Pages

KAPIPI TV

Monday, July 21, 2014

MAMIA YA WANANCHI SOMANGA KILWA WAJITOKEZA KUPIMA AFYA BURE,KAYA 70 ZAJIUNGA NA CHF PAPO KWA PAPO WAKIPOKEA MWENGE WA UHURU.

822
Na. Paul Marenga-NHIF LINDI
841
Wananchi wa Kilwa wakiwa kwenye foleni ya kupata huduma za vipimo kwenye banda la Mfuko wa taifa wa bima ya afya ambapo huduma za upimajiwa kiwango cha sukari kwenye damu (RBG),shinikizo la damu (BP),uwiano wa uzito na urefu wa mwili (BMI) na ushauri wa kitaalamu ulitolewa na madaktari,wakati wa mapokezi ya mwenge wa uhuru kwenye viwanja vya shule ya msingi Somanga-Kilwa.
868
Meneja wa mfuko wa taifa wa bima ya afya mkoa wa Lindi Fortunata Kullaya akitoa taarifa ya utekelezaji wa zoezi la upimaji afya na mwitikio wa wananchi wa kilwa ambapo takribani wananchi 257 walijitokeza kupimwa afya na  kaya 73 zilijiunga papo kwa papo na CHF Kwenye banda la mfuko kwa kiongozi wa mwenge kitaifa kwa mwaka 2014 Rachel Kassanda,ambaye alikagua shughuli mbalimbali zilizokuwa zikitekelezwa kwenye viwanja vya shule ya msingi somanga ambapo mwenge wa uhuru ulipokelewa,kulia  ni mkuu wa wilaya ya Kilwa mhe. Abdallah Ulega.
882
Mnafanya kazi kubwa kuisaidia serikali katika kutoa elimu kwa jamii kuchangia huduma za afya ili ziboreke sambamba na upimaji wa afya bure kwa magonjwa yasiyoambukiza  unaomuwezesha mwananchi wa kawaida kupata huduma pasipo gharama..hongereni sana alisema kiongozi wa mwenge kitaifa Rachel Kassanda,huku akisisitiza wananchi kutambua CHF ni mali yao hivyo kujiunga kwao kwa wingi ndiyo msingi wa maboresho ya huduma za afya hususani upatikanaji wa dawa,kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe.Abdallah Ulega,kushoto anayemsikiliza ni Meneja wa NHIF Mkoa wa Lindi Fortunata Kullaya.
892
Kiongozi wa mwenge kitaifa mwaka 2014 Rachel Kassanda akiwataka wananchi wa kilwa kujiunga na CHF,kwani ndiyo mkombozi wa matibabu sasa kwa kuzingatia maboresho ya huduma za afya yanavyowezekana chini ya sera ya urasimishaji wa majukumu kwa jamii hususani ya uchangiaji baina ya wananchi na serikali,ambapo mfuko wa taifa wa bima ya afya unasimamia mfuko wa afya ya jamii kwa niaba ya serikali ,kulia ni mkuu wa wilaya ya Kilwa mhe.Abdalla Ulega ambaye ndiye mwenyeji wa mapokezi ya mwenge wa uhuru.

No comments: