Pages

KAPIPI TV

Saturday, May 12, 2012

WACHIMBAJI WADOGO SINGIDA WASIOFUKIA MASHIMO KUCHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA

Mmoja wa wachimbaji wadogo wa madini waliohudhuria mafunzo juu uchimbaji wenye tija KALAEL IGUMI akionyesha cheti chake alichotunukiwa baada ya kumaliza mafunzo.
Baadhi ya wachimbaji wadogo wa madini mkoa wa Singida waliohudhuria mafunzo ya siku tatu yaliyohusu pamoja na mambo mengine kuboresha uchimbaji wao na kuwa na tija zaidi. (Picha zote na Nathaniel Limu).


Na.Nathaniel Limu-Singida

Wizara  ya nishati na madini, imeombwa kuwachukulia hatua kali za kisheria wachimbaji wote wadogo, wasiofukia mashimo wanayoyachimba wakati wakitafuta  madini.

Rai hiyo imetolewa  na wachimbaji wadogo 50 wa madini, waliomaliza mafunzo yao juzi ambayo pamoja na mambo mengine utafutaji na uchimbaji salama wa madini migodini.

Wamesema wachimbaji wengi wadogo wa madini, wamekuwa na utamaduni wa kuchimba mashimo wakati wakitafuta madini, lakini mashimo hayo huyaacha bila kuyafukia kama sheria inavyowataka na hivyo husababisha  ajali ambazo wakati mwingine, huchangia binadamu kupoteza maisha yao na mali zao. 

Akielezea mipango madhubuti serikali kuimarisha sekta hiyo Mjiolojia Sophia Omari amesema  “Uzalishaji wa madini, unaleta mapato kwa serikali, unasaidia kupatikana kwa ajira na mapato kwa wakazi wa vijijini na unapunguza umaskini”.

No comments: