Pages

KAPIPI TV

Friday, September 11, 2015

KAMPUNI YA SIMU YA TIGO NA DTBi WAZINDUA HUDUMA YA KUREJESHA KUMBUKUMBU NA KUZUIA WIZI WA SIMU ZA MKONONI DAR ES SALAAM

Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Dk.Binilith Mahenge (kulia), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kituo cha oparesheni  cha Kampuni ya MagilaTech, iliyotengeneza teknolojia ya tigo backup inayowezesha kurejesha kumbukumbu na kuzuia wizi wa simu za mkononi Dar es Salaam leo. 
Wanahabari na wadau wengine wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa DTBi, Mhandisi George Mulamula (kulia), akizungumza katika uzinduzi huo.
Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez (kulia), akitoa hutuba yake.
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dk. Hassan Mshinda (kulia), akizungumza katika uzinduzi huo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya DBTi, Balozi Ami Mpungwe.
Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Dk.Binilith Mahenge, kwa niaba ya Makamu wa Rais Dk.Mohammed Gharib Bilal aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo akisoma hutuba.
Meneja wa mradi huo kutoka Tigo, Atuletye Mwamila (kulia), akielekeza jinsi teknolojia hiyo inavyofanya kazi na kuwezesha kuipata simu iliyopotea na kumbukumbu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Magila Tech iliyotengeneza Teknolojia ya Tigo Backup, Godfrey Magila akielezea jinsi teknolojia hiyo inavyofanya kazi.
Mwenyekiti wa Bodi ya DBTi, Balozi Ami Mpungwe (kushoto), akizungumza katika uzinduzi huo. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dk. Hassan Mshinda.
Wanahabari wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Maofisa wa ufundi, Rahim Hussen (kushoto) na Mkupete Mkamba (kulia), wakitoa maelezo wa kifaa mfano wa ndege kinachorushwa angani na kuweza kubaini magonjwa katika mimea walicho kibuni.
Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Dk. Binilith Mahenge (katikati), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kituo cha oparesheni  cha Kampuni ya Magila Tech, iliyotengeneza teknolojia ya tigo backup inayowezesha kurejesha kumbukumbu na kuzuia wizi wa simu za mkononi Dar es Salaam leo, kilichopo Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech). Kituo hicho kinashirikiana na kampuni ya simu ya tigo, Dar Teknohama Business Incubator (DTBi), pamoja na Costech kuendesha mradi huo. Kutoka kulia ni Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Magila Tech iliyotengeneza Teknolojia ya Tigo Backup, Godfrey Magila na Ofisa Mtendaji Mkuu wa DTBi, Mhandisi George Mulamula
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Magila Tech iliyotengeneza Teknolojia ya Tigo Backup, Godfrey Magila (kulia), akitoa maelezo kwa Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Dk. Binilith Mahenge jinsi kituo hicho cha oparesheni kinavyofanya kazi.


Na Dotto Mwaibale


KAMPUNI ya Mawasiliano ya simu ya Tigo kwa kushirikiana na Kituo cha Kukuza Vijana Wenye Mawazo ya Sayansi na Teknolojia (DTBi), wamezindua huduma itakayowawezesha watumiaji wa simu za kisasa (smartphone) kurejesha kumbukumbu na kupatikana kwa simu iliyopotea au kuibiwa.

Akizungumza kabla ya kuzinduliwa rasmi huduma hiyo Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dar es Salaam leo asubuhi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Dk.Binilith Mahenge, Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez, alisema huduma hiyo inaitwa 'Tigo Backup' itakuwa na uwezo wa kurudisha majina yote kwenye simu, picha, video, ujumbe mfupi 'sms' na vitu vingine vilivyopotea.

Alisema mteja ataweza kugundua na kurejesha simu zao zilizopotea au kuibiwa na pia huduma hiyo itamuwezesha mteja kuwa na uwezo wa kupata picha ya aliyemuibia kwani simu itapiga king'ora.

" King'ora hicho kitaonesha simu ilipo, simu itajifunga ili kuzuia matumizi mabaya, kumjulisha mwenye simu pindi abadilishapo laini na kwamba huduma hiyo imebuniwa na mwanafunzi mzawa kutoka DTBi ," alisema Gutierrez.

Kwa upande wa Waziri, Dk. Mahenge alizishukuru kampuni hizo kuwajengea uwezo na kuwawezesha Watanzania kuleta maendelea katika nchi yao na kujijengea utajiri kupitia ubunifu huo.

Alisema Tanzania nchi inayoungwanishwa kidigitali zaidi kwa kutumia sismu kuliko kompyuta na kwa mujibu wa takwimu za watumiaji wa simu zinaonesha kuna ongezeko kubwa kutoka watu milioni 2.96 mwaka 2005 hadi milioni 33 mwaka huu.


Alisema kwa kutambua nchi ni changa ambayo watu wake asilimia 50 ni vijana, wamejikita katika kutoa elimu ya ufundi katika sayansi na teknolojia yenye ubunifu. 

A SAFE AND FUN HAVEN FOR FAMILIES

IMG_7896
Head of Marketing The Walt Disney Company Africa, Deirdre King, talking to journalists (not in picture) who were attending the second edition of MultiChoice Africa Content Showcase Extravaganza #OnlyTheBest which held in Outrigger Mauritius Beach Resort, Bel Ombre recently.(Photo by Zainul Mzige of Modewjiblog)

Disney Junior, which airs on DStv channel 309 and GOtv Plus channel 60, is learning-focused and reflects the emotional connection that generations of consumers have to Disney storytelling and characters, both classic and contemporary. It invites mum and dad to join their child in the Disney experience of magical, musical and heartfelt stories and characters, while incorporating specific learning and developmental themes.

Reaching over 1.3 million kids and their families across Africa every day, Disney Junior now airs in 111 countries, with 9 visual feeds in 16 languages, representing a total of 47 million households across EMEA.

Launched in June 2011 in Africa, Disney Junior is the multiplatform entry point to all things Disney, starting from preschoolers ranging up to 7 year olds, and their carers and parents. With creative storytelling and engaging characters we help make learning a playful experience, whilst ensuring that parent and caregivers can immerse their kids in a safe and fun environment.

Highlights across the Disney Junior channel includes:
Disney Junior's animated television series, Sofia the First, is set in the storybook world of Enchancia. It tells the story of Princess Sofia - an adventurous little girl who is learning how to adjust to royal life after her mother marries the king and she becomes a princess overnight. Sofia is learning how to adjust to life with her new family which includes her step-father, King Roland II, and step-siblings Amber and James. Along the way, this ordinary girl learns to navigate the extraordinary life of royalty, and in the process makes everyone around her feel special.

Showcasing the hallmarks of great Disney storytelling, fantasy and wish fulfilment, Disney Junior's animated series, Doc McStuffins, tells the story of a nurturing six-year-old girl who can talk to the stuffed animals and toys that she cares for in her playhouse clinic. When Doc puts on her stethoscope, something magical happens; toys, dolls and stuffed animals come to life and she can communicate with all of them, including the toys belonging to her friends and other neighbourhood children.

Not only a ratings hit, the show has sparked a cultural nerve in the U.S., generating applause on parent blogs, Facebook and even in academia for its positive vocational message for African-American girls. Viewer Dr. Myiesha Taylor, who watches the show with her four year-old, was moved to create an online collage featuring an image of Doc, encircled by photos of 131 black women who are Doc’s real life counterparts. “We are trailblazers,” Taylor proclaimed on her website. “We are women of colour. We are physicians. We ARE role-models. We are Doc McStuffins all grown up!”

Disney Junior's Annie Award-winning series, Jake and the Never Land Pirates, is a music-filled interactive treasure hunt that introduces a crew of kid pirates - leader Jake and pals Izzy and Cubby - and follows their Never Land adventures as they work to outwit two infamous characters, the one and only Captain Hook and Mr. Smee, from Disney's classic, Peter Pan.
Minnie, Goofy, Donald, Pluto and Daisy all join Mickey in Mickey Mouse Clubhouse, Disney Junior’s vibrant interactive series that invites young viewers to help solve challenges and overcome obstacles. Each engaging story features a different theme and offers cognitive, social and creative-learning opportunities through a dynamic, play-along experience. Interactivity is key from start to finish as Mickey speaks directly to preschoolers, asking questions and encouraging them to play games, participate in special phrases or cheers, and solve puzzles to reach a goal.

Together with heritage animated series such as Gummi Bears, Chip ‘n Dale, Ducktales and classic Disney movies Aladdin, Cinderella and more, Disney Junior continues to create shared Disney memories between young and old viewers alike.
As of 1 October 2015, Disney Africa will launch the Disney Junior Africa Facebook page, giving parents and caregivers their very own Disney Junior experience on social media.
For more information, please visit www.dstv.com or www.gotvafrica.com.

Saturday, September 5, 2015

LOWASSA APATA MAPOKEZI MAKUBWA TABORA,HAIJAWAHI KUTOKEA KWA KIONGOZI YEYOTE ALIYETEMBELEA MKOANI HUMO

Mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema kupitia Ukawa Bw.Edward Lowassa akizungumza na Maelfu ya Wananchi wakiwemo Wafuasi wa Vyama vinavyounda Ukawa mkoani Tabora ambapo katika mkutano huo wa Kampeni  za Uchaguzi  mkuu Wananchi wamejitokeza kwa wingi kuliko ilivyokawaida hatua ambayo wengi wao wameonesha kumuunga mkono mgombea huyo aliyewaahidi kuleta Mabadiliko makubwa ya Maendeleo  endapo kama Wananchi watampatia ridhaa ya kuongoza nchi. 
Maelfu ya Wananchi waliojitokeza kumsikiliza Mgombea Urais Bw.Edward Lowassa katika viwanja vya Town School mjini Tabora
Ummati mkubwa wa Wananchi  ukimshangilia Bw.Lowassa katika mkutano wa Kampeni za Uchaguzi mkuu
Mabango yenye ujumbe mbalimbali yalikuwa ni sehemu ya Shamrashamra za Mapokezi ya Bw.Lowassa  yaliyofanywa na Wananchi wenyewe kwa hiari zao.
Waziri mkuu wa zamani Bw.Fredrick Sumaye akizungumza na Wananchi wa Tabora mjini kabla ya kumkaribisha Bw.Lowassa kuzungumza na Wananchi hao walioonesha kuwa na shauku ya kumsikiliza mgombea Urais huyo.

Helkopta iliyomleta Mgombea Urais Bw.Lowassa katika viwanja vya Town School Tabora mjini mahali ambako mkutano huo wa kampeni ulifanyika.







MUNDE AFANYA KONGAMANO KUBWA NA WANAFUNZI WA KIKE VYUO VIKUU NA KATI TABORA

Mgombea Ubunge wa Vitimaalum  mkoa wa Tabora  kwa tiketi ya CCM Bi.Munde Tambwe akizungumza katika Kongamano la Wanafunzi wa Kike wa Vyuo vikuu na vya kati katika Ukumbi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tabora ambapo katika Kongamano hilo Wanafunzi walielezea Changamoto mbalimbali zinazowakabili ambazo ni moja ya sehemu zinazokwamisha maendeleo yao hususani ukosefu wa ajira mara baada ya kuhitimu masomo yao.
Wanafunzi wa Vyuo vikuu na vya kati wakimsikiliza kwa makini Mgombea Ubunge wa Vitimaalum Bi.Munde Tambwe wakati akihutubia ambapo pamoja na mambo mengine Wanafunzi hao walimpongeza Mgombea huyo ambaye amekuwa akiwajali kwa kuwatembelea katika vyuo vyao kutambua matatizo yanayowakabili na kujaribu kuyashughulikia.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tabora Bw.Hassan Wakasuvi akihutubia katika Kongamano hilo ambapo pamoja na kusikiliza kero zinazowakabili Wanafunzi hao wa vyuo aliwapongeza kwa kukiunga mkono Chama Cha Mapinduzi hususani wakati huu wa kuelekea Uchaguzi mkuu ambapo aliwataka kuwapigia Kampeni wagombea wa nafasi za Udiwani,Ubunge na Urais mahali popote wanapofanikiwa kuzungumza na wananchi huko mitaani.
Mgombea Udiwani kwa tiketi ya CCM kata ya Cheyo Manispaa ya Tabora Bw.Yusuph Kitumbo alipata fursa ya kuzungumza jambo katika Kongamano hilo aliwaomba Wanafunzi hao kukipatia ushindi Chama Cha Mapinduzi katika Uchaguzi mkuu wa mwaka huu.





Wednesday, September 2, 2015

CHAMA CHA UKOMBOZI (CHAUMA), CHAZINDUA KAMPENI ZAKE VIWANJA VYA BAKHRESA MANZESE DAR ES SALAAM LEO


 Mwananchi aliyevalia nguo za Chama Cha Mapinduzi (CCM), akiondolewa na askari polisi baada ya kujipenyeza kwenye uzinduzi wa kampeni za Chama cha Ukombozi Umma (Chauma), uliofanyika viwanja vya Bakhresa Manzese Dar es Salaam leo.
 Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama cha Ukombozi (Chauma), Dk. Hashim Rungwe, akihutubia wakati wa uzinduzi wa kampeni za chama hicho, uliofanyika viwanja vya Bakhresa Manzese Dar es Salaam leo.
 Mzee wa chama hicho, Mbwana Hassan Mbwana akihutubia kwenye uzinduzi huo.
 Mgombea ubunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Robinson Fulgence Lembo, akihutubia kwenye uzinduzi huo.
 Mgombea urais wa Zanzibar,  Mohamed Masoud Rashid, akihutubia.
 Wananchi wakishangilia.



 Mgombea Mwenza wa urais kupitia Chama cha Ukombozi (Chauma), Issa Abbas Hussein, akihutubia wakati wa uzinduzi huo.
Baadhi ya wananchi wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni za Chama cha Ukombozi Umma (Chauma), uliofanyika viwanja vya Bakhresa Manzese Dar es Salaam leo. 
(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

NTAGANDA KUSIMAMA KIZIMBANI ICC LEO.

Mwendesha mashtaka mkuu wa mahakama ya ICC, Fatou Bensouda, amemtaja Bosco Ntaganda kama mtu mwenye sifa mbaya.

Kesi dhidi ya kiongozi huyo wa zamani wa waasi Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC inatarajiwa kuanza kesho.

Ntaganda anatuhumiwa kupanga na kuendesha kampeini ya kikatili Mashariki mwa Congo.

Bensouda amesema Ntaganda aliwalazimisha mamia ya watoto kujiunga na jeshi lake na kwamba wanajeshi wasichana walibakwa na kuwekwa kama watumwa wa ngono.
Wakili wa Ntaganda anayetoka Canada, aliambia wanahabari kuwa tangu atupwe korokoroni, Ntaganda amepunguza sana uzani wake na anawakosa watoto wake 7.
 
Lakini kiongozi huyo wa zamani wa kundi la waasi, anasubiri sana kujitetea kwa kutoa hotuba kortini kesho.

Zaidi ya waathiriwa 2000 wameidhinishwa kushiriki katika kesi hiyo kama mashahidi.
Upande wa mashtaka unapanga kuita wanajeshi watoto wa zamani kama mashahidi katika kesi hiyo.

Kiongozi huyo wa mashtaka alisifu Congo kwa ushirikiano wake na ICC na kutoa wito kwa waathiriwa wawe na subira, akisema, lengo moja muhimu la haki ni kufichua ukweli.

''Shughuli yenyewe huenda ikaonekana kujikokota lakini hatua zote sharti zilenge kupata ukweli'' Alisema Bensouda.

Bosco Ntaganda anakanusha mashtaka yote 18 yaliyowasilishwa dhidi yake na kesi hiyo inatarajiwa kuchukua miaka kadha.
Chanzo:-BBC Swahili
 

MWILI WA BABA YAKE MWANAHABARI, PETER AMBILIKILE WAAGWA JIJINI DAR ES SALAAM, MAZISHI YAKE KUFANYIKA MBEYA LEO

 Marehemu Mzee Anyosisye Mwakyusa enzi za uhai wake.
 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Anyosisye Mwakyusa, baba mzazi wa mwandishi mwandamizi wa gazeti la Jambo Leo, Peter Ambilikile, wakati wa ibada ya kumuombea iliyofanyika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Ubungo Kibangu Dar es Salaam jana, kabla ya kuusafirisha kwenda mkoani Mbeya kwa mazishi yatakayofanyika leo.
 Ndugu jamaa na marafiki wakiaga mwili wa marehemu.

 Waombolezaji wakiwa kwenye ibada ya kuuga mwili wa mzee wetu Anyosisye Mwakyusa.
 Familia ya marehemu ikiwa na huzuni wakati wa ibada hiyo.
 Waomblezaji wakiwa ibadani.
 Wafiwa wakipewa pole.
 Mwanahabari Peter Ambilikile aliyefiwa na baba yake 
akiwa katika huzuni.
 Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Ubungo Kibangu, Kishe Mhando (katikati), akiomba kabla ya kuanza kwa safari ya kwenda mkoani Mbeya.
 Mwili ukiondolewa kanisani.
 Waombolezaji wakisubiri gari lililobeba mwili huo kuondoka kwendaa mkoani Mbeya kwa mazishi.
Ni huzuni tupu.

Na Dotto Mwaibale

MZEE Anyosisye Mwakyusa ambaye ni baba wa Mwandishi Mwandamizi wa Gazeti la Jambo Leo, Peter Ambilikile mwili wake umeagwa jana kwenda mkoani Mbeya kwa maziko. 

Anyosisye alifariki juzi jijini Dar es Salaam kutokana na ugonjwa wa saratani uliokuwa ukimsumbua kwa muda mrefu.

Ibada ya kuaga mwili wa marehemu huyo ilifanyika  katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Ubungo Kibangu jijini  Dar es Salaam jana  ikiongozwa na Mchungaji Kishe Mhando wa ushirika huo.

Mchungaji Mhando alimwelezea Mwakyusa  kama mtu jasiri ambaye siku zote alikuwa mtu wa ibada na alikuwa akihudhuria ibada zote. Aliwaambia waumini kuwa mshahara wa dhambi ni mauti na mshahara wa kuwa na ibada ni maisha ya milele na Bwana Mungu. 

Alisema watu huwa wana ratiba yao na hakuna mtu hata mmoja anayejua ratiba ya Mungu. "Msiba hauchagui mtoto mchanga, mtu mzima, mwanamke au mwanaume. Mipango yote ni ya Mwenyezi Mungu, yeye ndiye anajua anayefuata ni nani," alisema.

Mazishi ya Mzee Mwakyusa yanatarajiwa kutafanyika mkoani nyumbani kwa marehemu eneo la Makungulu jijini Mbeya leo. Mwakyusa alizaliwa Mei 10, 1942. Alifunga ndoa yake mwaka 1968. Alifanya kazi serikalini na alistaafu mwaka 1980. 

Mwaka 1999  Mwakyusa alianza kulalamika kuwa na matatizo ya koo na kuanza kupatiwa matibabu katika hospitali mbalimbali, ikiwemo Hospitali ya Ocean Road hadi kifo chake. 

MMLIKI WA ST. MATHEW ACHOMOLEWA KESI YA TALAKA NA MGAWANYO WA MALI

court_gavel
Na Mwandishi wetu
MAHAKAMA ya Mwanzo Mbagala, Dar es Salaam imesema haiwezi kumuamuru Mmiliki wa nne za Shule za Sekondari, St Mathew na St Marks ,Thadei Mtembei kutoa talaka kwa Magreth Mwangu kutokana na ndoa yao kuwa batili.
Akisoma hukumu hiyo leo, Hakimu Rajab Tamambele alisema ndoa aliyofunga Mwangu pamoja na Mtembei ambayo ni ya kimila ni batili kwa kuwa mdai hakutoa cheti cha ndoa hiyo ilipofungwa.
Alisema kwa misingi hiyo, mahakama haiwezi kumuamuru Mtembei kutoa talaka kwani aliwasilisha cheti cha ndoa ya mke mmoja aliyoifunga mwaka 1985.
pia alisema mahakama hiyo haiwezi kugawa mali kama ambavyo mdai ameiomba mahakama, ambapo amesisitiza kuwa mgawanyo wa mali unatokana na ndoa halali ambayo baba na mama wanaishi pamoja.
‘’Mashahidi wote wameeleza kuwa Mtembei na Mwangu walikuwa wanakutana hoteli ya Sleep Inn. Kwa hivyo mahakama inaona kuwa uhusiano kati ya mdai na mdaiwa ulikuwa wa kimapenzi pekee au hawara na kwa lugha ya kistaarabu tunaita mzazi mwenzie,’’ aliongeza Tamambele.
Alifafanua kuwa kulipa mahari ambapo mdai aliieleza mahakama kuwa alitolewa ng’ombe watano, sio njia ya kufunga ndoa bali ni kuelekea kufunga ndoa.
Aliendelea kusema kuwa kitendo cha baba kupewa mahari akiwa peke yake bila ya kuwa na mzee wa kabila hilo kuthibitisha, sio sahihi katika sheria za ndoa.
Akisoma hukumu hiyo kwa saa moja, Hakimu Tamambele alisema kuwa watoto watatu kati ya Mtembei na Mwangu ni batili kwani wamezaliwa nje ya ndoa, hivyo mahakama haiwezi kuamuru watoto hao kupatiwa matunzo.
‘’Mdaiwa anatakiwa kushukuru kitendo cha mdai kujenga nyumba tatu kwa ajili ya watoto kwani wengine hawawezi kufanya kitu kama hicho. Kila mzazi anatakiwa kuwatunza watoto hao, ’’ alisema.
Akizungumzia kuwakilishwa kwa mdaiwa, alisema kwa mujibu wa sheria ya kama mdaiwa ni mgonjwa anaweza akawakilishwa ambapo mtoto wake, Peter ndiye alichukua nafasi ya kumuwakilisha baba yake.
Aidha, alisema haki ya kukata rufaa kwa mdai iko wazi na kwamba inatakiwa kukatwa kwa siku 45.
Katika kesi hiyo ambayo ilifunguliwa Juni 5, mwaka huu, Mwangu aliiomba mahakama kumuamuru mdaiwa kutoa talaka, matunzo ya watoto na ya machumo ya pamoja yenye thamani ya Sh milioni 800.
Alisema kesi hiyo ilikuwa na jumla ya mashahidi nane ambapo watano kutoka upande wa mdai na watatu upande wa mdaiwa.
Alisema mdai alifungua kesi kupitia ofisi ya Ustawi wa jamii na ilipoanza kusikilizwa mdai alisema walianza mahusiano mwaka 1995 ambapo walizaa watoto watatu na walijenga shule nne, nyumba pamoja na hoteli tatu za Dar es Salaam na Bukoba.

MAHOJIANO NA TAUSI SUED JUU YA CSI FUNDRAISING


Dear All,

Come join the Embassy of Tanzania and Childbirth Survival International (CSI) for CSI’s first annual fundraising on September 12th at 4:30pm to 7pm, at the Embassy of Tanzania, Washington DC.

In Tanzania, many of the lives lost during pregnancy, childbirth, and immediately after birth, are often 100% preventable. We are calling upon You to join us and help save lives. This fundraising is to kickoff CSI’s saving lives at birth project in Biharamulo District in northwest Tanzania. Biharamulo is one of Tanzania’s poorly performing Districts that deserves immediate support and attention – We thank you for answering the call. Visit www.childbirthsurvivalinternational.org for more information.

There’s a registration fee of $100 and it includes a raffle ticket. All donations are tax deductible and will be used to implement project activities in Biharamulo. Registration link here.

Light Refreshments | Entertainment | Raffle Prizes | Networking

For information about the event, please contact
Sandra Kiyonga at sandra.kiyonga@childbirthsurvivalinternational.org or call 202-763-2100.

Tuko Pamoja!