Pages

KAPIPI TV

Saturday, May 12, 2012

WALIMU ZAIDI YA 450 WILAYANI NZEGA WAVAMIA KIKAO CHA MADIWANI"Walikuwa wakifisha madai yao,Madiwani wawaunga mkono wataka mkurugenzi aondolewe"

 Walimu wa Shule za msingi na Sekondari walipovamia ofisi ya halmashauri Nzega wakishinikiza kulipwa haki zao
 Baadhi ya viongozi wa Chama cha Walimu Wilayani Nzega wakiwa katika kikao cha pamoja ofisini kwao kabla ya kuvamia kikao cha baraza la madiwani.

 Madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Nzega wakisikiliza kwa makini walipovamiwa na viongozi wa Chama cha Walimu Nzega kueleza kilio chao.
 Mwenyekiti wa CWT Nzega Komredi Peter Mipawa Kashindye akizungumza mbele ya baraza la madiwani.
 Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Nzega Bw.Pelle Anthony akisisitiza jambo katika kikao hicho.

Komredi Peter Mipawa akiwa na walimu nje ya jengo la halmashauri wakisubiri tamko la madiwani kuhusu kero zao dhidi ya mkurugenzi.


ZAIDI YA WALIMU mia nne na hamsini wamelazimika kuvamia kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Nzega na kulitaka baraza hilo kusitisha ajenda walizokuwa wakijadili ili watoe nafasi ya kusikiliza matatizo na kero walizonazo zinazodaiwa kusababishwa na mkurugenzi wa halmashauri hiyo.

Amini usiamini ilikuwa kama mchezo wa kuigiza hapo jana katika ofisi za Chama cha Walimu wilayani Nzega ambapo walimu hao walikutana kuzungumzia namna ya kudai haki zao kutoka kwa mwajiri ambaye ni mkurugenzi.

Moja kati ya haki muhimu ambazo ndio zilizua kizaazaa hicho ni baadhi ya walimu waliandikiwa barua za kupandishwa madaraja(Promosheni)kasha baada ya siku kadhaa ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri hiyo Bw.Kyuza Kitundu ikaanza kuwaita mwalimu mmoja baada ya mwingine kumtaka arejeshe barua aliyopatiwa kwa kigezo kuwa serikali haina fedha za kuwalipa kutokana na kupandishwa kwa madaraja hayo.

Hili lilikuwa tukio ambalo likazua hata madai ya baadhi ya walimu waliokuwa wakidai marimbikizo ya mishahara na haki stahili nyingine ambazo wamekuwa wakisumbuliwa kila kukicha.

Kwaupande mwingine siku hiyo ya kizaazaa hiki tarehe 11 Mei 2012 ilikuwa ni siku ya kikao cha baraza la madiwani hivyo walimu hao wakiwa wanajadili ofisni kwao wakaazimia kufunga safari na kuvamia kikao hicho  na ndipo bila kumumunya maneno viongozi wa CWT Nzega walitamka mbele ya madiwani endapo kama watashindwa madiwani kumuwajibisha mkurugenzi watakuwa tayari kumfikisha mahakamani haraka iwezekanavyo.

Huku wakihusiana kupunguza jazba baadhi ya madiwani wakaonesha kukerwa kwao na madudu ambayo halmashauri hiyo imekuwa ikiyafanya na hivyo kufikia uamuzi wa kuitaka serikali imuondoe mkurugenzi huyo katika halmashauri yao.

Hata hivyo pamoja na CWT kuwapa mzigo madiwani kuhusu madai yao kuyashughulikia,walimu hao wamedai kupitia chama chao wataandamana hadi ofisi ya mkurugenzi na kumfungia mlango ikiwa ni sehemu ya shinikizo la yeye kuwajibika.   

No comments: