Pages

KAPIPI TV

Thursday, August 25, 2011

NYUMBA 317 ZACHOMWA MOTO,WATU 773 HAWANA MAHALI PA KUISHI KIJIJI CHA SHELA, USINGE MKOANI TABORA.

         KIJIJI CHA SHELA, USINGE WILAYANI URAMBO MKOANI TABORA KIMECHOMWA MOTO NA ASKARI WA MALIASILI NA POLISI NA KUZIACHA FAMILIA KADHAA ZIKIWA HAZINA MAKAZI.  

Mkazi wa Kitongoji cha Luganjo Mtoni katika Tarafa ya Usinge mkoani Tabora, Bahati Hussein (kulia), akiwa amekaa na familia yake nje ya mabaki ya nyumba yake, baada ya kuchomwa moto na askari wa wanyamapori na polisi agosti 15 mwaka huu kwa madai ya kujenga katika hifadhi. Nyumba 317 zilichomwa na watu 773 hawana mahali pa kuishi wanaishi vichakani.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Shela  Ngusa Maduhu (kulia) akiwa na familia yake baada ya nyumba yake kuchomwa moto.
Wakazi wa kijiji hicho wakiwaonesha mabaki ya baiskeli iliyoungua moto katika tukio hilo.
WATOTO PORINI:-Watoto wakicheza vichakani katika eneo la wazi walipopewa hifadhi na serikali ya kijiji huku wakiwa hawajui hatima yao.
KILIO:-Mama Mlemavu Magreth Jonas akilia  kwa uchungu wakati akihojiwa na waandishi wa habari waliofika kushuhudia adha iliyowakumba wananchi hawa.
MAISHA  MAPYA:-Baadhi ya wananchi wa kijiji  cha  Shela waliochomewa nyumba zao wakiwa wanalala nje porini pasipokujua hatima yao.
CHAKULA:-Mama akipikia nje baada ya nyumba yake kuchomwa moto huku watoto wake wakisubiri chakula kiive tayari kwa mlo wa mchana.
HASARA:-Mkazi wa kijiji hicho Elia Mrisho akionesha mafuvu ya nguruwe wake waliochomwa moto. Nguruwe 26 waliteketea.

No comments: