utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazokabili maisha ya kila siku ya mwanadamu ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa uhakika wa chakula cha kila siku huku ukitoa kipaumbele chenye umuhimu wa pekee katika suala zima la AFYA YA MSINGI....Ili kufikia hatua za kukabiliana ipasavyo na  uboreshaji wa huduma za AFYA,hakuna jambo kubwa zaidi ya kuwepo kwa mikakati makini na inayoweza kutekelezeka huku ikiwekewa misingi imara kwa kufuata taratibu,kanuni na sheria ili kuweza kufikia Malengo....Kwa mwananchi masikini njia pekee itakayomsaidia kufikia malengo ya kujiwekea ulinzi kwenye AFYA yake ni kujiunga na MFUKO WA AFYA YA JAMII unaosimamiwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF...Kwa kufanya hivyo mwananchi huyu masikini atakuwa amejihakikishia upatikanaji wa huduma muhimu za afya mahali popote alipo". 

No comments: