Pages

KAPIPI TV

Monday, July 21, 2014

WANANCHI WAITOLEA MACHO MANISPAA-KIGOMA

Na Magreth Magosso,Kigoma
 
Mradi wa ujenzi wa Gati katika mwalo wa kibirizi katani humo mkoani hapa,upo mashakani  kuanza kwake ,kutokana na  wahanga wa eneo hilo wapatao 53 kuipa siku 30 Manispaa ya kigoma ujiji ili kuboreshewa  stahiki zao  kwa mujibu wa Sera  na Sheria ya Ardhi husika.
Hayo yalisemwa juzi na mwanasheria wa kujitegemea Daniel Rumenyela katika ofisi za chama cha wandishi wa habari mkoani hapa,akiwakilisha adha za wananachi hao, juu ya ufinyu wa fidia usiozingatia sheria ya ardhi ya mwaka 1999 .
“uthamini  ulifanyika 2012 na malipo 2014,kifungu cha( 5),( 4 )ya sheria ya ardhi  na sera ya ardhi inataka fidia itolewe kwa wakati na haraka kwa wahanga na ikichelewa  tathimini  ifanywe   kila baada ya miezi sita, ili fidia ilingane na hitaji la leo” alibainisha Rumenyela.
Alisema  wamempa siku 30 Mkurugenzi wa manispaa ya kigoma Ujiji ,ili aweze kuboresha  haki stahiki za wahusika kwa sheria husika kwa lengo la kuboresha ustawi wa jamii na maendeleo kwa ujumla.
 

Meneja wa Mamlaka ya Bandari TPA wa hapa Patrick Namahuta alipohojiwa juu ya hili alisema mchakato wa kufidiwa kwa walengwa ulifanywa na mthamini wa manispaa hiyo kwa mujibu wa sheria husika na wao walitenga bajeti zaidi  ya milioni 600 ili kukidhi hitaji la walengwa.
 

Alisema TPA taifa ilitoa fidia kwa wahanga hao pasipo mkoa kuhusishwa kikamilifu katika kuhakiki picha na akaunti za walengwa, ili anayelipwa  akiri ni sahihi na kusisitiza malipo yalifanywa makao makuu na akaunti za wahanga zilipelekwa na manispaa husika.
 Namahuta  alisema lengo la mradi huo ni kuboresha huduma kwa wadau,ambapo  mwalo wa kibirizi  ni chachu kibiashara kwa nchi jirani za Burundi na jamuhuri ya watu wa kongo(DRC)  na    ili kukidhi haja za walengwa kwa ukanda wa  ziwa Tanganyika  zinahitajika gati 19 ambayo  itaongeza ufanisi kwa mamlaka hiyo.
Mkuu wa wilaya ya hapa Ramadhan Maneno amekiri mchakato ulifanywa na manispaa husika kupitia mthamini wao na walicholipa TPA ni matokeo ya uthamini na kusisitiza wananchi walishirikishwa kwa kila hatua na kuwasihi walengwa wasitake malipo yalingane.
 Alisema mfumo mbovu wa  malipo  ya fidia hauko vyema, kutokana na  TPA mkoa kutoshirikishwa katika kila hatua  na endapo ingeshirikishwa  ni rahisi kubaini haki na batili kwa lengo la kuondoa utata wa fidia hizo kwa wananachi,ambao  wanamtazamo  hasi kwa  manispaa  katika uwajibikaji .
Kaimu  Mkurugenzi  wa  manispaa  hiyo Moses Weransari alisema mthamini alizingatia uhalisia wa thamani za wahanga  na kwa mara ya mwisho kufanya tathimini ilikuwa 2013 na  wahanga kulipwa rasmi kupitia akaunti zao ni  Juni,2014 .

No comments: