Pages

KAPIPI TV

Wednesday, September 19, 2012

WANANCHI WAOMBA KIVUKO DARAJA LA MBUTU IGUNGA

Na Lucas Raphael,Igunga

 WANANCHI wa kijiji cha mbutu na kata ya mbutu katika  wilaya ya  Igunga Mkoani Tabora wameitaka serikali wilayani humo kuharakisha ujenzi wa Daraja la mto mbutu kabla ya msimu wa mvua za masika hazija anza kunyesha ,ikiwa na kuwapatiwa kivuko endapo Daraja hilo litachukua muda mrefu kukamilika.

Wakizungumuza na gazeti hili lilipo tembelea Daraja hilo wa lisema kuwa Daraja hilo limekuwa nitatizo kubwa kwa wananchi wa Igunga hasa katika kipindi cha masika.

Wameiomba serikali kuharakisha ujenzi huo wa daraja kwa muda uliopangwa ikiwa na kuwapatia kivuko cha dharula ili kuwa epushia adha ambazo walikuwa wakizipata.

Evalist Juma ni mmoja ya wananchi wa kata ya Mbutu akizungumuza kwa nyakati tofauti alisema kuwa Daraja hilo ni kiungo muhimu kwa wananchi wa igunga katika shuguli mbalimbali za kijamii na biashara.

Alisema kuwa kwakipindi hiki ujenzi unaendelea serikali iwapatie kivuko cha dharula ambacho kitaweza kuwa saidia kuvuka wakati shuguli za ujenzi huo zinaendelea.

Evalist alisema katika Daraja hilo watu wengi wamepoteza maisha  wakati wa mvua za masika hali ambayo imekuwa tishio kubwa kwa wananchi wa igunga pamoja na kwa wanasiasa.

‘’Daraja hili nitishio kubwa sana kwa wananchi watu wengi wamekufa hapa kutokana na kubebwa na maji wakati wa mvua za masika tunaiomba serikali ifuatilie suala hili mapema hata viongozi wa siasa wanalijua hili’’alisema Evalist.


Mkuu wa wilaya ya Igunga Elibariki Kingu aliwaha kikishia wananchi wa Igunga kuwa serikali inaendelea na ujenzi huo wa Daraja kwa viwango vikubwa ili kuhakikisha linatumika mapema.

Alisema kuwa Mkandarasi wa ujenzi huo yupo kazini anaendelea na kazi hata hivyo kuhusu suala la kivuko mkuu huyo hakuweza kuzungumzia suala hilo.

Aliwataka wananchi wa Jimbo hilo kuwa watulivu kwa kipindi hiki na kuwataka kuwa kazi zote za kimaendeleo zitaendelea kufanyika kama hapo awari jinsi zilivyo kuwa zikifanyika.

No comments: