Pages

KAPIPI TV

Monday, September 12, 2011

MKAPA AZINDUA KAMPENI IGUNGA





 MKAPA  ATINGA  IGUNGA AZINDUA KAMPENI  ZA CCM, ROSTAM ASHANGAZA WALIOFIKIRIA  HATOFIKA KWENYE KAMPENI. 



 *Rais mstaafu wa awamu ya tatu na mwenyekiti mstaafu wa CCM Benjamin William Mkapa akimnadi mgombea ubunge jimbo la Igunga kwa tiketi ya Chama hicho,wakati wa uzinduzi wa kampeni hizo

*Mbunge mstaafu wa jimbo la Igunga akimuombea kura mgombea ubunge wa jimbo 
hilo Dr.Peter Kafumu Dallaly wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uchaguzi mdogo wilayani Igunga.


Kundi la wachkeshaji maarufu nchini ZEKOMEDY nao hawakubaki nyuma  katika kampeni hizo ambao walifanya ongezeko la idadi ya watu katika uzinduzi huo.          

 KAMPENI IGUNGA  ZAANZA KUCHUKUA KASI KATIKA KINYANG'ANYIRO CHA UBUNGE.
JUMA  KAPIPI
TABORA.

Rais mstaafu wa awamu ya tatu na mwenyekiti  mstaafu wa Chama cha mapinduzi Benjamini  Wiliam Mkapa  amezindua  kampeni  ya uchaguzi mdogo wa jimbo la Igunga  na huku  akisema  kuwa  sera  ya Chama  hicho ya
kujitegemea  ndio  msingi  pekee  utakaosaidia  kuleta  maendeleo  ya wananchi na Taifa
zima kwa  ujumla.

Rais Mstaafu  Benjamini  Mkapa akihutubia
umati  mkubwa  wa  wananchi  waliohudhuria  katika uzinduzi  huo wa  kampeni  hapa  wilayani Igunga  ,akatumia   fursa  hiyo  pia  kuwataka  wananchi  kuwabeza  wapinzani  wanaodai  kuwa  serikali  ya  ccm hadi  hivi  sasa  haijafanya   lolote huku akianisha  mafanikio  kadhaa  yaliyopatikana  ikiwa  ni pamoja  na  uboreshaji  wa sekta  mbalimbali zikiwemo  za  elimu,afya na kilimo.  

Amesema serikali ya CCM itaendelea kuwahakikishia huduma
bora wananchi wake ingawa kila jambo linafanyika kwa wakati kulingana  na  changamoto zinazozikabili sekta mbalimbali na hasa za kiuchumi.

Kwa upande mwngine akatumia fursa hiyo kuumbusha umma wa watanzania
kwa yale mafanikio yaliyopatikana  tangu
wakati wa serikali ya awamu ya tatu huku akiyaainisha kuwa ni pamoja na ujenzi
wa Bunge la kisasa la jamhuri ya muungano wa Tanzania,ujenzi wa barabara kwa
kiwango cha lami hatua ambayo pia bado amedai kuwa inaendelezwa na serikali ya
awamu ya nne ambayo  kwa sehemu kubwa
imeendelea kuboresha elimu kwa ujenzi wa chuo kikuu cha Dodoma.  

Kwa  upande  wake  mbunge mstaafu  wa  jimbo  hilo  Bw. Rostam  Azizi  ambaye  ilivumishwa  kuwa  huenda  asinge  shiriki  katika  uzinduzi  huo  wa  kampeni  kutokana  na  hatua ya  kujiuzuru  kwake,jambo  ambalo  kwasasa  lilikuwa  ni  kinyume  na  hivyo   akapanda  jukwaani  kumpigia  debe  mgombea  wa  ubunge  kupitia  chama  cha  mapinduzi  Dr.Peter  Kafumu.

Hata hivyo kitendo cha Rostam kupanda  jukwaani na kumnadi mgombea wa CCM kimeendelea kuzua minong'ono hapa wilayani Igunga kutokana na ukweli kwamba idadi kubwa ya watu walikuwa bado wanamhitajia kuwa awe mbunge wao na hata kufikia hatua kujiuzuru kwake


Aidha  katika  uzinduzi  huo  wa  kuanza  mbio  za  uchaguzi  mdogo  jimbo  la  Igunga  unaoshirikisha  vyama  vinane  vya  siasa,kwa  upande  wa  ccm  uzinduzi  huo  ambao  umefanyika  katika  viwanja  vya  sokoine  ulipambwa  kwa  ngoma  mbalimbali  ikiwemo  bendi maarufu  nchini  ya  T.O.T ,wasanii  maarufu  Vick kamata ,Dokii,Afsa  kazinja  na  kundi  la  orijino  komedi  toka  jijini  Dar-es-salaam.   

No comments: