Na Mwandishi Wetu
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi,
Rais Jakaya Kikwete kesho, Jumatatu, May 7, 2012, atawaapisha mawaziri
na Manaibu mawaziri aliowateua katika mabadiliko makubwa ya Baraza la
Mawaziri aliyoyatangaza Ijumaa iliyopita Ikulu jijini Dar es Salaam. Taarifa
iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu jijini Dar es
Salaam, imesema sherehe za kuapishwa kwa mawaziri hao zitafanyika kwenye
viwanja vya Ikulu kuanzia saa 5.30 asubuhi.



No comments:
Post a Comment