Pages

KAPIPI TV

Wednesday, August 6, 2014

BENKI YA POSTA YADHAMINI KLABU YA WAANDISHI, TASWA SC

1
2
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Moses Manyata (wa kwanza kushoto)akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusiana na hatua ya benki hiyo kuisaidia timu ya waandishi wa habari za michezo nchini Taswa SC. Benki hiyo ilikabidhi hundi ya Sh milioni 2 na pia itasaidia jezi kwa timu ya mpira wa miguu na netiboli. Kwa kwanza kushoto ni Afisa Mawasiliano wa TPB, Chichi Banda na wa kwanza  kulia ni  Taswa SC, Majuto Omary.
3 
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Moses Manyata (wa kwanza kushoto)akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusiana na hatua ya benki hiyo kuisaidia timu ya waandishi wa habari za michezo nchini Taswa SC. Benki hiyo ilikabidhi hundi ya Sh milioni 2 na pia itasaidia jezi kwa timu ya mpira wa miguu na netiboli
……………………………………………………………………………….
 
Benki ya Posta Tanzania (TPB) imeidhamini klabu ya waandishi wa habari za michezo nchini (Taswa SC), kufuatia juhudi zake za kuhamasisha na kuendeleza michezo nchini.
 
Benki hiyo imeisaidia klabu hiyo fedha taslims sh. Milioni 2 na inatarajia kuwapa jezi seti moja moja kwa timu ya mpira wa miguu na mpira wa pete (netiboli) ikiwa ni kuthamini mchango wao Taswa SC katika sekta ya michezo nchini.
 
Kaimu Afisa Mteandaji Mkuu wa TPB, Moses Manyatta alisema kuwa wanafuraha kubwa kusikia kuwa waandishi wa habari za michezo wameamua kufanyakazi kwa vitendo kwa kuanzisha timu ya mpira wa miguu ambayo kwa sasa ina miaka zaidi ya 20 na timu ya mpira wa pete (netiboli) ambayo ina mwaka mmoja na nusu.
 
“Tumefarijika kutokana na ukweli kuwa mbali ya kuandika, mmeamua kufanya michezo kwa vitendo na kuwa mfano wa kuigwa, TPB ipo bega kwa bega nanyi na tutaendelea kushirikiana katika sekta mbali mbali tofauti na michezo,” alisema Manyatta.
 
Alisema kuwa TPB ni benki halisi ya Kitanzania yenye kutoa huduma bora kwa wateja wake na kwa sasa imeingia katika sekta ya michezo ambapo kwa sasa inashirikiana na timu kongwe nchini, Yanga na Simba katika zoezi la kuandikisha upya wanachama na mashabiki wa timu hizo.
 
Mwenyekiti wa Taswa SC, Majuto Omary aliipongeza TPB kwa kutoa msaada huo na kuahidi kuwa wadau wakubwa wa benki hiyo katika shughuli zake mbalimabli.
 
Majuto alisema kuwa wameomba udhamini kwa makampuni mengi kutokana na ukweli kuwa timu yao inachangamoto nyingi pamoja na kuwa na mafanikio makubwa.
 
“Tunawapa pongezi kubwa sana TPB, mmeonyesha kuwa ni benki halisi ya Kitanzania yenye kutoa huduma bora hapa nchini, Taswa SC ipo bega kwa bega nanyi katika kuendeleza gurudumu la maendeleo la nchi hii,” alisema Majuto.
 
Majuto pia aliwaomba wanachama wa timu ya Taswa SC kuwa mstari wambele katika shughuli za TPB kwani wameonyesha kuwajali katika shughuli za kila siku.

No comments: