Na Mwandishi wetu
Mbunifu
 wa kimataifa wa mavazi kutoka Tanzania, Sheria Ngowi amedhihirisha kuwa
 yeye ni nguli katika ubunifu baada ya kufinika katika onyesho la mavazi
 la kimataifa lijulikanalo kama Mercedes Benz Fashion Week Africa 2014 
lililofanyika juzi Ijumaa mjini Johannesburg, Afrika Kusini.
Ngowi
 alionyesha mkusanyiko wa mavazi aliyoyaita ‘PRIDE’ yaani kujivunia, 
kama moja ya njia za kumuenzi Baba wa Taifa, Mwl. Julius Nyerere pamoja 
na viongozi mashuhuri waliopigania uhuru Afrika.
Afrika
 Kusini ilizizima na kuduwaa kwa muda usiopungua dakika 15 pale ambapo 
mavazi mbali mbali yaliyobuniwa na Ngowi yalipokuwa yakioneshwa katika 
ukumbi wa Melrose Arch.
Sheria
 Ngowi alionyesha mkusanyiko wa mavazi aina ya suti yenye ubunifu na 
ueledi wa hali ya juu kwa kutumia vitambaa vya kisasa na kale 
vilivyonakshiwa kwa maua na rangi za kuvutia kama nyekundu, zambarau, 
machungwa, nyeupe na nyeusi huku mengine yakiwa bila maua lakini 
yaliyong’aa kwa kutumia rangi imara kama blu, kahawia na kijivu.
Onyesho
 hilo la Mercedes Benz Fashion Week Africa 2014 lilihudhuriwa na watu 
mbali mbali wakiwemo viongozi wa umma kutoka Afrika kusini, Balozi wa 
Tanzania Afrika Kusini, Radhia Msuya, wabunifu wa mavazi kutoka nchi za 
Afrika kama Taibo Bacar kutoka Mozambique, David Tlale kutoka Afrika 
Kusini, waandishi wa habari kutoka sehemu mbali mbali za dunia na wadau 
wa mitindo.
Mercedes
 Benz Fashion Week Africa 2014 ni onyesho la kimataifa linalofanyika 
nchini Afrika Kusini mara moja kwa mwaka likikusanya zaidi ya wabunifu 
wa mavazi 35 kutoka Afrika kwa ajili ya kuonesha ubunifu wa mavazi yao 
ambapo kwa mwaka huu Sheria Ngowi ni mbunifu pekee aliyechaguliwa katika
 onyesho hilo kutoka Tanzania.
Sheria
 Ngowi anasifika kwa ubunifu wa mavazi aina ya suti, kanzu,sare za 
makampuni, mashirika, shule na hafla mbalimbali kama harusi.Mbunifu huyu
 alifungua rasmi ofisi zake zilizopo Masaki, mtaa wa Buzwagi mkabala na 
Ubalozi wa Angola mwaka mmoja na nusu uliopita ambapo alianza kazi kwa 
kuwatengenezea mavazi watu kutoka nchi mbalimbali duniani.
Pongezi nyingi kwa Sheria Ngowi, unaipeperusha vyema bendera ya Tanzania kwa kipaji chako na kazi zako nzuri.


















No comments:
Post a Comment