Pages

KAPIPI TV

Monday, November 24, 2014

TASAF LAWAMANI - KIGOMA


Na Magreth Magosso, Kigoma.
 
ZAIDI ya wakazi 200 wanaoishi katika kata ya Buhanda mtaa wa Mgeo Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani hapo, wamekosa malipo ya fedha zao kupitia mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF) ilihali wanavocha ya kupata fedha hizo na kudai viongozi husika wanahusika na uchakachuaji wa stahiki za malipo yao .

Lengo la serikali ni kuzinusuru kaya zilizogubikwa na hali duni ya kipato,lakini uchakachuaji wa majina kwenye zoezi la utojai wa fedha umekuwa na utata kwa walengwa hasa wazee.

Hayo yalisema mkoani humo na wakazi zaidi ya 200 , walisema kitendo cha kuondolewa kwa baadhi ya majina ambayo yalipitishwa awali kwa kufuata vigezo vilivyotolewa imewatia mashaka na kudai ni dhuluma inayofanywa na viongozi husika.

 Kassim Kagoma (73), Mwajuma Juma (62) na Mariamu Bakari (75) wote wakazi wa kata ya Buhanda na wahanga wa tukio hilo  kwa nyakati tofauti walisema majina yao yamekatwa katika mchakato wa ulipaji wa fedha za mpango wa TASAF ambapo awali majina hayo yalikuwemo katika orodha ya wanaolipwa.

“Hatuelewi sababu ya sisi wazee kukatwa majina ,tupo 50  ajabu vijana wamelipwa  wengi wao wana miaka 19 tu,wakiwa ni vijana wana  uwezo wa kumudu maisha  ya kila siku, wamedai  fedha zilizobaki zitarudishwa benki” walisema wakazi hao.

Serikali ina nia ya kuwakomboa raia wake lakini shida ipo kwa viongozi husika ,ambao si waminifu na hawana imani ya walengwa ili waondokane na adha zinazowakabili ,ambapo hutumia nafasi hiyo kujinufaisha wenyewe.


Aidha mwenyekiti wa kamati ya usimamizi wa mpango wa kulipa fedha katika kaya maskini Azizi Rusiga alisema jumla ya kaya zilizopo kwenye orodha ya malipo ni takribani kaya 533 kati ya hizo kaya 288 ndio zimelipwa na kaya 244  hazijalipwa fedha  hizo.

 Mchakato wa ulipaji ulianza rasmi Novemba 20 mwaka huu ambapo zaidi ya sh. milioni 13.9 kilitengwa kwa ajili ya kulipa kaya 533 na v kiasi kiongozi walilipa sh.milioni 7.6 na zaidi ya milioni 6.4 zikiwa zimebaki na kudaiwa zitarudishwa benki.

Alisema aligundua uongozi wa TASAF ulitumia orodha mpya ambayo hatukushirikishwa kama ile orodha ya awali haijakidhi kigezo,mbaya zaidi uongozi wa kata hawajui ilihali walengwa wana vocha za kupewa sh.17 kila baada ya miezi miwili na walipoomba orodha mpya walinyimwa.


Mratibu wa TASAF mkoa wa Kigoma Staphod Lilakoma alipohojiwa shutuma hizo alisema malipo yaliyolipwa yamelenga kuanzia mwezi Septemba hadi Octoba na majina yanayotumika kulipa ni majina yaliyofanyiwa marekebisho kwa mara ya pili katika kipindi cha Novemba hadi Desemba ambayo yalikuwa hayana mashaka.

Alisema chanzo cha kukatwa majina  ni kutokana na udanganyifu uliotokea awali na kwamba majina yaliyoorodheshwa awali yalikuwa na mashaka baada ya kugundua kuwepo kwa kaya ndani ya kaya  na lengo la mpango ni kusaidia kaya moja .


Alisema fedha zilizobaki zitarudi benki na taratibu za madai zipo wazi ikiwa ni pamoja na kujaza fomu husika  ili   makao makuu wa yafanyie kazi.

No comments: